Kura ya SIRI na WAZI kurudishwa kwa Wajumbe tena kwa Maamuzi

Kura ya SIRI na WAZI kurudishwa kwa Wajumbe tena kwa Maamuzi

ghilipolla

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2014
Posts
280
Reaction score
53
Ndivyo nilivyomsikia mwenyekiti wa kamati hiyo ya Siri na Uwazi katika taarifa ya habari akisema pande zote 2 zimetoa hoja za msingi na za kidemokrasia na kushindwa kutoa maamuzi na Usiri huo na Uwazi kurejeshwa tena kwa Wajumbe kwa maamuzi.,

Source: Chanal10
 
Kama hoja ya uwazi itapita, itawagawa sana wajumbe ndani ya bunge hilo la katiba! Wabunge wa bunge la katiba wajitaidi kuonyesha msimamo na mshikamano kama taifa badala ya kutetea itikadi ya vyama vyao! Taifa kwanza, vyama baadae!
 
Ni mwendawizimu tu mwenye ujasiri wa kusimama hadharani kutetea kura ya wazi kwenye suala muhimu kama hili. Hatuchagui monitor wa STD. III bali Katiba ya Nchi. Kwa kuwa tayari kuna mgawanyiko miongoni mwa wajumbe, ninashauri ili kuwa na maamuzi sahihi ya aina ya kura itakayotumika maamuzi yafanyike kwa angalau 2/3 ya makundi yote kuridhia kwa angalau 50% ya wajumbe wa kundi husika.

Hii itasaidia kuondoa ujinga wa kundi fulani kutaka kuburuza makundi mengine simply kwa sababu ya wingi wao ambao nao umefanywa ka makusudi. Makundi yote ya uwakilishi yanafahamika, hilo lifanyike haraka iwezekanavyo.
 
Hapa tutarajie katiba ya CCM sio katiba ya Watanzania. Kikwete alipopingana na matakwa ya chama chake ya kutokuandika katiba mpya nilimuona wa maana kidogo. Lakini kwa mambo yanavyokwenda, ni usanii tu unafanyika as usual. Tujiandae kuikataa rasimu ya katiba kwenye referundum.

Tiba
 
Napendekeza njia zote zitumike - Siri na wazi - wale wote wanopenda kupiga kura za wazi ruksa na wale wanaopendekeza kupiga kura za Siri ruksa. Uongozi wa Bunge unaweza kuorodhesha makundi hayo mawili na kusimamia wakati wa upigaji kura.

Nina hakika wale wanaotaka kura za wazi hawatakuwa wameangushwa kwa sababu watatuonyesha sisi watanzania misimamo yao ya kidemokrasia (ambayo ndiyo hoja yao kuu).
 
ccm wakishinda kwenye hili tutakuwa na katiba ya hovyo,kwa kura ya siri wanajua wazi muungano utakufa
 
Hapa tutarajie katiba ya CCM sio katiba ya Watanzania. Kikwete alipopingana na matakwa ya chama chake ya kutokuandika katiba mpya nilimuona wa maana kidogo. Lakini kwa mambo yanavyokwenda, ni usanii tu unafanyika as usual. Tujiandae kuikataa rasimu ya katiba kwenye referundum.

Tiba
mkuu unayosema yana ukweli kwa kiasi fulani, lakini watanzania hawana uwezo wa kukataa katiba hii ya ccm! Ccm na wapambe wao watamwaga pilau na vipesa kwa masikini wa kitanzania ambao ni wengi na watashinda tu! Tatizo la tanzania kwa sasa ni watanzania wenyewe na si kingine!
 
Ndivyo nilivyomsikia mwenyekiti wa kamati hiyo ya Siri na Uwazi katika taarifa ya habari akisema pande zote 2 zimetoa hoja za msingi na za kidemokrasia na kushindwa kutoa maamuzi na Usiri huo na Uwazi kurejeshwa tena kwa Wajumbe kwa maamuzi.,

Source: Chanal10

Swali bado lina baki je hii kura ya Siri au ya Wazi hitaamuliwa kwa kura ya Siri au ya Wazi?
 
Tatizo halipo kwa ccm tu,tatizo lipo kwa vyama vyote na wapambe wao,kwa sababu kila chama kimekwenda dodoma kikiwa tayari mkononi kina agenda ya katiba wanayo ihitaji na mifumo ya au serekali 2 au serekali 3,hili lilikua tayari nitatizo,na wanasiasa wanauwezo wa kuwashawishi wajumbe wawakilishi tokea kada mbali mbali na taasisi mbali mbali,kuwaunga mkono,TWAMBIENI NININI FAIDA YA SEREKALI 3 NAIPI NI FAIDA AU HASARA YA SEREKALI 2,
 
Tatizo halipo kwa ccm tu,tatizo lipo kwa vyama vyote na wapambe wao,kwa sababu kila chama kimekwenda dodoma kikiwa tayari mkononi kina agenda ya katiba wanayo ihitaji na mifumo ya au serekali 2 au serekali 3,hili lilikua tayari nitatizo,na wanasiasa wanauwezo wa kuwashawishi wajumbe wawakilishi tokea kada mbali mbali na taasisi mbali mbali,kuwaunga mkono,TWAMBIENI NININI FAIDA YA SEREKALI 3 NAIPI NI FAIDA AU HASARA YA SEREKALI 2,

Uliyoyasema ni kweli, ambapo inafahamika kuna wanaotaka muundo wa serikali2 na wengine serikali3. Lakini wale wanaohisi( niki declare interest hapa mimi napendelea serikali1, ila napenda pia serikali3 ikiwa 1 inashindikana) kuwa serikali 3 ni ANGALAU suluhisho naona wanamashiko. Tume zote zilizotangulia zilikuja na muundo wa serikali3, hapa chama tawala wajiulize mara mbilimbili, ushabiki uachwe kando, tafukuri ishike nafasi, je tume zote zimeleta mapendekezo ambayo wananchi kweli hawajapendekeza? Hivi ni kweli kuwa uongo uwe tu kwenye muundo wa Muungano?! Viongoz wetu mujifunze kukubali ukweli kama munamuogopa Mungu. Yaani kabisa unajua 4+4=8, halafu ulazimishe jawabu ni 4 4, 448,844, 8=8, 9 au 44?, nafsi haziwasuti kushabikia jambo ambalo kimoyomoyo unajua siyo sahihi ila kwa maslahi yaliyojificha unasema ni sahihi? Tuwe wacha Mungu.
 
Zimebaki siku ngapi bunge la katiba liishe? Naona hawana cha kufanya.
 
Uliyoyasema ni kweli, ambapo inafahamika kuna wanaotaka muundo wa serikali2 na wengine serikali3. Lakini wale wanaohisi( niki declare interest hapa mimi napendelea serikali1, ila napenda pia serikali3 ikiwa 1 inashindikana) kuwa serikali 3 ni ANGALAU suluhisho naona wanamashiko. Tume zote zilizotangulia zilikuja na muundo wa serikali3, hapa chama tawala wajiulize mara mbilimbili, ushabiki uachwe kando, tafukuri ishike nafasi, je tume zote zimeleta mapendekezo ambayo wananchi kweli hawajapendekeza? Hivi ni kweli kuwa uongo uwe tu kwenye muundo wa Muungano?! Viongoz wetu mujifunze kukubali ukweli kama munamuogopa Mungu. Yaani kabisa unajua 4+4=8, halafu ulazimishe jawabu ni 4 4, 448,844, 8=8, 9 au 44?, nafsi haziwasuti kushabikia jambo ambalo kimoyomoyo unajua siyo sahihi ila kwa maslahi yaliyojificha unasema ni sahihi? Tuwe wacha Mungu.

mkuu hapo ndipo akili yangu inaponilazimisha kuamini kua dodoma watu wanacheza mchezo wa kuigiza,ebu tutizame swala dogo tu mfumo wa upigaji wa kura unavyo wapotezea muda je watakapofikia kuanza kuichambua rasimu yenyewe ya katiba mkuu siitawachukua zaidi ya nusu mwaka?kiukweli hili bunge binafs naanza kupata hofu na mwenendo wake,
 
ipo siku moja zitapigwa ngumi huko bungeni mungu atunusuru.
 
Huo uamuzi utafanyika kwa kura ya wazi au ya siri? Kama ikiwa ya siri why? Na kama ni ya wazi why?
 
kinasumbua ni upuuzi wa kitu batili kinacho itwa muungano bila kutafsiri maana hali ya ''MUUNGANO'' maana hali ya muungano ni vitu kuanzia viwili kuhungana na kuwa kimoja na siyo viwili kuhungana na kuwa mbili au tatu hapo hakuna muungano bali kuna urafiki, na kilichofanyika kati ya mwalimu nyerere wa tanganyika nashekhe karume ni kuunganisha vyama TANU +ASP=CCM NA AIKUWA KUNGANISHA SEREKALI ndiyo maana zanzibar ikabaki na rais wake na serekali yake na tanganyika ikaendelea na uongozi wake kwa mgogo wa muungano na jambo hili ilitengamaa kwa sababu chama kilikuwa kimoja ccm ambayo ilikuwa na kiongozi mmoja na ndiye alikuwa rais wa jamhuri wa muungano,na muungano huo hauna faida kwa wananchi wa tanganyika, unafaida kwa wazanzibari kupata nafasi za upendeleo, pamoja na haki ya kumiliki ardhi tanganyika wakati mtanganyika hana haki ya kumiliki ardhi zanzibar huu ni unyonyaji kama wakati wa ukoloni, swali ya kujiuliza nilini makamu wa rais, waziri mkuu ,pamoja na mawaziri waliyopewa nafasi kwa sababu ya uzanzibar wao walienda zanzibar kufanya kazi ya muungano kwa wananchi wa zanzibar moja kwa moja kama wanavyofanya hapa tanganyika huu ni unyonyaji usizingatia haki sheria na usawa kwa misingi ya kichama na kulazimisha kupindisha ukweli kama wanataka muungano ni serekali moja tu pemba na unguja zinakuwa mikoa mbona ccm imekuwa moja huu ni muungano wa kitapeli usiyo na faida kwa wananchi wa tanganyika zaidi ya viongozi wa ccm na ikajengwa mfumo wa upendeleo wazanzibari wanauziwa umeme ilitolewa tanganyika kwa bei na fuu huku wanganyika wakiuziwa ka bei ya juu, mali iktolewa tanganyika kwenda zanzibar ailipiwi kudi, lakini ukitoa mali zanzibar kuja tanganyika unalipia kodi huu ni muungano wa aina gani, zanzibar ina katiba yake, zanzibar ina bnendera yake, zanzibar ina wimbo waka, na ina rais wake anayepingiwa mizinga 21 na kukangua gwaride hapa kuna nchi mbili inayotawaliwa na chama kimoja ndiyo ukweli mchungu kwa wanyonyaji weusi,walijaa kiburi na ulevi wa madaraka, kwa kungangania kulazimisha matakwa yao kwa gharama yoyote hii aikubaliki akiungwa mkono na watumwa wachache wa kiuchumi na kifikra na kuogopa kupinga matakwa ya manyabara wa wakoloni hao kwa kuofu ya kukosa chakula
 
kinachosumbua ni upuuzi wa kitu batili kinachoitwa muungano bila kutafsiri maana hali ya ''MUUNGANO'' maana hali ya muungano ni vitu kuanzia viwili kuhungana na kuwa kimoja na siyo viwili kuhungana na kuwa mbili au tatu hapo hakuna muungano bali kuna urafiki, na kilichofanyika kati ya mwalimu nyerere wa tanganyika na shekhe karume ni kuunganisha vyama TANU +ASP=CCM NA AIKUWA KUNGANISHA SEREKALI ndiyo maana zanzibar ikabaki na rais wake na serekali yake na tanganyika ikaendelea na uongozi wake kwa mgogo wa muungano na jambo hili ilitengamaa kwa sababu chama kilikuwa kimoja ccm ambayo ilikuwa na kiongozi mmoja na ndiye alikuwa rais wa jamhuri wa muungano,na muungano huo hauna faida kwa wananchi wa tanganyika, unafaida kwa wazanzibari kupata nafasi za upendeleo, pamoja na haki ya kumiliki ardhi tanganyika wakati mtanganyika hana haki ya kumiliki ardhi zanzibar huu ni unyonyaji kama wakati wa ukoloni, swali ya kujiuliza nilini makamu wa rais, waziri mkuu ,pamoja na mawaziri waliyopewa nafasi kwa sababu ya uzanzibar wao walienda zanzibar kufanya kazi ya muungano kwa wananchi wa zanzibar moja kwa moja kama wanavyofanya hapa tanganyika huu ni unyonyaji usizingatia haki sheria na usawa kwa misingi ya kichama na kulazimisha kupindisha ukweli kama wanataka muungano ni serekali moja tu pemba na unguja zinakuwa mikoa mbona ccm imekuwa moja huu ni muungano wa kitapeli usiyo na faida kwa wananchi wa tanganyika zaidi ya viongozi wa ccm na ikajengwa mfumo wa upendeleo wazanzibari wanauziwa umeme ilitolewa tanganyika kwa bei na fuu huku wanganyika wakiuziwa ka bei ya juu, mali iktolewa tanganyika kwenda zanzibar ailipiwi kudi, lakini ukitoa mali zanzibar kuja tanganyika unalipia kodi huu ni muungano wa aina gani, zanzibar ina katiba yake, zanzibar ina bnendera yake, zanzibar ina wimbo waka, na ina rais wake anayepingiwa mizinga 21 na kukangua gwaride hapa kuna nchi mbili inayotawaliwa na chama kimoja ndiyo ukweli mchungu kwa wanyonyaji weusi,walijaa kiburi na ulevi wa madaraka, kwa kung'ang'ania kulazimisha matakwa yao kwa gharama yoyote hii aikubaliki akiungwa mkono na watumwa wachache wa kiuchumi na kifikra na kuogopa kupinga matakwa ya manyabara wa wakoloni hao kwa kuofu ya kukosa chakula
 
hili ni bunge la katiba au bunge la posho mpya? Siku zote tunaamini katika kura ya siri ndio maamuzi sahihi ya mpiga kura yeyote. Hii kura ya wazi itakuwa ya ushabiki na bendera fuata upepo. Hivi hao wanaoshabikia kura ya ndio au hapana wanaitakia mema nchi hii? Labda tuendelee kusubiri tuone mwisho wake.
 
duh haya mambo huwa yanatokea tanzania tu, yaani kura ya cri itumike kuchagua kura ya wazi, ni -------- tu ndo anaweza kuwa na maamuzi ya kijinga kama haya
 
Back
Top Bottom