Alijichimbia kaburi baada ya kuaminishwa anaongoza awamu ya sita wakati ki uhalisia ni awamu ya tano, sasa vita kubwa ipo kwenye kigezo cha dini, awamu ya tano iliongozwa na mgalatia awamu ya sita (feki) inaongozwa na mvaa kobasi, sasa ikitokea mama akaachia madaraka awamu hii inategemewa anayepitishwa na chama awe mgalatia kitua ambacho kuna wavaa kobasi wa chama wanapinga kwa kusema hii bado ni awamu ya tano na kiongozi wake alikuwa mgalatia ila huyu aliyepo sasa hivi ni ''zali la mentali'' tu, vivyo hivyo akipendekezwa mvaa kobasi mwingine tofauti na mama kuna wagalatia wa chama wanasema inawezekanaje wavaa kobasi watuongoze katika awamu mbili mfululizo? kwahiyo ili kuua so ni bora mama aendelee ili kuizika awamu yake ya sita kisha ngoma irudi kwa wagalatia. Kuna vitu huwa havipo kikatiba ila ni utaratibu rasmi wa kikundi cha wezi wa rasilimali za taifa hili (Chama Cha Majambazi). Zimwi likujualo halikuli likamaliza. Huo ndio ukweli mchungu