Kusaga : Tulipopiga wimbo wa Mbosso tuliambiwa tujieleze kwanini tulikuwa hatupigi nyimbo za wasanii wa Wasafi. Uongozi wa WCB uulizwe

Kusaga : Tulipopiga wimbo wa Mbosso tuliambiwa tujieleze kwanini tulikuwa hatupigi nyimbo za wasanii wa Wasafi. Uongozi wa WCB uulizwe

Kuna swali la msingi hapa anatakiwa alijibu na amelikwepa " Kwanini Mwanzo waliacha kuzipiga nyimbo za wasafi ?
Hilo hawezi jibu.Lkn walikataa kupiga nyimbo za wasanii wengi akina Suma G,Mapacha,Lady Jay Dee,Rama Dee,Wagosi wa Kaya nk.Ila kwa WCB wameshindwa sababu walichotarajia,hakikuwa kama walivyotegemea kwa wasanii wengine waliowabania.

Nakumbuka Mchomvu siku moja anahojiwa akasema management ya CMG imesema isipige nyimbo za WCB.

Kwa hiyo jibu simple tu hata Management ya WCB imeamua nyimbo zao zisipigwe CMG,wao waliamua huko nyuma na WCB wameamua baada kutusua bila wao.Wameanza wenzao wakamaliza.
 
Tatizo la kua na Mameneja uchwara Waswahili na Walozi,.

Wiki Ijayo utamuona Salam kwenye icho kipindi akimwambafai,. Kama ilivyokua kwenye kauli ya penseli Mzee wa kwenda na bit
 
Yani mmiliki wa Kituo cha habari A na B ana enda kuulizwa maswali kuhusu kituo A huko kituo B...

Wakati huo huo mmiliki huyo huyo ndiye mmiliki wakundi lililo mwandikia barua... Ana jaribu kupuuza au wana jaribu kucheza na akili za wambea wa mjini...

Wambea wameshupaaaaa... Hawaelewi nini kina endelea wanashusha shutuma...

Mwisho was siku A na B, Mmiliki na Kundi wameshinda, nyasi zina baki kuumia
 
Wasafi Media iwe ni project ya Joe au isiwe, jamaa wanajitahidi kuwa tofauti sana kwenye hii industry.

Mfano maswali waliyomuuliza huyu boss ni yale yale ambayo yamekuwa debate mtaani.

Pia hawana noma kumpa airtime mtu yoyote hata kama anawadiss. Mfano Carry Mastory, Ney, TID (zamani) na wengine wengi. Naonaga wanapewa interview kabisa kiroho safi.

Hao Clouds sasa. Wakiwa na bifu na mtu au ukiwasema vibaya mpaka mtoto wa chekechea atajua. Mikausho mikali. Mfano hawawezi kabisa kumpa nafasi Dudubaya hata iweje kwa sababu jamaa huwa anawadiss kila siku. Angekuwa anawadiss Wasafi wangesema nae tu.

Wasafi wanajua business na kuoperate kama urban radio/tv.

Kudos!
 
Back
Top Bottom