Kusajili kampuni Brela hadi niwe na sh ngapi?

Kusajili kampuni Brela hadi niwe na sh ngapi?

Singo nakutafuta hapa, nahitaji msaada wako tafadhali.
 
Last edited by a moderator:
mkuu wewe uko mkoa upi kama uko dar nenda pale mnazi mmoja jengo la ushirika zipo ofisi za blrela kule juu horofani, wanasajilisha business name kwa sh 7000 tu kama unahitaji memorandum basi watafute consultant watakusaidia kujkuandikia memorandum au niambie nami nitakusaidia suala hilo

Nataka kufungua kampuni yangu ya udalali (commission agency). Directors ni mimi na rafiki yangu. Sasa pamoja na gharama zote hadi kampuni inasajiliwa, ni lazima niwe na pesa za mtaji kwenye akaunti? Au hata kama sina pesa (mtaji) kampuni yaweza kusajiliwa?
Nisaidieni kujua.
 
Oky aiseeee mpe hongera zake amepiga hatua nzuri sana maana waandishi wa vitabu wako wachache sana siku hizi hapa tanzania mpe hongera zake jamani
ni binti yangu,
mpe muda kidogo anahangaika na usajili huko chuoni kwao.
 
Ila swali lake la msingi halijajibiwa

je ni lazima awe na pesa ya mtaji kwenye account?
 
UFAHAMU KUHUSU KAMPUNI NA USAJILI WAKE: Kuna Kampuni za aina mbili, kampuni ambayo ni Limited by shares na zile ambazo ni limited by guarantee. Zote kati ya hizo zinaweza kuwa private company au public company. Uchaguzi wa ni kampuni ya aina gani itakufaa ufungue hutegemea sana na shughuli unayokusudia kuifanya. Consultant atakushauri vizuri.
Taratibu za kusajili kama zilivyoelezwa na mjumbe mmoja kwa kirefu hapo juu ni rahisi sana kuzitaja ila si rahisi sana kuzitekeleza. Wengi wamezoeshwa kuchakachuliwa, Unamkuta mtu hana uzoefu, elimu wala ufahamu sahihi wa kuandaa memorandum and article of association, anachofanya ni kubadilisha jina katika memorundum nyingine na kuweka jina la kampuni yako kisha kuisajili. Matokeo yake unapata memorundum and article of association ambayo kwanza haiakisi maono yako, pili inaweza ikakosa objectives mtambuka, tatu ni kwamba mambo muhimi ya umiliki wa kampuni yanaweza yakawa hayajawekwa vizuri ili kukulinda founder, ikasababisha watu watakaoingia baadae wakawa na upenyo wa kutake over kampuni yako, lakini kubwa na hatari zaidi, vitabu ambavyo utakuwa umekabidhiwa vinaweza kuwa tofauti na vile viliyobaki Brela. Mtu huyo maarufu kama (Vishoka) Anaweza kukufanyia uhuni wa kupunguza share capital ili alipe pesa kidogo pale brela. na hutaweza kujua mpaka umepata tatizo, au ukafanye rejea. Hivyo nawashauri kufanya kazi na watu competent. Ndio maana consulting company kama ANJOA COMPANY LIMITED zipo kwa ajili yako. wasiliana nasi kwa ushauri, huduma na maoni kwa namba 0759-692024 au 0688-510564 email: info@anjoa.co.tz
 
Ila swali lake la msingi halijajibiwa

je ni lazima awe na pesa ya mtaji kwenye account?

ni vema kuwa na mtaji ila sio lazima huko Brela kwenye kusajili. ila kwa vile unasajili kampuni ili ufanyie shughuli zako itakuwa sio vema kufungua kampuni wakati huna hata shs 100 ya kuendesha shughuli za kampuni unayoisajili
 
unaweza kusajiliwa kampuni yako brela ndani ya siku 3 za kazi. unaweza kuni PM kwa maelezo zaidi
 
KUANDIKISHA BIASHARA
Kabla ya kuanza biashara, sharti isajiliwe kwa
mujibu wa sheria za nchi.
Jina la Biashara
Biashara sharti iwe na jina na inaweza
kuandikishwa kama ya mtu mmoja, kampuni,
ushirika au ubia.
Kama biashara yako itakuwa ya mtu mmoja
(sole proprietorship) itakupasa kufuata
utaratibu huu:-
(1)Chagua jina la biashara (2) Andika barua
kwa Mkurugenzi wa BRELA ukiomba
kuangaliziwa jina ulilochagua kama halijasajili
na mwingine (kwa sasa unaweza kuangalia
mwenyewe kutoka tovuti: www.brela-tz.org),
(3) Baada ya jina kupita jaza fomu nambari 2
na 3 ambazo unaweza kuzipata toka tovuti ya
BRELA (4) Lipia ada ya usajili ya Sh. 6,000/=
(5) wasilisha fomu na baada ya siku chache
utapatiwa hati ya usajili.
Kama unataka kusajili kampuni yenye ukomo
(Limited Liability) itakulazimu kuzingatia
yafuatayo:-
(1)Kampuni lazima iwe na watu si chini ya 2 na
wasizidi 50 (2) hakikisha jina la kampuni
utakalopendekeza liwe halijawahi kutumika
katika tovuti ya BRELA: www.brela-tz.org (3)
Andaa hati ya makubaliano (MEMARTs) (4)
Jaza fomu nambari 14a na 14b (5)hakikisha
MEMARTs na fomu 14b zimesainiwa na wakili
au mwanasheria (6)Lipia gharama za usajili
kulingana na mtaji unaoanza nao, (7) wasilisha
maombi yako na hati ya usajili itatolewa baada
ya muda mfupi.
JISAJILI KAMA MLIPA KODI (TIN
NUMBER)
Mfanyabiashara pia anapaswa kujisajili
mamlaka ya kodi – TRA. Ili kujisajili unapaswa
kuzingatia yafuatayo: (1) uwe na hati ya usajili
(2) uthibitisho wa eneo la biashara.
LESENI YA BIASHARA
Biashara zote lazima ziwe na leseni na vibali
maalum ambazo hutolewa na ofisi za biashara
za halmashauri ya Manispaa au Wilaya ya eneo
la biashara yako. Baada ya kupata leseni na
vibali toka maamlaka husika unaweza sasa
kuanza biashara yako.


Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

Samahani, nataka kuuliza hii brela ni company ina deal na kitu gani hasa, nini maana ya brela?

Na mimi niko mbioni kufungua company yangu, nasubiri facilities zifike tanzania tu.
 
Kaka kuna jamaa huku JF anaitwa Singo jaribu kumtafuta ni mtu smart sana katika kazi na bei zake ni nafuu na anafanya kazi on time.

Ameshanifanyia kazi yangu ya kufungua kampuni ikiwemo name search Brela,Memorandum baada ya 1week amenikabidhi Certificate of Incorporation.Gharama zake ni ndogo sanaa compare na wengi wa humu ndani.
Mkuu nipm namba ya singo nicheck nae
 
ni vema kuwa na mtaji ila sio lazima huko Brela kwenye kusajili. ila kwa vile unasajili kampuni ili ufanyie shughuli zako itakuwa sio vema kufungua kampuni wakati huna hata shs 100 ya kuendesha shughuli za kampuni unayoisajili
Ni kweli nafikiri utakapolitumia hili jina kupata leseni na Tin unaweza kutozwa kodi kubwa ukidhaniwa umeanza kufanya kazi muda wakati ulikuwa wasubiri mtaji.....
 
Samahani, nataka kuuliza hii brela ni company ina deal na kitu gani hasa, nini maana ya brela?

Na mimi niko mbioni kufungua company yangu, nasubiri facilities zifike tanzania tu.

Brela -business registration and licensing agency,ni wakala wa serikali wa usajili na kusimamia makampuni na wapo chini ya wizara ya viwanda na biashara,ukihitaji kusajili waweza nitumia mimi,nimefanya kazi na watu kadhaa wa humu kwa mafanikio
 
Back
Top Bottom