Kusema Rais anashauriwa vibaya ni kujaribu kueleza kuwa Rais hana akili; naona ni ukosoaji wa kinafiki

Kusema Rais anashauriwa vibaya ni kujaribu kueleza kuwa Rais hana akili; naona ni ukosoaji wa kinafiki

You are nit being clear.

Nchi yetu haijakomaa kivipi?

Hatuna washauri wenye sifa? Hatuna mifumo ya kukubali ushauri...

Nafikiri sababu moja ya huu mjadala ni IGA ya Dubai na Tanzania...
Now hapo ndo tunaweza sasa ulizana tunao renown expert wa eneo hilo kwenye cabinet ya Rais?..je katika washauri wake nje ya cabinet?

Kuna hata majina yanayo sifika hata regional Tu kuwa ni mabingwa WA eneo hilo wako Ikulu?

Ndo maana nikakupa mfano wa Larry Summers....linapotajwa jina lake popote Una confidence ya kusema kuna Mtaalam wa uchumi kasema...au Rais Obama au Clinton ana Mtaalam wa uchumi ambae kama kapitisha hiki basi probably wako right.

Je hizo PhD zetu zina rank level ipi hata regional Tu?..ziko updated kiwango gani na mabadiliko ya dunia kutoka uchumi wa kuendeshwa na serikali hadi huu uchumi wa private companies dunia nzima?

PhD zipi ? Issa Shivji anaetaka hata Benki ziendeshwe na serikali? Au Kabudi ambae kwake Nyerere ni almost God mwaka huu wa 2023?
 
Ma Rais dunia nzima wanategemea ushauri....hakunaga kitu kama Rais mwenye akili...na Rais asie na akili..

Akili ya ma Rais wote hutegemea advisors ndo maana wenzetu wameenda mbali Sana na kuweka washauri rasmi wa Rais Kwa kila kitu...
Lakini Hawa dp-world au wachawi (majini)

Pamoja na hayo umesema ,marekani ikulu ya bush George iliingia mkenge ,bunge likaamua ugomvi

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Mzee
Kikwete senior alishasmea hili ,wanakuja kushauri ,likiingia mchanga lakwako pekee rais

Marais wetu wawe makini na watu kati wao (mawinga)

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Point yangu hapa ni kuwa kabla hata ya Rais hatujamlaumu Kwa kupokea ushauri ...kwanza tuna uhakika hata wapo hao washauri?na Wana qualify kuitwa washauri?..Kwa sababu Kwa uzoefu wangu huwa inapita miaka kadhaa ndo unakuja kusikia Fulani alikuwa mshauri wa Rais ..mfano Lipumba alipoingia CUF ndo tunaambiwa aliwahi kuwa mshauri wa Rais Mwinyi na Museven kwenye uchumi na wala hatuna namna ya Ku verify alikuwa mshauri Kwa kiwango gani?..
Nimekuelewa sasa, kwa nchi zetu hizi ni ngumu kupata 'a,b,c ' za washauri wa Rais, hivyo hatuwezi kupima hata athari/matokeo ya ushauri wao kama ulikuwa mzuri au la.
 
Nafikiri sababu moja ya huu mjadala ni IGA ya Dubai na Tanzania...
Now hapo ndo tunaweza sasa ulizana tunao renown expert wa eneo hilo kwenye cabinet ya Rais?..je katika washauri wake nje ya cabinet?...
Kuna hata majina yanayo sifika hata regional Tu kuwa ni mabingwa WA eneo hilo wako Ikulu?..
Ndo maana nikakupa mfano wa Larry Summers....linapotajwa jina lake popote Una confidence ya kusema kuna Mtaalam wa uchumi kasema...au Rais Obama au Clinton ana Mtaalam wa uchumi ambae kama kapitisha hiki basi probably wako right....

Je hizo PhD zetu zina rank level ipi hata regional Tu?..ziko updated kiwango gani na mabadiliko ya dunia kutoka uchumi wa kuendeshwa na serikali hadi huu uchumi wa private companies dunia nzima??..
PhD zipi ? Issa Shivji anaetaka hata Benki ziendeshwe na serikali? Au Kabudi ambae kwake Nyerere ni almost God mwaka huu wa 2023?......
Kwa mawazo yako kabisa, unafikiri kwamba tatizo la IGA ya Dubai na TZ ni washauri, si rushwa?

Mbona mimi wala si mwanasheria naishia kukagua mikataba ya kupangisha nyumba zetu tu, na nilivyoisoma IGA nikaona matatizo mengi sana ambayo wanasheria wa TLS wakaja kuyaona vilevile nilivyoona? Ina maana mimi nimewapita uwezo wanasheria wa serikali mpaka AG?

Unafikiri AG na team yake hawakuona yale madudu ambayo hata mtu asiye mwanasheria, anayejua Kiingereza tu, anayaona?

Unafikiri tatizo la ushauri, si rushwa, ndilo limefanya serikali iwahishe mkataba upate kupitishwa bungeni?

Umesoma review ya TLS? Rais angewachukua watu wachache tu wa TLS unafikiri kungekuwa kuna shida ya ushauri?

Unafikiri serikalini hakuna wanasheria wenye uwezo kama hao wanasheria wa TLS?

Unaamini kabisa kuwa hapa tatizo ni uwezo wa washauri, si rushwa na kuendesha mambo kwa amri kutoka juu?
 
Je hizo PhD zetu zina rank level ipi hata regional Tu?..ziko updated kiwango gani na mabadiliko ya dunia kutoka uchumi wa kuendeshwa na serikali hadi huu uchumi wa private companies dunia nzima??..
Hili ni muhimu sana kuzingatia.....hivi ni lazima washauri wa Rais wawe wazawa tu, je ni vibaya kuajiri wenye uzoefu kutoka nje mfano hata kukodisha mashirika, kampuni kufanya hivyo kama muda ?


PhD zipi ? Issa Shivji anaetaka hata Benki ziendeshwe na serikali? Au Kabudi ambae kwake Nyerere ni almost God mwaka huu wa 2023?.....
Hawa wazee wasoshalisti kwani hawawezi kushauri ?...huenda wakawa wazuri zaidi kutusaidia tusirudie makosa yaliyofanyika huko nyuma............kumbuka Deng Xioping wa China alikuwa m-communisti ila alileta mageuzi makubwa ya kiuchumi kwa kuruhusu soko huria mpaka kuitwa 'Father of modern China'
 
Kuwa na Washauri ni kawaida. Lakini washauri wanaokupotosha na ukafanya hapo ndipo mada yangu ilipo.
kama nimekuelewa vizuri taikun ni kwamba ushauri bora ni wa kwako mwenyewe as long as uko timamu ushauri mwingine unakuwa una confirmation tu which means unaweza kuukubali au kuukataa depending on ushauri wenyewe!
 
Nafikiri sababu moja ya huu mjadala ni IGA ya Dubai na Tanzania...
Now hapo ndo tunaweza sasa ulizana tunao renown expert wa eneo hilo kwenye cabinet ya Rais?..je katika washauri wake nje ya cabinet?...
Kuna hata majina yanayo sifika hata regional Tu kuwa ni mabingwa WA eneo hilo wako Ikulu?..
Ndo maana nikakupa mfano wa Larry Summers....linapotajwa jina lake popote Una confidence ya kusema kuna Mtaalam wa uchumi kasema...au Rais Obama au Clinton ana Mtaalam wa uchumi ambae kama kapitisha hiki basi probably wako right....

Je hizo PhD zetu zina rank level ipi hata regional Tu?..ziko updated kiwango gani na mabadiliko ya dunia kutoka uchumi wa kuendeshwa na serikali hadi huu uchumi wa private companies dunia nzima??..
PhD zipi ? Issa Shivji anaetaka hata Benki ziendeshwe na serikali? Au Kabudi ambae kwake Nyerere ni almost God mwaka huu wa 2023?......
Kama rais anawachagua akina bulembo eti ndo washauri wake unategemea nini
 
Nimekuelewa sasa, kwa nchi zetu hizi ni ngumu kupata 'a,b,c ' za washauri wa Rais, hivyo hatuwezi kupima hata athari/matokeo ya ushauri wao kama ulikuwa mzuri au la.
Juzi kamchugua bulembo
 
Hili ni muhimu sana kuzingatia.....hivi ni lazima washauri wa Rais wawe wazawa tu, je ni vibaya kuajiri wenye uzoefu kutoka nje mfano hata kukodisha mashirika, kampuni kufanya hivyo kama muda ?



Hawa wazee wasoshalisti kwani hawawezi kushauri ?...huenda wakawa wazuri zaidi kutusaidia tusirudie makosa yaliyofanyika huko nyuma............kumbuka Deng Xioping wa China alikuwa m-communisti ila alileta mageuzi makubwa ya kiuchumi kwa kuruhusu soko huria mpaka kuitwa 'Father of modern China'
Hatuna tatizo la ushauri, tatizo letu ni kwamba nchi inaendeshwa kwa amri kutoka juu, haiendeshwi kwa kusikiliza ushauri wa kitaalamu.

Lawrence Mafuru, a very respected banker, alimshauri Magufuli kuhusu kubana mzunguko wa pesa kwa kasi kutakavyokuja kuharibu uchumi. Akamshauri Magufuli aende polepole. Magufuli alimtoa Mafuru kuwa Registrar wa Hazina, Mafuru basically akawa jobless mpaka Samia alivyomkumbuka baada ya Magufuli kufariki.

Hata kwenye IGA, wanasheria nguli wachache tu wangeweza jutuonesha matatizo makubwa yote. Nchi ina watu milioni zaidi ya sitini hii. Kuna watu kama kina Dr. Nshala wame specialize kwenye mikataba kama hii, wamesoma Harvard and Yale mambo haya, na kufanyia research kubwa. I am sure rais angemuita Dr. Nshala hata kama unofficial advisor aangalie mkataba, Dr. Nshala angemuonesha madudu.

Washauri wa serikali wanaendeshwa kisiasa mpaka wanajistukia, wanakuwa wanasikiliza kinachotakiwa kushauriwa, na wao wanashauri hichohicho.

Hivi nyie hamuelewi wapi?

Mimi nilikuwa na rafiki yangu mmoja, very smart chap, kafanya kwenye NGOs za elimu, kasoma mpaka Harvard, anajua mambo ya mitaani, very well rounded kuanzia kwa watu chini, mpaka Ivy Towers huko Harvard and Yale and Wall St. circles.

Alikuwa mwanaharakati sana mambo ya elimu. Kikwete akamuona huyu anasema sana, ngoja nimchukue nimuoneshe mambo yanavyoenda serikalini.

Akamteua kuwa mshauri wake mambo ya elimu. Jamaa akaona sasa hapa nimepata sikio la rais, nimechaguliwa kuwa mshauri, nitaleta impact, yale mambo yangu yote niliyokuwa nafanya activism sasa nitamwambia rais, tubadili policy serikalini. Nina sikio la rais sasa.

Jamaa akawa anamwambia Kikwete, hapa tufanye hivi na hivi. Kikwete anamjibu, hilo, hilo mbona tunalijua miaka mitano sasa, mfuate fulani wizarani atakupa makabrasha yote, walishafanya study na ripoti anayo.

Jamaa anamwambia Kikwete hapa kwenye elimu ya msingi mitaala tufanye hivi na hivi, Kikwete anamjibu hilo, hilo tushalisoma tangu enzi za Mungai, mfuate Katibu Mkuu Elimu atakupa makabrasha yote, tumefanya study na ripoti tunazo, tena nyingine wamekuja Wazimbabwe ku copy hapa mwaka jana.

Kila jamaa anachoshauri, anaambiwa tushafanya study, matokeo yapo wizarani, nenda kwa fulani utapata ripoti.

Jamaa akajitafakari sana, kama hawa watu wanajua kila kitu nilichofikiri nataka kuwashauri, mimi hapa nafanya kazi gani kama mshauri?

Akaona kumbe ali wa underestimate sana watu wa serikali kwa kufikiri hawajui mambo. Akagundua kwamba serikali ya Tanzania ina taarifa nyingi sana, ripoti nyingi sana, ina ushauri karibu wote inaouhitaji.

Tatizo si ushauri, tatizo ni political will, tatizo ni ulaji wa watu, watu wanaona wakibadili mambo ulaji wao utapotea.

Jamaa akaona kazi yake ya mshauri wa rais haina impact aliyotegemea.

Akaenda New York akachukua kazi ya kuongoza Foundation moja kubwa ya kimataifa. Akawa anafanya kazi za kimataifa huko, anaongoza taasisi yenye bajeti ya mabilioni ya dola.

Siku moja nilikaa naye New York City akanipa story hii mwenyewe.

Ukiangalia habari hii utaona kuna matatizo ya kimfumo yaliyowapita washauri, kiasi cha washauri wengine wanaotaka kutetea mkate wao kuona ni bora wanyamaze tu au washauri kinachotakiwa kusikika na wakubwa lakini si kinachopaswa kusikika.
 
Hatuna tatizo la ushauri, tatizo letu ni kwamba nchi inaendeshwa kwa amri kutoka juu, haiendeshwi kwa kusikiliza ushauri wa kitaalamu.

Lawrence Mafuru, a very respected banker, alimshauri Magufuli kuhusu kubana mzunguko wa pesa kwa kasi kutakavyokuja kuharibu uchumi. Akamshauri Magufuli aende polepole. Magufuli alimtoa Mafuru kuwa Registrar wa Hazina, Mafuru basically akawa jobless mpaka Samia alivyomkumbuka baada ya Magufuli kufariki.

Hata kwenye IGA, wanasheria nguli wachache tu wangeweza jutuonesha matatizo makubwa yote. Nchi ina watu milioni zaidi ya sitini hii. Kuna watu kama kina Dr. Nshala wame specialize kwenye mikataba kama hii, wamesoma Harvard and Yale mambo haya, na kufanyia research kubwa. I am sure rais angemuita Dr. Nshala hata kama unofficial advisor aangalie mkataba, Dr. Nshala angemuonesha madudu.

Washauri wa serikali wanaendeshwa kisiasa mpaka wanajistukia, wanakuwa wanasikiliza kinachotakiwa kushauriwa, na wao wanashauri hichohicho.

Hivi nyie hamuelewi wapi?

Mimi nilikuwa na rafiki yangu mmoja, very smart chap, kafanya kwenye NGOs za elimu, kasoma mpaka Harvard, anajua mambo ya mitaani, very well rounded kuanzia kwa watu chini, mpaka Ivy Towers huko Harvard and Yale and Wall St. circles.

Alikuwa mwanaharakati sana mambo ya elimu. Kikwete akamuona huyu anasema sana, ngoja nimchukue nimuoneshe mambo yanavyoenda serikalini.

Akamteua kuwa mshauri wake mambo ya elimu. Jamaa akaona sasa hapa nimepata sikio la rais, nimechaguliwa kuwa mshauri, nitaleta impact, yale mambo yangu yote niliyokuwa nafanya activism sasa nitamwambia rais, tubadili policy serikalini. Nina sikio la rais sasa.

Jamaa akawa anamwambia Kikwete, hapa tufanye hivi na hivi. Kikwete anamjibu, hilo, hilo mbona tunalijua miaka mitano sasa, mfuate fulani wizarani atakupa makabrasha yote, walishafanya study na ripoti anayo.

Jamaa anamwambia Kikwete hapa kwenye elimu ya msingi mitaala tufanye hivi na hivi, Kikwete anamjibu hilo, hilo tushalisoma tangu enzi za Mungai, mfuate Katibu Mkuu Elimu atakupa makabrasha yote, tumefanya study na ripoti tunazo, tena nyingine wamekuja Wazimbabwe ku copy hapa mwaka jana.

Kila jamaa anachoshauri, anaambiwa tushafanya study, matokeo yapo wizarani, nenda kwa fulani utapata ripoti.

Jamaa akajitafakari sana, kama hawa watu wanajua kila kitu nilichofikiri nataka kuwashauri, mimi hapa nafanya kazi gani kama mshauri?

Akaona kumbe ali wa underestimate sana watu wa serikali kwa kufikiri hawajui mambo. Akagundua kwamba serikali ya Tanzania ina taarifa nyingi sana, ripoti nyingi sana, ina ushauri karibu wote inaouhitaji.

Tatizo si ushauri, tatizo ni political will, tatizo ni ulaji wa watu, watu wanaona wakibadili mambo ulaji wao utapotea.

Jamaa akaona kazi yake ya mshauri wa rais haina impact aliyotegemea.

Akaenda New York akachukua kazi ya kuongoza Foundation moja kubwa ya kimataifa. Akawa anafanya kazi za kimataifa huko, anaongoza taasisi yenye bajeti ya mabilioni ya dola.

Siku moja nilikaa naye New York City akanipa story hii mwenyewe.

Ukiangalia habari hii utaona kuna matatizo ya kimfumo yaliyowapita washauri, kiasi cha washauri wengine wanaotaka kutetea mkate wao kuona ni bora wanyamaze tu au washauri kinachotakiwa kusikika na wakubwa lakini si kinachopaswa kusikika.
Umenikumbusha juzi wakati mafuta yalipopanda bei baada ya Ukraine war .. serikali ndo ikagundua kuwa wazo la National Oil reserves lipo kwenye makbrasha ...research ilishafanyika imebaki utekelezaji tu since wakati wa Nyerere. Hadi sasa hatuna National Oil reserves....very very strange
 
Umenikumbusha juzi wakati mafuta yalipopanda bei baada ya Ukraine war .. serikali ndo ikagundua kuwa wazo la National Oil reserves lipo kwenye makbrasha ...research ilishafanyika imebaki utekelezaji tu since wakati wa Nyerere. Hadi sasa hatuna National Oil reserves....very very strange
Ndivyo hivyo sasa.

Hapo napo tutalaumu washauri?
 
Babako Kwa mfano akikosea pakubwa, waeza Sema hadhani kuwa......., Si utanyamaza au kutafuta namna ya kuwasilisha kosa lake,


Tukisema mkubwa hakosei, maana yake ni upande wa pili, kulinda Heshima ya uongozi na KITI.

Bt yapo makosa ambayo hapasi kukosea, mf baba kula mayai ya mama nk nk, haivumiliki.

Miiko ya uongozi ifuatwe. Na viongozi wajiheshimu, wasifanye makosa ambayo hata waongozwa watastuka.

Baba akikosea anaambiwa ndani ya familia. Zingatia neno ndani ya Familia.

Rais NI kama Baba au Mama wa familia. Anaongoza nchi. Akikosea ataambiwa amekosea ndani ya mipaka ya nchi yetu.

Zingatia, nchi inaongozwa na Katiba na sheria. Ikiwa hakuna sheria inayomkataza MTU kukosoa, wala kusema akosoe akiwa wapi,
Ingawaje Ipo namna ambayo sheria inaweza kumtaja mkosoaji asitoe Lugha ya matusi yanayovua utu wake.

Lakini kutaja kosa alilofanya Kiongozi na kumtaja kiongozi Kwa kosa alilofanya sio Tusi. Mfano kiongozi kaiba moja Kwa moja mkosoaji anamamlaka ya kumuita JIZI, au kama kafanya mauaji au karuhusu mauaji basi mkosoaji atamuita kiongozi huyo ni MUUAJI.
Halikadhalika na Baba, Mzee ukitaka uheshimiwe basi jiheshimu. Ukifanya upumbavu basi itaitwa majina yanayostahili Matendo yako.

Hayo mengine ya kustahi ubaya ni unafiki na ushetani
 
kama nimekuelewa vizuri taikun ni kwamba ushauri bora ni wa kwako mwenyewe as long as uko timamu ushauri mwingine unakuwa una confirmation tu which means unaweza kuukubali au kuukataa depending on ushauri wenyewe!

Hivyo ndivyo ilivyo.
Ukikuamini mtu mpaka ukaomba ushauri kwake, kisha akakushauri, ukafanya. Kama amekudandanganya, kosa ni lako.
 
Ma Rais dunia nzima wanategemea ushauri....hakunaga kitu kama Rais mwenye akili...na Rais asie na akili..

Akili ya ma Rais wote hutegemea advisors ndo maana wenzetu wameenda mbali Sana na kuweka washauri rasmi wa Rais Kwa kila kitu...kuanzia siasa Hadi Uchumi...washauri wanatangazwa wanajulikana na CV zao zimeshiba

Wamarekani wameenda mbali zaidi
Mfano kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Rais. Halafu kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Makamu wa Rais ...halafu kuna waziri WA fedha na yeye ana mshauri wa uchumi anaelipwa wa waziri WA fedha...bado kuna washauri Tele wa wizara wanalipwa, the list goes on..


So Kwa Wamarekani likija suala la uchumi mezani Kwa Rais ...unakuta kuna PhD kama 10 hivi zimechangia Hilo wazo.....na mapendekezo.

You are only smart if you surround yourself with people who are more smarter than you
Swali ni hili: Umewahi kumsikia mtu kule Marekani anamwambia Rais anashauriwa vibaya? Ni hapa tu kwa unafiki watu husema ati Rais anashauriwa vibaya. Kule nchi ikienda vibaya moja kwa moja Rais anaambiwa ndiyo mwenye makosa. Au hujamwelewa mleta mda? Rais hata akiwa na advisors akiwa kichwa kitupu kama huyu mama obvious hata washauri wakimshauri ataishia STUPID tu
 
Back
Top Bottom