Kusema ukweli Comedy ni sehemu ya kazi ya Wasemaji wa Kisasa

Kusema ukweli Comedy ni sehemu ya kazi ya Wasemaji wa Kisasa

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
1,016
Reaction score
2,195
Tunapitia wakati mgumu wa kuchunga kauli zetu tunapozungumza na media au tunapokuwa kwenye majukumu yetu.

Binafsi naendelea kuitafakari kauli ya CEO Kasongo kutupiga marufuku wasemaji kufanya mzaha kwenye statements rasmi za klabu. Ni kweli kuna kundi la watu hatuwatendei haki kwa kufanyia mzaha taarifa za timu zao wanazozishabikia. Lakini tukiwa serious sana mpira utaboa. Mpira ni mchezo wa kutambiana. Tambo zina raha yake.

Utani na vijembe ni culture ya mpira wetu iliyoasisiwa na Simba na Yanga. Pengine culture hii ndio inanogesha soka letu. Kwa mfano nakumbuka nilipokuwa serious sana nikaambiwa nimepooza nichangamke kidogo. Nimechangamka mambo yanaenda. CEO wa Bodi ya Ligi hataki!

Nadhani hili linahitaji mjadala zaidi au wakubwa waache tu culture iamue!
 
Sisi tunataka matokeo uwanjani.
Comedy au porojo za wasemaji kama haziendani na kinachooneshwa uwanjani, hayo yote ni ulaghai na kuwahadaa tu washabiki na wapenzi wa soka
 
Uko sahihi msemaji na ili jambo ndio uvutia ata wasiopenda soka kuanza kuzishabikia timu ,ivo kwa namna moja ama nyingine uongeza mashabiki Kwa kiasi chake. Shida nayoona tu tambo ama utani unazidishwa sana na kuwa chuki kitu ambacho mimi binafsi ndio nakipinga.
 
Sisi tunataka matokeo uwanjani.
Comedy au porojo za wasemaji kama haziendani na kinachooneshwa uwanjani, hayo yote ni ulaghai na kuwahadaa tu washabiki na wapenzi wa soka

Mpira una matokeo ya kikatili sometimes lazima tufariji watu wetu
 
Uko sahihi msemaji na ili jambo ndio uvutia ata wasiopenda soka kuanza kuzishabikia timu ,ivo kwa namna moja ama nyingine uongeza mashabiki Kwa kiasi chake. Shida nayoona tu tambo ama utani unazidishwa sana na kuwa chuki kitu ambacho mimi binafsi ndio nakipinga.

Naam. Kila kitu kwa kiasi.
 
Naam. Kila kitu kwa kiasi.
Sema msemaji, nawapongeza kwa kufanya usajiri mzuri kwa gharama kubwa sana kwailo nawapongeza lakini naomba mjaribu kukarabati uwanja wenu aseeh yani kiukweli ule uwanja haufahi kwa hadhi yenu ya sasa,Tuweke kila kitu pembeni ila suala la uwanja mmeniangusha sana nahakika viongozi na wadhamini wa Team hawashindwi kugeuza uwanja toka hali ile mbaya mpaka uwanja mzuri. Tuige mfano kwa Namungo SC klabu ya hadhi yenu na sio lopolopo za Kariakoo pale . Nawasilisha kama mpenda maendeleo ya soka nchini.
 
Sema msemaji, nawapongeza kwa kufanya usajiri mzuri kwa gharama kubwa sana kwailo nawapongeza lakini naomba mjaribu kukarabati uwanja wenu aseeh yani kiukweli ule uwanja haufahi kwa hadhi yenu ya sasa,Tuweke kila kitu pembeni ila suala la uwanja mmeniangusha sana nahakika viongozi na wadhamini wa Team hawashindwi kugeuza uwanja toka hali ile mbaya mpaka uwanja mzuri. Tuige mfano kwa Namungo SC klabu ya hadhi yenu na sio lopolopo za Kariakoo pale . Nawasilisha kama mpenda maendeleo ya soka nchini.

Asante kwa pongezi. Uwanja tunaoutumia sasa sio wetu ni mali ya CCM. Sisi ni wapangaji tu.

Habari njema ni kwamba tupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa uwanja wetu wa kisasa ambao haupishani sana na Azam Complex. Ujenzi umefikia 75%
 
Tunapitia wakati mgumu wa kuchunga kauli zetu tunapozungumza na media au tunapokuwa kwenye majukumu yetu.

Binafsi naendelea kuitafakari kauli ya CEO Kasongo kutupiga marufuku wasemaji kufanya mzaha kwenye statements rasmi za klabu. Ni kweli kuna kundi la watu hatuwatendei haki kwa kufanyia mzaha taarifa za timu zao wanazozishabikia. Lakini tukiwa serious sana mpira utaboa. Mpira ni mchezo wa kutambiana. Tambo zina raha yake.

Utani na vijembe ni culture ya mpira wetu iliyoasisiwa na Simba na Yanga. Pengine culture hii ndio inanogesha soka letu. Kwa mfano nakumbuka nilipokuwa serious sana nikaambiwa nimepooza nichangamke kidogo. Nimechangamka mambo yanaenda. CEO wa Bodi ya Ligi hataki!

Nadhani hili linahitaji mjadala zaidi au wakubwa waache tu culture iamue!
Wewe ni msemaji wa timu gani?
 
Asante kwa pongezi. Uwanja tunaoutumia sasa sio wetu ni mali ya CCM. Sisi ni wapangaji tu.

Habari njema ni kwamba tupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa uwanja wetu wa kisasa ambao haupishani sana na Azam Complex. Ujenzi umefikia 75%
Tupe picha na tueleze uko eneo gani ili tujiridhishe unayosema.
 
Sisi tunataka matokeo uwanjani.
Comedy au porojo za wasemaji kama haziendani na kinachooneshwa uwanjani, hayo yote ni ulaghai na kuwahadaa tu washabiki na wapenzi wa soka
Umenikumbusha 'big result now', hivi iliishajei ile
 
  • Thanks
Reactions: K11
Back
Top Bottom