Kusherehekea siku ya kuzaliwa hali ya kuwa wananchi wanateseka na umasikini

Kusherehekea siku ya kuzaliwa hali ya kuwa wananchi wanateseka na umasikini

Wakuu nisipende kuwachosha
Ila inasikitisha sana kuona ikulu ambapo Nyerere aliwahi kusema kuwa ni mahala patakatifu imebadilika na kuwa pango la walanguzi.

Leo ikulu hapafanyiki tena mikutano ya kujadili mikataba ya madini,utiaji saini miradi ya maendeleo n.k Bali imekuwa sehemu ya kufanya karamu kuonana na viongozi wastaafu kupongezana n.k

Kiongozi mkuu wa nchi amekuwa mwepesi kuhudhuri shughuli nyepesi nyepesi zisizokuwa na tija kubwa kwa taifa huku akiacha hoja za msingi na miradi ya msingi ya kimaendeleo

Kiongozi mkuu wa nchi amebaki kufanya makongamano,teuzi,birthday party n.k huku akisahau Luna miradi ya kimkakati kama JNHP, SGR pia anapaswa kubrinstorm kuja na miradi mingi ili uchumi ukue watanzania waondokane na umasikini

Wakuu nina mengi moyoni ila hasira zimenikaba kwenye koo mpaka nashindwa kuendelea. Naomba niishie hapa kwa Leo . View attachment 2097413View attachment 2097414
We hater...lazima utambue kila jambo lina nafasi yake na muda wake.

Hayo ya kusimamia miradi ya kiuchumi ni majukumu ya serikali yake na wapo watendaji wa kushughulika hilo, hata birthday ni haki yake kusherehekea maana hata yeye ni binadamu kama kwako haina umuhimu hilo ni juu yake.

Kila jambo lina muda wake, umuhimu wake na wakati sahihi wa kufanya usichanganye majukumu ya lazima ya Rais (taasisi) na majukumu yake ya kila siku kama binadamu wa kawaida (ikiwemo kusherehekea birthday party).
 
Hii inaitwa roho ya kwanini, sio kitu kizuri!. Mtu amelitumikia taifa kwa siku 364, hiyo siku moja tuu ya 365 ndio inakuuma?.

Tena sisi Tanzania tuna bahati, siku ya birthday ya mkuu wa nchi ni siku ya kawaida, wenzetu ikiwemo Uingereza, Birthday ya Queen ni public holiday!. Na sio UK pekee, ni Great Britain yote, na kwenye dominion zake site, Canada, Australia na Newsland.

Siku hiyo balozi zote za Uingereza dunia nzima zinaiadhimisha kwa tafrija mchapalo.

Nami nijiunge na Watanzania wenzangu kumtakia Happy Birthday President Mama Samia Suluhu Hassan.
P
Hizo nchi ulizotaja kama mifano labda utujuze na chumi zao + changamoto nyingine za uchumi kwa watu wake wa chini zikoje labda.
 
Kama ulikuwa unaniheshimu, then ulikuwa na sababu. Kama heshima hiyo sasa umeiondoa tuu kwasababu tuu mimi nimeunga mkono birthday ya Mama Samia!, then asante sana kwa heshima yako, nasikitika sana, nitamiss heshima yako nitaathirika sana kuikosa heshima yako. Sina jinsi asante.
P
Brother P, huwa natamani sana TABIA yako ya kutojali, hata utolewapo maneno makali!
 
Hii inaitwa roho ya kwanini, sio kitu kizuri!. Mtu amelitumikia taifa kwa siku 364, hiyo siku moja tuu ya 365 ndio inakuuma?.

Tena sisi Tanzania tuna bahati, siku ya birthday ya mkuu wa nchi ni siku ya kawaida, wenzetu ikiwemo Uingereza, Birthday ya Queen ni public holiday!. Na sio UK pekee, ni Great Britain yote, na kwenye dominion zake site, Canada, Australia na Newsland.

Siku hiyo balozi zote za Uingereza dunia nzima zinaiadhimisha kwa tafrija mchapalo.

Nami nijiunge na Watanzania wenzangu kumtakia Happy Birthday President Mama Samia Suluhu Hassan.
P
Queen (Monarchy) huo ni utamaduni wa Kifalme na wanaenzi culture yao...., Mtendaji ni Prime Minister, Queen ni just symbolically (Na ni hapo juzi tu Bwana Boris kaingia kwenye misukosuko kwa mambo ambayo huenda ungeweza kuyaona kwamba ni petty)

Kumuelewa mleta uzi sio kwamba mtu asisherekee, hata akiamua kusherekea mwaka mzima its okay so long as (he / she is eating matunda yake)..., ila mpaka mleta uzi kalalamika inaonekana anaona kile alichotumwa huyu mwajiliwa wetu hajakitekeleza kwahio kuonekana anakula Bata huenda ni Kejeli fulani (thus kama ningekuwa mshauri wake ningemwambia hizo Bata ale kwa siri) Yaani ajue kula na vipofu.....
 
Hizo nchi ulizotaja kama mifano labda utujuze na chumi zao + changamoto nyingine za uchumi kwa watu wake wa chini zikoje labda.
No matter how bad ones economic situation is, hakuna ubaya wowote mtu kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa with whatever s/he has, hata kama hana kitu, just a glass of water is enough. Na akiwa hana hayo maji, then hata kuambiwa tuu happy birthday is just enough.
Hata akikosa chakula anakula hewa kama wafanyavyo breatharians .
P
 
Nipo Shinyanga. Mwishoni mwa Novemba mwaka jana, nilinunua mtungi wa gesi wa kilo 30 kwa 54,000/=. Leo, nashangaa naambiwa 59,000/=.
Upandaji wa vitu, sisikii Serikali ikikemea!
Gesi ni biashara binafsi kama huwezi kununua pikia kuni.
 
Wakuu nisipende kuwachosha
Ila inasikitisha sana kuona ikulu ambapo Nyerere aliwahi kusema kuwa ni mahala patakatifu imebadilika na kuwa pango la walanguzi.

Leo ikulu hapafanyiki tena mikutano ya kujadili mikataba ya madini,utiaji saini miradi ya maendeleo n.k Bali imekuwa sehemu ya kufanya karamu kuonana na viongozi wastaafu kupongezana n.k

Kiongozi mkuu wa nchi amekuwa mwepesi kuhudhuri shughuli nyepesi nyepesi zisizokuwa na tija kubwa kwa taifa huku akiacha hoja za msingi na miradi ya msingi ya kimaendeleo

Kiongozi mkuu wa nchi amebaki kufanya makongamano,teuzi,birthday party n.k huku akisahau kuna miradi ya kimkakati kama JNHP, SGR pia anapaswa kubrainnstorm kuja na miradi mingi ili uchumi ukue watanzania waondokane na umasikini unaowatesa miaka nenda rudi.Sijakataa mtu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku moja kati ya 365 lakini vipi masikini wanaoteseka siku zote 365 huku yule waliyemtuma wakitegemea atawaondolea umasikini akiponda raha (kiujumla maisha ya Rais kwa mshahara wake ni bonus tosha kwa siku zote 365 ukilinganisha na watanzania wengi ) lakini bado pia kabla hajatimiza azma za waliomtuma tayari anafanya karamu tena hali ya kuwa wale waliomtuma hawakumbuki hata siku zao za kuzaliwa kwa tabu na masumbuko ya umasikini wanaoupitia!

Wakuu nina mengi moyoni ila hasira zimenikaba kwenye koo mpaka nashindwa kuendelea. Naomba niishie hapa kwa Leo . View attachment 2097413View attachment 2097414
Lini walikuwa matajiri? Je sherehe zilikuwa hazifanyiki? Rais ndio huwa anatafutia watu maisha mazuri?
 
Kawaida tu mkuu.....mwache afurahie hii siku muhimu kwake.....nna chojua hakuna kiongoz anayeweza kumaliza matatizo yote



Hiv legendary MAGU alikuwa anasherekea hivi vitu

Binafsi sjawahi kusikia bday yake
Manyang"au yote duniani huwa yanafanya sherehe za kunywa damu za watu na hufanya Kwa Siri sana.
 
Wakuu nisipende kuwachosha
Ila inasikitisha sana kuona ikulu ambapo Nyerere aliwahi kusema kuwa ni mahala patakatifu imebadilika na kuwa pango la walanguzi.

Leo ikulu hapafanyiki tena mikutano ya kujadili mikataba ya madini,utiaji saini miradi ya maendeleo n.k Bali imekuwa sehemu ya kufanya karamu kuonana na viongozi wastaafu kupongezana n.k

Kiongozi mkuu wa nchi amekuwa mwepesi kuhudhuri shughuli nyepesi nyepesi zisizokuwa na tija kubwa kwa taifa huku akiacha hoja za msingi na miradi ya msingi ya kimaendeleo

Kiongozi mkuu wa nchi amebaki kufanya makongamano,teuzi,birthday party n.k huku akisahau kuna miradi ya kimkakati kama JNHP, SGR pia anapaswa kubrainnstorm kuja na miradi mingi ili uchumi ukue watanzania waondokane na umasikini unaowatesa miaka nenda rudi.Sijakataa mtu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku moja kati ya 365 lakini vipi masikini wanaoteseka siku zote 365 huku yule waliyemtuma wakitegemea atawaondolea umasikini akiponda raha (kiujumla maisha ya Rais kwa mshahara wake ni bonus tosha kwa siku zote 365 ukilinganisha na watanzania wengi ) lakini bado pia kabla hajatimiza azma za waliomtuma tayari anafanya karamu tena hali ya kuwa wale waliomtuma hawakumbuki hata siku zao za kuzaliwa kwa tabu na masumbuko ya umasikini wanaoupitia!

Wakuu nina mengi moyoni ila hasira zimenikaba kwenye koo mpaka nashindwa kuendelea. Naomba niishie hapa kwa Leo . View attachment 2097413View attachment 2097414
Aseeeh! Kwani kila kitu lazima mkiseme vbaya tu
Rais ata asipokuwa na hiyo party unafikri wewe itakuongezea nini kwa mfuko wako,,majungu lawama malalamiko haya kila Siku ya nini,shida haziwezi isha kamwe ata wewe mleta Uzi upewe nchi hii...

Tufanye Kazi tu Dudes...Rais hawezi kuja kwako kukupa hela ...Au huwa mnaandika kujifurahisha Jf....
 
Kama ulikuwa unaniheshimu, then ulikuwa na sababu. Kama heshima hiyo sasa umeiondoa tuu kwasababu tuu mimi nimeunga mkono birthday ya Mama Samia!, then asante sana kwa heshima yako, nasikitika sana, nitamiss heshima yako nitaathirika sana kuikosa heshima yako. Sina jinsi asante.
P
Hapa issue sio birthday ya mama,hapa ni kwann asherehekee Ikulu? Kumbuka Ile ni Ofisi/Ikulu ya taifa,na sio sehemu ya mtu binafsi. Pascal Mayalla Acha kujipendekeza kaka,ww kama mwandishi ni mwandishi wa waheshima Sana,unapaswa kukemea hili swala Kwa kalamu. Huu no mfano mbaya Sana Rais anaonesha,tuendako tutaanza kuwa na viongizi wanaoenda kunywa chai London na Lunch Dubai huku wananchi wakiteseka.
 
Back
Top Bottom