Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,415
- 119,473
Habari ya weekend wana Jf,.
Waswahili huwa tuna msemo mmoja eti 'ukweli unauma'... Kwamba ukiongea jambo ukaona mhusika amekasirika basi hilo jambo ni la kweli. Mimi nakataa jamani jambo la kusingiziwa linauma sana, mimi binafsi mtu akikomaa kuning'ang'aniza nimefanya kitu ambacho sijafanya naweza kumchapa makofi na kama ni mtu ambae siwezi kumpiga wala kugombezana nae huwa najikuta nalia tu.
Mimi binafsi katika kukua kwangu nimesingiziwa mengi sana ila yapo mengine hadi leo hayafutiki. Nikiwa darasa la saba kuna mtu alipeleka taarifa kwa walimu kwamba natoka na wakaka fulani hivi wawili (msishangae enzi zetu tulikuwa tunamaliza la saba tukiwa wakubwa sio kama siku hizi watoto form three ndo anavunja ungo). Ni stori ndefu ilikuwa ila habari ilikuwa ndio hiyo, tulitajwa wengi tuliokuwa tunatuhumiwa kujihusisha na mapenzi tukaitwa kwa mwalimu mkuu akawa anatupatia nasaha eti 'kuweni makini siku hizi magonjwa mengi ikibidi basi mtumie kondom' lahaulaa mimi hakuna siku nililia kama siku ile nilijiapiza aliyefanya hivyo lazima nimkomeshe japo mwisho wa siku sikumfanya chochote. Ninachomshukuru Mungu mzazi wangu alinielewa na hakuwa na nongwa na hiyo ilitosha sana kunipa amani. Cha ajabu yule mwendawazimu baada ya kuingia sekondari form one tu kafukuzwa shule kwa kashfa ileile aliyonizushia mimi nikasema malipo hapahapa duniani pambaf.
Jambo lingine ninalokumbuka nikiwa form four kuna mtu alimpelekea maneno rafiki yangu wa karibu kuwa mimi nilikaa nilisema eti yeye anatembea na mkaka mwenye UKIMWI, Nilishangaa tu yule rafiki yangu anajiweka mbali na mimi hanichangamkii wako busy tu na rafiki yetu mwingine, siku anakuja kuniambia hayo nilishangaa sana maana kwanza sikuwahi kusema, pili sinaga tabia ya kumsema mtu wangu yeyote wa karibu iwe rafiki,ndugu,mpenzi or whatever kwa watu baki, lakini baadae nilikuja kuhisi labda ametunga tu mwenyewe kwa lengo la kukata urafiki.
Lingine nikiwa mdogo kuna dada yangu mmoja alinisingizia nimemuibia mia yake aliweka mezani na mimi ni mtu pekee nilikuwepo humo ndani, alinikomalia kuwa nimeichukua akaanza kunipiga kadri ninavyokataa sijachukua ndivyo kipigo kinazidi, baadae nilipoona kipigo kimenielemea ikabidi nikubali kuwa nilichukua ila mimi pia nimeipoteza nilikokuwa ninacheza ndio kuniacha. Kesho yake asubuhi akiwa anapiga deki akaiona uvunguni mwa kitanda. Akaniita tena nikasema si unaona, mimi sikuchukua akataka kunishushia tena kipigo kwa kuogopa kipigo na fimbo za jana yake hata hazijapona nikasema niliidondosha mwenyewe baada ya kuchukua sikujua imedondokea hapo. Hili tukio huwa linaniumiza na kila nikikumbuka machozi yanadondoka ila nimepanga ipo siku nitamkumbusha mhusika najua ye kasahau.
Kama umewahi kusingiziwa tupatie kisa na wengine wajifunze.
Waswahili huwa tuna msemo mmoja eti 'ukweli unauma'... Kwamba ukiongea jambo ukaona mhusika amekasirika basi hilo jambo ni la kweli. Mimi nakataa jamani jambo la kusingiziwa linauma sana, mimi binafsi mtu akikomaa kuning'ang'aniza nimefanya kitu ambacho sijafanya naweza kumchapa makofi na kama ni mtu ambae siwezi kumpiga wala kugombezana nae huwa najikuta nalia tu.
Mimi binafsi katika kukua kwangu nimesingiziwa mengi sana ila yapo mengine hadi leo hayafutiki. Nikiwa darasa la saba kuna mtu alipeleka taarifa kwa walimu kwamba natoka na wakaka fulani hivi wawili (msishangae enzi zetu tulikuwa tunamaliza la saba tukiwa wakubwa sio kama siku hizi watoto form three ndo anavunja ungo). Ni stori ndefu ilikuwa ila habari ilikuwa ndio hiyo, tulitajwa wengi tuliokuwa tunatuhumiwa kujihusisha na mapenzi tukaitwa kwa mwalimu mkuu akawa anatupatia nasaha eti 'kuweni makini siku hizi magonjwa mengi ikibidi basi mtumie kondom' lahaulaa mimi hakuna siku nililia kama siku ile nilijiapiza aliyefanya hivyo lazima nimkomeshe japo mwisho wa siku sikumfanya chochote. Ninachomshukuru Mungu mzazi wangu alinielewa na hakuwa na nongwa na hiyo ilitosha sana kunipa amani. Cha ajabu yule mwendawazimu baada ya kuingia sekondari form one tu kafukuzwa shule kwa kashfa ileile aliyonizushia mimi nikasema malipo hapahapa duniani pambaf.
Jambo lingine ninalokumbuka nikiwa form four kuna mtu alimpelekea maneno rafiki yangu wa karibu kuwa mimi nilikaa nilisema eti yeye anatembea na mkaka mwenye UKIMWI, Nilishangaa tu yule rafiki yangu anajiweka mbali na mimi hanichangamkii wako busy tu na rafiki yetu mwingine, siku anakuja kuniambia hayo nilishangaa sana maana kwanza sikuwahi kusema, pili sinaga tabia ya kumsema mtu wangu yeyote wa karibu iwe rafiki,ndugu,mpenzi or whatever kwa watu baki, lakini baadae nilikuja kuhisi labda ametunga tu mwenyewe kwa lengo la kukata urafiki.
Lingine nikiwa mdogo kuna dada yangu mmoja alinisingizia nimemuibia mia yake aliweka mezani na mimi ni mtu pekee nilikuwepo humo ndani, alinikomalia kuwa nimeichukua akaanza kunipiga kadri ninavyokataa sijachukua ndivyo kipigo kinazidi, baadae nilipoona kipigo kimenielemea ikabidi nikubali kuwa nilichukua ila mimi pia nimeipoteza nilikokuwa ninacheza ndio kuniacha. Kesho yake asubuhi akiwa anapiga deki akaiona uvunguni mwa kitanda. Akaniita tena nikasema si unaona, mimi sikuchukua akataka kunishushia tena kipigo kwa kuogopa kipigo na fimbo za jana yake hata hazijapona nikasema niliidondosha mwenyewe baada ya kuchukua sikujua imedondokea hapo. Hili tukio huwa linaniumiza na kila nikikumbuka machozi yanadondoka ila nimepanga ipo siku nitamkumbusha mhusika najua ye kasahau.
Kama umewahi kusingiziwa tupatie kisa na wengine wajifunze.