Uchaguzi 2020 Kusipokuwa na uchaguzi wa kuchagua Rais kuna haja ya kufanya uchaguzi?

Uchaguzi 2020 Kusipokuwa na uchaguzi wa kuchagua Rais kuna haja ya kufanya uchaguzi?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Wana CCM wengi sana wanatamani kwa mtizamo wao ghushi na uliojaa ugoto katika kufikiri, kuwa John Magufuli asipingwe na mgombea toka CHADEMA. Wao wanadai kwa aliyoyafanya Magufuli kama Rais wa Tanzania hakuna haja ya kupingwa.

Lakini najiuliza kama Magufuli wanataka apite bila ya kupingwa, je kutakuwa na haja ya kufanya uchaguzi kuwachagua wabunge na madiwani? Kama kuna ulazima wa kuwepo kwa uchaguzi huo kigezo kitakuwa ni nini? Je, Madiwani na Wabunge hakuna cha kutukuka walichofanya kuwafanya wasipingwe kwenye uchaguzi ujao?

Na kama itakuwa na wabunge na madiwani nao wasipingwe kigezo kitakuwa ni nini na je na wabunge na madiwani toka vyama vingine mbali na CCM nao hawatapingwa?
 
Sasa kama Dr Magufuli atashindanishwa na mchungaji Msigwa wa Chadema hiyo ni sawa na kupita bila kupingwa.....kwanini tuwapangishe watu foleni ya kupiga kura?

Uchaguzi wa wabunge lazima uwepo kwa sababu hata wabunge wa CCM wengi hawajafanya vizuri majimboni!
 
Nimeipenda hii para -

Lakini najiuliza kama Magufuli wanataka apite bila ya kupingwa, je kutakuwa na haja ya kufanya uchaguzi kuwachagua wabunge na madiwani? Kama kuna ulazima wa kuwepo kwa uchaguzi huo kigezo kitakuwa ni nini? Je, Madiwani na wabunge hakuna cha kutukuka walichofanya kuwafanya wasipingwe kwenye uchaguzi ujao?
 
Sasa kama Dr Magufuli atashindanishwa na mchungaji Msigwa wa Chadema hiyo ni sawa na kupita bila kupingwa.....kwanini tuwapangishe watu foleni ya kupiga kura?

Uchaguzi wa wabunge lazima uwepo kwa sababu hata wabunge wa CCM wengi hawajafanya vizuri majimboni!
Kwanza kipimo cha "Kufanya vizuri" kwa Magufuli anacho nani. Lakini pia hata kama Mchungaji Msigwa atapata kura mbili, haki ya hao watu wawili wanaotaka kumpigia Msigwa kura inaondolewa kwa misingi ipi?

Tuwaze huku tukitanguliza mbele mantiki na kuweka pembeni utashi wetu unaoendekeza mapenzi ya kijinga kwa siasa za nchi yetu.
 
Kwanza kipimo cha "Kufanya vizuri" kwa Magufuli anacho nani. Lakini pia hata kama Mchungaji Msigwa atapata kura mbili, haki ya hao watu wawili wanaotaka kumpigia Msigwa kura inaondolewa kwa misingi ipi?

Tuwaze huku tukitanguliza mbele mantiki na kuweka pembeni utashi wetu unaoendekeza mapenzi ya kijinga kwa siasa za nchi yetu.
Mchungaji Msigwa kihesa pamemshinda ndio apewe nchi..... Tusiwachoshe wapiga kura jamani!
 
Wananchi wakiamua apite bila kupingwa atapita na NEC itamtangaza hakuna wa kumzuia.

Hadi sasa vyama vya siasa vinne vimeshamuunga mkono!
Hao "wananchi" wanaamua kupitia utaratibu upi? Na kuna tofauti gani kati ya wananchi na vyama vya siasa maana naona kama umetenganisha. Jee CHADEMA siyo chama cha siasa na hakina wananch ndani mwake?
 
Hao "wananchi" wanaamua kupitia utaratibu upi? Na kuna tofauti gani kati ya wananchi na vyama vya siasa maana naona kama umetenganisha. Jee CHADEMA siyo chama cha siasa na hakina wananch ndani mwake?
Chadema ilishaamua muda mrefu kumuunga mkono Rais Magufuli na imetoa mawaziri wawili kwenye serikali Mwita Waitara na Dr Mollel.

Vyama vya siasa ndio wananchi kwa sababu katiba yetu hairuhusu mgombea binafsi!
 
Anayetuumiza kichwa ni wakili msomi Hashimu Spunta Rungwe wa Chaumma pekee...... Hawa akina Chadema, ACT wazalendo, Cuf, Nccr nk kazi tulishamaliza kitambo!
Kuna Yule ambae akifungua mdomo lazima mvae pamper kuzuia visivyotakiwa kutoka muda huo.
 
Back
Top Bottom