Mackanackyyy
JF-Expert Member
- Mar 26, 2019
- 2,338
- 5,271
Una uelewa wowote kweli kwenye investments za namna hiyo au ni akili matope tu zimekujaa kichwani? Kama kitu hukielewi heri kukaa kimya maana kukaa kimya pia ni hekima!Magufuli ni mzalendo wa kweli Hawezi kubali mkataba wa kuikabidhi bandari yetu kwa nchi nyingine kwa miaka 100. Kama huo mkataba utakuwa bila kipengele cha wajenzi (funders) kuiendesha bandari kwa miaka mia JPM anaweza kuufikiria upya lakini siyo huu wa kinyonyaji Kabisa. Jamani kina Zito muwe na mshipa wa aibu. Siyo kila kitu kupinga tu!
Waimba kwaya hata kukusoma hawataki, hilo ndilo tatizo kubwa sana nchi yetu ililonalo sasa hivi.Pesa yote hiyo inatolewa na mwekezaji kwa 100%. Tulitakiwa tujadiliane namna ya uendeshaji ya kuwa labda kwa usalama kuwepo na local content ambapo tutaweza kuweka watu wetu kwa ajili ya usalama wa nchi. Na pia Je uendeshaji wake utakuwa wa muda gani kabla ya ku transfer? Kwa ujumla faida ni kubwa kuliko kutokuwa na huo mradi (Kuna multiplying effect kubwa kiuchumi na kijamii in the long run). Kuna haja ya kushirikiana kwenye majadiliano kama taifa bila kujali vyama.
Hongo kama "u-Profesa"?Naona mheshimiwa Zitto hawajui vizuri wachina ila sijajua kama anafanya makusudi kwa ajili ya kujiimarisha kisiasa au wachina walishafanya yao tayari. Kwa kumsaidia tu angeangalia kwanza mkataba mdogo tu wa Star times walioingia wachina na TBC aone jinsi hawa viumbe walivyo hatari ndio sasa aje atoe ushauri kuhusu huu mkataba wa ujenzi wa bandari Bagamoyo kama utakuwa na manufaa. Mchina akikupa milioni moja ujue yeye anategemea kupata zaidi ya bilioni moja hawa viumbe ni hatari sana kwa ustawi wa Taifa letu. Wako tayari kutoa hongo kwa gharama yoyote kwa wanasiasa ili mradi tu wafanikishe wanachokitaka, ndiyo maana sishangai kuona wanapata watetezi wa huo mradi.
Huu mradi ungebaki kwenye makaratasi tu as utekelezaji wa mradi wa Trilion 23 kwa usawa huu wa kuchangishana buku buku hautekelezeki Kwa sasa!
ZZK usisahau kuwa jimboni kwako maji tu yanayohitaji bajeti chini ya 20 B yameshindikana kupatikana! Then unatetea 23Trilion ziende Bagamoyo?
Nyinyi ndio wale watz wachache mnaotegemea akili za mtu kuishi.
Yaani kila mtu unataka akubaliane na huyo zitto, kwanini una imani naye kiasi hicho!!!
Kwenye hili swala mnaonyesha upumbavu kiwango sana bila kusita.
hapo Lumumba mnatumia bange kufikri
Huyu ndie aliyekuwa waziri kivuli was fedha alyeshindwa kutengeneza bajeti mbadala tuna bandari Dar es Salaam, Mtwara na Tanga badala ya kuimarisha bandari ya Mtwara ili ihudumie nchi za Zambia, Malawi na Congo na kupanua bandari ya Dar es Salaam tunataka kujenga bandari mpya kwa huu uamuzi naipongeza serikali kwani imekuwa sikivu
Kusoma na kuandika inawatosha!!!
Hata koroshow aliwaonya huyohuyo...
Acheni kufananisha chura na kambale...
Kuna mtu anataka kuwafanya watz wajinga na serikali yote, ila yeye tu ndiye anafikiri sawa sawa.Waambie hayo masharti magumu watu watoe maoni yao, waambie ukweli mda wa wachina katika uwekezaji wa huo mradi ni mpaka miaka 99, tena ukiwa na conditions za kukataza bandari zingine kuendelezwa. Wape na mifano ya miradi kama hii iliyofanyika nchini Eritrea na baadhi ya nchi za Asia ni jinsi gani walifaidika?? Weka wazi masharti hayo ya mikataba..
Wachina wa leo ni hatari kuliko hata mabepari wa kizungu, ukiona mpaka trump anawawekea vikwazo kwa kupandisha kodi kwenye bidhaa zao ujue kuna kitu, hakuna sehemu ambayo serikali inapata pesa nyingi kama bandarini, ikijengwa bandari ya b moyo automatically utaua bandari ya dar. Yaani utacha mapato ya uhakika utaenda kuchukua kodi kwenye biashara ambayo mpaka ipate faida ndo walipe kodi.
Hakuna asiyejua makampuni makubwa yanavojua kucheza na mahesabu kukwepa kodi, kwenye hili naipongeza serikali. Hakuna haja ya haraka kwenye mradi huu. Wasomi wauchambue, usalama wa taifa wauchambue, wabunge na wadau waupitie.... then serikal ifanye maamuz
Huu mradi ungebaki kwenye makaratasi tu as utekelezaji wa mradi wa Trilion 23 kwa usawa huu wa kuchangishana buku buku hautekelezeki Kwa sasa!
ZZK usisahau kuwa jimboni kwako maji tu yanayohitaji bajeti chini ya 20 B yameshindikana kupatikana! Then unatetea 23Trilion ziende Bagamoyo?