Kusitishwa Mradi wa Bagamoyo SEZ kumedhihirisha udhaifu wa Rais Magufuli kwenye Uchumi na Diplomasia

Kusitishwa Mradi wa Bagamoyo SEZ kumedhihirisha udhaifu wa Rais Magufuli kwenye Uchumi na Diplomasia

Financer wa mradi 100% ndio hafai.

Umesoma uchumi wapi nyumbu wewe!!!

Maana yake hiyo bandari ni mali ya hao wachina 100%, unajua madhara yake, au mauno tu kama kawaida yenu!!
Migodi yote ya dhahabu imewekezwa na wageni kwa 100% na wanatulipa mrabaha kiduchu. Mwekezaji wa SEZ ana wekeza naye kwa 100% na faida zake (Multiplier effect) yaweza kuwa kubwa kuliko migodi ambayo imewekezwa kwa mitaji ya wageni 100%.

Tunapaswa kujadili bila jazba kwa hoja kama kuna faida au la. Bandari zetu za kikoloni zimebanwa sana na hazitoi nafasi nzuri ya kuboresha (modernization), hivyo mradi huu unaonekana ungetupatia bandari nzuri ya kiushindani kwa ukanda wa Afrika. Lazima tuamue kiuchumi, kuwa na uwekezaji huo na kutokuwa nao kabisa ni maamuzi gani yenye faida?
 
So sad kwamba pamoja na uchambuzi wa kina uliofanywa kwenye uzi huu hujaelewa chochote, na bado umefanya kosa lile lile la kudhani huo mradi ni bandari tuu. Kwa nini hamsomi mada mkaelewa kwanza? Mnajidhalilisha sanaa...

Mkuu hilo ndio Tanzania mojawapo kwa sasa hapa Tanzania, Propaganda imekuwa ni sehemu ya maisha kwa sababu wahusika wanajua watanzania waliowengi ni wavivu na sio waelewa wa kufuatilia mambo..

Huyo jamaa uliyemjibu inaonekana hata hizo content hakuzisoma na kuona faida kubwa ya huo mradi ila kakimbilia kwenye propaganda, hatari sana.
 
Kumbe unafahamu si za serikali, haya unajua zitarudishwaje!!! Baada ya muda gani!!!
Ni swali la msingi ambalo si yeye tu hajui jibu Ila hata wewe inawezekana hujui majibu na hujapima matokeo. Unatakiwa uwe na majibu halafu ndipo uone kama ni muhimu kuendelea nao au ni pasua kichwa. Kama umesoma makala kuna sehemu inasema kama masharti ni magumu tusiweke mpira kwapani bali tuendeleze mazungumzo maana hawa ni marafiki zetu wa mda. Mpaka sasa sioni kosa la makala labda kama kosa liwe ni makala ya nani?
 
Na Mwamba wa Kaskazini, Ngarenaro, Tanzania
WIKI hii wakati ndugu zetu waislamu wakiwa katika tafakuri kuu ya Mfungo wa Ramadhani, kwa sisi Wakatoliki Tafakuri ya Pasaka ilishapita. Hata hivyo nimekuwa katika tafakuri binafsi juu ya hoja ya Katibu Mkuu wa CCM, kamaradi Dkt. Bashiru Ally, kuhusu umuhimu wa vijana kuandaliwa leo ili kuwa viongozi wazuri wa baadaye.

Nikiwa katikati ya tafakuri hiyo, napokea taarifa njema kutoka Bungeni Dodoma kuwa Serikali imeamua kusitisha maombi ya Uwekezaji wa Bandari ya Bagamoyo yaliyokuwa yatekelezwe na kampuni ya China Merchant Group yenye makao yake Hong Kong na Shengzhen, China.

Hata hivo, wakati furaha yangu ikiwa juu, hasa kwa sisi tunaojua kwa kina undani wa mfumo ambao Wachina walikuwa wanaupendekeza na madhara yake kwa Taifa, ghafla, na kama kawaida yake ya kukurupuka, anajitokeza Kiongozi wa ACT Zitto Zuberi Kabwe na kubeza uamuzi huo wa Seikali.

Katika makala yake aliyoipa anuani ya “Kufutwa Kwa Mradi wa Bagamoyo SEZ Kumedhihirisha Udhaifu wa Wa Rais Magufuli Kwenye Uchumi na Diplomasia,” Zitto anajenga hoja nyingi za kuonesha anataabikwa kwa uamuzi huo lakini hoja zake ni hizi kuu mbili:

Mosi, Kwamba kwa Serikali ya Awamu ya Tano kuachana na uwekezaji huo wa Wachina wa China Merchant na wabia wao wa Oman, Tanzania itapoteza fedha nyingi za kigeni, mapato na ajira kwa watu wake (faida za kiuchumi); na

Pili, Kwamba kidiplomasia mradi huu unagusa uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na China na kwamba kuusitisha ni kuathiri diplomasia.

Nitazijadili hoja hizi kwa kifupi sana leo ili nione kwanza pumzi ya Zitto katika uelewa wake wa uchumi na diplomasia.

*Ya Bandari ya Bagamoyo na Uchumi wa Nchi*

Nianze kwa kumshauri Zitto Kabwe, najua amesoma uchumi bila kuufanyiakazi, atafute sehemu akapige “kafield” kauchumi ili kujipa uhalali wa kuchambua masuala mazito ya kiuchumi kama uwekezaji mkubwa wa aina ya Bandari ya Bagamoyo bila kujipotosha wala kupotosha umma.

Katika miradi kama hii inayohusisha nchi na raslimali ya Taifa kama ardhi na bahari hoja mbele ya wachumi waliobobea sio kama Zitto anavyoziwasilisha kiwepesi sana kama kuonesha idadi ya watu watakaoajiriwa, kodi (dhaniwa) zitakazokusanywa wala si sahihi kuangalia kwanza masuala madogo madogo na yenye taathira ya kishamba kama kusema “tutakuwa Dubai ya Afrika?” au maneno matamu tu ya kizungu eti kuwa “main logistics hub!”So what?

Badala yake, katika mambo haya hoja pana ni mapana ya kufaidika kwa nchi, umiliki wa mindombinu itakayojengwa na maslahi mengine mapana ya nchi.

Ndio maana kwa hoja ya umuhimu wa mradi licha ya MoU yake kupitishwa mwaka 2013 hata Mstaafu Kikwete mwenyewe ambaye Zitto anamtajataja sana hakuweza kuuharakisha mradi huo. Aliweka umakini fulani.

Alipoingia madarakani Rais Magufuli (rejea hotuba yake ya 6 Februari, 2018 jijini Dar es Salaam) aliweka bayana kuwa Serikali yake imeridhia mradi huo na kuruhusu majadiliano ya wataalamu yaanze.

Wanaofahamu yaliyotokea katika majadiliano ya mradi wanaweza kucheka mpaka kuvunjika mbavu wakimuona Zitto anavyotetea mradi asioujua na akitumia nadharia nyepesi sana kiuchumi za “ajira, mapato na kuwa Dubai ya Afrika.”

Taarifa kutoka kwenye majadiliano zinapasha kuwa ghafla Wachina walipoona Serikali mpya imebariki mradi wakaanza “kupanua goli” kwa kuja na madai mapya kila siku. Hapa ndipo linapokuja suala la maslahi mapana ya nchi sio ujinga wa vitu kama ajira na mapato.

Mara wakaleta sharti la pamoja na kuiendesha bila kuingiliwa wao ndio wawe wanapanga bei wakishaijenga Bandari ya Bagamoyo, mara wakaja nasharti kwamba ikijengwa Banadari ya Bagamoyo kusiendelezwe Bandari yoyote nyingine kutoka ukanda wa Mtwara hadi Tanga!-hii maana yake ni kwamba Bandari za Mtwara, Mafia, Kilwa, Dar es Salaam mpaka Tanga zingebaki kama zilivyo sasa na zingekufa!

Kubwa zaidi na ambalo bado nasisitiza hoja yangu kuwa Zitto akatafute “field” ajinoe upya kuhusu uwezo wake katika masuala ya kiuchumi ya sasa, ni jinsi Wachina anaowatetea, durusu za majadiliano zinapasha, walivyokuja na dai la KiCarl Peters.

Mnaukumbuka Mkataba wake na Sultani Mangungo wa Msovero uliosainiwa Novemba 29, 1884?

Hayo ndiyo yalikuwa yajirudie. Kama ambavyo Zitto ametaja bayana kuwa mradi huu sio Bandari tu-sahihi kabisa, unahusisha mambo mengi ikiwemo ujenzi wa eneo la viwanda na mji wa kisasa. Safi kabisa, ahadi tamu kama za Carl Peters kwa Sultan Mangungo.

Sasa sikiliza hii-katika eneo lote la viwanda na mji wa kisasa Wachina wakataka si tu hati ya eneo hilo lote isomeke kwa jina lao bali walimiliki kabisa eneo hilo kwa zaidi ya miaka 33!!!

Na si kumiliki tu, wakataka kwa kuwa wao ndio “wamiliki” wa kipande hicho cha ardhi ya Tanzania ndio wawe wasimamizi, wasajili na wenye uamuzi juu ya viwanda vyote vitakavyotaka kuwekeza kwenye eneo hilo kuanzia kuvisajili, kodi wanazolipa hadi uamuzi wa mwisho wa nani aweke kiwanda na nani asiweke! Bandari ya Eritrea leo nje kumejaa viwanda vya China vitupu. Nasi tulikuwa tunawelekea huko.

Kwa kifupi mbaya zaidi wanasema, imeelezwa, kuwa hata hiyo miaka 33 haitaisha “automatically” inaweza kuongezeka hadi umilikiwa miaka 99 iwapo watakuwa hawajarejesha faida yao.

Nani atahakiki urejeshaji wa faida?Hii ni hatari heri wakupe mkopo ufanye mwenyewe, ulipe mkopo hata kama ni wa ghali.

Kwa nini mfumo huu kiuwekezaji ni hatari heri ukope na kulipa, tofauti na uelewa mdogo sana wa Zitto, kwa wao kuwekeza hizo Dola bilioni 10, Wachina wangeendesha wenyewe biashara zote na wao ndio wangekuwa wanaandaa mahesabu na kila mwaka wangekwambia wanapata hasara lakini wangeendelea kuwepo kwa zaidi ya hiyo miaka 33.

Wachina wanapataje hasara ili kujustify kuendelea kukutawala katika biashara?

Uzoefu wa nchi nyingi zilizoingia mkenge huu wa kusubiri “faida ya Mchina” unaonesha haya: Mosi, watacheza na hesabu kwa kutumia mifumo yao ya kisasa ya kidigitali na iliyo kwenye codes na lugha ya Kichina pekee.

Pili, zabuni zote watapewa makampuni rafiki (third party companies and related parties) ambao watawachaji kwa makusudi China Merchant bei kubwa ili gharama ya uwekezaji uwe kubwa kiasi mapato yawe chini kila mwaka.

Hapa utaambiwa kwa miaka 100 “hakuna faida” kwa hiyo Bndari na mji na eneo la viwanda vinabaki kwenye umiliki wao!!

Katika hili Tanzania inayo mifano mingi ya aina hii lakini moja ya uwekezaji unaotukumbusha falsafa ya Wachina na staili zao za upigani ni ubia wa TBC na StarTimes ya China ambao hata Zitto Kabwe, Bunge na CAG wameupigia kelele weee lakini miaka zaidi ya 10 sasa Wachina wanatangaza kupata hasara lakini kuondoka hawataki!

Kwa hiyo katika uelewa, maono na kutetea maslahi mapana ya Taifa namuona Zitto na Magufuli kuwa viongozi wenye mitazamo miwili yenye tofauti ya “mlima na kichuguu.”

Wakati Zitto anawaza vitu vya kishamba shamba (sawa na Sultan Mangungo wa Msovero aliyepewa shanga na maua akauza ardhi), Magufuli ni kiongozi imara, makini na anayefuatilia mambo kwa umakini “wa mawinguni.’

*Bandari na Diplomasia ya Tanzania na China.*

Katika hili nimshauri tu Ndugu Zitto yapo maeneo ni ya kukaa kimya. Hajui misingi ya diplomasia ya Tanzania, hajui sayansi na sanaa katika utekelezaji wa diplomasia za dunia, hivyo kamwe hawezi kuhitimisha kuhusu diplomasia ya Tanzania na China kwa sababu ya Bandari ya Bagamoyo.

Labda nianze hivi-msingi wa diplomasia ya China na Tanzania haukujengwa katika ubepari unaooneshwa sasa na baadhi ya kampuni za China na Serikali ya China inajua hilo.

Msingi wa diplomasia ya mataifa haya mawili na ambao hauwezi kutetereshwa na mradi wa Bagamoyo ni manufaa na imani.

Ndio maana makubaliano ya awali kabisa rasmi ya mataifa haya mawili yaliyofikiwa mwanzoni mwa miaka ya 1960 mataifa haya mawili yote yakiwa maskini wa kutupwa yalijengwa katika “udugu na ujamaa,” uliounganishwa na imani na ushirikiano/ubia wenye manufaa kwa pande mbili

Misingi hii iliendelezwa na kuhuishwa miaka ya 1970 Tanzania ailipotumia ushawishi wake wa kisiasa kuisaidia China kurejea kwenye Baraza la Usalama la UN na China ikatumia nguvu yake kidogo wakati huo kuisaidia Tanzania na Zambia kutekeleza mradi wa Tazara.

Labda kwa faida ya Ndugu Zitto anayevamiua mawanda asiyoyaelewa, nimesema msingi wa kwanza wa diplomasia ya Tanzania na China ni imani. Asome andiko la mwandishi mahiri wa historia Goran Hyden katika *“Mao and Mwalimu; The Soldier and the Teacher as Revolutionary”* la mwaka 1967.

Atabaini kuwa uhusiano wa China ya Mwanajeshi Mao na Tanzania ya Mwalimu Nyerere uliunganishwa kwanza na “imani” yao katika mageuzi, maendeleo ya watu wao na usawa katika jumuiya ya kimataifa.

Msingi wa pili ni nimetaja ni ubia wenye manufaa kwa pande zote. Nikimnukuu Mwalimu Nyerere, ushirikiano wa Tanzania na China, haukuwa wa kuwekeana masharti, kuingiliana katika sera na mipango ya ndani bali ubia wenye manufaa kwa wote.

Katika hotuba yake akishukuru Serikali ya China kuhusu mkopo wa ujenzi wa Reli ya Tazara iliyochapishwa katika uk. Wa 232 hadi 239 katika kitabu “Freedom and DevelopmentiIUhuru na Maendeleo” Nyerere anafafanua msingi huu wa ushirikiano wa Tanzania na China akisema:

*"Let me state quiet clearly that we appreciate this loan, and we appreciate the fact that it is interest free…And I repeat-the Chinese people have not asked us to become communist to qualify for this loan! They know that we would not sell our independence, even for the railway; and they have never at any point suggested that we should change any of our policies-internal or external (uk. 235)”*

Kwa hiyo nimwambie tu Ndugu Zitto wakati katika eneo la uchumi anahitaji tu “field” tena, katika eneo la diplomasia asiingize kabisa miguu kujaribu kupima kina cha maji, atazama. China anayoizungumzia yeye si hii na Tanzania inayoitolea mfano ilikuwa sambamba na China sio hii ingawa misingi yao inabaki ile ile lakini mchezo wa diplomasia umebadilika sana.

Ingawa ushirikiano wa Tanzania na China uliojengwa katika misingi hiyo miwili mikubwa unaendelezwa sawa sawia katika uongozi wa sasa wa Mwalimu Magufuli na ‘Mwanajeshi’ Xi Jinping, wabobezi wa diplomasia watakwambia ukweli: Hii sio China ya kukaa nayo kichwa kichwa kama ya mwaka 1970.

Kwa sababu hiyo, nihitimishe kwa kumtaka Zitto kuachana na mkakati wake unaojulikana wa kubeza kila jambo au uamuzi wa Rais Magufuli bila kujipa muda wa kutafakari kwa kina. Serikali hii nimeifahamu kuwa makini sana hata kama wanaweza kukosea hapa na pale kama wanadamu lakini si katika hili la kuwatosa Wachina.

Narudia tena na tena, China ya mwaka 2019 sio ya mwaka 1969, muda umepita sana. Ndio maana Zitto akitaka anaweza kuangalia kelele zinazowaandamana Wachina sehemu mbalimbali duniani kwa sasa. Na kuna miradi yao mingi tu imesitishwa.

Akitaka kujua madudu na kashikashi ambazo uwekezaji mwingine wa kampuni anayoitetea ya China Merchant unaendelea nchini Djibouti kwenye Bandari kama ya Bagamoyo asome na sasa kuna kesi kubwa kwenye Mahakama ya Hong Kong, asome makala iitwayo “China Tightens Grip on East African Port” na makala nyingine iitwayo “A legal Tussle over a Strategic African Port sets up a Challenge for China’s Belt and Road Plan”

Lakini pia kwa rejea yake Ndugu Zitto kuhusu mawanda ya “kigeopolitics” (kama anaelewa vyema diplomasia) kuhusu uamuzi wa China kutaka Bandari nyingi katika nchi za Asia na Afrika anaweza kujibidiisha na kusoma hapa na kuona Je, ni malengo ya kiuchumi pekee:
https://www.scmp.com/comment/insigh...-key-success-all-sides-belt-and-road-projects

Lakini nimgusie tu Zitto, rafiki yake mpendwa Mzee Mahathir Mohammed wa Malaysia naye majuzi tu amesitisha mkataba wa Dola za Marekani takribani bilioni 20 (mara mbili ya huu wa Tanzania) na kuziondoa kampuni za China zilizokuwa na mradi wa kujenga reli ya “SGR” kwa nini?Atueleze katika andiko lake lijalo kama ataendelea kuwa na pumzi.

Lakini Zitto anajua kuwa nchi za Pakistani, Myanmar na hata Nepal nazo zimesitisha mikataba kadhaa ya matrilioni na kampuni za China? Kwa Pakistani asome:
https://www.nytimes.com/2018/12/19/world/asia/pakistan-china-belt-road-military.html lakini kwa yaliyoikuta Sri Lanka hadi Bandari yao kuchukuliwa kabisa na China asome: https://www.nytimes.com/2018/06/25/world/asia/china-sri-lanka-port.html?module=inline

Nisisitize tu kama kuna wakati Tanzania imempata kiongozi anayetazama mbali na si mbele tu, anayetazama keshokutwa na si kesho tu basi tumshukuru Mungu kumpata Rais Magufuli anayesimamia maslahi mapana ya nchi yetu. Leo kuna watu wangekuwa kwenye mamlaka tungeshauza kipande hicho cha Bagamoyo.

Ndio maana nilianza na namalizia kwa hoja ya Dkt. Bashiru ya kutafakari kama kweli katika viongozi vijana tulionao na waina ya hoja za Zitto tunao kweli vijana walio tayari kurithi uongozi wa nchi hii na wakaendeleza safari sahihi ya kufikia Ndoto Ya Taifa na kutuepusha na makosa yale yale ya akina Mangungo wa Msovero?
Tuendelee kutafakari.

*Mwandishi wa makala haya ni mimi Mwamba (sema mara tatu) wa Kaskazini.*
 
Na [.....] & Kabwe Z. Ruyagwa Zitto, Mb


(Makala haya kwa sehemu kubwa yametokana na makala iliyoandikwa na mtu mwengine [....]. Mimi nimeiboresha tu Katika baadhi ya maeneo)

Juzi Serikali imetangaza bungeni kuwa Mradi mkubwa wa Ukanda Maalumu wa Kiuchumi wa Bagamoyo (Bagamoyo SEZ) wa thamani ya Dola za Marekani 10 Bilioni (sawa na TZS 23 Trilioni) umesitishwa na kuwa hautafanyika tena. Mradi huu mkubwa wa uwekezaji ambao thamani yake ni zaidi ya Bajeti ya Maendeleo ya Wizara nzima ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa miaka minne (TZS 18 Trilioni) haupaswi kufutwa tu bila mjadala wa kina. Ni lengo la makala haya kuibua mjadala huo.

Kwangu kufutwa kwa mradi wa Bagamoyo SEZ ni kielelezo cha uelewa mdogo wa Uchumi na Diplomasia uliotamalaki miongoni mwa watawala wa sasa wa nchi yetu Tanzania. Kwanza ni muhimu kuuelewa mradi wenyewe kabla ya kubomoa hoja za Serikali zilizotumika kufuta mradi huu. Watanzania wanapaswa kutambua kuwa mradi huu ni wa Uwekezaji kutoka nchi mbili ambazo tuna historia nazo kubwa, Oman na China, hivyo tutazama athari za maamuzi haya ya Serikali pia katika eneo hilo la mahusiano na nchi hizi mbili.

Kiujumla watanzania wengi wakisikia mradi wa Bagamoyo SEZ wanajua ni ujenzi wa bandari ya Bagamoyo tu, La si hivyo. Bandari ni sehemu tu ya mradi. Lakini Bagamoyo SEZ ni mradi wenye lengo la kuufanya mji wa Kihistoria wa Bagamoyo kuwa Kituo kikubwa Cha Usafirishaji Mizigo (Main Logistics Hub) Katika Bara zima la Afrika. Ni Uwekezaji wa Ubia (Joint Venture Investment) kati ya wawekezaji kutoka China na Oman, ambao walikuwa tayari kuutekeleza kama Special Economic Zone (Eneo la Ukanda Maalum wa Uchumi Bagamoyo). Ujenzi wa Bandari ni moja tu kati ya maeneo Manne ya Mradi huo mkubwa, maeneo mengine ya mradi ni pamoja na;

1. Ujenzi wa eneo la viwanda (industrial park) ambalo katika awamu ya kwanza litakuwa na viwanda 190 vitakavyozalisha ajira mpya za moja kwa moja 20,000 na awamu ya pili na tatu ikikamilika kutakuwa na viwanda 790 vitakavyozalisha ajira mpya 100,000.

2. Ujenzi wa Mji wa Kisasa wa makazi unaonendana na mahitaji ya karne ya 21. Ujenzi wa mji huu ulilenga kusaidia kupunguza msongamano wa jiji la Dar es saalaam kwani shughuli nyingi za uchumi zitakazotokana na Bagamoyo SEZ ungepelekea watu wengi kuhamia kwenye mji mpya kutoka Dar es Salaam.

3. Ujenzi wa Kituo Cha Usafirishaji (Logistics Park) ambacho kingeifanya bagamoyo kuwa kitovu cha usafirishaji wa mizigo na hivyo kuiimarisha Tanzania kama njia kuu ya usafirishaji mizigo ‘transit route’ inayotoka na kuingia kwenda nchi mbalimbali tunazopakana nazo. Hii ‘Logistics Park’ ndio ililenga kuhudumia Meli (handle transshipment) kutoka Afrika kwenda Ulaya na Marekani.

Mradi huu na maeneo yake hayo manne (4) ungekamilika, na haswa hilo eneo la nne (Logistics Hub), jumla ya Kontena 20 milioni zilitarajiwa kupita Bagamoyo kwa mwaka na kuifanya kuwa bandari kubwa kuliko ile ya Rotterdam ya Uholanzi ambayo ndio kubwa kuliko zote Bara la Ulaya. Kwa hakika ndani ya miaka 10 Bagamoyo ingekuwa Dubai ya Bara zima la Afrika.

Wazo la mradi huu linafanana na wazo la Mradi wa Shenzhen - Special Economic Zone, ambapo Kampuni inayotaka kuwekeza Bagamoyo ilikuwa mojawapo ya kampuni zilizowekeza huko. Ukanda Maalumu wa Uchumi wa Shenzhen ulikuwa Mpango Maalumu wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi ya China chini ya Kiongozi Deng Xiaoping.

Ulikuwa mji wa majaribio ya sera za Kiuchumi ambazo zimeibadilisha nchi ya China na kuwa inavyoonekana sasa. Bagamoyo ilikuwa inajengwa kuwa Shenzhen ya Afrika kupitia mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone ambayo wengi hupenda kuita Bagamoyo Port kiufupi na kwa hakika kwa makosa.

Hii Ndio bahati mbaya iliyotokea, watu wengi wanajikuta kuzungumzia bandari na huenda hata maamuzi ya kusitisha mradi yamefanyika kwa kuzingatia sehemu moja tu ya bandari na wameacha kufikiria manufaa makubwa ya ajira kutoka maeneo mengine matatu ya mradi, hasa kipindi hiki ambacho vijana wengi wa Tanzania wanamaliza shule bila matumaini ya kupata ajira rasmi au hata kujiajiri wenyewe.

Mradi huu mkubwa umekuwa gumzo sehemu mbalimbali ulimwenguni kutokana na ukubwa wake pamoja na athari zake kwa maslahi ya makundi mbalimbali ulimwenguni. Jambo moja muhimu sana kukumbukwa ni kuwa Biashara ni vita ya makundi yenye maslahi mbalimbali. Rais John Pombe Magufuli amekuwa akihubiri kuwa nchi yetu ipo kwenye vita vya kiuchumi, masikini kwenye ‘The Bagamoyo Battle’ ameshindwa vita kabla hata risasi ya kwanza kupigwa. Maslahi yapo kutoka maeneo kadhaa;

1. Kwa mataifa ya Ulaya Magharibi mradi huu ulikuwa tishio kwa hoja za kiushindani na ushawishi ndani ya ukanda wa Bahari ya Hindi ambao unabashiriwa kuwa kitovu muhimu katika bishara ya kimataifa katika miaka michache ijayo. Wazungu waliuona mradi huo kuwa utaipa China nguvu kubwa zaidi ya kiuchumi. Ilikuwa ni muhimu sana kwa wao kuhakikisha mradi huu hautekelezwi kwa namna yeyote ile ili kuzuia nguvu ya China Katika ukanda huu.

2. Kwa mataifa mengine ya Afrika, mfano kwa SADC nchi kama Afrika ya Kusini - mradi huu ulikuwa tishio kwa maslahi yao ya kiuchumi kwa kuwa ungepelekea ushindani mkubwa kwa Biashara ya Bandari ya Durban ambao hivi sasa ndio kuna bandari pekee zenye uwezo wa kuhudumia meli kubwa kabisa za mizigo (4th generation ships). Inawezekana kabisa Afrika Kusini haikufanya kitu kuhujumu Mradi huu lakini kutofanyika kwake ni faida kubwa wa Durban kwani Bagamoyo ilikuwa inakwenda kuwa mshindani wake Mkuu. Hali ni hiyo hiyo kwa Angola ambayo inataka kujenga reli ya kuiunganisha DRC Kongo ili mizigo ya nchi hiyo ipitie bandari yao ya Luanda.

3. Kwa Afrika Mashariki, hasa Kenya, mradi wa Bagamoyo ulikuwa ni tishio kubwa kwa mradi wa Bandari mpya wanayopanga kuijenga huko Lamu, ambayo nayo itakuwa na uwezo wa kuhudumia meli kubwa (4th generation ships) na pia itakuwa na kitovu cha usafirishaji wa mafuta barani Afrika. Siamini kuwa Kenya imefanya chochote kuhujumu mradi huu wa Bagamoyo SEZ, lakini maamuzi ya Tanzania kusitisha mradi huo yametoa ushindi wa bure bure kwa Kenya, kwani sasa Meli kubwa zitahudumiwa Lamu na kuipa Kenya nafasi kubwa sana Katika Biashara ya Usafirishaji Katika eneo la Afrika Mashariki na Kati (The Great Lakes Region).

4. Taasisi nyingine za kimataifa zimeingia katika vita hii kusaidia nchi zenye nguvu Duniani. Benki ya Dunia (WB) kwa Mfano haikuupenda mradi huu, na ni dhahiri kuwa imetumia ushawishi wake Serikalini kuupiga vita Mradi wa Bagamoyo SEZ. Ushawishi huo uliwezekana kutokana na misaada na mikopo ambayo Benki ya Dunia inaipatia Tanzania na hivyo kupenyeza ushawishi wa kuupinga mradi. Hoja kubwa iliyotumika kupinga mradi wa Bagamoyo ni kwamba kwakuwa wao WB wameipa Serikali mkopo wa maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam, hivyo mradi wa Bagamoyo hauna tija, na endapo ungefanyika utaleta ushindani kwa Bandari ya Dar es salaam na hivyo kushindwa kulipa mkopo. Hoja hii ni muflisi, lakini Serikali yetu ikaingia kingi na kupoteza Uwekezaji wa Fedha za Kigeni (FDI) wenye thamani ya USD 10 Bilioni (TZS 23 Trilioni) kwa tishio la mkopo wa USD 400 milioni (TZS 920 Bilioni). Inasikitisha sana!

Makundi hayo yote yalikuwa na maslahi yanayofanana ya kuhakikisha|kuombea kwamba Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone usitekelezwe. Maamuzi ya Serikali yetu yamewezeshwa matakwa ya Makundi hayo, kwa kujua ama kutokujua. Najua kuwa imetumika nguvu kubwa ya ushawishi kwa kutumia; Propaganda za vyombo vya habari, Ujasusi wa kiuchumi (economic intelligence) na hata Ushawishi wa kisiasa (political influence and scaremongering).

Mfano ni kugonganisha utawala wa Awamu ya 5 na Uongozi uliopita wa Awamu ya 4 (kwa kuonyesha kwa kuwa Rais aliyepitisha mradi huu anatoka Mkoa wa Pwani, na hivyo amepeleka mradi huu kwao Bagamoyo kwa kujipendelea). Ndio maana Kikao Cha Baraza la Mawaziri, vikao vya mwanzo mwanzo tu vya utawala wa awamu ya tano, viliufuta mradi huu bila hata mjadala wa kina unaozingatia faida pana za mradi, na wala mahusiano ya kidiplomasia kati yetu na nchi za Oman na China.

Sasa tutazame hoja zinazotolewa dhidi ya mradi wa Bagamoyo SEZ ili kuona kama kuna mantiki.

1. Hofu ya Serikali kupoteza mapato kutokana na ushindani wa Bandari ya Bagamoyo

Serikali imejengewa hofu kuwa Bandari ya Bagamoyo itafanya mapato ya Bandari ya Dar kupungua na hivyo Serikali kukosa Mapato yake. Ukiangalia kwa juu juu hoja hiyo ina mantiki. Kwamba kutakuwa na ushindani na Dar es salaam itapoteza mapato. Lakini yapo mambo matatu yanayothibitisha kwamba hoja hiyo sio sahihi.

Mosi: Bandari ya Bagamoyo itahudumua meli kubwa (4th generation ships) ambazo hivi sasa haziwezi kuingia katika bandari ya Dar es salaam. Katika biashara ya kimataifa hivi sasa, usafirishaji kwa kutumia meli kubwa ndio wenye tija, unafuu na faida. Kwa mfano leo hii kusafirisha zao la korosho kutoka Tanzania hadi China au Marekani kwa kutumia meli ndogo inagharimu mara mbili ya gharama ya usafirishaji kwa meli kubwa.

Kutokuwa na uwezo wa kuhudumia meli kubwa kumefanya gharama za usafirishaji wa bidhaa kutoka Nchi zetu kwenda kwenye masoko mengineyo kuwa kubwa na ghali mno (uncompetitive). Ndio maana leo hii nchi za Latin America ambazo zipo mbali kabisa na China, zinauza bidhaa zake nyingi katika soko la China kuliko nchi za Afrika ambazo zipo karibu na China kijiografia.

Mfano halisi umetokea karibuni tu, Marekani ilipoanza vita ya biashara na China kwa kuongeza kodi katika bidhaa za China, ili kujibu mapigo China nao waliongeza kodi kwa maharage ya soya kutoka nchini Marekani. Ikumbukwe kwamba biashara ya maharage ya soya ni kubwa sana kwa Marekani, kila mwaka wanauza soya ya thamani ya USD 35 Billioni na zaidi kwa nchi mbalimbali, China ikinunua 60% ya soya yote.

Hivyo basi, kitendo cha China kuongeza kodi, gharama za soya zikapanda na hivyo wanunuzi wa soya kutoka China walitafuta soko mbadala la kununua soya (altenative source). Lakini badala ya kuja kununua Afrika, ambako ni karibu zaidi, waliamua kwenda kwa nchi za Amerika ya Kusini (Latin Amerika), hasa Brazili. Moja ya sababu ya kwenda kununua Soya huko ni pamoja na uwepo wa bandari zenye uwezo wa kuhudumia meli kubwa (4th Generation Ships) ambazo ni nafuu katika usafirishaji. Afrika imekosa fursa ya biashara kubwa sababu hiyo.

Pili: Uwepo wa bandari kubwa katika eneo moja unasaidia kuongeza wingi wa shughuli za usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye bandari kubwa kwenda kwenye bandari ndogo, na hivyo kuongeza mnyororo wa thamani wa sekta ya usafirishaji. Mizigo mikubwa mkubwa ambao ungeshushwa katika bandari ya Bagamoyo ungetengeneza fursa ya biashara kwa meli ndogo na za kati kuuchukua Bagamoyo na kuupeleka kwenye bandari za jirani za Dar, Tanga, Mombasa, na Beira. Mapato yangeongezeka badala ya kupotea.

Tatu: Ajira zitakuwa nyingi kwenye Bagamoyo SEZ kuliko kwenye upanuzi wa bandari ya Dar es salaam. Ni vizuri pia kujiuliza kuwa upanuzi wa Bandari ya Dar manufaa yake ni zaidi ya manufaa tutakayopata katika Mradi wote wa Bagamoyo SEZ? Hivi sasa Bandari ya Dar es salaam inaajiri watu wangapi? Baada ya upanuzi utakaofanywa ni ajira ngapi mpya zitaongezeka?

Ukweli ni kwamba kwa teknolojia za karne ya 21 shughuli za bandari nyingi ziko kidijitali (digitalized) sana kiasi kwamba ile asili ya kuzalisha ajira nyingi haipo tena. Hivyo kwa vyovyote vile ajira mpya zitakazozalishwa baada ya kumalizika upanuzi hazitozidi 1000. Kwa upande mwingine, ajira zitakazozalishwa kwenye mradi wa Bagamoyo SEZ katika awamu ya kwanza tu ni 20,000. Je faida ipo wapi? Mapato ya Kodi za Wafanyakazi hao 20,000 tu yatazidi mara 10 Mapato yote ya Serikali kutoka Bandari ya Dar Es Salaam.

Nne: Kwa upande wa mapato (direct revenues) kwa Bandari ya Dar es salaam- serikali inapata kiasi gani? Kwa vyovyote vile mapato ya jumla ambayo serikali itakayapata katika mradi wa Bagamoyo SEZ yatakuwa ni makubwa zaidi, kwani mbali na mapato itakayopata katika component ya bandari kwa njia ya Wharfage charges; Imports Duties kwa bidhaa nyingi zitakazopitia katika bandari hiyo, serikali pia itapata kodi za aina mbalimbali katika viwanda 190 na baadaye viwanda 790 vitakavyojengwa.

Watumishi 20,000 PAYE yao itakuwa ni kiasi kikubwa cha uhakika kwa serikali. Achilia mbali multiplier effects zitokanazo na shughuli za viwanda. Katika mji mpya utakaojengwa Serikali itapata kodi za majengo na kodi nyingine zitokanazo na ardhi na pango, achilia mbali kodi za shughuli nyingine za biashara zitakazofanyika Bagamoyo. Hoja ya Mapato kupotea ni hoja dhaifu na haina mashiko kabisa.

2. Hofu ya Mgeni Kuendesha Bandari

Hoja nyingine inayotolewa ni kwamba kumpa mwekezaji mgeni aendeshe bandari ni hatari kwa usalama wa nchi. Hapa cha kujiuliza ni kuwa ndani ya Bandari ya Dar es salaam kuna kampuni ya Uwekezaji ya Kigeni - TICTS, ambayo imeendesha shughuli zake ndani ya bandari kwa miaka 20 na zaidi sasa, je ni usalama upi wa nchi umeathirika?

Inapokuja hoja za kiusalama ni nchi ya China yenye mahusiano ya karibu sana ya kijeshi na Tanzania. Kila leo tumeona vikifunguliwa vyuo (Chuo cha Ulinzi cha Jeshi Kunduchi), viwanja vya ndege (Uwanja wa Ndege wa Kijeshi wa Ngerengere, Morogoro) nk kwa msaada wa China. Wanajeshi wengi wa Tanzania wamepata mafunzo China, na vifaa vingi vya kivita vimetoka China. Ni jambo la kawaida kukuta gari yenye namba za usajili za JWTZ ndani yake kuna askari wa Tanzania na China.
Sasa kwa ukaribu huo wa kihistoria tangu JWTZ ilipoanzishwa baada ya kuvunja jeshi lenye asili ya kikoloni lililojaribu kufanya mapinduzi miaka ya 60, leo hii sisi ndio watu wa kuhofia usalama dhidi ya Wachina? Hata hivyo, kama hoja hii ni ya kweli, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama haviwezi kuweka mkakati mbadala wa kudhibiti masuala ya Usalama katika eneo la mradi la Bagamoyo SEZ?

3. Hofu ya China kuchukua Mali za Taifa kama Zambia na Sri Lanka

Hoja nyingine inayozungushwa ni kwamba eti Wachina watanyang’anya mali za taifa endapo mradi huo utapata hasara kama ilivyokuwa kwa mradi wa Bandari wa Sri Lanka. Ukweli ni kwamba mradi wa Bagamoyo sio sawa na mradi wa Sri Lanka au mradi wa ujenzi wa Reli ya Kenya. Tofauti na miradi hiyo miwili ya Kenya na Sri Lanka, mradi wa Bagamoyo unatekelezwa kwa njia ya uwekezaji (FDI) kwa asilimia 100, wakati ile miradi ya Kenya na Sri Lanka inatekelezwa kwa mikopo ambayo nchi inawajibu wa kuweka dhamana (sovereign guarantee).

Hii maana yake Maana yake nini? Hata kama mradi wa Bagamoyo utendeshwa kwa hasara, atakayeumia ni mwekezaji na sio nchi yetu. Lakini kwa uzoefu wa kampuni ya China Merchant katika uwekezaji wa miradi mikubwa ya aina hii, haiwezekani wakafanya uamuzi wa kuwekeza mradi wa kupata hasara kirahisi namna hiyo. Ikumbukwe kwamba kampuni ya China Merchant ina uwezo wake kimtaji unaofikia mara 20 ya GDP ya Tanzania. Yaani Mapato ya Kampuni hiyo kwa mwaka ni USD 1,200 Bilioni, wakati GDP ya Tanzania ni USD 55 Bilioni.

4. Masharti Magumu

Hoja nyingine inayosemwa ni kuwa masharti ya kuendesha mradi wa bagamoyo ni magumu. Inawezekana kuwa hoja hii ina mashiko na ndio maana ni hoja pekee ambayo Serikali inaitaja. Hata Bungeni ndio hoja Waziri wa Uchukuzi ameizungumza katika hotuba yake ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa mwaka 2019/2020.

Lakini tuulizane, hivi mahala ambapo watu wanazungumza, kila upande una wajibu wa kuja na mapendekezo yake (proposal) na upande wa pili una haki ya kuja na counter proposal. Kuweka mpira kwapani sio njia sahihi hata kidogo, ni udhaifu uliopitiliza.
Kama serikali iliweza kwenda hatua ya ziada kuvutia mradi wa Bomba la Mafuta la Uganda kwa kutoa vivutio maalum vilivyopelekea hadi kufanyika mabadiliko ya sheria Bungeni iweje ishindwe kufanya hivyo kwa Mradi wa Bagamoyo? Kwa faida za ajira na kodi zinazokuja na mradi wa Bagamoyo kwa hakika zinazidi faida za mradi wa bomba la mafuta ambalo sehemu kubwa ya ajira zake zitatokea wakati wa ujenzi wa bomba lenyewe na likishakamilika ajira zitapungua kwa 80%.

Ukiachilia faida za moja kwa moja zilizotajwa kuhusu mradi wa Bagamoyo, ni wazi kwamba ujenzi wa mradi huo pia utasaidia kuufanya mradi wa reli ya Kati ya Standard Gauge kupata idadi kubwa ya mizigo ya kusafirisha ili uweze kurejesha mikopo iliyochukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo. Serikali yetu inashindwa kuona fungamanisho hili kati ya Mradi wa Reli ya Kisasa na Mradi wa Bagamoyo SEZ? Kwa ujumla na vyovyote iwavyo, faida za mradi wa Bagamoyo SEZ ni kubwa kuliko madhara tunayodhani tunayaepuka.

Athari za Maamuzi Haya Kiuchumi na Kidplomasia

Inawezekana kuwa sababu zinazotajwa hadharani sio sababu haswa zilizopelekea Mradi wa Bagamoyo SEZ kusitishwa. Sababu zisizotajwa zinatamanisha kuzifahamu. Tuna wajibu wa kuzitafuta hizi sababu zisizotajwa. Kama zinazotajwa ndio sababu basi si sababu maana hazina mashiko kulinganisha na faida kubwa za mradi huu kwa Taifa, na hasa Ajira na kwenye kukuza nafasi ya nchi Katika dunia ya Usafirishaji.

Nimalize kwa hoja ambayo sasa kama Tanzania tunapaswa kuwa nayo makini sana. Kwa miaka ya Hivi karibuni nchi yetu imeanza kupoteza heshima yake kimataifa na hata kuelekea kupoteza marafiki wa kudumu (all weather friends). China na Oman, nchi ambazo zilikuwa zishirikiane na Tanzania kwenye mradi wa Ukanda Maalumu wa Kiuchumi wa Bagamoyo (Bagamoyo SEZ) ni nchi muhimu sana kwa historia ya Tanzania.
China ilipoanzisha mikutano na Afrika (FOCAC) mwaka 2000 ni nchi 4 tu za Afrika zilihudhuria ikiwemo Tanzania. Hivi sasa FOCAC inahudhuriwa na marais wengi zaidi kuliko Mkutano wa AU wa kila nusu mwaka. Rais Magufuli hajahudhuria mkutano hata mmoja wa FOCAC tangu aingie madarakani na hivyo kutoonana na Rais wa China kuzungumzia masuala ya Maendeleo ya nchi zetu hizi. Mradi wa Bagamoyo ulikuwa mradi muhimu mno kwa wazo la Rais wa China la ‘Belt and Road Initiative’. Kutofanikiwa kwa mradi huu ni udhaifu wa kidiplomasia wa nchi yetu na udhaifu huu una gharama kubwa kwa Maendeleo ya nchi yetu.

Mshirika mwengine wa mradi huu ni nchi ya Oman. Oman Ina historia kubwa kwa Tanzania na hususan Zanzibar. Katika raia takribani milioni 5 wanaoishi Oman, takribani nusu yake wanaongea kiswahili. Kama kuna nchi ambayo Tanzania inapaswa kuwa na mahusiano nayo ya karibu zaidi nje ya Afrika ni Oman. Hivi karibuni Oman imekuwa ikijitahidi kuimarisha mahusiano yake na Afrika Mashariki na Mradi wa Bagamoyo ilikuwa ni moja ya Miradi ya kuonyesha nia na dhamira ya dhati ya Serikali ya Oman kuboresha mahusiano na Tanzania.

Oman inaagiza takribani vyakula vyote kutoka nje, na Tanzania ingeweza kufaidika sana na soko la Oman kwa Bidhaa za kilimo na mifugo. Hivi sasa nchi zinazofaidika ni India na Sri Lanka. Mradi wa Bagamoyo ulikuwa mradi muhimu sana kuifungua Oman kwa Tanzania. Kutofanikiwa kwa mradi huu ni udhaifu wa kidiplomasia wa nchi yetu na udhaifu huu una gharama kubwa kwa Maendeleo ya nchi yetu kiuchumi, hasa kwa wakulima na wafugaji.
Jambo linalonishangaza kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano ni uwezo wake wa kukumbatia miradi inayotoa Fedha nje (outflows) na kuua miradi yote iliyoikuta ya kuleta fedha nchini (inflows). Mradi wa kinu Cha kuchakata Gesi Asilia cha Lindi (LNG) wenye thamani ya USD 30 bilioni (TZS 69 Trilioni) umecheleweshwa, Mradi wa Uwekezaji kwenye Makaa ya Mawe ya Mchuchuma na Liganga wenye thamani ya USD 3.5 Bilioni (TZS 8.05 Trilioni) nao pia umecheleweshwa, na sasa Mradi wa Ujenzi wa Ukanda Maalumu wa Kiuchumi wa Bagamoyo kuifanya Tanzania kuwa Kituo Kikuu Cha Usafirishaji Afrika nzima, wenye thamani ya USD 10 Bilioni nao umesitishwa.

Utekelezaji wa miradi hii mitatu ungerahisisha sana utekelezaji wa miradi ambayo Serikali inafanya sasa. Mradi wa LNG ya Lindi ungeipa nchi mabilioni ya fedha za Kigeni kutekeleza mradi wake pendwa wa Stiegler’s Gorge kama ingekuwa kuna haja kuendelea nao. Mradi wa Mchuchuma na Liganga ungewezesha kuzalisha Mataruma ya Reli hapa hapa nchini kujengea Reli ya SGR na kuokoa mabilioni ya Fedha za Kigeni tunayotumia kununulia mataruma nje ya Nchi. Mradi wa Bagamoyo ungeleta mizigo yote ya Afrika hapa Tanzania na Reli mpya kupata Biashara na hivyo kupata faida ya Uwekezaji.

Iweje sasa maamuzi yawe kuchelewesha na kufyeka miradi muhimu kama hii? Hakika Sina majibu ya maamuzi ya namna hii, ila najua ni maamuzi ya hovyo yasiyo na faida kwa Taifa letu.


Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Mbunge, Kigoma Mjini

Mei 12, 2019
Sijasoma bandiko lote..
But nilicho notice nyie majamaa mnatuchezea akili nyie kina ZITTO na MAGUFULI.

kama SGR na stiglersgorge huwa mnaipinga mpka mishipa inawasimama kwa kusema ni miradi inayoigharimu taifa pesa nying lakin mnaend mbali zaid kwa kusema miradi Hyo Sio kipaumbele kwa wananchi kwa sasa..

Inakuaje Leo unakuja kutetea kusitishwa kwa mradi wenye kugaharimu matrioni ya pesa. [emoji1745][emoji1745][emoji1745]
 
Pesa yote hiyo inatolewa na mwekezaji kwa 100%. Na pia Je uendeshaji wake utakuwa wa muda gani kabla ya ku transfer? Kwa ujumla faida ni kubwa kuliko kutokuwa na huo mradi (Kuna multiplying effect kubwa kiuchumi na kijamii in the long run). Kuna haja ya kushirikiana kwenye majadiliano kama taifa bila kujali vyama.

Ushauri mzuri kbs - dunia ya leo ili upate lzm mwingine apate pia (win - win situation)
 
Kudeal na.china kunahitaji watu makini na kama huyu muonyesha njia angekuwa makini angeluona na hilo akajua pesa nyingi za china zinazokuja adrika zina madhara makubwa kuliko faida sijaisoma yote ila pia achambue faida itakayopata nchi ikilinganishwa na faida wanayovuna wawekezaji. Zama.za awamu.hii ni win win
Sasa hiyo win win utaishauri vipi kama hujasoma yote? Na kwanini usisome yote kama ni mada umeiona nzuri na yenye tija kwa kiwango cha wewe kutumia mda na akili yako kutoa maoni? Halafu unataka achambue zaidi wakati husomi.
 
Tuna Bandari za DSM, Tanga na Mtwara na zote hizo hazijawa utilized to their potentials, halafu nchi iingie ktk madeni yatakayogharimu Taifa, Hapana tunasema, hapana, Mhe. JPM umeonyesha njia. Pia, bandari ni lango la uchumi kwa nchi, halafu wapewe nchi nyingine waimiliki kwa muda (Jenga, Endesha na Transfer!!), tunasema hapana. Pia kumbuka bandari ni maeneo ya kimkakati kwa ulinzi wa nchi, tunasema hapana, Mhe. JPM tupo pamoja. Akina Zito, waache na ujinga wao. Tunasema, hapana, tupo pamoja na Serikali ya Awamu ya Tano. Aluta Continua!!!!
 
Unadhani hajui braza, huyu jamaa ni opportunist tu kama wengine tunao wakataa humo kwenye system.
Mchina ni wa kujiaminisha utashindana naye kibiashara[emoji23][emoji23], aulize kenya na sgr yao.

Kwa hiyo hao Wachina ni wabaya tu kwenye huo mradi wa Bagamoyo! ila kwenye misaada wanayoitoa mfano ujenzi wa ukumbi wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere - Dar, ule wa ccm kule Dodoma, nk.

Na pia kupewa tenda mbalimbali za kujenga miundombinu ya barabara, nk. inayoendelea nchini na mwisho wa siku pesa yetu nyingi kuirudisha kwao; hapo hakuna madhara!

Mimi kwa mtazamo wangu nadhani serikali yetu ilitakiwa ikae na hao wawekazaji na kuangalia namna ya maridhiano ya huo mradi hasa kwenye namba 2, 3 na 4 kama alivyoelezea mtoa mada madala ya kumshutumu tu. Ni kweli tunahitaji pia pesa iingie kwa wingi nchini mwetu badala ya kuendelea na huu utaratibu wa kuwapa tu hao watu weupe pesa zetu nyingi kupitia hii miradi mikubwa tuliyoianzisha! Hali mtaani itazidi kuwa tete.
 
Migodi yote ya dhahabu imewekezwa na wageni kwa 100% na wanatulipa mrabaha kiduchu. Mwekezaji wa SEZ ana wekeza naye kwa 100% na faida zake (Multiplier effect) yaweza kuwa kubwa kuliko migodi ambayo imewekezwa kwa mitaji ya wageni 100%.

Tunapaswa kujadili bila jazba kwa hoja kama kuna faida au la. Bandari zetu za kikoloni zimebanwa sana na hazitoi nafasi nzuri ya kuboresha (modernization), hivyo mradi huu unaonekana ungetupatia bandari nzuri ya kiushindani kwa ukanda wa Afrika. Lazima tuamue kiuchumi, kuwa na uwekezaji huo na kutokuwa nao kabisa ni maamuzi gani yenye faida?
Ni nyinyi ndio mnajua ni muwekezaji gani anafuata haki za kibinaadam kama sharti la kukukopesha ikiwemo democrasia safi, kwenye hili china hayupo,leo hii hao walitukopesha wameonekana kutukandamiza bado.

Tunayo haki kuangalia ni nani atatufaa kuliko wale, ila sio china kwa 23trillion.

Na kwa hili niseme leo, hata serikali ikilipitisha, maana haitabiriki serikali ya magufuli. Sitatengua kauli yangu. Huu ni mradi wa ajabu.
 
Huyu ndie aliyekuwa waziri kivuli was fedha alyeshindwa kutengeneza bajeti mbadala tuna bandari Dar es salaam, Mtwara na Tanga badala ya kuimarisha bandari ya Mtwara I'll ihudumie nchi za Zambia, Malawi na kongo na kupanua bandari ya DAR es salaam tutaka kujenga bandari mpya kwa huu uamuzi naipongeza serikali kwani imekuwa sikivu
Jamani kweli kuna watu wana vichwa vigumu..

Ni bagamoyo special economic zone, na sio bagamoyo port..

Daaah..
 
JPM juzi amesema bayana kwamba hakuna Rafiki wakweli kama china kwa bishara au mikopo. Maana wao hawana tabia ya kuingilia tamaduni za waafrika na kulazimisha kubadilisha mifumo ya siasa ama kulazimisha mambo kama ushoga..
Ukiona JPM amesita kuendelea na Bagamoyo licha ya kuwa rafiki wa kweli(china) wako mstari wa mbele hapo jua kuna Jambo. Magufuli ni mzalendo sana hata ukiwa rafiki, Tanzania kwanza
 
Sijasoma bandiko lote..
But nilicho notice nyie majamaa mnatuchezea akili nyie kina ZITTO na MAGUFULI.

kama SGR na stiglersgorge huwa mnaipinga mpka mishipa inawasimama kwa kusema ni miradi inayoigharimu taifa pesa nying lakin mnaend mbali zaid kwa kusema miradi Hyo Sio kipaumbele kwa wananchi kwa sasa..

Inakuaje Leo unakuja kutetea kusitishwa kwa mradi wenye kugaharimu matrioni ya pesa. [emoji1745][emoji1745][emoji1745]
Hivi mtu unawezaje kocomment bila kusoma hapa umeambiwa mradi unagharamiwa na nchi 2 china na oman watatoa hizo fedha 23trilion, kama umemuelewa zitto sisi hatukupaswa kuweka mpira kwapani bali kurndelea na majadiliano ili vile vipengelele vinavyotubana tujadiliane kuliko kusema mradi wote ni useless.
 
Naamini kabisa kama mambo yangeenda kama yaluvyopangwa tungekuwa tunasoma uzi wa kukosoa uamuzi huo.
NIMEMUELEWA ZITTO

YUKO SAHIHI

LKN ILI KUJUA NA KUTHIBITISHA KUWA ANAPOITWA YUDA ISKARIOTE CHADEMA HAWAKUKOSEA!!!!! FUATILIA HANSARD ZA BUNGE UONE WAKATI ANACHANGIA KUHUSU MIRADI YOTE MUTATU ALIVYOKUWA ANAIPONDA!!!
AKITHIBISHA KUWA NI MIRADI YA KIFISADI..
HAINA TIJA KWA TAIFA...
NCHI ITAKWENDA KUUZWA KWA SABABU YA DENI KUUUBWA LA KULIPA

LEO AMEBADILIKA NA KUONYESHA RANGI TOFAUTI AKIUNGA MKONO UTEKELEZAJI WAKE

HUYO NDIYE ZITTO!!!!!!

ANASADIFU UPINZANI WETU NCHINI UKOJE

KWAMBA UNAPINGA CHOCHOTE KINACHOFANYWA NA SERIKALI HATA KAMA KINA MANUFAA KWA NCHI

UPINZANI UNAOUNGA MKONO FAILURES ZOOOTE AMBAZO NCHI KUPITIA SERIKALI ITAFANYA ILI KUJIONYESHA WAO WAKIPEWA NCHI WATAFANYA TOFAUTI

ASSESS NOW!!!!
WHO IS ZITTO
WHAT KIND OF OPPOSITION DO WE NEED IN OUR COUNTRY????
 
Kwa hiyo hao Wachina ni wabaya tu kwenye huo mradi wa Bagamoyo! ila kwenye misaada wanayoitoa mfano ujenzi wa ukumbi wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere - Dar, ule wa ccm kule Dodoma, nk.

Na pia kupewa tenda mbalimbali za kujenga miundombinu ya barabara, nk. inayoendelea nchini na mwisho wa siku pesa yetu nyingi kuirudisha kwao; hapo hakuna madhara!

Mimi kwa mtazamo wangu nadhani serikali yetu ilitakiwa ikae na hao wawekazaji na kuangalia namna ya maridhiano ya huo mradi hasa kwenye namba 2, 3 na 4 kama alivyoelezea mtoa mada madala ya kumshutumu tu. Ni kweli tunahitaji pia pesa iingie kwa wingi nchini mwetu badala ya kuendelea na huu utaratibu wa kuwapa tu hao watu weupe pesa zetu nyingi kupitia hii miradi mikubwa tuliyoianzisha! Hali mtaani itazidi kuwa tete.
Hata wewe unaweza ukawa mshikaji kwenye deni la efu 2,ila sio laki nane.

Kama serikali imekaa na kutathmini faida hakuna, au ipo lakini kwa miaka 120 ijayo kwanini tuibeze!!!

Kumbuka wanaweza pesa yao 100% hayo makubaliano ni yepi yatakuwa na mshiko kama hela ya watu haijaonekana!!!
 
NIMEMUELEWA ZITTO

YUKO SAHIHI

LKN ILI KUJUA NA KUTHIBITISHA KUWA ANAPOITWA YUDA ISKARIOTE CHADEMA HAWAKUKOSEA!!!!! FUATILIA HANSARD ZA BUNGE UONE WAKATI ANACHANGIA KUHUSU MIRADI YOTE MUTATU ALIVYOKUWA ANAIPONDA!!!
AKITHIBISHA KUWA NI MIRADI YA KIFISADI..
HAINA TIJA KWA TAIFA...
NCHI ITAKWENDA KUUZWA KWA SABABU YA DENI KUUUBWA LA KULIPA

LEO AMEBADILIKA NA KUONYESHA RANGI TOFAUTI AKIUNGA MKONO UTEKELEZAJI WAKE

HUYO NDIYE ZITTO!!!!!!

ANASADIFU UPINZANI WETU NCHINI UKOJE

KWAMBA UNAPINGA CHOCHOTE KINACHOFANYWA NA SERIKALI HATA KAMA KINA MANUFAA KWA NCHI

UPINZANI UNAOUNGA MKONO FAILURES ZOOOTE AMBAZO NCHI KUPITIA SERIKALI ITAFANYA ILI KUJIONYESHA WAO WAKIPEWA NCHI WATAFANYA TOFAUTI

ASSESS NOW!!!!
WHO IS ZITTO
WHAT KIND OF OPPOSITION DO WE NEED IN OUR COUNTRY????
Ajabu watu wazima na kende mbili huwaelezi kitu.
 
Hii ndo Mwalimu Nyerere aliita "Kuwekea question mark mambo ya maana ya tawala zilizopita"

Wachina watatuona hopeless, kama tumeshindwa kuchangamkia fursa ya uwekezaji kama ile then sisi tupewe nini tena?

Wachina jinsi walivyojikomboa kiuchumi walikubali kuvuta investments za Watu wa Magharibi wainvest kwao leo hii wanapiga hatua.

Leo wachina wamejaribu kutumegea na sisi kainvestment ili tupate chochote kitu tunaanza kuleta nyodo!

Laiti hiyo investment ingefanywa na Mzungu basi tungepiga vigelegele huku tukishangilia!- Slave Mentality!
 
Sijasoma bandiko lote..
But nilicho notice nyie majamaa mnatuchezea akili nyie kina ZITTO na MAGUFULI.

kama SGR na stiglersgorge huwa mnaipinga mpka mishipa inawasimama kwa kusema ni miradi inayoigharimu taifa pesa nying lakin mnaend mbali zaid kwa kusema miradi Hyo Sio kipaumbele kwa wananchi kwa sasa..

Inakuaje Leo unakuja kutetea kusitishwa kwa mradi wenye kugaharimu matrioni ya pesa. [emoji1745][emoji1745][emoji1745]
Hivi inakuaje mtu husomi makala halafu unataka kuijadili? Yaani natafakari nashindwa kuelewa kabisa. Kwanini upoteze mda wako na rasilimali akili kutoa maoni kwa mada ambayo hujaisoma? Sasa jibu la hoja yako huoni ni rahisi tu? Rasilimali zote za nchi ni lazima zijadiliwe kama zina manufaa au la na ni lazima mishipa iwatoke watu wanapopinga au kusapoti ili Kuwe na muafaka. Na wewe ungesoma makala yote ukaichambua huenda mishipa ingekutoka kwa kutetea au kupinga sababu ungejua unachojadili.
 
Huu mradi ungebaki kwenye makaratasi tu as utekelezaji wa mradi wa Trilion 23 kwa usawa huu wa kuchangishana buku buku hautekelezeki Kwa sasa!

ZZK usisahau kuwa jimboni kwako maji tu yanayohitaji bajeti chini ya 20 B yameshindikana kupatikana! Then unatetea 23Trilion ziende Bagamoyo?

Nahisi kama utakuwa umesoma heading tu, hujasoma kilicho ndani au kama umesoma, basi akili yako ilishakuwa na majibu kabla ya kumjibu Zitto.
 
Huu mradi ungebaki kwenye makaratasi tu as utekelezaji wa mradi wa Trilion 23 kwa usawa huu wa kuchangishana buku buku hautekelezeki Kwa sasa!

ZZK usisahau kuwa jimboni kwako maji tu yanayohitaji bajeti chini ya 20 B yameshindikana kupatikana! Then unatetea 23Trilion ziende Bagamoyo?
Huyu Zito huwa ni mchonganishi hana la maana. Kila alifanyalo JPM yeye analiangalia kwa jicho la husda
 
Back
Top Bottom