Kusugua au kusigina meno wakati mtu yupo usingizini

Kusugua au kusigina meno wakati mtu yupo usingizini

Pole sana Lupituko. Huu sio ugonjwa kama magonjwa mengine. Unahitaji kumuona daktari wa meno kwa ushauri zaidi.
inawezekana kuwa utahitaji kifaa kinachoitwa "occlusal/mouth guard".

Ukisahau kukivua hicho kifaa watu watatoka mbio ofisini wakidhani unabadilika kuwa Zombi.
 
Tafadhali naomba msaada kwa mtu au doctor mwenye uelewa anisaidi kupata ushauri au dawa kwa nini natafuna meno ucku.
Umri nina miaka 50.
Mwanaume.
Naishi na kula vzr , kifupi sina shida ndogo ndogo za kusema labda lishe imepungua.
Nafanya mazoezi na afya yangu ni nzuri na nimepima.
Nimetoa maelezo haya ilimwenye uelewa wa tatizo langu aweze kupunguza wigo wa kujiuliza chanzo cha tatizo langu.
Historia yake.
Natafunaga meno usiku mpaka kelele zinasikika kama vile panya anavyokula vitu ucku mkilala.
Natafuna nikipata usingizi mzito.
Swali.
Je kuna dawa?
Ni ugonjwa?
Nifanyeje.

Huku ni kulika kwa meno kwenye sehemu ambapo meno ya juu na chini hukutana (occlusal surfaces). Katika hali ya kawaida meno hulika sehemu hizi kutokana na kadri yanavyoendelea

kutumika kusaga vyakula. Hali hii huendelea polepole kadri mtu anavyoendelea kuishi (umri), kitaalamu inajulikana kama physiological attrition. Si rahisi kuhisi dalili zake kwani mwili

hujaribu kuziba vitundu vya mifereji midogo inayotoka kwenye kiini cha jino kwenda kwenye sehemu ngumu ya kati (dentine). Ni vitundu hivi ambavyo vikiwa wazi husababisha msisimko

(sensitivity). Kulika kwa meno sehemu ya kusaga huwa ugonjwa pale tu unapotokana na mambo mengine zaidi ya kule kwa kawaida kwa kuongeza umri.


Sababu za kusagika kwa meno (attrition)

Baadhi ya mambo yanayosabisha hali hii ni

Kusaga meno (bruxism):
- hii ni hali ambayo mtu husaga meno yake wakati hatafuni kitu

chochote na mara nyingi mtu huwa hajitambui kama ana tatizo hili. Hali hii mara nyingi

hujitokeza wakati wa usiku mtu akiwa amelala (nocturnal bruxism) japo kwa wachache

wanaweza saga mchana pia. Si rahisi mtu wa namna hii kujitambua mpaka pale

atakapoambiwa na mtu wanayelala pamoja au atakapo kwenda kwa mtaalamu wa meno na

kuelezwa.

Nini husababisha hali hii?

Yapo baadhi ya mambo yanayoweza kusababisha tatizo hili ingawa zaidi linahusishwa na mabadiliko ya kisaikolojia. Watu wenye mawazo mengi wanaonekana kuwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili.

Tatizo hili pia linaweza kutokana na jino lililozibwa na kujazwa zaidi ya kawaida. Mwili hufanya harakati za kupungua sehemu iliyozidi kwa kuisaga na hatimaye kujikuta umejenga mazoea, kiasi kwamba hata jino likisha kuwa kiasi sawa bado mwili utaendelea kusaga tu.

Pia wale wanaokaa kwenye meza kwa muda mrefu wakisoma au vyovyote huku wameshikiria kidevu kwa nguvu, nao ni waathirika wa ugonjwa huu. Katika hali ya kawaida mtu ukiwa

umefunga mdomo umetulia meno ya juu na ya chini huwa hayakutani bali huacha nafasi kama milimita mbili hivi (resting space). Sasa ukiyabana pamoja kwa muda mrefu kwa kushikilia

kidevu, utayafanya yajenge mazoea ya kushikana hata pale ambapo hujashika kidevu na mwishowe kuanza kusagana

Dalili zake na viashiria vyake

Mgonjwa mwenyewe kuhisi msisimko wakati wa kunywa vitu vya baridi, maumivu kama kiwango cha uharibifu ni kikubwa kiasi cha kuacha kiini jino wazi (dental pulp exposure).

Ukiangalia meno utakuta yamelika sehemu ya kutafunia kwenye magego na visaidizi vyake (molars and premolars), sehemu za kukatia na kuchoma kwa meno ya mbele (canines and

incisors). Kusagika huanzia sehemu za meno zilizoinuka (cusps) ambazo hatimaye huondoka kabisa na kuwa bapa au flati. Meno huweza kusagika mpaka wakati mwingine kufikia kwenye

usawa wa fizi. Watu wenye tatizo hili huonekana kuwa na uso wa mraba kutokana na msuli

mkubwa wa kuvuta taya (masseter muscle) kunenepa kutokana na kutumika zaidi. Mgonjwa pia huweza kuchoka kirahisi misuli wakati wa kutafuna katika hali ya kawaida.

Tatizo linaweza kuathiri hata sehemu ya muunganiko wa taya la chini na fuvu

(temporomandibular joint - TMJ). Mgonjwa huweza kusikia maumivu kwenye kiungo (joint) hiki

na wakati mwingine kufyatuka fyatuka (TMJ dislocation) au kutoa sauti wakati wa kufungua na

kufunga kinywa (popping or cricking sound in TMJ).








picha ya juu-kinachoonekana kama kuvimba shavu ni msuli wa kuvuta taya (masseter muscle) ulioongezeka ukubwa

kutokana na kusaga meno. Picha ya chini mwezi mmoja baada ya kupata matibabu ya uhakika, msuli unarudi katika hali

ya kawaida.


Matibabu

Ni vizuri kujua chanzo cha tatizo hili na kukishughulikia kwanza kabla ya kufanya matibabu

zaidi ya meno kurekebisha uharibifu uliotaka na msagiko. Utafiti unaonesha wengi wenye

matatizo haya ni wenye mawazo yaliyozidi kiwango (stress). Lazima ujue kwanini mtu

anawaza sana ili ummpatie ushauri nasaha au hata kumpeleka kwa wataamu wa mambo ya

saikolojia ili waweze kumsaidia.

Wakati hayo yakiendelea inabidi kumfundisha mgonjwa kulegeza taya (relaxation exercise) na

kuachanisha meno kila anapohisi meno ya juu na ya chini yamekutana. Akifanya mazoezi haya

kwa muda mrefu mwili huweza kujenga mazoea kuwa kila meno yakikutana yaachanishwe

(conditioned reflex action). Mgonjwa akiacha kusaga basi matibabu ya kurekebisha madhara

yanaweza kufanyika kwa mafanikio makubwa, iwe kuziba, kuua mzizi wa jino na kuyavalisha

meno kofia ngumu hasa metal reinforced porcelain crown.

Kwa wale ambao ni vigumu kuacha tabia ya kusaga wanaweza kutengenezewa kifaa maalumu

cha kulinda meno wakati wa usiku (night guards), ambacho huvaliwa na mgonjwa usiku wakati

wa kulala kuzuia meno kugusana na baada ya muda atazoea pia na kuacha kusaga. Kifaa hiki

husaidia pia kuondoa matatizo yaliyokwisha jitokeza kwenye jointi.




kifaa cha kukinga meno yasisagane (night guard) mgonjwa akiwa amevaa kifaa

Ni vizuri kumuuliza mwenzako kama amewahi kukusikia ukisaga meno usiku ili uweze kuchukua hatua za kuwaona

wataamu mapema. Kumbuka kujua tatizo mapema na kulitibu ni sehemu ya hatua za kinga.

Niishie hapa kwa leo, siku nyingine nitaongelea aina nyingine za kulika kwa kwa meno kama kuyeyuka kwa meno (tooth

erosion
), abrasion na abfraction wakati huo nitakuwa nimejaribu kupata maelezo ya “abfraction na abrasion”
 
Pole mkuu kwa tazizo lako..
- muone "dentist" atakusaidia...
- atakupima na utatengenezewa "frem" kava ya plastiki unavaa juu ya meno wakati wa kulala...
-tatizo hili mara nyingi husababishwa na msongo wa mawazo...
-athari zake ni kulika kwa "layer" ya juu ya meno hivyo kupata ukakasi mara kwa mara (yaani meno kuwa sensitive sana..
-yupo mtu mwenye tatizo kama lako yeye baada ya kushindwa gharama za hospitali aliamua kufikicha vipande vya magazeti na kuvijaza mdomoni kabla hajalala " ilimsaidia"
Kila la kheri

Ushauri mzuri kabisa..
 
Kuna hili tatizo la mtoto mara nyingine kumsikia kama anatafuna meno kwa sauti kubwa kama vile mtu anayekula mahindi magumu yaliyokaangwa.

Ninaomba kuuliza nini hasa chanzo cha tatizo hili?
Na ni kwa nini iwe ni usiku tena akiwa kwenye usingizi?
Je,tatizo hili linaweza kuishaje?

cc.
MziziMkavu na wengineo naombeni ufafanuzi wa kitaalam kutokana na ujuzi mlio nao
 
Hali hiyo humtokea mwanangu pia, hasa pale anapoumwa. Ngoja tuwasubirie wataalamu watujuze
 
Mwezi wa tatu mwishoni nilimpa dawa ya minyoo.

Basi mkuu jaribu kumpeleka hospital akachekiwe zaidi maana katoto change kalishawah kuwa na hali kama hii tukashauriwa tumpe doz ya minyoo mbona aliacha kabisa kutafuna meno.
 
Basi mkuu jaribu kumpeleka hospital akachekiwe zaidi maana katoto change kalishawah kuwa na hali kama hii tukashauriwa tumpe doz ya minyoo mbona aliacha kabisa kutafuna meno.


Nashukuru sana kwa ushauri wako .Hata hilo la minyoo nitalifanyia kazi.
 
jamani na mim nimeona nichukue furusa hii kuwauliza swala la mtoto kuota MENO mwanangu ana miezi minane lkn hajaota meno nifanye nin
 
WATOTO NA TATIZO LA KUSIGINA MENO:





1%20bruxism%20intro.jpg


Naitwa Kissu K. Mpini, ni mwenyeji wa wilaya ya Ifakara,mkoa wa Morogoro, Tanzania, utakumbuka mara ya mwisho nilivyotoa ushuhuda wangu kuhusu shida ya kusigina/kusaga meno-bruxism ilivyonitatiza kwa muda mrefu bila kupata nafuu, kwa kifupi baada ya kupata huduma pale kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili, Kitengo cha Meno, ninaendelea

vizuri sana kwa sasa, ninalala usingizi vema, na kazi zangu nazifanya vizuri, hakika nimekuwa mwenye furaha kama wenzangu. Utakumbuka nilijiuliza sana kama watoto pia hupata tatizo la kusigina meno kama inavyotokea kwa watu wazima, hivyo ili kukata mzizi wa fitina, nilimwandikia barua daktari aliyenihudumia pale Muhimbili siku ile, nimeona ni

vema pia elimu aliyonipatia daktari nishirikishe wadau wengine, maana sio wote tunaweza kufika Muhimbili kirahisi, vilevile ninaamini kuwa yeyote atayeweza kusoma maelekezo haya ya daktari itakuwa ni msaada mkubwa sana kwake binafsi, familia na rafiki zake. Majibu ya daktari yamebainisha kwa kirefu kuhusu tatizo la kusigina meno linavyoathiri watoto, ifuatayo ni barua ya daktari kama alivyoniandikia.

Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 20 ya watoto kati ya mwaka 1 hadi miaka 11 husumbuliwa na kusigina/kusaga meno tatizo ambalo kwa kitaalamu linajulikana kama Bruxism. Ingawa takwimu hii inakadiriwa kuwa chini ya hali halisi kwa vile wazazi wengi wanashindwa kutambua tatizo hili kwa watoto wao. Kama ilivyo kwa watu wazima kwa vyanzo mbalimbali

vinavyosababisha kusigina meno, kwa watoto dalili za tatizo hili zinafanana sana na matatizo mengine ya watoto hivyo inawawia vigumu wazazi ama walezi kutambua tatizo hili na hata kupuuzia.
Kusigina meno kwa watoto kunasababishwa na mihemko usiku-nocturnal arousal- na hugawanywa kama tatizo la

usingizi-sleeping disorder-, vile vile kusigina meno husababishwa na mwitikio-response- wa mihemko ya usiku ambayo inashabihiana na matatizo ya usingizi-sleeping disorders- Tatizo hili mara nyingi huwapata watoto ambao huwa na shida ya kupumua vizuri hivyo hupumua kwa kutumia mdomo, watoto walio na vivimbe vya tezi-adenotonsillat hypertrophy-, watoto wenye tatizo la kuziba kwa njia ya hewa wanapokuwa usingizini-obstructive sleeping apnoea,

watoto wenye tatizo la meno kuota kwa mpangilio mbaya-dental occlusion- pamoja na watoto wenye matatizo ya akili ama mtindio wa ubongo. Vile vile tatizo hili hushabihishwa na tatizo la ungano la taya na fuvu temporomandibula joint disorder pamoja maumivu ya kichwa yasiyokoma.

Matokeo ya kusigina meno kwa watoto mara nyingi hujitokeza kwenye mabadiliko ya tabia na mwenendo wa mtoto kwa sababu ya mihemko na mwitikio wake unaomsumbua akiwa amelala usiku. Tafiti zimeonesha kuwa watoto wenye tatizo la kusigina meno hutatizwa na hofu, mashaka na kukosa utulivu kwenye mambo ya kawaida sana. Tatizo hili la

kusigina meno pia linahisianishwa na Tatizo la kukosa utulivu kitaalamu linajulikana kama Attention Deficit Hyperactivity Disorder (ADHD). Utafiti mwingine ulionesha kuwa tatizo la kusugua meno kwa watoto linashabihiana na msongo wa mawazo kwa mama wakati akiwa mjamzito. Wazazi ambao wameripoti kuwa na tatizo la akili ama mwili , watoto wao pia wameripotiwa kuwa na tatizo la mabadiliko ya tabia mara kwa mara pamoja na mihemko nyakati za usiku.
2%20bruxism%202.jpg


Matukio ya kusigina meno kwa watoto hudumu kwa sekunde 4 na hutoke kwa wastani wa mara 6 ndani ya saa 1. Matukio haya huwa na kawaida ya kutokea kwa mafungu usiku mzima huku yakiwa na nguvu zaidi kwenye hatua ya pili ya usingizi ambayo kitaalamu hujulikana kama Stage 2 and REM sleep. Utafiti mwingine umeonesha kuwa asilimia 60 ya

matukio ya kusigina meno huambatana na mihemko, ilhali asilimia 40 ya watoto waliojumuishwa kwenye utafiti huu waliripotiwa kuwa na tatizo linalohitaji uangalizi wa tiba wa karibu ama tatizo la kubwa la tabia.
Ni vigumu sana kutambua ikiwa kusigina meno kunasababishwa na mihemko na uangalizi wa karibu na tatizo la tabia,

ama ikiwa watoto wanaopata uangalizi wa karibu na tatizo la tabia wanapata shida ya usingizi pamoja na kusigina meno. Hata hivyo, inafahamika kuwa usingizi wa mafungu unaosababishwa na kupumua kwa mtoto akiwa usingizini kunaweza kusababisha matatizo ya tabia, kujali na utawala wa kazi za mwili kwa mtoto.

Kuna uhusiano mkubwa baina ya kusigina meno na kuziba kwa sehemu ya juu ya njia ya kupitisha hewa. Kuvimba kwa tezi-tonsillar hyperplasia- ni moja ya chanzo kikubwa kinachosababisha tatizo la kupumua ukiwa usingizini.hewa.

Watoto wanaopumua kwa mdomo mara nyingi huwa na tatizo la kuvimba kwa tezi ambazo huziba sehemu ya juu ya njia ya hewa. Inaaminika kuwa kuzibwa kwa njia ya hewa wakati ukiwa usingizini husababisha kuongezeka kwa msuguano baina ya misuli ya taya, meno na baina ya mifupa ya taya la juu na chini.

Kuziba kwa njia ya hewa kwa watoto husababisha watoto kusukuma taya la chini mbele kwa nguvu ili waweze kuvuta hewa, kufanya hivi kunachokoza vihisishi vya fahamu kwenye sehemu ya juu ya njia ya hewa hivyo kusababisha kusigina meno. Kukoroma na kupumua kwa mdomo ni dalili ya watoto kuwa na tatizo ambalo mara nyingi wazazi huwa hawajali sana, kwa sababu hii tatizo la kuziba kwa njia ya hewa wakati mtoto yupo usingizini huchelewa kutambuliwa na kutibiwa kwa miaka mingi.

Utafiti uliofanyika kulinganisha tatizo la kusigina meno kwa watoto kabla na baada ya upasuaji wa vivimbe vya tezi vilivyosababisha kuziba kwa sehemu ya juu ya njia ya hewa, ulionesha kuwa watoto wote walikuwa na wastani wa asilimia 75 ya kuziba kwa njia ya hewa kabla ya upasuaji. Miezi mitatu baada ya upasuaji , watoto wote waliokuwa na

tatizo la kupumua vizuri, walikuwa wametibiwa vema,na hivyo kupunguza tatizo la kusigina meno kwa kiasi kikubwa sana, ingawa asilimia 24 kati yao hawakuacha tabia ya kupumua kwa kutumia mdomo-mouth breathing.
Hii ilikuwa ni barua ya daktari akinijulisha uwepo wa tatizo la kusigina meno miongoni mwa watoto, ambapo kwa kifupi

ameandika kuwa vyanzo na madhara ya kusigina meno kwa watoto havina tofauti na wakubwa, ametaja vyanzo hivi kuwa ni mihemko usiku-nocturnal arousal- , mwitikio wa mihemko-arousal response ambayo inashabihiana na matatizo ya usingizi, vilevile kusigina meno hutokea miongoni mwa watoto ambao huwa na shida ya kupumua vizuri hivyo

hupumua kwa kutumia mdomo, watoto walio na vivimbe vya tezi-adenotonsillat hypertrophy-, watoto wenye tatizo la kuziba kwa njia ya hewa wanapokuwa usingizini-obstructive sleeping apnoea, watoto wenye tatizo la meno kuota kwa mpangilio mbaya-dental occlusion- pamoja na watoto wenye matatizo ya akili ama mtindio wa ubongo. Tatizo la ungano la taya na fuvu temporomandibula joint disorder pamoja maumivu ya kichwa yasiyokoma navyo husababisha tatizo la kusigina meno kwa watoto.

Matokeo ya kusigina meno kwa watoto mara nyingi hujitokeza kwenye mabadiliko ya tabia na mwenendo wa mtoto kwa sababu ya mihemko na mwitikio wake unaomsumbua akiwa amelala usiku.

Katika barua yake, daktari ameshauri kuwa ni vema wazazi wasipuuzie wanapoona watoto wao wanakoroma wawapo usingizini, ama wanapopumua kwa kutumia mdomo, pia daktari ameelekeza kuwa, upasuaji wa tezi zilizovimba ni tiba kwa tatizo la kusigina meno kwa watoto.http://tanzmed.com/index.php?option...:watoto-na-tatizo-la-kusigina-meno&Itemid=175
Mungu akubariki sana
 
Back
Top Bottom