Kutembewa na kitu mwilini

Mine eyes

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2016
Posts
6,496
Reaction score
7,162
Habari wakuu
Nahitaji msaada wenu hata kwa hili tatizo kuna mtoto wa dada yangu age 9 1/2...siku za karibuni aliwahi kusema huwa anajisikia baridi ya ghafla mwili mzima..na inakuja na kupotea katika mda mfupi.

Halafu kuna kitu kinamtembea mwilini kuanzia kichwani kushuka chini anakihisi na anaweza kueleza kwa kuonesha kipo wapi kwa mda ule mimi mwenyewe nimeona sehemu kinapotembea panakuwa panatuna kitu na kinakwenda kweli. bàada ya kuzunguka mwili wote huwa kinarudi na kutulia tumboni mda huo kikitembea kwenye mishipa ya damu huwa anaskia maumivu...


Mawasiliano wakuu nahitaji msaada kwa anayejua hili ni tatizo gani maana sijawahi hata kusikia!
 
Nani mwenye tatizo? Wewe au mtoto wa dada?
 
Poleni sana
 

damu kuwa chafu nayo ni tatizo
 
Mmmmmh poleni sana Mkuu
 
Kama ni mkristo mpeleke apate maombi huyo mtoto mfunge na kukesha.. pia kama mwislam mna swala zenu kutoa madudu kama hayo..hiyo sio damu chafu bali ni maroho na madudu machafu yanamsumbua huyo mtoto...
 
Kama ni mkristo mpeleke apate maombi huyo mtoto mfunge na kukesha.. pia kama mwislam mna swala zenu kutoa madudu kama hayo..hiyo sio damu chafu bali ni maroho na madudu machafu yanamsumbua huyo mtoto...
Asante mkuu kwa ushauri mzuri....

maana..

Wiki ilopita tulimpeleka hospital hawakuona kitu .akapewa dawa tu.
 
Asante mkuu kwa ushauri mzuri....

maana..

Wiki ilopita tulimpeleka hospital hawakuona kitu .akapewa dawa tu.
Mm naiman mnachezewa na mtu hapo.. hilo tukio la ajabu sana.. na isitoshe msiwe na haja ya kumjua nani mbaya wenu muhimu mtoto apone.. hosp kama wakisema operations itafanyikaje kutoa hiko kitu ambacho kinatembea kwa spidi si mtamtoboa mtoto mwili wote..!!# ni mawazo yangu huyo anahitaji maombi au swala kwa wale waislamu sijui ni dua au nn atapona tu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…