Kuteua Watu walewale ni dalili kuwa nchi haina Rasilimali Watu

Kuteua Watu walewale ni dalili kuwa nchi haina Rasilimali Watu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Habari za Sikukuu ya Pasaka!

Moja ya dalili kubwa kuwa taifa fulani halina rasilimali Watu ni kwa kuangalia safu ya viongozi na watawala.

Ukiona Watu wanaoteuliwa ni walewale yanaitwa miaka nenda rudi Watu ni walewale basi sababu kubwa ya jambo hilo ni kuwa nchi Hiyo haina Rasilimali Watu. Tunaposema Rasilimali Watu tunazungumzia watu wenye Tija, ili mtu awe Rasilimali inampasa awe na Tija.
Ndio maana kuna Miti na mitishamba. Miti yenye tija na matumizi ndio huitwa mitishamba.

Sababu ya pili, ni Ufisadi. Hapa nazungumzia kulindana. Únamteua huyu kisha unamuweka pembeni, kisha baadaye únamteua tena. Alafu naye atakuteua akiwa juu yako. Kisaikolojia na kisosholojia, Watu wanaolindana hu-share pia uhalifu.
Wenye Haki hawalindani. Kwa sababu Haki ndio ulinzi wenyewe.

Nchi au taifa linaloteua Watu walewale au kuongozwa na Watu walewale haliwezi kukwepa Ufisadi.
Huwezi kuwa Fisadi sehemu ambayo viongozi au watawala hawajirudii mara kwa mara au wanabadilika badilika.
Kuteuana teuana huunda undugu katika uhalifu.

vyombo vya Dola haviwezi kuwa na nguvu Katiak nchi au taifa linalochagua Watu walewale. Nguvu ya chombo cha Dola itakuwa juu ya Raia wanyonge na watawaliwa.

Kuteuana kwa Watu walewale ni kula Yamini. Kiapo cha damu cha kulindana.

Raia wa kawaida huna uwezo wa kumshitaki kiongozi katika taifa linaloteua Watu walewale. Utaishia kupoteza muda wako na gharama ngumu unaweza kuzipata.

Taifa la viongozi wanaoteuana kila mara yaani wao ni kila siku huwezi kumkuta Kiongozi amefungwa Jela.
Atafungwa na nani? Ni kweli kabisa amefanya kosa na anaweza kukiri hadharani kabisa kuwa kafanya kosa. Lakini nani wa kumfunga?
Hakimu au Jaji? Thubutu!
Vyombo vya Dola? Haupo serious!

Ushaambiwa chombo cha Dola sio chombo cha wananchi. Kipo kwajili ya serikali na sio wewe mwananchi. Hapa nazungumzia kwenye taifa au nchi ambayo viongozi miaka nenda rudi ni walewale.

Taifa la kuteuana walewale huzalisha watumwa, Machawa na waabudu viongozi ili nao waonekane. Ni jamii ya hovyo ndio maana nikasema haina rasilimali Watu.

Haiwezikaniki wala haiingii Akilini taifa la Mamilioni ya Watu ati Watu wawe walewale. Hiyo haiwezekaniki bila sababu hizo hapo juu.

Acha Nipumzike sasa. Nipo Maeneo ya Mlimani City. Karibuni Sikukuu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Wameenda mbali zaid, sasaivi wana-rithishana nafasi za uongozi.

KEKI YA TAIFA NI TAMUU SANA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Watu wapo, tatizo ni uzembe wa mfumo tulionao kuongoza nchi, kama nchi inaongozwa na mfumo uliochoka basi ni lazima utuletee watu walewale waliochoka, ajabu nasi taratibu tunaanza kuingia kwenye mfumo uliochoka kwa kushangilia teuzi zile zile za watu waliochoka tukitarajia maajabu.
 
Watu wapo, tatizo ni uzembe wa mfumo tulionao kuongoza nchi, kama nchi inaongozwa na mfumo uliochoka basi ni lazima utuletee watu walewale waliochoka, ajabu nasi taratibu tunaanza kuingia kwenye mfumo uliochoka kwa kushangilia teuzi zile zile za watu waliochoka tukitarajia maajabu.
Tulishawaambia ccm inaendeshwa kwa cartel system..hakuna chama hapo, ni kikundi cha watu wachache kinashikiliwa na mercenaries, nadhani unaelewa..walishawaona watz vipofu hawawezi kuona kitu chochote nyuma ya pazia, wamepumbazika na maigizo ya hapa mbele..kina makonda, kigogo, usimba, uyanga nk
 
Habari za Sikukuu ya Pasaka!

Moja ya dalili kubwa kuwa taifa fulani halina rasilimali Watu ni kwa kuangalia safu ya viongozi na watawala.

Ukiona Watu wanaoteuliwa ni walewale yanaitwa miaka nenda rudi Watu ni walewale basi sababu kubwa ya jambo hilo ni kuwa nchi Hiyo haina Rasilimali Watu. Tunaposema Rasilimali Watu tunazungumzia watu wenye Tija, ili mtu awe Rasilimali inampasa awe na Tija.
Ndio maana kuna Miti na mitishamba. Miti yenye tija na matumizi ndio huitwa mitishamba.

Sababu ya pili, ni Ufisadi. Hapa nazungumzia kulindana. Únamteua huyu kisha unamuweka pembeni, kisha baadaye únamteua tena. Alafu naye atakuteua akiwa juu yako. Kisaikolojia na kisosholojia, Watu wanaolindana hu-share pia uhalifu.
Wenye Haki hawalindani. Kwa sababu Haki ndio ulinzi wenyewe.

Nchi au taifa linaloteua Watu walewale au kuongozwa na Watu walewale haliwezi kukwepa Ufisadi.
Huwezi kuwa Fisadi sehemu ambayo viongozi au watawala hawajirudii mara kwa mara au wanabadilika badilika.
Kuteuana teuana huunda undugu katika uhalifu.

vyombo vya Dola haviwezi kuwa na nguvu Katiak nchi au taifa linalochagua Watu walewale. Nguvu ya chombo cha Dola itakuwa juu ya Raia wanyonge na watawaliwa.

Kuteuana kwa Watu walewale ni kula Yamini. Kiapo cha damu cha kulindana.

Raia wa kawaida huna uwezo wa kumshitaki kiongozi katika taifa linaloteua Watu walewale. Utaishia kupoteza muda wako na gharama ngumu unaweza kuzipata.

Taifa la viongozi wanaoteuana kila mara yaani wao ni kila siku huwezi kumkuta Kiongozi amefungwa Jela.
Atafungwa na nani? Ni kweli kabisa amefanya kosa na anaweza kukiri hadharani kabisa kuwa kafanya kosa. Lakini nani wa kumfunga?
Hakimu au Jaji? Thubutu!
Vyombo vya Dola? Haupo serious!

Ushaambiwa chombo cha Dola sio chombo cha wananchi. Kipo kwajili ya serikali na sio wewe mwananchi. Hapa nazungumzia kwenye taifa au nchi ambayo viongozi miaka nenda rudi ni walewale.

Taifa la kuteuana walewale huzalisha watumwa, Machawa na waabudu viongozi ili nao waonekane. Ni jamii ya hovyo ndio maana nikasema haina rasilimali Watu.

Haiwezikaniki wala haiingii Akilini taifa la Mamilioni ya Watu ati Watu wawe walewale. Hiyo haiwezekaniki bila sababu hizo hapo juu.

Acha Nipumzike sasa. Nipo Maeneo ya Mlimani City. Karibuni Sikukuu.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa kujuana juana na kwa fadhila fadhila labda ?!
Au ni vipi ?
 
That means
Watu wapo ila kwa siasa zetu ni risk sana kuingiza mtu mpya kwenye mfumo. Hujui ataleta nini, Sasa inakuwa bora shetani umjuaye.
bora liende tu style ?!
 
Hapana.

Nchi ina rasilimali watu nyingi tu lakini huwezi kumantain dola kama utakua unawapa position random people. Ili uweze kubaki na madaraka inabidi uwape watu unaowafahamu na unaowamudu position nyeti ili uendelee kuwa na control.

Si unaona mjomba alivyoingia ni almost dola iliwaponyoka wale mabwana kwa sababu hawakujua mshua atakua that unpredictable??

Sema kwa mtizamo wangu, nafasi zote za kiutendaji zingezingatia merits na sio utaratibu huu wa sasa. Nafasi za wakurugenzi wa halmashauri, wakurugenzi wakuu wa mashirika ya umma, wakuu wa taasisi mbali mbali etc walitakiwa washindanie hizo nafasi na mwenye uwezo, ujuzi, ubunifu, maarifa na uzoefu stahiki apewe na apimwe based on results na akishindwa taratibu ziwe wazi.

Otherwise mtaja skia kijana mdogo, graduate wa Petroleum Engineering mwenye zero exposure, zero experience na industry atapewa uDG wa TPDC kwa sababu ni wa kwetu ili akafundishwe basics na subordinates wake. Wakati utaratibu ni kuwa alitakiwa aanzie chini na apande kwa kuonesha uwezo.

 
Ni dalili za utwala mbovu uliojaa umimi, ufamilia, undugu, urafiki na upendeleo.

Appointments are not based on meritocracy.
 
Hao Watu wangekuwepo pasingekuwepo huo uzembe wa Mfumo.

Mfumo uliopo ndio mfumo sahihi. Kwa aina ya Watu waliopo
Ili tupate mabadiliko ya kweli inabidi turudi kwenye factory reset, aidha kutokee machafuko, ama mapinduzi ya kijeshi, kisha katiba mpya kutokana na rasimu ya Wariob. Kinyume na hapo tungoje Mwigulu awe rais Hadi amrithishe mtoto wake.
 
Watu wapo ila kwa siasa zetu ni risk sana kuingiza mtu mpya kwenye mfumo. Hujui ataleta nini, Sasa inakuwa bora shetani umjuaye.
Risk inaanzia kwenye katiba yetu mbovu na style ya watanzania kuwa watu wa hewala hewala. Uoga na unafiki ndo unaotuponza na utatutesa vizazi kwa vizazi. Mtu anaona akisema ukweli na kusimama imara katika kweli atachukiwa kwahio anachagua kukaa kimya na kulalamikia chooni.

Nchi hii haiwezi kubadilika na hali kuwa tofauti kama raia hawatabadilika mindset mfumo utaendelea kuwa ule ule wa kupachikana kwenye madaraka watu wale wale na familia zao.

Mtu akila mihogo na watoto wake anaridhika anaona ndio maisha yale 😂 akiumwa anaenda hospitali za huduma mbovu watoto shule za hovyo usafiri shida kila kitu cha kipuuuzi tu. Wakati watawala wao wanahodhi mabilioni kama vile ma foreigner kumbe wabongo wenzetu na hawajali kuhusu watanzania maskini.
 
Back
Top Bottom