Kuteuliwa na mamlaka za nchi ni heshima kubwa, anayekataa basi kuna maovu anataka kuficha kwenye nafasi aliyo nayo

Kuteuliwa na mamlaka za nchi ni heshima kubwa, anayekataa basi kuna maovu anataka kuficha kwenye nafasi aliyo nayo

Una hoja muhimu na kimsingi nakubaliana na wewe ila tukumbuke mambo kadhaa wakati tunalitafakai hili:

1. Mambo ya watu kuteuliwa na kutangazwa kabla hawajaambiwa hayajaanza leo. Nakumbuka kwa mbali story ya John Malecela kupewa taarifa ya kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Serikali za Tanzania kubadilisha tararibu zake za kufanya kazi huwa ni ngumu sana ndiyo maana mpaka leo tunakalishana barabarani masaa kusubiri viongozi wapite bila kujua dunia imebadilika, idadi ya raia pia imeongeeka mno kwa hiyo utaratibu huo unaleta karaa kuzidi zamani.

2. Vyeo vya Mkuu wa Wilaya na Mkoa ni purely vya kisiasa, wanateuliwa kisiasa na wanakwenda kufanya kazi za kisiasa. Kwa muktadha huo kuna watakaokwambia Rais hawezi kujishusha na "kujikomba" kwa mtu ambaye kimsingi anakwenda kuwa mwakilishi wake katika wilaya au mkoa. Kuna suala hapa la nani amsujudie mwenzie. Hilo unalosema nadhani linafanyika pale mteuliwa anapotolewa kwenye sekta binafsi au ni jobless ila kama tayari uko ndani ya mfumo wa ajira serikalini sioni mfumo wetu ukiadapt hilo unalopendekeza (ingawa kiungwana linatakiwa kufanyika kama unavyosema). Kuna hali ya Serikali kujaribu kuviongezea thamani hivi vyeo vilivyopitwa na wakati mfano kwa kuwa na hizi "elements of surprises" wakati wanavyoteuliwa. Wewe hauoni jinsi Nyuzi za Teuzi zinavyokuwaga maarufu humu? Watanzania kwa ujumla wetu tunathamini sana vyeo.

3. Wengi tunajua CWT imekuwa compromised muda mrefu sana na ni kama wamekuwa wanatimiza matakwa ya Serikali badala ya kusimamia maslahi ya waalimu. Kuwatoa viongozi wao kwa mkupuo ni ama serikali ilianza kupoteza ushawishi ndani ya CWT wakataka kufanya mabadiliko ya haraka (labda hawa hawakuwa watu wao) au Serikali ilishawachukulia poa CWT wakajisahau tu wakijua "hawa ni wanetu".

Nadhani issue kubwa hapa ni kwa nini Serikali haikuzingatia nyazfa za hawa wateule ndani ya CWT na kwamba wana majukumu makubwa ambayo kimsingi ni kuisimamia serikali kuhusiana na masuala ya waalimu. Kuwatoa pale tena kwa mkupuo kunaweza kutafsiriwa kama njia ya kuidhoofisha CWT. Wangekuwa waalimu tu wa kawaida ingekuwa story nyingine.
Mkuu,

1. Speaking of Malecela, Nyerere alitaka kumteua Malecela kuwa PM, Malecela akaambiwa na watu wa system, akafanya bonge la party, kabla hajatangazwa, Nyerere akaona huyu sijamtangaza kafanya party, nikimtangaza si ndo itakuwa balaa? Akaghairi.

Serikali ya Nyerere ilikuwa si tu unapewa taarifa kabla ya uteuzi, bali hata unapopewa taarifa unakuwa bado unaangaliwa.

2. Mimi naona kama vyeo wanataka kuviongezea thamani, basi wateule wangepata hata ka simu tu ka kutoka Ikulu, si lazima itoke kwa rais, mfanyakazi tu wa kawaida wa Ikulu anaweza kupiga simu ku verify kwamba mteule mzima, na rais angependa kujua mtu huyo akipewa heshima ya kulitumikia taifa katika nafasi ya ukuu wa wilaya atakubali?
Majority ya watu wangefurahi sana kupata simu hiyo na inge wa motivate sana kwenye kazi. Ikulu ime miss opportunity kuwa motivate watu hapo.

3. CWT teuzi zimetumika kumaliza migogoro, nimelitaja hapo juu (post #57 na #60). Hili jambo baya kwa sababu kama nafasi ya ukuu wa wilaya ina umuhimu, tunaifanya kama chaka la kumalizia migogoro tu. Kama haina umuhimu isiwepo kabisa.
 
Mkuu,

1. Speaking of Malecela, Nyerere alitaka kumteua Malecela kuwa PM, Malecela akaambiwa na watu wa system, akafanya bonge la party, kabla hajatangazwa, Nyerere akaona huyu sijamtangaza kafanya party, nikimtangaza si ndo itakuwa balaa? Akaghairi.

Serikali ya Nyerere ilikuwa si tu unapewa taarifa kabla ya uteuzi, bali hata unapopewa taarifa unakuwa bado unaangaliwa.

2. Mimi naona kama vyeo wanataka kuviongezea thamani, basi wateule wangepata hata ka simu tu ka kutoka Ikulu, si lazima itoke kwa rais, mfanyakazi tu wa kawaida wa Ikulu anaweza kupiga simu ku verify kwamba mteyule mzima, na rais angependa kujua mtu huyo akipewa heshima ya kulitumikia taifa katika nafasi ya ukuu wa wilaya atakubali?
Majority ya watu wangefurahi sana kupata simu hiyo na inge wa motivate sana kwenye kazi. Ikulu ime miss opportunity kuwa motivate watu hapo.

3. CWT teuzi zimetumika kumaliza migogoro, nimelitaja hapo juu. Hili jambo baya kwa sababu kama nafasi ya ukuu wa wilaya ina umuhimu, tunaifanya kama chaka la kumalizia migogoro tu. Kama haina umuhimu isiwepo kabisa.
Hiyo ya Malecela ninayoongelea ni tofauti kidogo ingawa nimeisahau kidogo. Nadhani alipata taarifa kupitia kwenye Radio, labda cheo kilikuwa ni kingine.

Nadhani unaposema watu wataarifiwe kabla, hii inaweza kuwa applicable pale mtu anapotokea nje ya mfumo wa Serikali. Ukisema iwe ndiyo general procedure ya serikali, inaweza kuleta ukiritimba katika uteuzi, tetesi zitakuwa zinazidi maana hakutakuwa na jinsi ya kudhibiti taarifa za teuzi kutoka kabla ya wakati, nk. Pia imagine kila mawaziri wakiwa wanahamishwa kutoka Wizara moja hadi nyingine wawe wanaulizwa kwanza, hiyo backlog ya kusubiri watu itakuwa kubwa. Wazo lako ni zuri kakini sidhani kama liko practical sana hasa kwa nchi yetu ambapo si wengi wenye options nzuri kuliko teuzi hizi wanazopewa.

Kimsingi nadhani tupunguze vyeo vya kuteuliwa na tutafute tararibu zingine za kupata watendaji na tuwe na verification system mfano kupitia Bunge kabla ya kuwaidhinisha.
 
Hiyo ya Malecela ninayoongelea ni tofauti kidogo ingawa nimeisahau kidogo. Nadhani alipata taarifa kupitia kwenye Radio, labda cheo kilikuwa ni kingine.

Nadhani unaposema watu wataarifiwe kabla, hii inaweza kuwa applicable pale mtu anapotokea nje ya mfumo wa Serikali. Ukisema iwe ndiyo general procedure ya serikali, inaweza kuleta ukiritimba katika uteuzi, tetesi zitakuwa zinazidi maana hakutakuwa na jinsi ya kudhibiti taarifa za teuzi kutoka kabla ya wakati, nk. Pia imagine kila mawaziri wakiwa wanahamishwa kutoka Wizara moja hadi nyingine waulizwe. Wazo lako ni zuri kakini sidhani kama liko practical sana.

Kimsingi nadhani tupunguze vyeo vya kuteuliwa na tutafute tararibu zingine za kupata watendaji na tuwe na verification system mfano kupitia Bunge kabla ya kuwaidhinisha.
Unaweza kuweka mfumo watu wanataarifiwa, hata kama ni muda mfupi tu kabla ya kutangazwa, wakajua kwamba mpaka unataarifiwa bado upo kwenye vetting, na mteuzi akisikia umevujisha habari, anakuona huna kifua anaghairi, kama alivyofanya Nyerere kwa Malecela.

Ukisoma kitabu cha Mkapa "My Life, My Purpose", ameeleza kabisa jinsi Nyerere alivyokuwa anamuita, anaongea naye, anamwambia anataka kumpa kazi fulani, tena kazi za kimataifa balozini. Nyerere alijua umuhimu wa kuwasiliana na watu kabla ya teuzi, hususan mawaziri nyeti. Hizi cabinet reshuffle unaweza kumbadili mtu tu kwa sababu ile si appointment mpya ni reshuffle tu. Hata kwa wakuu wa wilaya ingewezekana kufanyika hivyo, not necessarily from the president, but from te Ikulu bureaucracy.

Kuhusu point yako ya mwisho, hivi vyeo vya ukuu w awilaya mimi hata sielewi umuhimu wake. Ni kama vimekaa kuongeza posts tu za rais kuchomeka watu wake anaowataka kwa siasa zake.
 
Au hukubaliani na sera za aliyekuteua na hutaki kuwa sehemu ya yale anayofanya.
 
Unaweza kuweka mfumo watu wanataarifiwa, hata kama ni muda mfupi tu kabla ya kutangazwa, wakajua kwamba mpaka unataarifiwa bado upo kwenye vetting, na mteuzi akisikia umevujisha habari, anakuona huna kifua anaghairi, kama alivyofanya Nyerere kwa Malecela.

Ukisoma kitabu cha Mkapa "My Life, My Purpose", ameeleza kabisa jinsi Nyerere alivyokuwa anamuita, anaongea naye, anamwambia anataka kumpa kazi fulani, tena kazi za kimataifa balozini. Nyerere alijua umuhimu wa kuwasiliana na watu kabla ya teuzi, hususan mawaziri. nyeti. Hizi cabinet reshuffle unaweza kumbadili mtu tu kwa sababu ile si appointment mpya ni reshuffle tu. Hata kwa wakuu wa wilaya ingewezekana kufanyika hivyo, not necessarily from the president, but from te Ikulu bureaucracy.

Kuhusu point yako ya mwisho, hivi vyeo vya ukuu w awilaya mimi hata sielewi umuhimu wake. Ni kama vimekaa kuongeza posts tu za rais kuchomeka watu wake anaowataka kwa siasa zake.
Utajuaje amevujisha yeye? Mpaka umeanza kuchunguza, utawachunguza wangapi? Point yangu inaweza kuwa inaleta mkanganyiko ambao kwa utaratibu wa sasa haupo. Mwingine wabaya wake wanaweza kuvujisha kwa makusudi ili kumharibia, nk.

Vyeo vya wakuu wa wilaya na mkoa zina umuhimu mkubwa kwa CCM. Ni layer nyingine ya kimamlaka inayotumika kuhakikisha maslahi ya chama yanalindwa. Pia wanatumika kuwatambua mapema watu wanaoweza kukisaidia chama au kukiletea chama shida mbele ya safari. Kwa maslahi ya taifa ni vyeo visivyo na maana ila kichama vina maana kubwa sana. Kimsingi Serikali inatumia rasilimani zake kuwalipa watendaji ambao kazi yao ya msingi ni ya chama.
 
Mheshimiwa rais anajua mapato Yao hata kabla hajawateua Ila aliwateua kwa manufaa mapana ya taifa.
Ngoja tuwafanyie audit kidogo tu tuone Nani mjanja.
Kwani lazima kufanya kazi na WAHUNI? Suluhisho ni katiba mpya sasa
 
Kama umeteuliwa ni kwamba umekidhi vigezo kwa maana una sifa stahiki lakini pia umepewa heshima kubwa na Mamlaka iliyokuteua.

Jiulize kuna Watanzania wangapi wenye sifa zaidi yako lakini hawakupewa nafasi hiyo?

Vyombo vya habari vimetoa taarifa kuna Watu wamekataa Heshima waliyopewa na Mamlaka ya Uteuzi.
Itoshe kusema watu hawa kama ni kweli wapo hawana chembe ya uzalendo hata kidogo, umetumwa ukawatumikie Watanzania ukiwakilisha Mamlaka ya Uteuzi unakataa na bado unataka uendelee kwenye nafasi yako ya sasa?

Kuna mambo yanatakiwa kutiliwa shaka kwa watu hawa ikiwa ni pamoja na

1. Yawezekana nafasi walizopo sasa kuna maovu mengi wamefanya hivyo wanaogopa kuachia ghafla mengi yataibuka.

2. Yawezekana kile wanacholipwa ni kikubwa sanaa kuliko wanavyostahili, Wote tunajua Waajiri wao ni Wanachama. Je Wanacholipwa kama Mshara na Stahiki nyingine zinalingana na Waajiri wao?

3. Waajiri wa hawa watu (Wanachama) Je, ni kweli wanawapima utendaji wao kwa Maana ya Investment zinazofanyika chini ya Chama Chenu? Tutakuwa na Michango isiyokoomaa au tutafute uwezekezaji wenye tija na tupunguze michango?

Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania

Mwenyezi Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

View attachment 2501128
Ficha ujinga wako
 
“Nitampa ofa asiyoweza kuikataa”.

Lakini wao wameikataa!

Labda wameona hatima ya Godmother iko mashakani.
 
mkuu inasikitisha ila unaonekana umeweka imani yako na future yako kwa Gov sana...but maisha ni zaidi ya kufanya kazi Gov..siku ukitoka kwenye hilo gereza utaona life is full of enjoyable things kuliko kuwaza ajira na teuzi za Gov.
Mie siko huko Gov
Ila nawazungumzia wahusika wa hii mada walioko Gov

Nafikiri kwa ajira zao zilivyo hawapaswo kumkatalia mwajiri wao labda wajifute utumishi

Wa private huku no rahisi tunaendelea na maisha yetu

Si kama sijui life is good
Life is gooood anywhere
Ni wewe tu kujiset
Ukae unawaza uteuzi wanakujua??
 
Kwani lazima?

Kutangaza uteuzi kabla ya kupata ridhaa ya mteule ni dharau na ujinga.
Labda kama umejiajiri
Kwenye ajira huko ni mwendo wa kupangiwa vituo hadi akili ziwakae watu sawa
Hutaki jiajiri ujipangie
 
Utajuaje amevujisha yeye? Mpaka umeanza kuchunguza, utawachunguza wangapi? Point yangu inaweza kuwa inaleta mkanganyiko ambao kwa utaratibu wa sasa haupo. Mwingine wabaya wake wanaweza kuvujisha kwa makusudi ili kumharibia, nk.

Vyeo vya wakuu wa wilaya na mkoa zina umuhimu mkubwa kwa CCM. Ni layer nyingine ya kimamlaka inayotumika kuhakikisha maslahi ya chama yanalindwa. Pia wanatumika kuwatambua mapema watu wanaoweza kukisaidia chama au kukiletea chama shida mbele ya safari. Kwa maslahi ya taifa ni vyeo visivyo na maana ila kichama vina maana kubwa sana. Kimsingi Serikali inatumia rasilimani zake kuwalipa watendaji ambao kazi yao ya msingi ni ya chama.
Vyeo vifutwe na hilo litampunguzia rais kazi za uteuzi.

Mlipa kodi naye atapunguziw amzigo wa viongozi wasio na maana.
 
Boss una mawazo mazuri sana: Ila nakukumbusha uzingatie hizi principle mbili,
1:Boss hakosei
2:Endapo boss akikosea rejea principle namba 1.
Kwahiyo hao ndg zetu wanaweza kupoteza vyote kwa pamoja. Mfano tu mdogo mimi nimpe kazi ya kufanya mwanangu halafu akatae aniambie mimi hiyo kazi sitaki nina kazi nyingine na wakati huo kazi zote ziko chini ya mamlaka yangu, sitakubali, huo ni utovu wa nidhamu wa kiwango cha juu
Nashangaa watu wanavyopuyanga kwenye hii ishu
 
Labda kama umejiajiri
Kwenye ajira huko ni mwendo wa kupangiwa vituo hadi akili ziwakae watu sawa
Hutaki jiajiri ujipangie
Mimi nilishasema sitafanya kazi za serikali ya Tanzania maisha yangu yote.

Sitaki ujinga wa kupewa kazi bila makubaliano kama manamba.
 
Mimi nilishasema sitafanya kazi za serikali ya Tanzania maisha yangu yote.

Sitaki ujinga wa kupewa kazi bila makubaliano kama manamba.
Waliokubali kuwa watumishi wanakinywea kikombe and they know it
Sana sana wanakushangaa wewe
 
Waliokubali kuwa watumishi wanakinywea kikombe and they know it
Sana sana wanakushangaa wewe
Wao wanafurahia kula kwa urefu wa kamba zao.

Mimi nawashangaa wameridhika kufungwa kamba, tena fupi!

Siwalaumu, ila ni maisha ambayo nimeyakwepa tu siyataki.

Mama yangu alifanya kazi Ikulu ya Nyerere na Ofisi ya PM, najua ukiritimba wa serikalini.
 
Kama umeteuliwa ni kwamba umekidhi vigezo kwa maana una sifa stahiki lakini pia umepewa heshima kubwa na Mamlaka iliyokuteua.

Jiulize kuna Watanzania wangapi wenye sifa zaidi yako lakini hawakupewa nafasi hiyo?

Vyombo vya habari vimetoa taarifa kuna Watu wamekataa Heshima waliyopewa na Mamlaka ya Uteuzi.
Itoshe kusema watu hawa kama ni kweli wapo hawana chembe ya uzalendo hata kidogo, umetumwa ukawatumikie Watanzania ukiwakilisha Mamlaka ya Uteuzi unakataa na bado unataka uendelee kwenye nafasi yako ya sasa?

Kuna mambo yanatakiwa kutiliwa shaka kwa watu hawa ikiwa ni pamoja na

1. Yawezekana nafasi walizopo sasa kuna maovu mengi wamefanya hivyo wanaogopa kuachia ghafla mengi yataibuka.

2. Yawezekana kile wanacholipwa ni kikubwa sanaa kuliko wanavyostahili, Wote tunajua Waajiri wao ni Wanachama. Je Wanacholipwa kama Mshara na Stahiki nyingine zinalingana na Waajiri wao?

3. Waajiri wa hawa watu (Wanachama) Je, ni kweli wanawapima utendaji wao kwa Maana ya Investment zinazofanyika chini ya Chama Chenu? Tutakuwa na Michango isiyokoomaa au tutafute uwezekezaji wenye tija na tupunguze michango?

Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania

Mwenyezi Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

View attachment 2501128

Kuteuliwa na viongozi wa kisiasa walioko madarakani kwa wizi wa kura kuna heshima gani?
 
Wao wanafurahia kula kwa urefu wa kamba zao.

Mimi nawashangaa wameridhika kufungwa kamba, tena fupi!

Siwalaumu, ila ni maisha ambayo nimeyakwepa tu siyataki.

Mama yangu alifanya kazi Ikulu ya Nyerere na Ofisi ya PM, najua ukiritimba wa serikalini.
Kupanga ni kuchagua
Kila mtu na lwake
 
Boss hakosei hata akiiteua maiti?

I mean these people don't even call to see if the appointees are still breathing.

Come on man.

Mfano wako ni mbaya, serikali si baba wa Watanzania.

Na hata mtoto wako anaweza kuwa na sababu nzuri za kukukatalia kufanya kazi fulani kama unambambikia tu kazi bila kusikilizana naye kwanza.

Mtoto ana pumu inayokuwa triggered na vumbi, wewe unamwambia afagie uwanja wenye vumbi. Hiyo si kazi, hiyo ni child abuse.

Mtoto ana haki ya kukataa kazi kwa sababu za kiafya.

Sasa hawa wateule hata kama wana sababu za kiafya, hawapewi nafasi za kukataa kazi.

Halafu wakishindwa kufanya kazi tutalalamika ma DC hawana ufanisi?

Wakati kazi wanalazimishwa kuzifanya, hawajataka kwa utashi wao wenyewe.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] aise una hoja nzito halafu zinafikirisha na kuchekesha at the same time [emoji936]
 
Nimecheka sana ulipoandika "utovu wa nidhamu wameanza ikulu kwa kuwatangaza watu kwenye teuzi bila hata ya kuwasiliana nao"

Nikacheka tena uliposema kuwa je kama mtu anaichukulia serikali iliyopo kuwa si ya halali?"

Yote kwa yote jamani anayoyaandika Kiranga ni ya kweli sana ukiyatafakari mfano swala la mtu kukataa tunaweza kuingiza tafsiri ya bwana Kiranga hapo kwamba haikubali serikali iliyomteua ndomana amekataa, na yet kwanini serikali iteue mtu ambae hakubaliani na serikali hiyo, ina maana hawakumjua mapema?

Hilo la kuwasiliana, kwakuwa uteuzi ni mchakato na unahusisha watu wengi (si raisi peke yake) basi baadhi yao wawe wanachukua jukumu la kuwasiliana na mteuliwa ili ajue kama anakataa aseme ili ateuliwe mwingine na kama anakubali aanze kujipanga kwa maisha mapya. Tena katika hili Kuna waliotolea mifano kwa mwalimu na mwajiri wake (yaani DED) kwamba eti mkataba unasema "na majukumu mengine atakayopangiwa na mwajiri". Well hatukatai lakini walimu wenyewe mashahidi zile barua za teuzi zinakuwaga Siri kiasi kwamba hata muda mwingine wakuu wako wa kazi wanachelewa kujua (hasa mwalimu mkuu) na ukishapewa Kuna siku unapewa za maandalizi mpaka tarehe fulani, hapo kwenye hizo siku tumeshuhudia walimu mara kadhaa wakiitwa halmashauri kwa kukataa uteuzi japo wamepata tabu sana lakini kazi zao wanazo na wengine walipata teuzi kwa muda walipokuwa tayari kuzikubali. Point kuu ni kwamba hawatangazwi kabla ya kuteuliwa na kuarifiwa kwa barua tofauti na ikulu ambapo wanatangazwa kwenye media moja kwa moja
Sana jamaa kiranga ana hoja nzito na ambazo kama serikali imejisahau basi wajirekebishe kuanzia hapa siyo dhambi kujisahihisha huwezi kumteua mtu bila kumwambia.
 
Back
Top Bottom