Kutoa ajira kwa waliofeli divisheni 4 tena kuanzia point 28 mpaka 31 ni kutuharibia jamii

Kutoa ajira kwa waliofeli divisheni 4 tena kuanzia point 28 mpaka 31 ni kutuharibia jamii

Umeeleweka sana mkuu. Wasomi sio wafia nchi bali ni wapigadili tu jeshini hamna kitu mle sema tu mambo yameshakuwa magumu siku hizi.

Tangu mwanzo majeshi yalikiwa ni kazi za watoto wa familia maskini na watu wa mkoa wa mara.

Wakati ajira hazijawa shida na jeshi kuboreshwa kimaslahi na kimuundo watoto wa masikini tu ndio walikuwa na option pekee ya jeshi.
Yaah mkuu now jeshi limevamiwa na wasomii
 
Mfungwa halipwi,we umesahau kuwa mrema ni mchaga,na sifa yao kuu hupenda vya bure
 
Chuki ni mbaya acha....mnalilia ajira zikitolewa mnavimba mpaka mnataka kupasuka...kama ajira zinawahusu four div 28-31 wewe si usubiri zikitoka za 1&2 ukaombe mkuu.
Halafu hao necta wanapopanga madaraja ya ufaulu hawajawahi kusema kwamba div four ni failure acha kupotosha umma,unaweza kufaulu sana lakini ukafeli katika utendaji wa kazi.
Wameamua kutoa ajira kwa form 4 huku wakijua nyie wasomi mpo cha msingi subiri zikitoka zinazowafaa wasomi wetu.
 
Siyo kweli katika sekta ambayo inahitaji wasomi na wanasayansi ni jeshi, polisi, magereza na uhamiaji.
Kila siku technolojia mpya inaibuka, huyu aliyefeli anaweza kupewa kazi ya ujasusi? Huyu aliyefeli anaweza kutengeneza website au virus au software yoyote kulinda taarifa zisiharibiwe na virus?
Wasomi wanahitajika sana, sasa hivi siyo km miaka ile ya 1945 ya vita ya pili kutegemea bunduki.
Sasa hivi mtu 1 au 5 wanaweza kuingamiza nchi na mkafa wote. Watu wanaingia laboratory wanatengeneza virus kisha watuma kwenye nchi yako kisha wanatengeneza na dawa. Unakufa huku unamtajirisha adui
Zama za nguvu zishapitwa na wakati sasa hivi watu wanatumia akili nyingi nguvu kidogo

jeshini pia kuna vyuo vyao kwa kiwango walichopima hata aliepata dv 4 ya 28 anaweza kumudu masomo yao pia inapofikia jeshi kuhitaji masuala makubwa huwatumia wanasayansi wakubwa ktk vyuo vikuu vya inchi hiyo nao si wanajeshi alietengeneza bom la atomic hakua mwanajeshi waliotengeneza virusi vya ukimwi hawakua wanajeshi.
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Taifa haliendelei kwasababu ya fikra kama hizo. Kuthamini sana ujuzi wa kwenye makaratasi (vyeti) kuliko kuwapima vijana kwa uwezo wao wote. Binadamu wana uwezo wa kukariri aliyofundishwa, kugundua mambo mapya na uwezo wa kukubalika kwenye jamii kutokana na kipaji alichonacho.
Kupata Divesheni 4 kwenye mtihani - sio kwamba huyu kijana hana akili. Nao wapewe nafasi kwenye ajira.
 
Mambo yamebadilika ndugu yangu. Yale mambo ya kutumia nguvu yameshapitwa na wakati. Sasa hivi nchi zinazojitambua kila kitu wanatengeneza wenyewe (wanajeshi wenyewe)
Hawa dvn 4 ndiyo wale wanavunja matofali kwa kichwa, mara analala, gari inapita juu yake. Ukitupiwa bomu nalo utalipiga kwa kichwa?
Tunataka tuone jeshi linatenda haki, watu wamevumbua bunduki, drone, gari n.k
Chukulia makambora 50 yamerushwa kwenye nchi yako, unatumia teknolojia gani kuyalipua yote kabla hayajatua kwenye ardhi yako? Wanaotakiwa kwenda jeshi ni 1-3 hawa utawaendeleza mpk watakuwa na PHD
Jeshi linahitaji madaktari, marubani, wanaIT (teknolojia), wanasaikolojia n.k ukiaangalia ni wasomi ndiyo wanaohitajika.
jeshini pia kuna vyuo vyao kwa kiwango walichopima hata aliepata dv 4 ya 28 anaweza kumudu masomo yao pia inapofikia jeshi kuhitaji masuala makubwa huwatumia wanasayansi wakubwa ktk vyuo vikuu vya inchi hiyo nao si wanajeshi alietengeneza bom la atomic hakua mwanajeshi waliotengeneza virusi vya ukimwi hawakua wanajeshi.
 
Badala kupigana kugombania ajira tufikirie kuongeza ajira..., Cha maana ni utendaji kazi na uwezo wa mtu kufanya kazi husika, sio cheti chake kinasema nini.

Hivi hujawahi kusikia mtu anaambiwa overqualified ? Sometimes ni bora uchukue mtu average na kumpa training kuliko mtu anayejiona ni qualified na anajua kila kitu kwahio huwezi kumfundisha (theory zimejaa na much know)
 
Sekta kama magereza, uhamiaji, polisi na jeshi walitakiwa waajiriwe watu wenye elimu kuanzia form 6, diploma, degree na kuendelea.
Lengo la kuwajiri waliofeli ni kuendelea kutumika kisiasa leo hii jeshi la polisi limekuwa la kisiasa.

embu taja tasisi moja yenye wasomi wasiotumika.
 
Badala kupigana kugombania ajira tufikirie kuongeza ajira..., Cha maana ni utendaji kazi na uwezo wa mtu kufanya kazi husika, sio cheti chake kinasema nini.

Hivi hujawahi kusikia mtu anaambiwa overqualified ? Sometimes ni bora uchukue mtu average na kumpa training kuliko mtu anayejiona ni qualified na anajua kila kitu kwahio huwezi kumfundisha (theory zimejaa na much know)
Baadaye huyu form IV wa point 31 anapanda cheo hadi kuwa kamishna wa uhamiaji.
 
Baadaye huyu form IV wa point 31 anapanda cheo hadi kuwa kamishna wa uhamiaji.
Inategemea hio baadae ni muda gani, hivi unadhani wewe hapo na elimu yako ya chuo hakuna jambo ambalo mtu uliyemkuta kwenye kazi husika kwa miaka 15 anaweza kuelewa kukushinda?

Ogopa watu waliopanda from bottom up hakuna cha kuwadanganya wanajua organisation culture inside out (sadly watu tunaangalia shuleni fulani alifanya nini na sio utendaji wake akiwepo kazini) yaani results oriented
 
Inategemea hio baadae ni muda gani, hivi unadhani wewe hapo na elimu yako ya chuo hakuna jambo ambalo mtu uliyemkuta kwenye kazi husika kwa miaka 15 anaweza kuelewa kukushinda?

Ogopa watu waliopanda from bottom up hakuna cha kuwadanganya wanajua organisation culture inside out (sadly watu tunaangalia shuleni fulani alifanya nini na sio utendaji wake akiwepo kazini) yaani results oriented
Nafasi ya uongozi, hata wa ofisi, inahitaji mtu mwenye uelewa mpana na anayeweza kubadilika kulingana na mazingira, si huyu aliyebobea kwenye urasimu wa taasisi. Uhamiaji unahusu ndani yake uchumi, Afya nk.

Mtazamo kama wako ndiyo maana tunazalisha watu wa kusema "Hatufanyagi hivyo." Na ndiyo maana hadi leo wapo wa kusema "Nyerere angefanya hivi na vile."
 
Sasa wakichukua waliofauli nani ataanza cheo cha chini jamani lazima jeshi liwe na watumishi kwanza mengine baadae. Jeshi linaakili sana hawa waliofaulu kwanza wengi hawakai wanakimbia kimbia so jeshi lalitaki hayo mambo sasa
 
Kazi za jeshi hakuna mambo ya division maana wanataka wapiga kazi sio wanaotaka mishahara mikubwa mkuu.
Twendeni kwa Zama ,sera zakuajiri watu wa levo hizo ili kukidhi haja za mishahara imepitwa na wakati kila siku ccm inadai uchumi umekua haya matakataka Yann kwazama hizi...
 
Nimeona matangazo ya ajira ya uhamiaji kuwa wanahitaji kidato cha 4 waliopata divishen 4 kuanzia pointi 28 mpaka 31 nikajiuliza sana.

Hivi taifa hili akili huwa tunazipeleka wapi? kwa nini uwe specific kutoa upendeleo kwa waliofeli? unaipeleka wapi jamii yetu kwa upendeleo wa aina hiyo?

Tangazo hilo nimeliona wizara ya mambo ya ndani upande wa uhamiaji.

Lakini kwa kumbukumbu zangu wizara hii huwa inaibuka na mambo ya ajabu ajabu tu, nakumbuka mwenyekiti wa parole ndugu Augustine Mrema naye aliwahi kuomba ujenzi wa reli SGR watumike wafungwa. Mimi nilimshangaa Mrema, mtu ambaye aliwahi kugombea Urais wa nchi hii unawaza vile? Kwamba wakati una vijana wengi wako mitaani hawana ajira unatoa kipaumbele kwa wafungwa kwenye ajira maana yake ni kuwaambia vijana wakafanye uhalifu wafungwe ndipo wapate ajira.

Ndiyo maana yake maana kama unawanyima vijana walioko mtaani ajira na unatoa jira kwa wafungwa unakuwa unapeleka ujumbe kwa vijana kuwa wakawe waarifu ndiyo wapate kazi na uhalifu utaongezeka maana vijana waliokata tamaa kwa kukosa ajira ni wengi na ukiwaonyesha wafungwa wanapewa kipaumbele watafuta kufungwa ili kupata ajira.

Tukirudi kwenye mada yetu ya kutoa kipaumbele kwa waliofeli.

Wapo wachache wanaodai ukimuajiri aliyefaulu anafanya kazi miaka michache na kutaka kwenda kusoma. ninasema wapuuzi wachache tena ambao hatuwezi kuwasikiliza tunapotaka kufanya maendeleo katika nchi hii.

Tunalo tatizo kubwa sana la ajira katika nchi hii kwa kuwa na vyuo vingi na shule nyingi zikizalisha wahitimu kila mwaka na wengi wanakosa ajira na kuishia kufanya shughuli za kipuuzi mitaani. watu hawa wanaweza kuajirika popote na wakakaa makazini kwa masharti ya mwajiri.

Mbona kuna watumishi wameajiriwa na kukaa kazini miaka zaidi ya 5 bila kupanda vyeo wala mishahara na humu kuna watu walikuwa na elimu kubwa lakini wakawa wanafanya kazi za chini.

Nina ndugu yangu amesoma ana masters ya business admnistration na kwa sasa anafanya kazi ya mtendaji wa kata

Halafu kuna mpuuzi mmoja sehemu anasema wasomi ukiwaajiri hawafanyi kazi hivyo tuajiri waliofeli??????

Hawa hawatujengei taifa bali kulibomoa
Ishu ya mlema kutaka wafungwa watumike kujenga SGR,ilikuwa kwa sababu ya cheap labour,mfungwa asingelipwa posho tofauti na kijana wa uraiani.
Kwa hili la uamiaji kutaka vijana wenye ufaulu hafifu ni mwendelezo wa upuuzi mwingi unaoendelea kwenye utumishi wa umma.hata jeshini JWTZ ukiwa jeshini n una taaluma fulani kuanzia kiwango Cha diploma,kupata nafasi ya kwenda kusoma uofisa cardet ni mbinde sana ukiuliza unaambiwa vijana wasomi wakipata vyeo wanakimbia jeshi kwahiyo suruhisho ni kuajiri vijana wa kidato Cha sita na kuwapa kipaumbele kuwa maofisa.Jamaa zangu walikuwa na diploma wakajiendeleza Tena kwa mkopo wa serikali wakapata shahada,masters lakini kupewa nyota ikawa mbinde,jeshi likataka wabaki kama private,wakaona uzushi wakapiga jeshi chini.
Alisema Prof Assad asilimia 60 ya watumishi wa umma ni vilaza!!harafu leo Bado wanasisitiza kuingiza vilaza zaidi!!
Miaka kadhaa iliyopita kuna mwamba alisisitiza kwa vile kibaha ajari za magari zimeongezeka basi serikali ijenge hospitari ya mifupa karibu kuwasaidia majeruhi!!hii Kwake aliona ndio ufumbuzi wa tatizo la ajari?!!!!!
 
Kuna chuo kikuu na chuo. Huyo aliyefeli anaweza kufundisha chuo na siyo chuo kikuu. Kwasababu kuna chuo cha mapishi, cha mapenzi, mabaunsa, muziki n.k
Chuo kikuu hakuna mwenye GPA mbovu yupo pale anafundisha. GPA zote ziwe zinaruhusu kusoma Masters. 2015 UDOM walikuwa wanashinikiza wakufunzi wote wawe na masters
Duh mpaka Chuo cha mapenzi Kipo?
 
Hahahaaaaa, yani nimecheka sana.Ktk nchi ambazo watu wanaelewa maana ya jeshi huwa raia wake hawakimbilii kujiunga na jeshi.Bali hujiunga na jeshi baada ya kushawishiwa sana aidha kimaslahi au kipropaganda. Nashangaa Bongo watu wanapigana vikumbo kujiunga jeshini.
Hali Ya Maisha Mkuu.... Mtu anaona Liwalo na liwe..
Nshapiga degree yangu moja nipo mtaani mwaka wa tatu inatokea nafac ya jeshi... Haikua kazi ya malengo yangu ila kutokana na ugumu wa maisha najitupa tu!
 
Back
Top Bottom