Kutoka Chato: Rais Magufuli amwapisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Kwanini Mbuzi, papai, fenesi na Kware wawe na Corona?

Kutoka Chato: Rais Magufuli amwapisha Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Kwanini Mbuzi, papai, fenesi na Kware wawe na Corona?

“Ugonjwa mpya unapoingia Watu huwa na uoga, UKIMWI ulipoingia kupitia Kagera ilikuwa ukikutana na Mtu mwenye UKIMWI unamkwepa, kulikuwa na Surua wakati inaingia ukiwa na Surua hakuna anayekuja kukutazama, kwahiyo niwahikikishie Watanzania ugonjwa huu utapita, tupunguze hofu”-Rais Magufuli baada ya kumuapisha Waziri Nchemba Chato
• •
“Waziri Mwigulu Nchemba nimekuapisha hapa uende mkacheki vizuri Maabara inayohusika na upimaji corona kuna vitu vingi haviko sawa, kulikuwa kila siku ni positive positive, namshukuru sana Katibu Mkuu mpya” - JPM
• •
“Tulifanya mambo kadhaa ili kujua ubora wa Maabara tukapeleka sampuli za wanyama, ndege na vitu vingine bila wao kujua, tukazipa majina ya Watu, tumepeleka sampuli ya mbuzi akawa positive, kondoo Negative, mapapai nayo positive, maana yake mbuzi,mapapai yote yana corona”-JPM

“Kama tunapeleka sampuli za wanyama zinakutwa Positive inawezekana wafanyakazi wa Maabara wanatumika na Mabeberu, kama mapapai, mbuzi yana corona WHO wanapaswa kufanya kazi kubwa ya ziada, kwa hili lililotokea lazima kuna Watu wameambiwa wana corona wakati hawana”
 
Mzee anavyoongea utadhani yeye sio Rais wa hii nchi.. yaani as if yeye ni mpinzani yuko anaikosoa serikali ya nchi ili apewe madaraka yeye.

Sasa huo utopolo wa maabara, hio si maabara ya serikali na yeye si ndio Rais sasa anatulalamikia sisi tumsaidie nini?
Jamaa kama nchi imemshinda aniachie hata mimi.
Hiyo maabara ya kupimia corona sio mali ya serikali, zimetengenezewa huko huko nje.
 
Kiukweli watu wanaweza kubisha lakini ukweli unabaki kuwa ukweli kuwa Rais Magufuli ni chaguo la Mungu.

Ujasiri wa Dr Magufuli ni wa kinabii na kitume na hili naliona katika vitabu mbalimbali vya kiimani na inahitaji nguvu ya Roho mtakatifu kulielewa hili.

Naomba Mungu aendelee kumlinda Rais Magufuli ili aweze kuisaidia Dunia hasa katika wakati huu mgumu ambao viongozi wote duniani wanaiogopa Corona.
Naamini kabisa Tanzania ndio nchi ya ahadi.

Mungu mbariki Magufuli

Mungu ibariki Tanzania.
Mwambie atoke Chato, najua muziki wa corona ndiyo maana amejichimbia Chato! Anajua akitoka tu akakutana na watu amekwisha! halafu unasema bila aibu eti ni shujaa, Mwoga kama kunguru
 
Meko kanikumbusha yule spokesperson wa Iraq wakati US ilipovamia Iraq. Alikuwa akiitwa Tariq Aziz nadhani.

Marekani anawaua wairaq lakini Tariq anasema "tumewashinda wamarekani, hawatuwezi hata kidogo".
 
Kuna maswali mengi sana ambayo yanahitaji majibu.

Huu mhimili wa 4 (vyombo vya habari) ungekuwa huru, naamini majibu yangepatikana.
Swadaqta!

Ameminya uhuru wa vyombo vya habari. Nashindwa hata kumuelezea! Wallahi huyu jamaa wallahu aalam.
 
Brazilian President Bolsonaro rejects calls for coronavirus lockdown, says "we're all going to die one day"

Coronavirus: Brazil reports over 1,000 deaths

Nakumbusha tuu [emoji115]


I'm on that good kush and alcohol
 
Kuna mambo mengi ya kushangaza kuhusu Corona!. Kwanini watu wasizikiwe kwao?.
Kwanini Evod Mmanda amezikwa Mtwara kwa lazima ambao sio kwao!.
P

Hapa pana point kubwa sana.

Wafiwa wamzike ndugu yao walipoamua .lakini iwe chini ya usimamizi wa serikali.
Siyo kulazimishwa na serikali mahali pa kuzika.
 
Hv hizo sampuli za papai zilizopelekwa maabara zilikuwa kwenye damu au kwenye nini. Maana nadhani sampuli zote ziwe ni damu.

Yawezekana papai ikawa na damu pia.
 
Back
Top Bottom