Elections 2015 Kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma: Mwigulu Nchemba atangaza nia kugombea Urais

Elections 2015 Kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma: Mwigulu Nchemba atangaza nia kugombea Urais

Ficha ujinga wako hujui chochote Lowasa aliomba wimbo wa komba kumekucha ulipigwa?

Rejea kauli yako ya kwanza. "Lowassa aliomba wimbo wa komba, Dj hakupiga hata mmoja". Hii inaonyesha jinsi ulivyo na uhaba wa kumbukumbu wewe unaejifanya sio mjinga na mwenye kujua vingi. Sijui unajuaje vingi na kuwa sio mjinga kama huna kumbukumbu ya statement unazotoa?
 
Hata Kikwete DHAIFU alikuwa na hoja yenye mashiko. "Nitaipitia tena mikataba ya madini ili kuhakikisha ina maslahi kwa nchi yetu" "Ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya" "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" lakini alipoingia Ikulu akaweka kipaumbele kwenye ufisadi, kupokea pesa toka kwa marafiki zake AKA rushwa, kuwa VDG kiguu na njia na kuweka rekodi ya Rais aliyesafiri nchi nyingi za kigeni na pia aliyekuwa nje ya nchi yake kwa muda mrefu kuliko Rais yeyote yule duniani, kuwakingia kifua wezi, wapokea rushwa, wauza unga, majangili na kuwa na matanuzi makubwa ndani ya Ikulu. Kumbuka huyu kuna wakati aliitwa mpaka chaguo la Mungu kumbe si lolote si chochote naye ni fisadi tu. Watanzania tusirudie makosa ya 2005 ya kusikia hizi ahadi nzuri nzuri ambazo ni hewa na wakishaingia Ikulu ahadi zao wanaziweka pembeni kabisa. Ndani ya MACCM hakuna yeyote yule, narudia hakuna YEYOTE yule anayestahili kuliongoza Taifa letu.


Wezi wanatangaza nia. Tuangalie nani ataleta hoja zenye mashiko.
 
Mwiguru, tangaza nia kwa mgombea binafsi utapata, ndani ya ccm kutekeleza hayo uliyoyasema chama chako kitakubali?
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Mwigulu haongozi serikala wala wizara. Yeye ni naibu waziri tu.

Alikuwa anatoa maoni yake as mchumi na changamoto alizoziona Serikalini.

Kaongea vizuri tumpe hongera yake.
Cha kujiuliza je ataweza kutekeleza?? Kwa sababu sio mara ya kwanza kusikia maneno ya kutia moyo kama hayo.

Maoni tu.

Kuongea vizuri tu haitoshi.... angejiuzuru basi kama alivyofanya Edwin Mtei enzi za Mwalimu...hawezi kutudanganya!!
 
Hata mm Mwigulu kagusa moyo mara yangu kwa mara ya kwanza naanza kukubali kuwa hela iliyomsomesha haikupotea bure....

Ninamwomba Mungu CCM imlete huyu ili watanzania tumpambanishe na mtu wa UKAWA.

Sema waswas wangu ni kwamba siamini kama mfumo wa chama chake utamwezesha kututoa hapa tulipo japo yeye ana nia njema sana
 
Hapana Mkuu mbopee jaribu kuitafakari vizuri. Na ili ufanikiwe lazima ujifunze ambapo mwenzako kakosea ni zama za ukwel na uwazi

yeye alikuwa ndani ya hiyo hiyo serikali iliyoshindwa yote hayo.hana jipya
 
Last edited by a moderator:
Haya majibu yake kuhusiana na kushuka kwa fedha yetu ni mepesi sana action zake ni miaka itachukua so tutaendelea kuteseka tu

Of course huwezi kujenga uchumi kwa siku 2. Lazima uwe na mipango ya muda mrefu.

Mfano Kagame na 2020 vision, aliwaahidi wananchi wake hivyo mwanzoni mwa 2000, na ime work sasa hivi Rwanda iko mbali kabla hata mwaka 2020 haujafika.

Kifupi hakuna shortcut kwenye kujenga uchumi bora.
 
Lazima tutengeneze equilibrium point kati ya dola na sh.yetu ili vyote viwili viweze kushindana kwa uwiano ulio sawa, ndo hapo linakuja swala la kujenga viwanda ili tuuze kwa wingi nje na kupata pesa za kigeni nchini, pia lazima kuzuia kununua vitu kwa dola ndani ya nchi yetu, hata kodi za nyumba eti wanapangisha kwa dola? Hawa mafisadi yanatuumiza sana af leo wanalialia hapa!
 
sijui ugaidi wala ugoni wa mwigulu - ni siasa kama zingine lakini nikimtathmini kwa hotuba yake, Mwigulu amempita EL kwa kilomita nyingi sana. Kaka amepanga hoja zake vizuri. "Tone" na ujumbe vinashabihiana, kasema vipaumbele vyake na jinsi ya kuvitekeleza, hajanisomea neno moja baada ya jingine kana kwamba kaandikiwa - anajua anachokisema, ana upeo mkubwa (IQ). Mpaka sasa kwangu EL ana point 0, Mwigulu 1. Nachotaka kujua tu sasa ni nani mshika remote wake. Washika remote wa EL nawajua, na ndo maana nikifikiria kumpa kura vinywele vinanisimama. Tukio la Nchemba pia limenionyesha ni kwa kiasi gani mbwembwe na ufahari kwa EL vilitumika kufunika udhaifu binafsi wa EL kama mwanasiasa. Nchemba amevuta hisia zangu bila helikpta wala diamond platinum. Tukiwa chuo nilikuwa namchukulia poa tu, lakini kwa jinsi alivyoweza kuweka nia na juhudi katika maono yake ya kisiasa naona ni mtu anayeweza kujiongoza na kusimamia kile anachokiamua. Huo uwezo ni vigumu kuuona kwa watu hawa wagombea wazee. Kupanda kwao kisiasa hakukuhitaji bidii kubwa. Kuingia kwenye mfumo wa siasa wakati ule haikuwa kazi ngumu na walikuwa wachache kulingana na mahitaji ya nchi kwa wakati ule, lakini kwa rika la Nchemba si kazi rahisi kuwapiga vikumbo hawa wazee na kutoboza bila kujiamini. Kwangu mimi hii ni sifa ya kiongozi. Nawasubiri kina Membe ila katika hawa wawili Mwigulu ameamsha hamu ya kusikiliza wagombea kwa makini.
 
Hili suala la kushuka kwa shilingi nilikuwa nahitaji sana majibu.atueleze immediately actions ya kuokoa shilingi sasa.kusubiri ajenge viwanda siyo leo.

Ulitegemea nini ? wakati Wachaga na Wanyalukolo kutwa wanapanda Guan Zhou na Beijing kwenda kuimarisha viwanda vya China
 
Tatizo la wanasiasa wengi ni kueleza NGONJERA nyingi za mipango bila kujibu swali la msingi la HOW(Strategies ZINAZO TEKELEZEKA). Hatutaki kuambiwa nitafanya nchi iwe na this and that, iwe hivi na vile. Tunataka HOW utatekeleza hizo "this n that" zako.
Thats why nakuwa mtu wa mwisho kumuamini mwanasiasa wa AINA YOYOTE
 
Nionavyo mimi mpaka sasa kama mmoja wa hawa waliotangaza nia akija kuwa raisi:

Lowassa: Masikini hawana lao, tutakua taifa lenye matajiri sana wachache na maskini sana wengi.

Wassira: Maendeleo katika sekta zote yataenda polepole mno hata kusimama. Sijamwona kama ni visionary leader mwenye uwezo wa kusukuma maendeleo yaendani na kasi ya maendeleo ya kisasa. Kabaki ki zama za kale sana.

Mwigulu: Akili anayo, uwezo anao ila uzoefu katika maswala ya international relations na diplomacy ambayo ni muhimu sana pia kwa maendeleo, je atachukuliwa seriously na the likes of Putin, Angela Merkel, Obama, Kagame, Uhuru e.t.c. Nahisi anaweza onekana bwana mdogo sana na kuwa side lined sometimes. Unajua hizo meetings status ya mtu ina matter sana.
Nilishawahi kuandika hapa kipindi ambako nilibahatika kukaa na Jeffrey Sachs kutokana na kum accompany ndugu yangu ambaye ni Prof. Ilikua informal meeting to kwenye lobby ya hotel, jumla tulikua watu 5 tu. Yani mimi nilbaki kukaa kimya na kusikiliza watu na taaluma zao wakishusha vitu. Hawakunionyesha dharau, lakini nilijiona kabisa huu sio uwanja wangu. Nina fikiri Mwigulu anaweza patwa na hili pia kimataifa kutokana na umri.

Thats my opinion.
 
Hata Kikwete DHAIFU alikuwa na hoja yenye mashiko. "Nitaipitia tena mikataba ya madini ili kuhakikisha ina maslahi kwa nchi yetu" "Ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya" "Maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana" lakini alipoingia Ikulu akaweka kipaumbele kwenye ufisadi, kupokea pesa toka kwa marafiki zake AKA rushwa, kuwa VDG kiguu na njia na kuweka rekodi ya Rais aliyesafiri nchi nyingi za kigeni na pia aliyekuwa nje ya nchi yake kwa muda mrefu kuliko Rais yeyote yule duniani, kuwakingia kifua wezi, wapokea rushwa, wauza unga, majangili na kuwa na matanuzi makubwa ndani ya Ikulu. Kumbuka huyu kuna wakati aliitwa mpaka chaguo la Mungu kumbe si lolote si chochote naye ni fisadi tu. Watanzania tusirudie makosa ya 2005 ya kusikia hizi ahadi nzuri nzuri ambazo ni hewa na wakishaingia Ikulu ahadi zao wanaziweka pembeni kabisa. Ndani ya MACCM hakuna yeyote yule, narudia hakuna YEYOTE yule anayestahili kuliongoza Taifa letu.

Hawakumbuki watz jamani! Nimesema haya humu watu hawaelewi. Nimeamua kumwelewesha mwanangu wa darasa LA kwanza kanielewa!
 
Wezi wanatangaza nia. Tuangalie nani ataleta hoja zenye mashiko.

Mashiko yapi yatakayotushawishi tuwape kura zetu...
Iwe sera ya kweli au uongo yeto nikwaajili ya mianya ya Dill zao..
 
Back
Top Bottom