Elections 2015 Kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma: Mwigulu Nchemba atangaza nia kugombea Urais

Elections 2015 Kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma: Mwigulu Nchemba atangaza nia kugombea Urais

Sasa ni zamu ya Mwigulu Nchemba na anatarajia kutangaza nia kuanzia saa 9 mchana wa leo na atafanya hivyo live kupitia star tv akiwa Chuo cha Mipango, Dodoma.
View attachment 255981
Muda: saa 9 Alasiri hadi Saa 12 Jion.
Mahali: Chuo cha Mipango Dodoma.
Ukumbi: Mwl. Nyerere Hall

KAULI MBIU YA MWIGULU: MABADILIKO NI VITENDO, WAKATI NI SASA

Mwigulu anadai alibeba zege baada ya kumaliza chuo kikuu na mke wake akiwa mama ntilie akiwapikia yeye na vibarua wengine wa ujenzi.

Pia naona Mwigulu anamponda EL kiani kwa kusema watu wanajisifu kuwa wamekuwepo serikalini muda mrefu wakati huo huo wamelisababishia Taifa hasara kubwa katika muda huo mrefu waliokaa serikalini.

Inasikitisha kumuona analalamikia mambo mengi yanayoendelea chini ya serikali hii ya CCM wakati kila siku wanawakejeli wapinzani wanapolalamikia na kuhoji mambo hayo Bungeni.

Kwa kifupi,Mwigulu leo anaivua nguo CCM hadharani na zaidi leo anamponda kiana mh.sana na pia anaonyesha kuwa Mkulu na chama chake wamekuwa ni dhaifu.
Hapo kwenye red hapo umechemka, sidhani kama ndivyo ilivyokuwa, utatutia mashaka kama na wewe ni team makundi mkuu... tunataka genuine nutral analysis.
 
Heshima iwe kwenu wadau.

Baada ya kumsikiliza mtangaza nia namba 3 kutoka CCM ndugu Mwigulu Nchemba nimeingiwa na wasiwasi kidogo.

Kwa wale waliofuatilia na kumsikiliza mh. naibu waziri mtagundua kuwa Mwigulu alikuwa anaongea kama vile yeye si sehemu ya serikali.

Lakini cha ajabu zaidi mtakumbuka kuwa Hoja alizokuwa anaziongelea leo ni zile zile zilizokuwa zikiongelewa na wapinzani bungeni na yeye kuamka kuzipinga kwa kuwakejeli.

Kwa lugha nyepesi tunaweza sema kuwa Mwigulu katumia hoja za wapinzani kujinadi wakati ndye aliyekuwa mstari wa mbele kuzicrash hadi akasifiwa na Mwenyekiti wa chama na kupewa unaibu katibu mkuu bara pamoja na unaibu waziri kwa hiyo kazi.

Kwa lugha yepesi Mwigulu Nchemba tunaweza kumuita Chichidodo (Ndege mnafiki anayechukia kinyesi wakati chakula chake kinatokana na kinyesi)

Na hapa ndipo ninapopata wasiwasi kujua hasa nimwamini Mwigulu Nchemba yupi?!

1) Yule aliyekuwa anazipinga hoja za wapinzani?!

Au

2) Huyu aliyetumia hoja za wapinzani kutangaza nia?!
 
TUTAWANYANG'ANYA LESENI, TUTAWAFUNGA JELA.

'Hakika usilolijua ni kama usiku wa giza" Nimeshangazwa sana na kauli ya Mh Mwigulu ambaye ni naibu waziri wizara ya fedha.
Ameonesha wazi hajui ni dawa gani zinazoruhusiwa kuuzwa kwenye maduka ya madawa ya binadamu katika nchi yake.

Siwezi kushangaa sana japo kanisikitisha kuona kiongozi mkubwa wa kitaifa hajui tofauti ya Dawa zinazokuwepo hospitalini na zile ambazo wamiliki wa maduka wanauza.

Kabla hajalizungumza hili kama mtia nia alitakiwa kujiuliza kwa wadau wa Afya wampe tofauti lakini pia hili jibu kuwa wao hawatibiwi hapa kwetu bali ni ughaibuni

Eti "Tutawanyang'anya leseni na kuwafunga" japo hao wamesomeshwa kwa kodi za wa Tanzania hawa si wengine ni madaktari, najiuliza huyu jamaa kala maharage ya wapi hadi anashindwa kuelewa dawa zinazomilikiwa na serikali zina nembo ya MSD na hizi haziuzwi katika la madawa kamwe.

Namshari afuatilie namna dawa hizi zinavyotolewa huko mahospitali na ajiulize kwanini madaktari wanawaonesha wagonjwa sehemu ya kununua kuliko kukurupuka.
Shame on u Mwigulu

Msema kweli haogopi kufungwa wala kufa

Dr Kilawa the Iron

Sioni tatizo katika tamko la Mchemba kuhusu madawa ya hospitali yanayopashwa kuweko katika hospitali za serikali kukutwa katika maduka binafsi ya madawa. Ni ukweli usipingika kwamba maduka mengi ya madawa yaliyojengwa karibu na hospitali za umma yanauza madawa ya serikali. Ni aibu kwa serikali kwamba mgonjwa anaenda hospitali na kuelekezwa akanunue dawa zenye nembo ya serikali katika duka la jirani ambalo aghalabu ukiuliza mmiliki uataambiwa ni dakitari anayefanya kazi katika hospitali ya umma. Ni aibu namuunga mkono Mwigulu kwamba ikithibitika mahakamani kwamba dawa zilizokamatwa ni za serikali, duka lililohusika lifungwe na mmiliki apelekwe jela.
 
Kwanza..huyu jamaa...alikuwa..hana...mtiriko mzuri....kataka hotuba yake...alikuwa...analalamika...huku alikuwa mshauri wa Rais...nikagundua..ana tatizo la intellectual myopia ...anashindwa..kutupa..national interest itakuwa nn..??Amegeuka mlalamikaji....
 
Watanzania bwana!! Urais siyo kuongea vizuri. Kuongea vizuri kunaweza kumsaidia mgombea kuwaaminisha watu kuhusu uwezo wake especially kama hammfahamu. Kwa bahati nzuri hawa watu tunawafahamu vizuri sana, uwezo wao na mapungufu yao. Sasa badala ya kuwa assess kwa hayo tumeamua kutumia hotuba zao za leo ambazo hatuna hata uhakika kama ni wao wenyewe wamezitayarisha. Hivi kesho Lowasa akiongea vizuri kuliko Mwigulu kuna watu watabadili misimamo yao!?
 
Watu wanapotea sehemu moja tu...Mwigulu yuko kwenye serekali na wanalijua hilo wameshindwa nini kudhibiti hilo. ..kama sio kutuona majuha.

Issue ya MSD na deni wanalodai serikali anaijua vizuri..na pia anajua kwa nini hospitali dawa hazitoshelezi. ..yeye kuja hapa na kusema dawa zinaibiwa ni kujitoa ufahamu na kusema uongo.


In any rate mwananchi atie akili hamna jipya hapo hao wanalinda mfumo uliopo huwez kuendelea kuchagua ccemu alafu utegemee mabadiliko katika kuendesha serikali.

Kwa kushindwa kupambambanua mambo watanzania wataendelea kuburuzwa tu mpaka akili ziwakae sawa.
 

Tuweke ushabiki pembeni, kati ya watangaza nia watatu kati ya jana na leo, Mwigulu Lameck Nchemba is the most bonafide genuine mgombea so far, ukimuangalia huku unamsikiliza, utaiona his genuinity kutoka moyoni mwake ku practice what he preach na kiukweli nadhani kwa kati ya hawa watangaza nia so far, naamini Mwigulu can make the best president this nation has ever had tangu mwalimu Nyerere!.

Jee wewe mwenzangu ulibahatika kumsikia, unamuonaje?!.

NB Ku make the best president ni jambo moja, mgombea anayependwa zaidi so far ni Edward Lowassa, na mgombea the most experieced so fat ni Stephen Wasira, nikichukulia mchakato wa 2005 wakati JK alipochaguliwa, kama reference, assuming hawa watatu ndio wameingia tatu bora, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakipewa choice ya kuchagua between "the most loved", "the most experienced" and the "the best president", watachagua mtu anayependwa na watu, mtu atakayechagulika kwa urais na kuwatupa the rest, na hivi ndivyo JK alivyochaguliwa ile 2005 kwa sababu kwenye the finalist watatu, kulikuwa na "the most experienced" Dr. Salim, "The best Brain", Prof. Mwandosya, na "the good looking" Jakaya Kikwete, akapitishwa kwa hoja kuwa ndiye anayependwa na watu, as if mapenzi ya watu ndio uongozi wa nchi!.

JF has a role to play kuwaelimisha wananchi wetu waweze kufanya informed decisions kwenye choice of president, ili ifike mahali chaguo la mgombea wa CCM sio lazima ndio automatikally awe rais, wakituletea ule ujinga ujinga kama wa 2005, tunapiga tuu chini only if huko kungine kuna the better alternative!.

Ushauri wangu wa kwanza kwa wana JF, Mwingulu Nchemba is the man to keep watching seriously!.

NB. Kwa walionidhania mimi niko kambi fulani, uzi huu ni uthibitisho kuwa Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, hana mtu, ila kuna watu anawakubali akiwemo yule 'jamaa yetu', hivyo sitarajii kuulizwa kama nimehama kambi kwa sababu sijawahi kuwepo kambi yoyote!.

Kiukweli mimi Pasco wa jf, nimeguswa na Mwigulu Nchemba!.

Pasco

wewe na LIZABORN toka ile insu ya ESCROW mume kuwa wa uvugu vugu sana.mnashindwa muwe upande upi.
 
Mkuu ngoja kwanza kesho tumsikilize wa Mwitongo naye ndipo hoja yako inaweza kuwa na mashiko. Ila the bottomline ni kwamba ni rahisi kumuuza Makongoro kwa wananchi kuliko Mwigulu. Maana yangu ni kwamba kesho Makongoro akionyesha vision inayokubalika, ni bora yeye kuliko Mwigulu. Nasema hivi kutokana na hizi kashfa zinazonyong'oneza CCM na serikali yake

hivi huyu makongoro ni yule aliyewahi kuishi arusha? mwanasheria? sijui aliwahi pia kuwa mbunge? kama ndo huyo basi mwigulu ni bora mara 20
 
Duuu,haya bwana,ila mi nimeuona ni jembe sana,anafaa kuwa kiongozi wangu na namkaribisha kwa moyo wote aje kwetu Mvomero atangaze nia kwa mara nyingine,anajua sana

ile kushindwa kudhbiti sarafu against dollar ni udhaifu mkubwa
 
Tuache utani, na ushawishi Mwigulu hafai kwa lolote, hata uwaziri wenyewe unampwaya. Ni mtu hatari kwa umoja wa kitaifa: mtu ambaye yuko tayari hata kuua, ambaye hamuungi mkono. Kumbuka mauaji ya Arusha alipokuwa ameweka kambi, na kupoteza majimbo yote. Kwa ushauri wangu, Mwigulu apewe nafasi zaidi ya kuchunguzwa, atajifunua wazi jinsi alivyo.
Kwa maoni yangu anafaa kuwa jasusi, ajiuunge nao kama bado.
Watu tunaridhika tu akituimbiwa wimbo wake kuwa katoka familia maskini, kwani nani hakutoka huko?
Yupo ndani ya serikali iliyotufukarisha, na inaendelea kufukarisha anafanya nini cha msingi isipokuwa kutuhadaa na hadithi zake kuwa katoka familia maskini?
Tatizo tunasahau haraka.
 
So far katika wote wanaogombea, Upinzani na CCM kwa ujumla wake, naelekeaelekea kwa Mwigulu.

Ngoja nimsubirie na Mzee wa Utendaji, Magufuli.

huyu abaki tu kwenye utendaji, uongozi hauwezi.
 
Kwa hiyo kila jema likiongelewa na CCM ni idea ya upinzani?

Mwigulu ni jembe na ni kiboko ya upinzani, lazima mpanick..

Kwa wenye akili za kushikiwa ni wazi ataonekana jembe la mkono (la kuwekwa makumbusho)...

Ila wenye akili timamu lazima wahoji... Mbona mara nyingi anafanya personal cum criminal attacks hoja hizo hizo zikizungumzwa na upinzani..??

I really hate those who don't commit to use atleast 0.5% of their brains in as much as I disrespect politicians who deceive common wananchi....Hypocrites who can't walk their talk...!!
 
TUTAWANYANG'ANYA LESENI, TUTAWAFUNGA JELA.

'Hakika usilolijua ni kama usiku wa giza" Nimeshangazwa sana na kauli ya Mh Mwigulu ambaye ni naibu waziri wizara ya fedha.
Ameonesha wazi hajui ni dawa gani zinazoruhusiwa kuuzwa kwenye maduka ya madawa ya binadamu katika nchi yake.

Siwezi kushangaa sana japo kanisikitisha kuona kiongozi mkubwa wa kitaifa hajui tofauti ya Dawa zinazokuwepo hospitalini na zile ambazo wamiliki wa maduka wanauza.

Kabla hajalizungumza hili kama mtia nia alitakiwa kujiuliza kwa wadau wa Afya wampe tofauti lakini pia hili jibu kuwa wao hawatibiwi hapa kwetu bali ni ughaibuni

Eti "Tutawanyang'anya leseni na kuwafunga" japo hao wamesomeshwa kwa kodi za wa Tanzania hawa si wengine ni madaktari, najiuliza huyu jamaa kala maharage ya wapi hadi anashindwa kuelewa dawa zinazomilikiwa na serikali zina nembo ya MSD na hizi haziuzwi katika la madawa kamwe.

Namshari afuatilie namna dawa hizi zinavyotolewa huko mahospitali na ajiulize kwanini madaktari wanawaonesha wagonjwa sehemu ya kununua kuliko kukurupuka.
Shame on u Mwigulu

Msema kweli haogopi kufungwa wala kufa

Dr Kilawa the Iron

Mwigulu yuko sawa mkuu hili swala la madawa labda wewe ndo hulijuwi na mimi nilifikiria mwigulu ataenda mbali zaidi kwa adhabu na siyo kuishia jela tu.

Hizo chapa za MSD wewe tu ndo unazifahamu ukienda ospital ukiambiwa nunua dawa nje apo ni asilimia 0.0001% wanaolichunguza hilo la MSD. mara nyingi wanaoenda hospital za kawaida za serikali na kuamriwa kununua dawa ni wanyonge maskin ata elimu ya kusoma hiyo MSD hawana.

Binafsi nishaenda hospitali ya Serikali nikaelekezwa niende chumba katika vile vile vyumba vya milango ya mule hospital nigonge ntamkuta daktari ataniuzia dawa niliyoandikiwa nikafanya hivyo na kwa taarifa yako sasaivi mahospital karib yote ya Serikali bei za kununua dawa zimebandikwa katika milango ya hospital tunanunua dawa ndani ya jengo la hospital yaani ukiikuta hospital ya Serikali unanunua dawa duka lipo nje ya hospital saivi ni nadra haya mambo mkuu hayafichiki tena saiv ni waziwazi Mwigulu ameliona hili nimefurai kwamba ameahidi kulifanyia kazi akipata ridhaa.
 
Mwigulu ni mtu nae mwamini kuliko mtu yoyote, nikimwangalia kwa kimoyo naona anastahili % 100, nikimwangalia kimacho ni mtu ambae anania ya dhati kuijenga Tanzania tunayoitaka wananchi wa Tanzania. Binafsi nimekuwa nikimwangalia bungeni ni mtu ambae kwenye swala la wananchi ata kama limetoka upinzani nilimwona akiunga hoja kwa mwili na kimoyoni hata kama alikuwa pengine kimya. Kwenye ukweli tuwe wakweli Mwigulu anastahili kwa %100 kuwa Raisi wa Jamuhuli ya Muungano wa Tanzania. Mungu akubariki usonge mbele.. haya ni maoni yangu na mtazamo wangu, na endapo akipitishwa na CCM ntampigia kampeni kwa jamii inayonizunguka kwa sababu nina ushawishi. Narudia tena Mungu akubariki ndugu Mwigulu.
 
Back
Top Bottom