kutoka katika kitabu cha "My Life, My Purpose" by Mkapa: Vyeo vya kitaaluma kugeuzwa vyeo vya kisiasa

kutoka katika kitabu cha "My Life, My Purpose" by Mkapa: Vyeo vya kitaaluma kugeuzwa vyeo vya kisiasa

MR BINGO

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2016
Posts
1,164
Reaction score
2,500
Habari wanajamvi

Katika kitabu chake cha "My life,My purpose"ndugu mkapa aliyepata kuwa rais wa Tanzania katika kipindi cha miaka 10(1995-2005) ameelezea katika sura ya 11 aliyoiita "reforms and yet more reforms" swala la vyeo mbalimbali vya serikali kufanywa kuwa vya kisiasa wakati vinampa mtu majukumu ambayo yanamhitaji awe na uwezo wa kupambanua vitu mbalimbali kupitia nafasi yake.

Raisi Mkapa katika hoja yake hiyo alitolea mfano wa cheo cha "district comissioner"(DC) ambacho tumeona siku hizi kikitumika kisiasa zaidi na kutoa nafasi kwa watu ambao hawako katika mfumo huo wa uongozi kiujumla na wamekuwa wakitolewa katika sekta mbalimbali kama sekta ya habari,sanaa,michezo.

Kupitia maneno ya Rais Mkapa anauliza "Je kumtoa mtu katika sekta tofauti kabisa na uongozi wa serikali na kumkabidhi wilaya aiongoze kupitia semina wanazopewa ndani ya wiki moja kuna ufanisi wowote?"

Nililete kwenu hili wanajamvi je ni suala lenye afya kumchukua mtu maarufu yeyote na kumpa ukuu wa wilaya ama ingekuwa ndo wakati sahihi wa kuwatumia wanataaluma wanaohitimu katika vyuo mbalimbali nchini katika fani za uongozi? Mfano Chuo cha Hombolo,Mipango,Udom,UDSM n.k
 
Zamani wakurugenzi walitokana na wakuu wa idara hata ma DC walikuwa ma senior staff's toka kwenye taasisi za serikali.
Hata huu ujinga wa kina sabaya haukuwepo kabisa.

Alipoingia JPM tu kwakuwa alikuwa hajui lolote kuhusu siasa wala utawala akabadilisha kabisa mfumo na kuchukua makada wa lumumba tena waliokosa ubunge na kuwapa UDC na Ukurugenzi.

Matokeo yake ni haya ya kina BASHITE
 
Zamani ukisikia
Mkuu wa Mkoa,
Mkuu wa wilaya,
Mbunge,
Atafika eneo fulani kulikuwa na heshima kubwa sana.

Mtu analia bungeni then unampa ukuu wa wilaya.
Kimekuwa cheo cha kuwapa watu ambao hawana vyeo yaani kama kuna kada anarandaranda basi unampa wilaya as if wilaya ni kitu kidogo HV
 
habari wanajamvi
Katika kitabu chake cha "My life,My purpose"ndugu mkapa aliyepata kuwa rais wa Tanzania katika kipindi cha miaka 10(1995-2005) ameelezea katika sura ya 11 aliyoiita "reforms...
Ni tabu
 
Sasa fikiria mkuu wa wilaya anapewa mtu kama JOKETI jamani. Yaani wakina kiba wamekula mbususu we hadi wameacha nani atamuheshimu huyo???
Kimajukumu pia haina afya maana MTU anapewa ukuu wa wilaya na muundo tu wa uongozi haujui hivyo ni lazima majukumu yatampiga chenga tu
 
Jiwe alikuwa anagawa vyeo kama zawadi ndio maana wakina Luoga wakaambulia kuwa BOT governor baada ya ushabiki tu wa MAKINIKIA ambao mpaka Leo hatujaambiwa kuwa walilipwa shilingi ngapi walizotuaminisha walikuwa wanawadai mabeberu!!

Yote haya ni mapungufu ambayo rasimu ya KATIBA iliyopendekezwa na wananchi ilikuwa inayapatia majibu ya kudumu lakini watawala hawataki yashuhulikiwe kwani yanawapa nyenzo za kuwakandamiza wanyonge wao!!
 
Busara zinawarudia wakitoka madarakani. Nikiwaza hilo hiwa sioni mantiki yoyote ya maneno matamu ya hawa wanasiasa. Namkumbuka JKN na speech yake ya kutaka vijana wawe jeuri wa kuhoji mambo wakati yeye kitendo cha kutofautiana mawazo na Kambona kilifanya mwenzake kwenda uhamishoni.
 
Kimajukumu pia haina afya maana MTU anapewa ukuu wa wilaya na muundo tu wa uongozi haujui hivyo ni lazima majukumu yatampiga chenga tu
Kabisa tena kwa mbali sana. Hapa wataelewa watu waliowahi kufanya kazi za management tu.

Ndiyo maana hata magufuli mambo mengi ya utawala yalimshinda maana kabla ya kuwa raisi hajawahi kuwa kiongozi zaidi ya kuwa waziri tena bulldozer.

Bashiru alitka chuo UDSM hakuwahi kiongoza popote akapeleka chama pabaya mpaka kuanza kununua wapinzani.

Mitano ipo mingi mkuu
 
Busara zinawarudia wakitoka madarakani. Nikiwaza hilo hiwa sioni mantiki yoyote ya maneno matamu ya hawa wanasiasa. Namkumbuka JKN na speech yake ya kutaka vijana wawe jeuri wa kuhoji mambo wakati yeye kitendo cha kutofautiana mawazo na Kambona kilifanya mwenzake kwenda uhamishoni.
Na bado atakuwa mtakatifu mida mida hivi ijayo.
 
Mkuu wa wilaya
"Tuliza mawowo wewe"
Angekuwa mwingine ametukana,amedhalilisha,ametumia lugha ya kuudhu.
DC kada hana hatia
 
Zamani wakurugenzi walitokana na wakuu wa idara hata ma DC walikuwa ma senior staff's toka kwenye taasisi za serikali...
Nitajie iyo zamani unayosema matokeo chanya kutokana na kuwapa wakurugenzi wakuu wa idara au madc kutokana na senior staffs kutoka kwenye taasisi za serikali. Nipe maarifa mkuuu tafadhali coz knowledge is power

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Wakuu mwenye kitabu cha big Ben naomba anisaidie nikisome
 
Mzumbe ilianzishwa lengo kuandaa wasomi katika nafasi mbalimbali katika tawala za mikoa na serikali za mitaa ie public administration na local government management
 
Mzumbe ilianzishwa lengo kuandaa wasomi katika nafasi mbalimbali katika tawala za mikoa na serikali za mitaa ie public administration na local government management
Na hawakutaka unafiki... wakawa specific.... INSTITUTE OF DEVELOPMENT & MANAGEMENT - IDM
 
Na hawakutaka unafiki... wakawa specific.... INSTITUTE OF DEVELOPMENT & MANAGEMENT - IDM
ndio maana yake tulitegemea maofisa wengi watoke huko lakini sasa hivi wanatoka UVCCM, MATANGA na CHAWA
 
Back
Top Bottom