Kutoka kitabu cha Kabendera: Mohamed Dewji alipotekwa alikuwa anapelekwa Benki jioni baada ya wafanyakazi wengine kutoka

Kutoka kitabu cha Kabendera: Mohamed Dewji alipotekwa alikuwa anapelekwa Benki jioni baada ya wafanyakazi wengine kutoka

Toa ushahidi badala ya ubabaishaji kuwa umesoma. Kwani, ukisoma unamsomea nani? Kwani Kabendera hawezi kudanganya au kutunga stori kama shigongo? Kwanini wangoje Jiwe atoweke ndiiyo waje kutuletea umbea? Si alikuwa nje si angeandika tu.
kama yale yaliyomo kwenye kitabu cha kabendera unaona ni uongo mtupu una haki ya kwenda mahakamani.....kafungue kesi
 
Hapa umejibu nini ? Kipi ni hatari zaidi? Kumteka mtu ili utembee nae kila jioni kwa kuwapigia watu simu ili wakae overtime ili uchukue pesa (as if hizo pesa ni kama pilau mnakenda kuipika kwenye hio benki), kumbuka kwa kufanya hivyo unaongeza uwezekano wa leakage hakuna siri ya watu wawili Au kutumia uwezo wako (power) na madudu ya mtu (mfanyabiashara hayakosekani) na kumshikiza (kufreeze akaunti) kwamba atoe kiasi fulani apeleke sehemu fulani au mtu fulani atakuja ampe kiasi fulani ?
Issue ya kutekwa kwa Mo ilijuikana kitaifa. Hata benki lazima ilijua, hivyo ingekeuwa ajabu kwa benki kuona millions zinatolewa kutoka kwenye akaunti ya tajiri wanayemfahamu na wanajua kuwa katekwa. Lazima wangetoa story polisi.
Kwenye hii script, mwandishi hakufikiria vizuri.
 
Fanya utafiti wako bado MO yupo hai halafu uje na hoja kukipinga hoja za kitabu
Huo muda wa kupoteza sina..., hizi zitabakia kuwa hearsay na He Say / She Say.., hata kama ilitokea, kufanya hio connection kwamba exactly fulani alihusika na ukizingatia ameshakufa na scene yenyewe ni political iliyojaa wazandiki, wahongo na self selfing people, chochote kitakachopatikana sasa hivi sio evidence bali upigaji ramli....

Thus ni bora hizo nguvu tukazitumia kwa majambazi wa sasa ambao bado wapo hai na kama kuna ujambazi wowote ulitumika then (wakati huo) basi na wao waliopo sasa wanahusika by association sababu walikuwa part of administration (and they were paid by taxpayers money kwahio even kukaa kimya wakati huo ilikuwa a betrayal)
 
Ebu mda mwingine tuwe tunashirikisha akili zetu vizuri alizotujaalia Mwenyezi Mungu,hivi kweli late Mkapa kwa pesa alizokuwa nazo alishidwa kwel kwenda south kwa matibabu kwa vile magu alikataaa yeye kwenda soutg
Mimi nilivyoelewa si kwamba familia ya mkapa haikuwa na uwezo wa kwenda South afrika kwa ajili ya matibabu, ila tatizo ni hayati magufuli alikataa kutoa ruhusa ya hilo kutokea.

Swali la kujiuliza ni kwanini magufuli akatae kutoa ruhusa kwa hayati mkapa kwenda kutibiwa South Africa? Mkapa alikuwa na athari gani kwake mpaka akatae kutoa ruhusa!? Bado nipo njia panda!
 
Okay, hata kama walitofautiana….

Kwa nini ahitaji [Mkapa] kibali toka kwa Magufuli cha kusafiri nje ya nchi?

Au labda mimi ndo sielewi. Hivyo nieleweshe.

Kila Mtanzania aliyetaka kusafiri nje ya nchi alihitaji kibali cha Magufuli?
Nyani mbona hivi! Unaposema kila Mtanzania ,unafikiri tunalingana kwa status! Mkapa alikuwa daraja la juu !hivi hujui kuwa Viongozi walizuiwa kwenda kumuona Tundu Lissu Hosp.kuna wachache wakajitoa ufahamu wakaenda akiwamo...
SAMIA! Unajua kilichompata Balazi Sokoine....kumtetea Magufuli kwenye eneo la ukatili ni ngumu Mno! Au umesahau kuwa watu walikatazwa kwenda Makanisani kumuombea Tundu Lissu!
Jamaa alikuwa katili kweli kweli hata mkewe na watoto wanajua!
Sijui kama Kabendera ametolea mfano kuwa Mshikaji alikuwa anakuja anakuja kulala Mabibo Hostel kwa Sundi Malomo?!😁
 
Mimi nilivyoelewa si kwamba familia ya mkapa haikuwa na uwezo wa kwenda South afrika kwa ajili ya matibabu, ila tatizo ni hayati magufuli alikataa kutoa ruhusa ya hilo kutokea.

Swali la kujiuliza ni kwanini magufuli akatae kutoa ruhusa kwa hayati mkapa kwenda kutibiwa South Africa? Mkapa alikuwa na athari gani kwake mpaka akatae kutoa ruhusa!? Bado nipo njia panda!
Roho mbaya tu.

Humjui Lucifer wewe! Kwani CCTV CAMERA pale Area D kwa Lissu zilizimwa na nmi au wale walinzi walitoroka LINDO.kwenda kwa michepuko?!
 
Acha upotoshaji wa kijinga, ccm haiko madarakani kwa ridhaa ya wananchi, bali iko kwa mbeleko ya vyombo vya dola.
Kama wapiga kura wengi ndio wenye akili kama zako, sio ccm tu, hata chama kingine chochote wala hakihitaji mbeleko ya dola kubaki madarakani, labda mbeleko ya nyasi.
 
Watanzania bwana, unakuta mtu mzima kabisa na bahati nzuri ameenda shule ajabu utakuta anapoteza muda wake eti ananunua kitabu cha Yerico Nyerere ama Kabendera na anasoma kabisa na mbaya zaidi anaamini ule ujinga ulioandikwa mule😂.

Ndio maana ccm inaendelea kua madarakani miaka na miaka na hakuna wanachokifanya cha kimaendeleo lakini wanaendelea tu kwa sababu watu wa kuwatoa hawapo maana ccm imekua ikiwadanganya na kuwafukarisha kwa miaka zaidi ya 60 na bado wanaichagua.

Nadhani Tanzania ni nchi yenye binadamu wa aina yake Duniani, special human species.
True hii nchi imejaa wajinga sana ndio maana Ccm inajua ifanye nini ili iendelee kutawala ni simpe tu,
 
Roho mbaya tu.

Humjui Lucifer wewe! Kwani CCTV CAMERA pale Area D kwa Lissu zilizimwa na nmi au wale walinzi walitoroka LINDO.kwenda kwa michepuko?!
Siwezi kukupinga ndugu yangu.

Ila kwa mazingira ya Tundulisu tunaweza kuamini kutokana na harakati alizokuwa akizifanya pamoja na matamko ya hayati magufuli akisema anataka kuhakikisha anafuta upinzani.

sasa kwa stori ya hayati mkapa kunyimwa kibali bado nipo njia panda, kama raisi anaweza kuhamisha pesa kutoka kwenye akaunti za wafanyabiashara, ku-freeze pasi na shaka anayo nguvu ya kuzuia pia kibali.

Lakini swali ni kwann azuie? Labda walikua na ugomvi unaoendelea chini kwa chini? Mimi bado nina maswali mengi.

Lakini pia stori ya hayati magufuli kuwa na tuhuma za unyanyasi wa kingono (sexual harassment) kwa kiongozi ambaye ni mkubwa ni kashfa kubwa sana. Hatuelewi je lilipotokea tukio alifanikisha au hakufanikisha?

Na kwanini anayehusika na tukio hilo yupo kimya mpaka sasa na ni kiongozi mkubwa wa nchi? Binafsi nabaki na maswali mengi yasiyo na majibu
 
Mimi nilivyoelewa si kwamba familia ya mkapa haikuwa na uwezo wa kwenda South afrika kwa ajili ya matibabu, ila tatizo ni hayati magufuli alikataa kutoa ruhusa ya hilo kutokea.

Swali la kujiuliza ni kwanini magufuli akatae kutoa ruhusa kwa hayati mkapa kwenda kutibiwa South Africa? Mkapa alikuwa na athari gani kwake mpaka akatae kutoa ruhusa!? Bado nipo njia panda!
Kuna mdau hapo juu kasema, ni kwakuwa mzee B alisema akiwa hai hakuna mtu atakayeongoza zaidi ya mihula miwili.
 
Kwamba Fingerprint ya Mo ilikuwa inatakiwa kutoa hizo Pesa ? Yaani watu wenye Power ya kuteka, kufreeze akaunti na kupigia mameneja wakae mpaka jioni kutoa pesa wanashindwa kushinikiza pesa iwe transferred popote wanapotaka au wakati wowote wanaotaka ?

This is insulting our intelligence...
mkuu nimeamini hii inchi imejaa wajinga sana ndio maana hata Wanasiasa wanadharau wananchi unakuta mbuge mwaka wa uchaguzi anawaletea wananchi drafti sababu watu hatuwezi kutafakar vizuri kabla ya kuamua, tunaongozwa na hisia
 
CCM inabaki madarakani kwa kutumia mtutu wa bunduki na wala sio kwa sababu watu wananunua vitabu vya yeriko na kabendera usijitoe ufahamu mkuu
mdau amemaanisha watanzania wengi ni low IQ na ndio maana ametolea mfano wanaonunua vitabu vya Yeriko na Kabendera
 
###Kwa wale wavivu wa kusoma vitabu Matukio mbalimbali ndani ya kitabu cha kabendera yatakuwa huku kwenye huu uzi ###

Fedha zilikuwa zinatolewa kwenye account za kampuni, bank manager walikuwa wanapigiwa simu kusubiria bank jioni, kisha Mo anatokea akiwa na watu wa mfumo kutoa fedha. Mo bana kumbe anaficha vitu vya ajabu hivi kwa mujibu wa kitabu,

Mgogoro ulikuwa ni wa kikodi, baada ya kuchallenge Jiwe akamdaka na kushinikiza ile pesa ilipwe, ikalipwa cash akachukua Jiwe cash na haikuingia serikalini, wafanyabiashara wengi wamefanyiwa huu mchezo na ndio fedha baadhi alitumia kwenye uchaguzi huu

Nawakumbusheni msome kitabu
Kabendera kdanganya sana kwenye kitabu chake
 
Back
Top Bottom