SoC02 Kutoka kuajiriwa mpaka kujiajiri

SoC02 Kutoka kuajiriwa mpaka kujiajiri

Stories of Change - 2022 Competition

Leetom

Member
Joined
Aug 28, 2022
Posts
21
Reaction score
49
Katika kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira ulimwenguni, serikali na wadau mbalimabli husisitiza dhana ya kujiajiri. Jamii inaamini kuwa kujiajiri ndiyo tiba mbadala ya janga la ukosefu wa ajira. Ukisikiliza maoni ya vijana wengi kuhusu kujiajiri ni lazima utakumbana na changamoto ya ukosefu wa mitaji. Ndiyo, changamoto ni mtaji! Lakini mtaji si changamoto pekee iliyopo inayokwamisha vijana kujiajiri……

Ili kutekeleza dhamira yangu ya kujiajiri, nilianza kuweka akiba mara baada ya kuoa. Si unajua tena harusi zilivyo na mambo mengi, hivyo nililazimika kujichanga upya. Tulikubaliana kuweka akiba ya 200,000/- kila mwezi. Kama ilivyo kwa vijana wengi, kichwani mwangu tayari nilikuwa na wazo la biashara hivyo niliamini kilichobaki ni kutafuta mtaji. Nilitamani sana kufanya biashara ya kuuza nafaka.

Nikiwa bado sijakusanya mtaji wa kutosha, kazini kulitokea mgogoro ulionilazimu kujiudhuru. Kwangu mimi niliona ni fulsa ili nipate muda wa kutekeleza wazo langu la biashara. Ikumbukwe kuwa hapo awali sikuwahi kufanya biashara yeyote ile. Huu ulikuwa ni uthubutu wa pekee katika maisha yangu.

Baada ya kuacha kazi, mwezi huohuo nilisafiri kutoka Geita kwenda Mbeya kununua mahindi. Wakati huo familia yangu nilikwisha ihamisha kutoka kwenye nyumba ya kampuni kwenda kwenye nyumba ya kupanga. Nililipa kodi ya miezi sita (720,000/-) kutoka kwenye akiba niliyokuwa nimeiweka.

Nikiwa Mbeya, mambo yalikwenda kinyume na matarajio kwani haukuwa msimu wa mavuno. Bei ya mahindi ilikuwa ghali na upatikanaji wake ulikuwa mgumu. Dalali alinitafutia mzigo pamoja na usafiri wa kwenda Dar Es Salaam. Kwa sababu ya bei kuwa ghali na mtaji mdogo (4,000,000/-), niliweza kununua magunia ya mahindi 85 tu.

Nikiwa Manzese (Dar Es Salaam) dalali aliniuzia mzigo wangu, tukiwa kwa mteja ilionekana baadhi ya mahindi hayakuwa na ubora hivyo nililazimika kuyauza kwa bei ya chini na kupata hasara ya Tsh. 200,000/-. Pamoja na kupata hasara lakini nilirudi tena Mbeya kununua mzigo mwingine. Niliongeza umakini katika kuchagua mahindi yanayokidhi ubora wa soko. Nilipofika sokoni nilikuta kuna mahindi mapya kutoka Handeni (Tanga) hivyo soko la mahindi ya zamani liliendelea kushuka siku hadi siku.

Baada ya kupata hasara mara mbili mfululizo huku soko la mahindi likiyumba, niliamua kugeukia biashara ya maharage. Pale Mbeya ulikuwa ni msimu wa maharage na nilishafuatilia soko lake Tandika. Nilipanda gari kwenda kununua maharage. Kwa kuwa mtaji wangu ulikuwa umepungua sana, nilinunua magunia 19 tu kwa thamani ya 160,000/- kwa gunia. Bei ya maharage sokoni ilikuwa nzuri ila changamoto ni kwamba baadhi ya maharage hayakukauka vizuri hivyo nililazimika kuwalipa watu fedha ili wayaanike na kuyachambua vizuri. Kutokana na urefu wa safari na joto kali baadhi ya maharage yaliharibika na nililazimika kuyatupa.

Kwa kuwa maharage yalikuwa yanachukua muda mrefu sokoni, ilinilazimu kuchukua fedha kidogo iliyopatikana na kwenda Handeni kununua mahindi wakati huo nikisuburi dalali anitumie fedha inayopatikana kutokana na mauzo ya maharage yaliyobakia sokoni.

Nikiwa Handeni, madalali walinitafutia mzigo nikajikuta nimetumia kiasi chote cha fedha niliyokuwa nayo. Huko Tandika (sokoni), dalali alidai kuwa biashara siyo nzuri hivyo fedha hakuna. Hapo nilijikuta kwenye wakati mgumu kwani sikuwa na pesa mfukoni. Nililazimika kuomba hifadhi kwa watu japo kwa usiku huo tu bila kujali kwamba nilikuwa nimeshinda njaa. Tatizo halikuwa njaa tu kwani siku hiyo nilikuwa nimetembea umbali wa takribani kilomita 10 katika harakati za kufuatilia mzigo.

Asubuhi ninaamka baada ya usiku mrefu usio na matumaini ya kuifanikisha kesho mara nakutana na SMS kutoka kwa mke wangu akiomba fedha ya matumizi. Ikumbukwe kuwa sikuwa nimeonana na familia yangu kwa miezi 3 sasa na wakati naondoka tulikuwa tuna mtoto wetu wa kwanza mwenye mwezi mmoja. Nililazimika kukopa fedha pasipo matarajio ya kuilipa.

Pamoja na kupoteza biashara na ajira lakini kuna shule nilipata. Haya ni baadhi ya mambo niliyojifunza; mosi ni uthubutu wa kuweza kuanzisha biashara, pili ni kuweza kuishi nje ya mfumo rasmi wa ajira, tatu nilijifunza mnyororo wa thamani katika mazao ya nafaka na kubwa zaidi ni kuweza kuitazama fedha kwa jicho la kiujasiriamali, hii ilinijengea uwezo wa kuthamini fedha kwa nidhamu kuliko hapo awali. Hali kadhalika niligundua kuwa mtaji siyo takwa pekee ili vijana waweze kujiajiri. Ili majasiliamali kijana aweze kufanya vizuri anahitaji wazo la biashara, elimu ya biashara, mtaji, eneo sahihi la biashara, usimamizi madhubuti na kuwa mbunifu kulingana na mwenendo wa soko.

Wazo pekee lenye nguvu lililonijia ni kuanza upya, watu husema kuanza upya siyo ujinga! Niliamua kuuza mahindi yote ili nipate nauli pamoja na fedha za kujikimu. Nikiwa nyumbani na familia yangu nilianza kutuma maombi ya kazi katika kampuni mbalimbali na baada ya miezi mitatu ya machozi na damu nifanikiwa kupata kazi Dar es Salaam.

Huu ndiyo ulikuwa wakati pekee wa kudhihirisha kuwa nilishapitia mafunzo kwa vitendo na kufuzu katika maeneo ya nidhamu ya fedha na kutafuta mtaji ili kuendelea na safari ya kujiajiri. Niliweza kuishi kimkakati kwa kuweka 65% ya mshahara kama akiba. Hii si rahisi hata kidogo! Iko hivi, kama mshahara ni 500,000/- inabidi utenge 325,000/- kama akiba na kiasi kinachobaki (175,000/-) ni kwa ajili ya matumizi mengine. Hili haliwezekani isipokuwa umejikana kwelikweli! Lakini pia mkoa niliokuwa nafanyia kazi ulikuwa ni wa kimkakati kwani niliweza kufanya kazi ya kuajiriwa na baadae kujiajiri pasipo kuihamisha au kutengana na familia yangu.

Baada ya miezi 15 tayari nilikuwa nimepata fedha ya kutosha, mara moja nilianzisha biashara huku nikiendelea na ajira. Nilifungua biashara ya kuuza mchele kwa jumla na rejareja pale Tandika sokoni. Mke wangu ndiye alikuwa msimamizi wa biashara yetu na mimi nilikuwa nikifanya ufuatiliaji kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha kila kitu kipo sawa. Biashara iliendelea kustawi hadi kufikia hatua ya kuuza mpaka tani 30 za mchele kwa mwezi. Faida iliyopatikana kwa mwezi ilikuwa ni mara tatu zaidi ya mashahara wangu.

Kadri biashara ilivyozidi kukua ndiyo niliona umuhimu wa kuongeza usimamizi. Hii ilinilazimu kuacha kazi ya kuajiriwa ili nipate muda wa kutosha wa kusimamia biashara yetu na kupanua wigo wa masoko. Ninalenga kujenga ghala la nafaka na kusimika mashine za kisasa za kuongeza thamani zao la mpunga na mahindi jijini Mbeya. Sanjari na hilo, kwa upande wa masoko ninalenga kuzifikia taasisi za elimu kama vile vyuo na shule ili niweze kuuza nafaka kama mzabuni.

Screenshot_20220831-093701_Instagram[1].jpg
Picha: Mashine ya kukoboa na kusaga mahindi (Chanzo: afi_green)

1.Hongdefa-maize-milling-plant-570x350[1].png

Picha: Mashine ya kukoboa mpunga (Chanzo: maizewheatmill.org)
 
Upvote 18
Sasa hapa ndio unaanza kushusha nondo mkuu,kulejuu sawa Ila ndio hivyo wingi wa maneno ulikubana,
Imelipenda andiko lako Ila nadhani kunaziada kidgo hasa codes za kinidhamu ambazo ulizipata baada ya kuanguka Mara ya kwanza ukazirekebisha ukaweza kusimama na kupiga hatua.
Unajua sisi watz huwa tunatatizo la kutoangaliaga mambo kwa upande wake,wabinafsi hatupendi kwenda mbaali tukiwa pamoja tuna penda kwenda haraka pekeyetu,sasa sikutukianguka ni kifo maana hakuwa na wenzako nani atakuinua?
Tujifunze kushirikishana namna ya kufanikiwa maana katika Yale uyasemayo katika watu 10 watakao yasikia na kuyajaribu watakao weza kuyaishi labda ni m1 so tusiogope kutoa codes maana hizo codes ni funguo zako za mafanikio ambazo mtu anaweza kuzitumia Kama reff zake wakati nae anajaribu kutafuta codes zake,maana naamini hata wewe ukujafuatilia kwa undani hakuna jipya ambalo umegundua ni just principles ambazo waliotangulia walishazisema Ila uliweza kuzitilia maanani baada ya kupitia anguko lako.
So usihofu ndugu,huwa inakaa vizuri kichwani ile inayosemwa na mtu alieziishi na zikamsaidia kusogea na akathibitisha.
Nimejaza bando la week nasubiri nondo hizo muungwana.
 
Ushauri wako ni ipi kwetu tuliobado ajirani hasa ktk eneo la usimamizi, nakuona kama kikwazo kikubwa sana
 
Kwa wale ambao mmeajiriwa iwe serikalini au sekta binafsi nadhani changamoto mojawapo ni mshahara kutokukidhi mahitaji na uhuru wa fedha (financial freedom).​

Kama umekuwa na ndoto ya kutaka kujiajiri lakini unashindwa, nakushauri usome makala yangu inayosema "KUTOKA KUAJIRIWA MPAKA KUJIAJIRI"​

Kama utakuwa na maswali niulize tujadiliane kwani mimi nimepitia njia hiyo na kuzishinda changamoto.​
Asante sanamkuu kwa makala nzuri yenye kujenga naukombozi wa kiuchumi.
 
Hongera sana broh!! Kuna jambo nimejifunza maana nishafeli mara mbili kwenye biashara ila imenipa funzo kubwa tu
 
Mwaka 2014 nilihitimu Chuo na Mungu akanijalia kuingia moja kwa moja kwenye ajira Rasmi ya Serikali nilifanya kazi ile kwa miaka mitatu ila sikuona kama ni Ajira ambayo ingenitoa/kunipa Maisha Mazuri Ambayo Yalikuwa ya Ndoto Yangu,,Baada ya kutafakari niliona ili nifanikiwe Kumiliki Nyumba nzuri,watoto kusoma shule za kisasa ni lazima niingie kwenye mikopo ambayo inaweza fanya kwa mwezi mshahara ukakatwa hadi kubaki laki mbili na deni unaweza lipa hata kwa miaka 15,,nikatizama ndugu yangu ambae aliishia Form Four akashindwa kuendelea na masomo(alifeli) akajikita kwenye biashara alikuwa kapiga hatua kiasi kuna muda nakwama ananiazima hela,,nilitegemea Kupanda Daraja mwaka 2016+nyongeza ila hayati JPM alikuja na sera tofauti,Mwaka 2017 nikaamua Rasmi kuacha kazi ya serikali kwa Hiyari japo watu wasiojua asili yangu hata waajiri na watumishi wenzangu walinishangaa sanaa sanaa na kuninyooshea vidole wakinitisha mtaani kugumu mwingine akaapa kuwa ifikapo 2019 kama sitakuwa nimepiga simu kumuazima fedha ya kutumia nimuite MBWAA
HISTORIA YANGU KWA UFUPI MNO
Mimi nimezaliwa katika familia ya Wazazi,Ndugu(baba wadogo,baba wakubwa) wafanyabiashara tu,,toka tuko wadogo sana tulikuwa tunazoeshwa biashara(kuuza duka)kiasi nafika drs la tano mama alikuwa na uwezo wa akapata dharura akatuacha mimi na dada yangu mimi La Tano yeye la Sita tukauza bila shida yeyote na jioni tukafunga mahesabu vizuri,,kufika namaliza drs la Saba tayari nilikuwa naagizwa kwenda Mjini kufunga mzigo na kurudi nao dukani,,


Wazazi wangu na ndugu zangu walibariki mimi kuacha kazi,,kaka Yangu Mkubwa yeye pia aliajiriwa seriakalini 2007 akaacha 2013 alikiwa mmoja ya watu waliobariki uamuzi huo na Rasmi nikajikita katika baishara,,nilirudi sikutaka kuishi au kufanya Mjini nilienda moja ya wilaya iliyo pembezoni na Mkoa wa Arusha kufika kule nlikuta hakuna mtu anatoa huduma Rasmi za huduma za Fedha,,wapo walokuwa wanatoa ila hawakuwa Rasmi ilikuwa kama mfano kama unataka kutoa hela ni umtumie kwenye laini yame binafsi kiasi alafu kila elfu 10 anakata Elfu kumaanisha laki atakukata Elfu 10

Nikatafuta eneo nikafungua ofisi kubwa ya kutoa huduma Rasmi za kifedha kufika leo nadhani hakuna wakala maarufu kunizidi na anaefanya miamala mingi na kupata comision kubwaa kuzidi hata walio city centre(mwaka 2020 vodacom walikuwa na shidano la mawakala kwa zone Arusha North kwa wakala ambae atafanya Miamala mingi zaidi+kusajili wateja wengi zaidi niliibuka namba Moja)

Pia nilifungua Biashara ya Grocery+pooltable na kwa sasa nimeongeza huduma zaidi nauza Simu+vifaa vya umeme na ninauza Mbao(nazitoa Mafinga)


Kwa ufupi Hali niliyonayo sasa imepelekea wale watu waliona nitafeli kutamani kuacha,bado nipo katika group letu la kule nilipoacha kazi wengi wao wanatamani kuacha na huwa wanaiomba ushauri ila Mimi huwa nawaambia Kamwe siwezi mshauri mtu kuacha kazi sababu sijui kama una uzoefu na unachotaka kwenda kufanya japo kuna wawili waliacha nao wanapambana huko



NB:kama una biashara zoesha watoto wako mapema wafanye wazoee hela mapema sio kijana anafika hadi drs la saba hajawahi ona laki tano ina wingi gani,anafika Chuo lile Boom ndo inakuwa hela yake kubwa ya kwanza kuona na kushika,hili litakuja mtesa sana uraiani...



Tchao
 
Mwaka 2014 nilihitimu Chuo na Mungu akanijalia kuingia moja kwa moja kwenye ajira Rasmi ya Serikali nilifanya kazi ile kwa miaka mitatu ila sikuona kama ni Ajira ambayo ingenitoa/kunipa Maisha Mazuri Ambayo Yalikuwa ya Ndoto Yangu,,Baada ya kutafakari niliona ili nifanikiwe Kumiliki Nyumba nzuri,watoto kusoma shule za kisasa ni lazima niingie kwenye mikopo ambayo inaweza fanya kwa mwezi mshahara ukakatwa hadi kubaki laki mbili na deni unaweza lipa hata kwa miaka 15,,nikatizama ndugu yangu ambae aliishia Form Four akashindwa kuendelea na masomo(alifeli) akajikita kwenye biashara alikuwa kapiga hatua kiasi kuna muda nakwama ananiazima hela,,nilitegemea Kupanda Daraja mwaka 2016+nyongeza ila hayati JPM alikuja na sera tofauti,Mwaka 2017 nikaamua Rasmi kuacha kazi ya serikali kwa Hiyari japo watu wasiojua asili yangu hata waajiri na watumishi wenzangu walinishangaa sanaa sanaa na kuninyooshea vidole wakinitisha mtaani kugumu mwingine akaapa kuwa ifikapo 2019 kama sitakuwa nimepiga simu kumuazima fedha ya kutumia nimuite MBWAA
HISTORIA YANGU KWA UFUPI MNO
Mimi nimezaliwa katika familia ya Wazazi,Ndugu(baba wadogo,baba wakubwa) wafanyabiashara tu,,toka tuko wadogo sana tulikuwa tunazoeshwa biashara(kuuza duka)kiasi nafika drs la tano mama alikuwa na uwezo wa akapata dharura akatuacha mimi na dada yangu mimi La Tano yeye la Sita tukauza bila shida yeyote na jioni tukafunga mahesabu vizuri,,kufika namaliza drs la Saba tayari nilikuwa naagizwa kwenda Mjini kufunga mzigo na kurudi nao dukani,,


Wazazi wangu na ndugu zangu walibariki mimi kuacha kazi,,kaka Yangu Mkubwa yeye pia aliajiriwa seriakalini 2007 akaacha 2013 alikiwa mmoja ya watu waliobariki uamuzi huo na Rasmi nikajikita katika baishara,,nilirudi sikutaka kuishi au kufanya Mjini nilienda moja ya wilaya iliyo pembezoni na Mkoa wa Arusha kufika kule nlikuta hakuna mtu anatoa huduma Rasmi za huduma za Fedha,,wapo walokuwa wanatoa ila hawakuwa Rasmi ilikuwa kama mfano kama unataka kutoa hela ni umtumie kwenye laini yame binafsi kiasi alafu kila elfu 10 anakata Elfu kumaanisha laki atakukata Elfu 10

Nikatafuta eneo nikafungua ofisi kubwa ya kutoa huduma Rasmi za kifedha kufika leo nadhani hakuna wakala maarufu kunizidi na anaefanya miamala mingi na kupata comision kubwaa kuzidi hata walio city centre(mwaka 2020 vodacom walikuwa na shidano la mawakala kwa zone Arusha North kwa wakala ambae atafanya Miamala mingi zaidi+kusajili wateja wengi zaidi niliibuka namba Moja)

Pia nilifungua Biashara ya Grocery+pooltable na kwa sasa nimeongeza huduma zaidi nauza Simu+vifaa vya umeme na ninauza Mbao(nazitoa Mafinga)


Kwa ufupi Hali niliyonayo sasa imepelekea wale watu waliona nitafeli kutamani kuacha,bado nipo katika group letu la kule nilipoacha kazi wengi wao wanatamani kuacha na huwa wanaiomba ushauri ila Mimi huwa nawaambia Kamwe siwezi mshauri mtu kuacha kazi sababu sijui kama una uzoefu na unachotaka kwenda kufanya japo kuna wawili waliacha nao wanapambana huko



NB:kama una biashara zoesha watoto wako mapema wafanye wazoee hela mapema sio kijana anafika hadi drs la saba hajawahi ona laki tano ina wingi gani,anafika Chuo lile Boom ndo inakuwa hela yake kubwa ya kwanza kuona na kushika,hili litakuja mtesa sana uraiani...



Tchao
Wewe Ni Kama mie tu. Sema la kwanza naachiwa duka nasimamia ,shida ambayo bado napambana nayo Ni kujiajiri bado nasaka Ajira nipate kamtaji kadogo. Kuna muda nilipata kubwa sema ndugu akawa kikwazo nikawa nimerudi zero
 
Wewe Ni Kama mie tu. Sema la kwanza naachiwa duka nasimamia ,shida ambayo bado napambana nayo Ni kujiajiri bado nasaka Ajira nipate kamtaji kadogo. Kuna muda nilipata kubwa sema ndugu akawa kikwazo nikawa nimerudi zero
Sometime kunakuwaga na ndugu miyayusho sana
Ila nachoshukuru MUNGU kama familia tulikuzw katika misingi ya Dini sana na tumeshikana hadi leo[emoji120][emoji120]
 
Sometime kunakuwaga na ndugu miyayusho sana
Ila nachoshukuru MUNGU kama familia tulikuzw katika misingi ya Dini sana na tumeshikana hadi leo[emoji120][emoji120]
Kuna point kubwa mno umeongea sema Kama Kuna somo inabidi kulielewa sijui mpaka uwe umeumwa na ama umeona utamu ama uchungu wake ndio utaelewa. Yaani lazima mtt angalau ajue kufanya kazi ama biashara mbali na kumeza mno masomo ya darasani.
"The only thing you can learn from a business school professor is how to become a business school professor." - Nassim Nicholas Taleb
 
Back
Top Bottom