Kutoka kuwa mke wa ndoa na kuwa mchepuko

Kutoka kuwa mke wa ndoa na kuwa mchepuko

M2WAWA2

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2014
Posts
3,285
Reaction score
5,598
Asante Mungu!!!

Ni miezi 18 tangu Mahakama kutengua ndoa iliyofungwa miaka 8 iliyopita.

Na huu ukawa mwanzo wa maisha mpya, maisha ya utulivu wa akili, amani moyoni na huru wa maamuzi.Na ukawa Mwisho wa maisha ya mateso ya Kihisia, kiakili, na kisaikolojia-hapa wanaume wengi wanapitia mateso ya hivi.


Maisha yale, yalikuwa ya ushindani, upinzani, kesi za uongo na vikao vya kila mara vya usuruhishi, bila kusahau zile dharau na jeuri na kiburi vyote hivi vikitakaswa na utetezi wa "Hata biblia inasema tuishi na wanawake kwa akili".

washauri wako wakuu kwenye kila kitu ni wale wana kikundi wenzio, wakifuatiwa na ndugu. Hawa waliweza kutoa ushauri na maamuzi makubwa ya ndoa yako bila hata ya kujua ya upande wa pili. bila Kujali una ongeza thamani gani kwenye familia.Walikuona wewe u mtakatifu na kusahau kwamba "kila matokeo, yana sababu zake", "kila mtu huvuna kile alicho panda". Walikushauri na ukatenda Ogopa sana wajumbe wa kwenye ndoa! Wakiharibu hutawanyika


Ninachotaka kusema ni hivi:

1. Ulitoa nafasi kwa wale watu kuwa washauri na wasemaji wakuu wa ndoa yako.Naam nao walikuwa nawe bega kwa bega, mpaka pale ndoa ilipo vunjika na sasa kila mtu kachukua njia yake na kuendelea na maisha yao na watoto wao. wengi walikushauri mambo ambayo hata wao hawawezi fanya kwenye ndoa zao!

2. Kwamba ule uzuri wa sura na maumbile na elimu na kazi nzuri na ile biashara yako, ilikufanya uonekane wewe ni wewe, ule wajibu na majikumu ya mke uliona ni takataka, hata majukumu ya unyumba hukuona kama ni muhimu kujitoa. Biblia ina sema tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala mwanzo 3:16

Ni kupitia drama zako na kipaji cha uongo ndoa ilifika tamati na nina amin uko uliko uhalisia wa maisha unauona sasa!
  • Nasikia ile nyumba umejenga kwa nguvu, nguvu ya uchi, nguvu ya kutembea na waume za majiran zako, ili kuniumiza!
  • Nasikia hata yule aliyetelekeza mke wake kwa ajili yako naye amekutelekeza wewe pia. Malipo ni hapa hapa
  • Nasikia hata yule kijana dereva unaye tembea naye, alikwenda kuoa mwanamke kwao, na kukuacha wewe mwenye sifa zote za uzuri na kipato! nasikia kijana huyu huyu anatembea na msichana wako wa kazi, na ndio mtoa taarifa zote hizi.
  • Nasikia sasa unatafuta danga litakalokupa pesa za kutosha , milion milion tu, na uko mbioni kumkamata yule mwalimu wa chuo kikuu.
  • Nasikia unatumia maji ya upako siku nikija kuona watoto nirudishe moyo nyuma!
  • Nasikia hata kuroga umeroga sana ili turudiane, bila shaka ni baada ya kusikia makubwa niliyofanya kwa kipindi kifupi. Nawe umeshuhudia ustawi wangu wa kiuchumi, kijamii,na kiimani. Hata wale ulio kuwa unanilinganisha nao sasa hivi si kitu.

Je unajisikiaje kutoka kuwa mke wa mtu na kuwa mchepuko wa kitaa?, na umri ndio hivyo tena.
Wakati Mwanaume ni mbegu!, na mashamba ya kupanda ni mengi, mengine hayajatumika kabisa.

Funzo: Ulicho nacho kitunze!
 
"Ukimuelimisha mwanamke umeelimisha jamii, na ukimkomboa mwanamke umeikomboa jamii......."

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Huwa natikisa kichwa tu kisha na sonya naendelea na shughuli zangu.
 
Kama kweli wewe uliyeandika hii ndio umeachana na mkeo basi kuna mawili either wote ni waimba taarabu au mume umezidi uongeaji na kuna uwezekano alikuwa anakudharau kwa sababu kwa sababu hii.

Mi mwenyewe imebidi nirudi juu kuangalia id ya mleta mada, nilidhani ni yule dokta remember.
 
Kama kweli wewe uliyeandika hii ndio umeachana na mkeo basi kuna mawili either wote ni waimba taarabu au mume umezidi uongeaji na kuna uwezekano alikuwa anakudharau kwa sababu kwa sababu hii.
Siku ukiyapitia haya ndio utamwelewa jamaa alieandika hapa.

FACT: Hakuna kazi ngumu kama kuishi na mwanamke aliekuzidi kipato
 
Asante Mungu!!!

Ni miezi 18 tangu Mahakama kutengua ndoa iliyofungwa miaka 8 iliyopita.

Na huu ukawa mwanzo wa maisha mpya, maisha ya utulivu wa akili, amani moyoni na huru wa maamuzi.Na ukawa Mwisho wa maisha ya mateso ya Kihisia, kiakili, na kisaikolojia-hapa wanaume wengi wanapitia mateso ya hivi.


Maisha yale, yalikuwa ya ushindani, upinzani, kesi za uongo na vikao vya kila mara vya usuruhishi, bila kusahau zile dharau na jeuri na kiburi vyote hivi vikitakaswa na utetezi wa "Hata biblia inasema tuishi na wanawake kwa akili".

washauri wako wakuu kwenye kila kitu ni wale wana kikundi wenzio, wakifuatiwa na ndugu. Hawa waliweza kutoa ushauri na maamuzi makubwa ya ndoa yako bila hata ya kujua ya upande wa pili. bila una ongeza thamani ganai kwenye familia.Walikuona wewe u mtakatifu na kusahau kwamba "kila matokeo, yana sababu zake", "kila mtu huvuna kile alicho panda". Walikushauri na ukatenda Ogopa sana wajumbe wa kwenye ndoa! Wakiharibu hutawanyika


Ninachotaka kusema ni hivi:

1. Ulitoa nafasi kwa wale watu kuwa washauri na wasemaji wakuu wa ndoa yako.Naam nao walikuwa nawe bega kwa bega, mpaka pale ndoa ilipo vunjika na sasa kila mtu kachukua njia yake na kuendelea na maisha yao na watoto wao. wengi walikushauri mambo ambayo hata wao hawawezi fanya kwenye ndoa zao!

2. Kwamba ule uzuri wa sura na maumbile na elimu na kazi nzuri na ile biashara yako, ilikufanya uonekane wewe ni wewe, ule wajibu na majikumu ya mke uliona ni takataka, hata majukumu ya unyumba hukuona kama ni muhimu kujitoa. Biblia ina sema tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala mwanzo 3:16

Ni kupitia drama zako na kipaji cha uongo ndoa ilifika tamati na nina amin uko uliko uhalisia wa maisha unauona sasa!
  • Nasikia ile nyumba umejenga kwa nguvu, nguvu ya uchi, nguvu ya kutembea na waume za majiran zako, ili kuniumiza!
  • Nasikia hata yule aliyetelekeza mke wake kwa ajili yako naye amekutelekeza wewe pia. Malipo ni hapa hapa
  • Nasikia hata yule kijana dereva unaye tembea naye, alikwenda kuoa mwanamke kwao, na kukuacha wewe mwenye sifa zote za uzuri na kipato! nasikia kijana huyu huyu anatembea na msichana wako wa kazi, na ndio mtoa taarifa zote hizi.
  • Nasikia sasa unatafuta danga litakalokupa pesa za kutosha , milion milion tu, na uko mbioni kumkamata yule mwalimu wa chuo kikuu.
  • Nasikia unatumia maji ya upako siku nikija kuona watoto nirudishe moyo nyuma!
  • Nasikia hata kuroga umeroga sana ili turudiane, bila shaka ni baada ya kusikia makubwa niliyofanya kwa kipindi kifupi. Nawe umeshuhudia ustawi wangu wa kiuchumi, kijamii,na kiimani. Hata wale ulio kuwa unanilinganisha nao sasa hivi si kitu.

Je unajisikiaje kutoka kuwa mke wa mtu na kuwa mchepuko wa kitaa?, na umri ndio hivyo tena.
Wakati Mwanaume ni mbegu!, na mashamba ya kupanda ni mengi, mengine hayajatumika kabisa.

Funzo: Ulicho nacho kitunze!
Mkuu,kuna kitu hapa,For the past two years nimeshuhudia wanawwake kadhaa wakiondoka kwa waume zao kwa mbwembwe na kuishiwa kuwa michpeko ya mtaa.Kuna tatizo mahali inagwa sijajua hasa ni nini.
 
Hawa wanao sema unampenda rudiana nae wanamatakataka kichwani katu usifanye hivyo hata Kama unampenda. Licha ya kuvunja ndoa ameenda kufanya udangaji.hajamaliza kafanya ushirikina ....bro Bible inatuasa Nini juu ya mwanamke Malaya na Mshirikina ......?

Bro wewe ni wa thamani sana ..... Kuna pissi nyingi Sana jikaze endelea kunilia good time yako.

Hakuna mwanamke mjanja .....ila ukiona mwanamke mjanja jua Kuna mwanaume yupo nyuma na huyo mwanamke ndio alie sambaratisha ndoa yako na saizi huyo jamaa kamkimbia ndio maana anatapatapa ...

#ukimkuta Kobe juu ya mti we jua kapandishwa
 
Anaendelea na maisha yake. Nyumba amejenga kwa uch.i, hongera zake.

Wewe hujamtoa akilini mwako au unamuombea mabaya mtalaka wako.

Usijali, atapata wengine wa kuwapa uch.i tena. Uch.i mali yake anatumia apendavyo. Pambana na hali yako
 
Hapo wanaume wengi ndio wanapo-fail. Unaachana na mwanamke bado unamfuatilia na kuulizia ulizia hatua zake. Mnapoteza muda sana. Hapo ujue bado unampenda. Na ndio wanaume wengi wanaume wengi wanaumia mpaka wengine kuingia kwenye ugomvi mpaka kuuana akisikia mtalaka wake amepata mwingine na unakuta wako njema kimaisha. Nakuusia kama umeamua kuachana na mtu (mke) hakikisha hata hatua yake moja usiijue,funga masikio watu wasikuletee ya toka kwa huyo alikuwa mke wako. Ikiwezekana hamia mbali kabisa na upande alipo,hakikisha moyoni unamsahau kabisa,iwe kwa mabaya au mazuri sahau kabisa kama uliwahi kuwepo nae,anza upya. Huku ukikomaa sana kuweka sawa maisha yako kwa njia ya shughuri unazozifahamu. Sasa hivi umeleta taarabu na mipasho hiyo eti imfikie mkeo wa zamani,wewe ndio mwanamke sasa,tena zaidi ya mwanamke. Ume-fail sana. Wanaume wa hivyo sijui nawaonaje
 
Aiseeee

Kwahiyo bado unamfuatilia????

Hilo ndo kosa kubwa unalo fanya kwa sasa.Pale unapoamua kuachana Na mtu forget about him/her completely..

Mpaka siku utakapokutana nae akiwa anauza mihogo au aendesha Bmw X6.

Sababu hata ukiachana na mtu hatma ya maisha yake ipo mikononi mwake.Anaweza kukufanyia wewe upuuzi na bado akaweza kujisamehe mapema sana na aka move on kwa haraka sana na siku unayokutana nae unamkuta ndo kwanza mtoto kawa mzuri km malaika.

Forget about Karma ni upuuzi tu sa nyingine kutegemea eti mtu kisa alikufanyia upuuzi flani basi lazima atalipa kwa namna jinsi unavyowaza wewe....

Jinsi unavyozidi kutafuta story zake ndo unavyozidi kuumia.Yes anaweza kuwa na majuto flani lkn majuto yake hayakusaidii chochote sababu ushamove on na maisha yako,Atajijua mwenyewe huko na upuuzi wake..

Usiruhusu ujinga kwenye maisha yako km ulivyokataa ujinga mkaachana basi kataa ujinga wa kutaka kujua anaendelea labda km bado unampenda
 
“Wakati huo mwanamme ni mbegu, na mashamba ya kupanda ni mengi.... mengine hayajatumika kabisa”.
 
Back
Top Bottom