Huu ni waraka wa wazi kutoka kwetu tulio wahanga watarajiwa wa covid-19 kuja kwenu nyie tuliowapa mamlaka na sasa mnatutoa kafara wakati nyie mko pema.
Ninaandika waraka huu kwa kudra za mola nikiwa ningali hai na nikiwa na imani ya dhati kuwa marehemu wengi mliowatoa kafara wangeandika waraka kama huu laiti wangalipata nafasi au wangalijua au kuyahisi yaliyokuwa mbele yao muda kabla ya changamoto za kupumua kuwafika.
Hii ikizingatiwa hawakujua ni ndani ya muda mfupi kiasi gani wangalishindwa kupumua na kuiaga dunia kimzaha mzaha kama ilivyowatokea. Waswahili wanasema wenzio wakinyolewa zako tia maji.
Ni dhahiri kuwa mmeligeuza janga hili ambalo kwa hakika ni la taifa na dunia kuwa janga letu sisi binafsi katika familia zetu. Mmekuwa mkitumia nguvu zote zikiwamo tulizowapa, ili kuzuia taarifa zozote kuhusiana na athari na uwepo wa ugonjwa huu kwa nia ya kuficha ukweli kwa maslahi yenu.
Matokeo ya ukandamizwaji wa taarifa hizo yamekuwa hakuna ajuaye (isipokuwa nyie) maeneo yaliyo hatari kuhusiana na ugonjwa huu ni yapi, hali ya ugonjwa inakwenda vipi na nini mategemeo ya baadaye.
Pasi na taarifa watu wasiokuwa na majina makubwa wamekuwa wakiugua na wakidondoka kimya kimya kama ilivyo kwa wachuma majanga na kula na wakwao.
Mitaani watu wameaminishwa Corona imekwisha. Angalia jitihada hata za kunawa zilivyopoa. Nani wanavaa mabarakoa tena? Vipi nyomi kwenye mwendo kasi na hata kwenye ma school bus?
Kwani hata mashuleni pana maji tiririka na sabuni tena?
Hali inaendelea hivyo kana kwamba kila kitu sawa sawa kabisa hadi kimya kimya na mmoja mmoja na familia kwa familia wanapo kula janga lao peke yao na kivyao vyao.
Enyi tuliowapa mamlaka kutulinda likiwa ni moja ya wajibu wenu ulio mkubwa zaidi. Tumewakosea nini nyie, sisi tulio wazee na hata wenye magonjwa mengine kiasi cha kutuweka katika hatari kubwa na maisha yetu kiasi hiki?
Suala zima la kuhakikisha makundi yaliyo katika hatari zaidi yanalindwa kwa nini halina umuhimu wowote ule kwenu?
Siyo kuwa kwa sababu nyie taarifa kamili za msingi za uathirika na maeneo yaliyoathirika zaidi mnazo kwa uzuri zaidi, mmezikumbatia wenyewe na familia zenu mkitutoa sisi kafara?
Kwingine wanajali sisi tofauti yetu nini?
Sweden's prime minister orders an inquiry into the failure of the country's no-lockdown coronavirus strategy
Burundi’s President Ndayishimiye: new cabinet, new COVID strategy
Siyo ubinafsi wenu kweli?
Jana mbunge fulani, leo Profesa fulani, kesho fulani nk.
Haiwahusu kwa sababu kimya kimya kila familia inaathirika na janga lake kivyake vyake?
Ninaandika waraka huu kwa kudra za mola nikiwa ningali hai na nikiwa na imani ya dhati kuwa marehemu wengi mliowatoa kafara wangeandika waraka kama huu laiti wangalipata nafasi au wangalijua au kuyahisi yaliyokuwa mbele yao muda kabla ya changamoto za kupumua kuwafika.
Hii ikizingatiwa hawakujua ni ndani ya muda mfupi kiasi gani wangalishindwa kupumua na kuiaga dunia kimzaha mzaha kama ilivyowatokea. Waswahili wanasema wenzio wakinyolewa zako tia maji.
Ni dhahiri kuwa mmeligeuza janga hili ambalo kwa hakika ni la taifa na dunia kuwa janga letu sisi binafsi katika familia zetu. Mmekuwa mkitumia nguvu zote zikiwamo tulizowapa, ili kuzuia taarifa zozote kuhusiana na athari na uwepo wa ugonjwa huu kwa nia ya kuficha ukweli kwa maslahi yenu.
Matokeo ya ukandamizwaji wa taarifa hizo yamekuwa hakuna ajuaye (isipokuwa nyie) maeneo yaliyo hatari kuhusiana na ugonjwa huu ni yapi, hali ya ugonjwa inakwenda vipi na nini mategemeo ya baadaye.
Pasi na taarifa watu wasiokuwa na majina makubwa wamekuwa wakiugua na wakidondoka kimya kimya kama ilivyo kwa wachuma majanga na kula na wakwao.
Mitaani watu wameaminishwa Corona imekwisha. Angalia jitihada hata za kunawa zilivyopoa. Nani wanavaa mabarakoa tena? Vipi nyomi kwenye mwendo kasi na hata kwenye ma school bus?
Kwani hata mashuleni pana maji tiririka na sabuni tena?
Hali inaendelea hivyo kana kwamba kila kitu sawa sawa kabisa hadi kimya kimya na mmoja mmoja na familia kwa familia wanapo kula janga lao peke yao na kivyao vyao.
Enyi tuliowapa mamlaka kutulinda likiwa ni moja ya wajibu wenu ulio mkubwa zaidi. Tumewakosea nini nyie, sisi tulio wazee na hata wenye magonjwa mengine kiasi cha kutuweka katika hatari kubwa na maisha yetu kiasi hiki?
Suala zima la kuhakikisha makundi yaliyo katika hatari zaidi yanalindwa kwa nini halina umuhimu wowote ule kwenu?
Siyo kuwa kwa sababu nyie taarifa kamili za msingi za uathirika na maeneo yaliyoathirika zaidi mnazo kwa uzuri zaidi, mmezikumbatia wenyewe na familia zenu mkitutoa sisi kafara?
Kwingine wanajali sisi tofauti yetu nini?
Sweden's prime minister orders an inquiry into the failure of the country's no-lockdown coronavirus strategy
Burundi’s President Ndayishimiye: new cabinet, new COVID strategy
Siyo ubinafsi wenu kweli?
Jana mbunge fulani, leo Profesa fulani, kesho fulani nk.
Haiwahusu kwa sababu kimya kimya kila familia inaathirika na janga lake kivyake vyake?