Kutoka kwa wahanga watarajiwa wa Covid-19

Kutoka kwa wahanga watarajiwa wa Covid-19

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Huu ni waraka wa wazi kutoka kwetu tulio wahanga watarajiwa wa covid-19 kuja kwenu nyie tuliowapa mamlaka na sasa mnatutoa kafara wakati nyie mko pema.

Ninaandika waraka huu kwa kudra za mola nikiwa ningali hai na nikiwa na imani ya dhati kuwa marehemu wengi mliowatoa kafara wangeandika waraka kama huu laiti wangalipata nafasi au wangalijua au kuyahisi yaliyokuwa mbele yao muda kabla ya changamoto za kupumua kuwafika.

Hii ikizingatiwa hawakujua ni ndani ya muda mfupi kiasi gani wangalishindwa kupumua na kuiaga dunia kimzaha mzaha kama ilivyowatokea. Waswahili wanasema wenzio wakinyolewa zako tia maji.

Ni dhahiri kuwa mmeligeuza janga hili ambalo kwa hakika ni la taifa na dunia kuwa janga letu sisi binafsi katika familia zetu. Mmekuwa mkitumia nguvu zote zikiwamo tulizowapa, ili kuzuia taarifa zozote kuhusiana na athari na uwepo wa ugonjwa huu kwa nia ya kuficha ukweli kwa maslahi yenu.

Matokeo ya ukandamizwaji wa taarifa hizo yamekuwa hakuna ajuaye (isipokuwa nyie) maeneo yaliyo hatari kuhusiana na ugonjwa huu ni yapi, hali ya ugonjwa inakwenda vipi na nini mategemeo ya baadaye.

Pasi na taarifa watu wasiokuwa na majina makubwa wamekuwa wakiugua na wakidondoka kimya kimya kama ilivyo kwa wachuma majanga na kula na wakwao.

Mitaani watu wameaminishwa Corona imekwisha. Angalia jitihada hata za kunawa zilivyopoa. Nani wanavaa mabarakoa tena? Vipi nyomi kwenye mwendo kasi na hata kwenye ma school bus?

Kwani hata mashuleni pana maji tiririka na sabuni tena?

Hali inaendelea hivyo kana kwamba kila kitu sawa sawa kabisa hadi kimya kimya na mmoja mmoja na familia kwa familia wanapo kula janga lao peke yao na kivyao vyao.

Enyi tuliowapa mamlaka kutulinda likiwa ni moja ya wajibu wenu ulio mkubwa zaidi. Tumewakosea nini nyie, sisi tulio wazee na hata wenye magonjwa mengine kiasi cha kutuweka katika hatari kubwa na maisha yetu kiasi hiki?

Suala zima la kuhakikisha makundi yaliyo katika hatari zaidi yanalindwa kwa nini halina umuhimu wowote ule kwenu?

Siyo kuwa kwa sababu nyie taarifa kamili za msingi za uathirika na maeneo yaliyoathirika zaidi mnazo kwa uzuri zaidi, mmezikumbatia wenyewe na familia zenu mkitutoa sisi kafara?

Kwingine wanajali sisi tofauti yetu nini?

Sweden's prime minister orders an inquiry into the failure of the country's no-lockdown coronavirus strategy

Burundi’s President Ndayishimiye: new cabinet, new COVID strategy

Siyo ubinafsi wenu kweli?

Jana mbunge fulani, leo Profesa fulani, kesho fulani nk.

Haiwahusu kwa sababu kimya kimya kila familia inaathirika na janga lake kivyake vyake?
 
Kila mtu ajipambanie mwenyewe.... Nikisema nijilokidauni familia yangu watapataje mlo? Cha msingi ni kuchukua tahadhari maisha lazima yaendelee

Watoto wanakwenda mashuleni na kurudi majumbani. Nyomi hadi kwenye school buses achilia mbali kwenye mabasi ya mwendo kasi.

Nawanawa mashuleni hazipo tena. Mabarakoa ndiyo hivyo tena.

Maeneo yaliyoathirika zaidi hayajulikani.

Walio katika hatari zaidi wanalindwaje?

Kila mtu anajipambania je au ndiyo unaunga mkono kuwa hili ni janga la familia?
 
ninapoona daladala zimeanza kusimamisha abiria kiasi cha kushindwa hata kugeuka ndani ya daladala mkoani dodoma, napata huruma kubwa kwa watumiaji wa usafiri wa umma nchi...Buriani nchi yangu!!
 
ninapoona daladala zimeanza kusimamisha abiria kiasi cha kushindwa hata kugeuka ndani ya daladala mkoani dodoma, napata huruma kubwa kwa watumiaji wa usafiri wa umma nchi...Buriani nchi yangu!!

Hali inatisha sana.

Angalia school buses uone. Nimefika kwenye shule moja private. Hata anaye nawa hakuna!

Hili limefanywa janga la familia.
 
Unataka ukiugua mafua serkali ije nyumbani kwako? Fuata kanuni za afya

Unayasoma wapi hayo ya mafua na hata ya nyumbani kwangu mkuu?

Mliotangulia pumzikeni kwa amani si muda mrefu tutakuwa sote huko.

Washauri wenyewe mahiri kabisa wa suluhu ya ugonjwa huu eti ni pamoja na huyu alumni wa hapo kawe.
 
Huu ni waraka wa wazi kutoka kwetu tulio wahanga watarajiwa wa covid-19 kuja kwenu nyie tuliowapa mamlaka na sasa mnatutoa kafara wakati nyie mko pema.

Ninaandika waraka huu kwa kudra za mola nikiwa ningali hai na nikiwa na imani ya dhati kuwa marehemu wengi mliowatoa kafara wangeandika waraka kama huu laiti wangalipata nafasi au wangalijua au kuyahisi yaliyokuwa mbele yao muda kabla ya changamoto za kupumua kuwafika.

Hii ikizingatiwa hawakujua ni ndani ya muda mfupi kiasi gani wangalishindwa kupumua na kuiaga dunia kimzaha mzaha kama ilivyowatokea. Waswahili wanasema wenzio wakinyolewa zako tia maji.

Ni dhahiri kuwa mmeligeuza janga hili ambalo kwa hakika ni la taifa na dunia kuwa janga letu sisi binafsi katika familia zetu. Mmekuwa mkitumia nguvu zote zikiwamo tulizowapa, ili kuzuia taarifa zozote kuhusiana na athari na uwepo wa ugonjwa huu kwa nia ya kuficha ukweli kwa maslahi yenu.

Matokeo ya ukandamizwaji wa taarifa hizo yamekuwa hakuna ajuaye (isipokuwa nyie) maeneo yaliyo hatari kuhusiana na ugonjwa huu ni yapi, hali ya ugonjwa inakwenda vipi na nini mategemeo ya baadaye.

Pasi na taarifa watu wasiokuwa na majina makubwa wamekuwa wakiugua na wakidondoka kimya kimya kama ilivyo kwa wachuma majanga na kula na wakwao.

Mitaani watu wameaminishwa Corona imekwisha. Angalia jitihada hata za kunawa zilivyopoa. Nani wanavaa mabarakoa tena? Vipi nyomi kwenye mwendo kasi na hata kwenye ma school bus?

Kwani hata mashuleni pana maji tiririka na sabuni tena?

Hali inaendelea hivyo kana kwamba kila kitu sawa sawa kabisa hadi kimya kimya na mmoja mmoja na familia kwa familia wanapo kula janga lao peke yao na kivyao vyao.

Enyi tuliowapa mamlaka kutulinda likiwa ni moja ya wajibu wenu ulio mkubwa zaidi. Tumewakosea nini nyie, sisi tulio wazee na hata wenye magonjwa mengine kiasi cha kutuweka katika hatari kubwa na maisha yetu kiasi hiki?

Suala zima la kuhakikisha makundi yaliyo katika hatari zaidi yanalindwa kwa nini halina umuhimu wowote ule kwenu?

Siyo kuwa kwa sababu nyie taarifa kamili za msingi za uathirika na maeneo yaliyoathirika zaidi mnazo kwa uzuri zaidi, mmezikumbatia wenyewe na familia zenu mkitutoa sisi kafara?

Kwingine wanajali sisi tofauti yetu nini?

Sweden's prime minister orders an inquiry into the failure of the country's no-lockdown coronavirus strategy

Burundi’s President Ndayishimiye: new cabinet, new COVID strategy

Siyo ubinafsi wenu kweli?

Jana mbunge fulani, leo Profesa fulani, kesho fulani nk.

Haiwahusu kwa sababu kimya kimya kila familia inaathirika na janga lake kivyake vyake?
We endelea kupiga ramli ila maisha lazima ya endeleee.
 
Hili ni janga la familia?
We unatakaje kwani ,jiweke lockdown vaa barakoa kaa mbali mita moja hata na nusu,usipande daladala lililojaa na mengine kama hayo kinyume chake kutaka wote tulie mlio mmoja ni uzandiki.
 
Saa hizi daladala zinapiga nyomi na hakuna hata mmoja aliyevaa barakoa, wanafunzi wanahangaika mabarabarani usafiri wa kwenda na kurudi mashuleni. Hii serikali haiwezi kununua hata mabasi ya kuwabeba wanafunzi, kutwa kujisifia kununua ndege..
 
We unatakaje kwani ,jiweke lockdown vaa barakoa kaa mbali mita moja hata na nusu,usipande daladala lililojaa na mengine kama hayo kinyume chake kutaka wote tulie mlio mmoja ni uzandiki.

Watoto (hadi wa chekechea) wanapokwenda mashuleni waepuke madaladala. Wanapokuwa madarasani wakae mita moja hadi na nusu kutoka kwa mwingine.

Wakirudi majumbani tuhakikishe kila mtu anavaa barakoa kwa maana sasa hali si hali.

Ndivyo unavyosema mkuu?

Wewe unaishi nchi hii hii au nyie ndiyo mnaonufaika na hii declaration ya kuwa huu ugonjwa ni janga la familia? Tuelezeni basi na maeneo hatari ili tujue tuyaepuke?

Au nyie ndiyo wazandiki wenyewe?
 
Saa hizi daladala zinapiga nyomi na hakuna hata mmoja aliyevaa barakoa, wanafunzi wanahangaika mabarabarani usafiri wa kwenda na kurudi mashuleni. Hii serikali haiwezi kununua hata mabasi ya kuwabeba wanafunzi, kutwa kujisifia kununua ndege..

Pana tatizo kubwa la kutoona hatari ya ugonjwa huu kwenye maambukizi zaidi.

Watoto hawa na shule shule suala la mtu kuchukua tahadhari linakuwa rasmi ni irrelevant.
 
Tuchukue tahadhali..tujilinde wenyewe.

Hili lawezekana labda kama wewe ni bachelor au single au kama hamna watoto wanaokwenda mashuleni.

Kwamba hili kinyemela limefanywa kuwa ni janga la familia? Kwa hakika ni suala la muda tu.
 
Hili lawezekana labda kama wewe ni bachelor au single au kama hamna watoto wanaokwenda mashuleni.

Kwamba hili kinyemela limefanywa kuwa ni janga la familia? Kwa hakika ni suala la muda tu.
Muda gani mkuu? Mlisema hivihivi miezi kadhaa iliyopita mbona hali shwari, hiyo miili inayodondoka barabarani ipo wapi?
 
Muda gani mkuu? Mlisema hivihivi miezi kadhaa iliyopita mbona hali shwari, hiyo miili inayodondoka barabarani ipo wapi?

Nilisemea wapi hayo unayanukuu mkuu? Hata hivyo usisahau kuwa hili limefanywa kinyemela kuwa ni janga la familia.

Janga la familia, madhara yanatangazwa kifamilia. Ni majina makubwa makubwa tu ndiyo yanayo onekana hadharani.

Wapumzike kwa amani wote waliotangulizwa mbele za haki wakiwamo maprofesa wetu.
 
Watoto wanakwenda mashuleni na kurudi majumbani. Nyomi hadi kwenye school buses achilia mbali kwenye mabasi ya mwendo kasi.

Nawanawa mashuleni hazipo tena. Mabarakoa ndiyo hivyo tena.

Maeneo yaliyoathirika zaidi hayajulikani.

Walio katika hatari zaidi wanalindwaje?

Kila mtu anajipambania je au ndiyo unaunga mkono kuwa hili ni janga la familia?
Mwendokasi gani unaojaza abiria kiasi umeuandikia hapa wewe mkazi wa mpimbiji huko nachingwea vijijini.

Kwenye daladala sasa hivi wanaosimama ni wanafunzi tu.

Endelea kukaa hapo subili serikali ije ikifute makamasi yanayokumwagika ila kaa ujue corona ipo na inaua usipochukua hatua.
 
Mwendokasi gani unaojaza abiria kiasi umeuandikia hapa wewe mkazi wa mpimbiji huko nachingwea vijijini.

Kwenye daladala sasa hivi wanaosimama ni wanafunzi tu.

Endelea kukaa hapo subili serikali ije ikifute makamasi yanayokumwagika ila kaa ujue corona ipo na inaua usipochukua hatua.

Mpimbiji Nachingwea ni Tanzania kama ilivyo kwenu wewe mkazi wa Matombo Kisaki Morogoro, kijijini hohehahe kusiko na maendeleo kwa sababu ya watu mbumbu kama wewe (Kalagabaho!).

Kwamba ni dala dala au mwendo kasi peke yake?

Kaangalie hata kwenye vi school buses.

Usiishie hapo, pita pia na mashuleni jiridhishe wanafunzi wangapi hasa chekechea, primary na secondary wananawa na maji tiririka shuleni kwa siku.

Ndipo utatambua waraka wangu ni kutoka kwa wahanga watarajiwa ukiwamo wewe au nduguyo wa pale Matombo.

Wewe kama ni kutoka katika ile jamii yenye taarifa sahihi na wapi pa kuepuka basi wewe si mhanga mtarajiwa na uzi huu haukuhusu mkuu.
 
Back
Top Bottom