Kutoka kwa wahanga watarajiwa wa Covid-19

Unaandika kutoka kuzimu au peponi baada ya kufa
 
Kwa Tanzania Corona imefeli vibaya mno vimebaki vitisho tu kama vya huyu mleta maada. Pongezi nyingi kwa Rais wetu mwenye maono na NIMRI kwa kutupa fomula ya kutengeneza dawa ya kutibu na kujikinga na Corona yenye mchanganyiko wa tangawizi,vitunguu swaumu, vitunguu maji, limau na pilipili kichaa.
 

Itapofika kwenye familia yenu ndipo utajua kuwa ingalipo.

Kabla ya hapo wewe kama josepg1998 utajirejea mwenyewe kujipiga like.

Komaa hivyo hivyo.
 
Ajabu ni kwamba mpaka kifo cha Mzee Mkapa kinatokea na hadi siku ya kuagwa corona ilikuwa bado ipo na hata kifo chake wengine walisema ni corona,ajabu watu hao hao wakaenda kumpokea Lissu Airport nadhani hapo ndipo corona ilipoanza kupungua.View attachment 1688077
 
Lengo la kelele hizi ni lipi? Kama unaona wenzako wazembe jifungie ndani wewe
 
Lengo la kelele hizi ni lipi? Kama unaona wenzako wazembe jifungie ndani wewe


Nikijifungia ndani kodi tokea kwa wale wasiolipa hata ndururu uko pale pale?

Hivi mburula nyie kwanini mnadhani watu wengine ni majuha juha tu isipokuwa nyie?

Pana kipi wezeshi ambacho serikali dhalimu hii imekiweka in place kuwafanya wanaotaka kujifungia wafanye hivyo hata kama ni kwa gharama zao kiasi cha nyie kujinasibu na vihoja hoja uchwara kama hivi?

Kimsingi mnawaambia watu wajifungie ndani kama wanataka huku mkiwawekea mazingira ya kutokuweza kufanya hivyo hata kama ingekuwa uchaguzi ni wao.

Wauaji wakubwa nyie. Bure kabisa!
 
Acha kulialia jifungie ndani na familia yako hujazuiwa
 
Acha kulialia jifungie ndani na familia yako hujazuiwa

Unanifunga mikono kisha unataka nikapigane?

Hadaeni wa dongobeshi.

Hatarini nani wamo inajulikana. Wewe umo au hujui kuwa umo?


Au wewe ni kutoka katika yale makabila yetu pendwa yasiyokuwa na kuthamini maisha ya wazee wao?
 
Unataka ukiugua mafua serkali ije nyumbani kwako? Fuata kanuni za afya

Wako wapi mburula kama huyu?

Waraka wa July 4, 2020 ungali unaishi leo.

Maalim Seif, Balozi Kijazi na wengi wengine waliotangulia na hata tuliopo ungali unatuhusu sana.

Itakuwa hivyo hadi pale tutakapo pumzishwa kwa amani na Corona Virus kwa hisani na udhalimu mkubwa tokea pale Lumumba.
 
Waraka huu ulituhusu wengi. Wengine walidhani hauwahusu kabisa.

Ninakazia: waraka huu kama ulivyo mtego wa panya ungali unatuhusu sana!
 
Unataka ukiugua mafua serkali ije nyumbani kwako? Fuata kanuni za afya

Pole pole, tutaelewana tu hata kama tutaita cardiac arrest, ajali ya boda boda au hata surua.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Hakika imefeli vibaya pongezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…