Kutoka Shajara (Diary) Yangu 2 June 1991

Kutoka Shajara (Diary) Yangu 2 June 1991

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUTOKA KWENYE SHAJARA YANGU 2 JUNE 1991

Huenda msomaji utakachosoma hapo chini ukaona hakina maana kwako.

Kwangu mimi hayo niliyoandika yamenipa jibu la swali lililokuwa likinitaabisha kwa muda mrefu.

Hapo chini nimeandika sentensi mbili katika diary yangu tarehe 2 June 1991:

"June 2, 1953 coronation of the Queen (Elizabeth the II).

17 April, 1953 AW Sykes v Nyerere TAA Election Arnautoglo Hall Dar es Salaam."

Nimeandika maneno haya miaka 33 iloyopita.
Wakati huu nilikuwa niko katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.

Hiyo sentensi ya pili inaeleza tarehe ya uchaguzi wa kumtafuta Rais wa TAA uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo kati ya Abdulwahid Kleist Sykes na Julius Kambarage Nyerere.

Bahati mbaya sana historia hii haikuwa inafahamika.

Nyerere hakupata kueleza kama aligombea nafasi ya urais wa TAA na Abdul Sykes mwaka wa 1953.

Hii ni historia muhimu sana kwa Nyerere mwenyewe na kwa TAA kwani baada ya uchaguzi huu mwaka uliofuatia ndipo TANU ikaundwa 1954.

Baada ya miaka mingi kupita ikawa kila ninaposoma kwenye kitabu changu taarifa hii naangalia chanzo cha taarifa hii sikioni.

Hili jambo likawa linanikera.
Nami sikumbuki wapi nimetoa taarifa hii.

Leo nikawa napitia shajara yangu ya mwaka 1991 ndipo nikakutana na ukurasa huu na sentensi hizo mbili na hapo hapo nikakumbuka kuwa ilikuwa kila ninapopata taarifa muhimu tarehe ya tukio nilikuwa naandika kwenye shajara yangu ya mwaka ule.

Taarifa hii nilikuwa nimesoma kwenye Nyaraka za Sykes pamoja na mambo mengine yanayohusu kutawazwa kwa Malkia Elizabeth.

Hii ndiyo sababu ya mimi kuandika hayo katika shajara yangu.

Picha ya kwanza ukurasa katika shajara, Abdul Sykes, Dossa Aziz, Julius Nyerere na Lawi Sijaona wakiwa Ukumbi wa Arnautoglo dhifa ya kumuaga Nyerere safari ya pili UNO 1956, Ukumbi wa Arnautoglo na shajara katika Maktaba.

321909894_1595816757517203_4191494703161799153_n.jpg
320329703_549040640412841_2116387902964030825_n.jpg
321759972_2309265815913885_3160044051582284623_n.jpg
321826882_879525759904044_4496119530047234341_n.jpg

 
kwema mzee mohamed?
kama ikikupendeza tunaomba uandike japo kwa ufupi historia ya Ndugu Kassim Hanga.
mungu akubariki uwe na uhai mrefu na mwisho mwema
 
Sheikh Mohamed Said,

..Abdulwahid alifariki akiwa hana umri mkubwa nadhani miaka 44.

..unaweza kutukumbusha kifo chake kilitokana na nini?

..Je, aliugua? Na aliugua muda mrefu, au ilikuwa kifo cha ghafla?

..Je, alifariki Dar Es Salaam, au mji mwingine?
 
kwema mzee mohamed?
kama ikikupendeza tunaomba uandike japo kwa ufupi historia ya Ndugu Kassim Hanga.
mungu akubariki uwe na uhai mrefu na mwisho mwema
Kinoa miguu,
Kuna kitabu kinaandikwa kuhusu Abdullah Kassim Hanga.

Tukisubiri.

Lakini wakati tunasubiri tunaweza kumsoma Hanga katika hii taazia niliyoandika miaka mingi baada ya kifo chake:
 
Sheikh Mohamed Said,

..Abdulwahid alifariki akiwa hana umri mkubwa nadhani miaka 44.

..unaweza kutukumbusha kifo chake kilitokana na nini?

..Je, aliugua? Na aliugua muda mrefu, au ilikuwa kifo cha ghafla?

..Je, alifariki Dar Es Salaam, au mji mwingine?
JK
Abdul Sykes alipofariki mimi nilipata taarifa si muda mrefu na sababu ilipigwa simu nyumbani nikapokea.

Aliyepiga alitaka kuzungumza na baba yangu.
Nikamjibu kuwa baba hayupo.

Yule bwana akaniambia akirudi baba yako mwambie Abdul Sykes amefariki.
Katika shajara yangu ya mwaka wa 1968 nimeandika tukio hili.

Baba alikuwa kasafiri kenda Morogoro na aliporejea siku ya pili nilimpa taarifa ya msiba.

Baba akanieleza kuwa siku chache zilizopita alikutana na Abdul Sykes Matasalamat Building, Independence Avenue (sasa Samora Avenue) na wakazungumza kwa muda na walipokuwa wanaagana Abdul Sykes akamuaga baba yangu kwa kumwambia, "Bukra," neno la Kiarabu lenye maana ya kesho.

Naamini hiki ni Kiarabu chao walichosoma Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika Muslim School katika miaka ya 1930s.

Katika kumbukumbu ya miaka 50 ya kifo chake, mwanae Aisha Daisy Sykes aliandika makala iliyochapwa na Raia Mwema kwa matoleo matatu.

Katika makala hayo alieleza kuwa juma moja kabla ya kifo cha baba yake aliongozana na baba yake kwenda Msasani nyumbani kwa Mwalimu kwa minajili ya yeye Daisy kufanya mahojiano na Nyerere kuhusu historia ya TANU.

Daisy alikuwa amepewa ''assignment'' na mwalimu wake wa historia University of East Africa, John Iliffe kuandika maisha ya babu yake Kleist Sykes.

Mwalimu aliwapokea kwa furaha na Daisy alizungumza na Mwalimu kuhusu kuundwa kwa TANU.

Hii ilikuwa Jumamosi.

Jumamosi iliyofuatia Abdul Sykes akafariki.
 
Back
Top Bottom