Kutoka Ukumbi wa Mlimani City: Mkutano wa January Makamba Kutangaza nia ya Urais

Kutoka Ukumbi wa Mlimani City: Mkutano wa January Makamba Kutangaza nia ya Urais

Naona anakabidhiwa rungu. CCM kwa vituko siwawezi.
 
ukisoma kitabu chake kilichoandikwa na PD karugendo maswali yote hayo yamo na Majibu yake....kwa maana nyingine wauliza maswali wamepangwa
OK jamaa leo katupa sumup ya kitabu chake eeh?January hana lolote kwenye utekelezaji
 
January aandaa watu wa kuuliza maswali.Katika mkutano wa kutangaza nia ambao unaendelea mjini Dar es salaam ,katika ukumbi wa milimani city ,imeonekana wazi kuwa ndugu January Makamba ,ameandaa watu wa kuuliza maswali.Hali hiyo imejitokeza baada ya MC wa mkutano huo kutokuwa tayar kuchagua mtu yeyote aliyenyosha mkono mpaka amtafute kwa uhakika mtu aliyepangwa kuuliza swali.Hali hii inatokana na kwamba kijana huyu,ambaye amekuwa akibebwa sana na marafiki za baba yake ni kiraza wa uhakika ,na ambaye inasemekena alipata sifuri ktk mtihani wa form four
 
  • Thanks
Reactions: PPM
January yuko serikalini na CCM kwanini wasifanye hayo au kuandika situation paper kwa Rais na chama chake ikiwa na analysis na mapendekezo mazuri na rahisi kutekelezeka kama anavyotaka tuamini. Au wanahujumu serikali na chama chao. Ebu nisaidie kuelewa mwenye uzi huu, HAMY-D!. Maana maelezo yake ni kama yuko upinzani akionyesha njia mbadala kwa utawala wa CCM.
WanaJF,

View attachment 258214

View attachment 258215

KAULI MBIU YA JANUARI MAKAMBA: TANZANIA MPYA

-Ikiwa ni muendelezo wa watangaza nia kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), sasa ni zamu ya January Makamba kutangaza nia kutokea Mlimani City.

-January Makamba anaomba ridhaa ya chama kusimamishwa kuwa mgombea wa urais kufuatia wana CCM 15 kutangaza nia hiyo ya kuwania nafasi ya urais kupitia tiketi ya CCM.

-Hivi sasa kinachoendelea ni ushuhuda wa watu mbalimbali juu ya uongozi wa Januari Makamba.

-Mmoja wa wananchi wa jimbo la Bumbuli ametamka kuwa, "Januari ana kama Unyerere Unyerere hivi". Hii ana maanisha kuwa kijana ana ufuatiliaji wa hali ya juu na ana dhamira ya dhati ya kuwatumikia watu.

-Januari ameanza kuongea na amejielekeza moja kwa moja kutanga nia yake ya kuwania nafasi ya urais kupitia tiketi ya CCM, pia amesema kesho kutwa ataenda kuchukua fomu ya urais kutoka kwenye ofisi za CCM, Dodoma.

JANUARI ATATOA HOTUBA HII BILA YA KUSOMA POPOTE. HOTUBA YOTE IPO KICHWANI.

- Januari anasisitiza kuwa Tanzania MPYA itajengwa na viongozi wenye fikra mpya.

- Januari ahaidi kuwa na mawaziri wasiozidi 18 tu katika baraza lake la mawaziri endapo chama chake kikimpa ridhaa ya kugombea urais kupitia CCM.


-Januari Makamba anaorodhesha ajenda tano kuu atakazo simamia endapo chama chake kitampa ridhaa ya kugombea na hatimae kuunda serikali.

............Update............

....Januari ahaidi kuwa serikali yake itatoa mikopo maalumu kwa vijana watakaomaliza vyuo vikuu ambao watapata changamoto ya ajila ili na wao waweze kufungua makampuni yao ili waweze kujizalishia kipato.

....Pia amesema katika serikali yake atahakikisha sekta ya nyumba ina mchango wa zaidi ya 25%, wakati sasa hivi ni chini ya 4% ikimaanisha Watanzania wengi hawana makazi. Hivyo katika uongozi wake hilo la makazi atalipa kipaumbele tofauti na ilivyo sasa.

....UVUVI, serikali yake itaanzisha mifuko maaalumu ya kukopesha wavuvi ili waweze kununua vifaa vya uvuvi ili isaidie kuboresha vipato vya wavuvi na pia kukuza sekta hiyo kwa kasi.

....UHABA WA WALIMU, serikali yake itaongeza udahili wa walimu haswa kwa masomo ya sayansi. Pia ameahidi kutatua changamoto za walimu kama vile mishahara yao kuwa duni, kukosa posho na stahiki mbalimbali. Ahaidi serikali yake kutatua kero hizo kwa kukuza na kuboresha maslahi yao.

.... RUSHWA, amesema kuwa kulizungumza na kulipigia kelele tatizo la rushwa sio njia ya kulimaliza tatizo hilo.

...ARDHI, jinsi ya kuondoa migogoro kati ya wakulima na wafugaji. Serikali yake itabainisha kisheria maeneo ya kilimo, mifugo na makazi. Pia amesema wakulima na wafugaji watamiliki maeneo yao kisheria. Atatumia teknolojia mpya ya satellite kutekeleza hayo kupitia kituo maalumu kitachoundwa chini ya serikali yake. Lakini pia kituo hicho kitasaidia pia na mambo ya kiusalama.

....AFYA, kila Mtanzania lazima awe na bima ya afya, kila Mtanzania lazima apate huduma bora ya afya bila ya kujali kipato chake.

....MAJI, wakala na mfuko mpya wa maji utaanzishwa vijijini. Hapa kukazia hoja yake, ametolea mfano wa mawakala kama wa barabara (TANROADS) na wakala wa umeme vijijini (RERA) kuwa mafanikio makubwa yamepatikana kupitia uwepo wa mawakala hao. Hivyo sasa kuna haja ya kuwa wna wakala wa maji vijijini. Ahaidi ndani ya miaka kumi kusogeza hudumasafi na salama aya majikwa kaya karibu zote nchini.

....MAPATO YA SERIKALI, hapa anazungumzia namna atakavyopata fedha za kutekeleza ahadi zake. Mambo atayofanya ni yafuatayo:

1. Atahusisha sekta binafsi kwa kina zaidi ambapo serikali haina ulazima kutumia fedha zake yenyewe katika kutekeleza miradi mbalimbali.

2. Kupunguza misamaha ya kodi kufikia 1% ya pato la taifa. Ambapo serikali itaweza kupata kiasi cha kisichopungua bilioni 700 pesa za Tanzania.

3. Kupanua wigo wa kodi, hasa kwenye sekta isiyo rasmi. Serikali yake itaondoa mfumo wa sasa wa kutoza kodi kabla hata ya biashara kuanza. Pia ataweka adhabu kubwa kwa watakaokwepa kodi.

4. kuongeza ufanisi wa TRA, amenukuu rpoti ya kitaalamu iliyohitimisha kuwa TRA kama ikiongeza ufanisi wa asilimia 10% tu, itaongeza ukusanyaji wa kodi kiasi cha bilion 600 kwa mwaka.

5. Mradi wa makaa ya mawe, serikali itapata kiasi cha bilion 800 kama utafanywa kwa ufanisi zaidi.

6. Kila mwenye ardhi yenye hati atatozwa kodi stahiki, kiasi cha bilion 500 kitapatikana hilo likifanikiwa. Hapa ili afanikiwe atahakikisha kwamba wizara ya ardhi inashirikiana na sekta binafsi kupima ardhi ili kumilikisha watu wengi zaidi ili serikali iweze kupata mapato kutokana na ardhi hiyo iliyopimwa.

7. Sekta ya nyuki itatoa bilion 130 kwa mwaka kama itapewa kipaumbele.

8. Meli nyingi za kimataifa hazilipi kodi, serikali yake itarekebisha sheria ya uvuvi ya bahari kuu ili kuongeza mapata kiasi cha bilion 350 kwa mwaka.
.......Update.......





...Januari amemaliza kwa kutoa rai kwa wanaCCM wote kuacha kugombana..badala yake amewaomba watangaza nia wote kujikita zaidi katika kuelezea namna gani watapambana na matatizo na changamoto za Watanzania.

......Update.....

Wakati wa maswali:

1. Kuhusu michezo: Ni kwa namna gani atatatua tatizo la michezo kusuasua?

2. Namna gani atatatua changamoto za foleni jijini Dar es salaam?

3. Mkakati gani wa kuwasaidia wanamama waweze kupata mikopo midogo midogo?

4. Landa speculators: Hili swali linahusu wale wenye kuhodhi ardhi kubwa huku hawaiendelezi. Je, ni namna gani atawashughulikia watu wa aina hiyo?

Mhe Januari anaanza kudondosha nondo kujibu maswali yote yaliyoelekezwa kwake!

1. Majibu ya swali la kwanza:

- Kuunda academy za michezo ili watoto wadogo wa miaka 6, 7, 8 waanze kufunzwa michezo katika umri huo mdogo.

- Kuwezesha kifedha timu za daraja la kwanza ili iwe motisha kwao na kuepusha mfumo wa sasa wa kutembeza bakuli ambao unawavunja moyo wana michezo.

2. Katoa nondo nyingi sana ila kubwa ni kwamba atajenga flyovers ili kutanua zaidi njia za kutoka katikati ya jiji na kwenda kwenye zile four ateries (njia nne kuu za kutoa Dar). Hili linafanyika kwa miaka chini ya 10 tu, ila amegoma la kuweka foleni kwa sababu itahitaji miaka 50 ili mradi kukamilika. Hivyo kwa uharaka wa tatizo la foleni, njia ya flyovers ndio nzuri zaidi.


4. Majibu kwa swali la nne:

- Ataweka gharama kubwa kwa speculators. Hili ni jambo la muhimu sana na kiukweli dogo huyu ni kichwa! Ameni-impress.
 
Kijana mdogo umeshaanza kununua watu.. Eti hana kashfa!? Aliiba mradi wa Sugu wa maralia no more akaupeleka kwa ruge then wakagawana nusu kwa nusu fisadi mkubwa huyu.

ulikuwepo wakigawana nusu kwa nusu acha maneno ya vijiweni
 
kwangu mie wagombea walionyesha vision na ufumbuzi wa matatizo ya watanzania ni Makamba na Muhongo.
 
Kijana amejitahidi kuongea.....atleast ameonyesha nuwezo wa kujieleza, sio kama kina Muhongo waliokuwa wanajisifia tu sehem walizotembelea na kufanya kazi na kiwango chake cha elimu kama vile tulimuuliza
 
UKAWA wanaendelea kupata pigo kila mgombea wa CCM ni moto ....


£ndelea kujipa moyo ukifikiria huyo TeamNyweleNyeupe atakuletea maendeleo.

Sisi hatuna shida, ndio maana tupo kimya.. Tukiingia ni kwa kishindo.
 
Nampongeza hapo kwenye kujenga njia ya reli za usafiri wa ndani Dar,hapo kweli katoa idea nzuri tena sana.

..hawa wana-CCM wanatudanganya tu.

..huyu alikuwa mshauri wa karibu wa Raisi Kikwete.

..tena anadai yeye ndiye aliyekuwa akichukua notes za mikutano yote ya JK na watu mashuhuri kama George Bush, Bill Gates etc. Zaidi alikuwa akiandaa taarifa za ufuatiliaji wa mazungumzo kama hayo.

..sasa kwanini hakumshauri JK atekeleze walau robo ya hayo anayodai atakuja kutufanyia?

..hayo aliyoyasema yanafaa kutamkwa na mgombea ambaye siyo mwana-CCM.

NB:

..wengine wanadai watapambana na rushwa lakini miaka yote wako kwenye uongozi wamekuwa baridiiii huku ufisadi ukiendelea kila kona.

..halafu kupambana na rushwa si ni sawa na kupambana na CCM?

cc Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:
Watizedi bhana? ghafla topic humu imehamia kama Makamba na pia Obama hutumia teleprompter au la!!
Vichwa maji sana!
 
Nasema through experience kuwa hatotokea rais mpya toka ndani ya chama cha CCM. Si January pekee ambaye ni muongo kwa kutoa kauli mbiu finyu na ahadi kibao kabla ya kupata urais. Kikwete alikuja na kauli mbiu nzuri ambayo watanzania bila kufikiri walimpokea kwa mbinde na kumpamba kila kona ya nchi. Miaka kumi baadaye ndani ya utawala wake, nchi na wananchi wake bado masikini vile vile na ile kauli mbiu yake mashuhuri ya "Ari mpya, nguvu mpya....maisha bora kwa kila Mtanzania," imefikia wapi? Hawa wote waliotangaza nia hawana jipya endapo wako ndani ya CCM na wamekulia humo, kwani hata wakiwa na mawazo mazuri ya kuendeleza nchi kama Kikwete before, hawatafanya chochote cha maana kwa sababu watafuata mfumo uliopo ndani ya chama chao, hivyo kuichagua tena CCM ni sawa na kujipiga kitanzi kwa miaka mingine ijayo ya mateso. Ni takriban miaka 54 sasa chini ya utawala wa TANU/CCM na hakuna cha maana walichokifanya nchi bado ipo majaribioni na viongozi wanaiba tu mali za nchi na kuwachekea waharifu huku wenzetu ambao hawana mali ghafi kama sie wanapiga hatua na kutuacha mbali. To hell with CCM na viongozi wake.
 
mwislam kapewa bible...hawa wamasai hawako teamlowasa?
 
Watizedi bhana? ghafla topic humu imehamia kama Makamba na pia Obama hutumia teleprompter au la!!
Vichwa maji sana!

Kama Januari kaisoma hotuba kwenye prompter si vyema kudanganya watu kuwa hakuisoma hiyo hotuba popote pale, na kwamba ilikuwa ipo kichwani.

Huo ni uongo.

Sasa swali ni je, ni kweli alikuwa anasoma kwenye prompter au la?

Hakuna mwenye jibu la uhakika mpaka hivi sasa.
 
Nimesikiliza mambo machache aliyoongea, naye anawakilisha idadi iliyo kubwa ya Watanzania ambao tumepoteza mwelekeo na hata hatujui tunachohitaji!
Nimemsikia akitoa shukurani kwa baadhi ya watu waliomsaidia, hapa angelimshukuru baba yake na JK kwa kumzawadia uwaziri na hivyo vyeo vingine. Nimeshangaa anapowashukuru wananchi wa Bumbuli, hebu tuweke sawa historia: kwani kuna mtu hata mmoja aliyempigia kura huyu kijana kuingia bungeni!?
 
Nakubaliana na wewe, ukiangalia kiundani hii ni project ya jumba kuu, just kuharibia wagombea walio serious. Hawa jamaa wanadhani hii jnchi ni ya kifalme na hawakubali yaishe. Watanzania wenzangu plaese pleae say No to third Term of Fourth regime. No to uncle. No to project ya Jumba kuu Aka Membe. Princekubali yaishe, tulia Chalinze usije kujiharibia zaidi
 
Emma anasoma mahali mwangalie vizuri..kuna telemproter kwa mbele yake...ila duuu anaongea ndoto tupu..sijui meli,kila wila kujrnga chuo,mara satelite....

Hahahaha...nyimbo ya prof jizzo
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na wewe, ukiangalia kiundani hii ni project ya jumba kuu, just kuharibia wagombea walio serious. Hawa jamaa wanadhani hii jnchi ni ya kifalme na hawakubali yaishe. Watanzania wenzangu plaese pleae say No to third Term of Fourth regime. No to uncle. No to project ya Jumba kuu Aka Membe. Prince kubali yaishe, tulia Chalinze usije kujiharibia zaidi
 
Back
Top Bottom