Kutoka Ukumbi wa Mlimani City: Mkutano wa January Makamba Kutangaza nia ya Urais

Kutoka Ukumbi wa Mlimani City: Mkutano wa January Makamba Kutangaza nia ya Urais

Naona wameanza na clips za kumpamba hapa.

Dogo alianza kuni-impress kidogo kiutendaji lakini alivyokutana na mtonyo wa makampuni ya simu akafyata mkia kabisa, siku hizi na yeye hamna kitu, ni business as usual kama wengine tu
 
Eti ana kama "unyerere nyerere" fulan! Binafsi naona kuna watu vichaa ilahawajitambui kabisa!

Yaan mtu na akili zako na suruali umevaa unadhubutu kuandika vitu kama ivi!? Mwandikie mkeo hay mambo!
 
Duu kumbe yeye ndie katibu wa kamati ya maandalizi ya ilani ya ccm 2015!!! jamaa ametumia fursa.
 
Nakumbuka Mnyika nae alikuja na ahadi tamu Ubungo za kuwa akichaguliwa tu basi tatizo la maji linaingia kwenye historia.Leo yapo wapi??


Sugu yeye aliwaahidi Mbeya kuwa japo kuwa kwa kutumia ideas zake kama ilivyokuwa malaria no more ataanzisha miradi ya mabwawa ya kufuga samaki Mbeya ili vijana wengi wajiajiri kwa kufuga samaki.

Na akaongeza kuwa akichaguliwa tu basi kila mwanafunzi wa sekondary Mbeya atapata laptop.Ni uzembe tu wa mbunge aliyekuwepo kushindwa kuja na idea za maana.

Leo miaka 5 baadae ata kiyakumbushia hawakumbushi.

Hivyo kama unaona hawa wa CCM wanaongea ndoto tatizo sio la CCM, tatizo ni watanzania, ata hao wa Upinzani wanaongea ndoto hizihizi kama hawa



Uliyoyasema ni ya ukweli lakini pia ilibidi utizame na watu wenyewe waliotoa hizo ahadi. Kwa akili yako wewe, ulifikiri Mbilinyi angefanya nini, hivi, ulimuamini mtu msanii kama yule? Mnyika pia ni bonge la msanii, nafikiri mpaka sasa wewe mwenyewe ni shahidi. Ni kweli tatizo liko kwa watanzania kwa kufunga macho na akili zao na kuchagua recycled corrupted people. CCM kamwe haiko hapa Tanzania kuiendeleza nchi hii, nasema haitatokea hii.
 
Nilikuwepo ukumbini Mlimani City...wewe ulikuwa wapi wakati anahutubia?

Kama hiyo ya Makamba kueleza nini atafanya bila kusoma imewakeleketa sana, basi ndio mjue hao ndio aina ya viongozi ambao wapo CCM....sio kama waliofeli shule wa huko UKAWA

Hata boniphace Thomas ndengo nayeye hasomi . muangalie ITV sasa
 
nategema waganga wa kienyeji wa kutosha leo

Jamuary mskamba na wanaccm wenzake wanaanza leo kujua matatizo ya walimu?
Suala la mishahara toka 1995-2015 wamekuwa wakiboresha mishara ya walimukuongeza asilimia 0.5 ya mshahara wa Mwalimu,
Ccm yake imeachana na ujenzi wa nyumba inajali wanafunzi,

Ccm imeamua walimu wawe na waajiri zaidi ya watatu,

Ccm imekataa malipo ya likizo,imewanyima teaching allowance imekazia sitting allowance na posho za vikao!

Ccm haina tofauti na Nzige
 
Anaahidi mawaziri 18 tu,wakati katiba pendekezwa ya warioba waliikataa na iliweka limit ya idadi ya wabunge na mawaziri? Usanii
 
Kijana mdogo umeshaanza kununua watu.. Eti hana kashfa!? Aliiba mradi wa Sugu wa maralia no more akaupeleka kwa ruge then wakagawana nusu kwa nusu fisadi mkubwa huyu.

Akiwa ikulu kapiga sana 10% kwa mgongo wa Rais pia kamchuna sana Kenyata na Rostam Aziz kupitia Mdogo wake mwanvita, pia naona Sera zake ni kama amecopy za watangaza nia wengine hana jipya laana ya wapiga kura wake kule jimboni inamtafuna.
 
Mleta mada unapomwita kichwa,atatawala njw ya mfumo wa wezi wa ccm?, atafanyakazi bila makada wale 100 wa ccm?

Hivi hoja ya kukopesha,Wavuvi ni vipi wavuvi watakopeshwa wakati taasisi za fedha zinakanuni zake? Hata jk alisema yako wapi?
 
Na amekula sana milioni 10 kumi za kumuona rais ikulu.
»Yule shemeji yake wa ABG walimfanya mbaya sana.
»Kasharudisha cheti cha watu cha form 4?

Hana lolote sasa bila aibu anachukua pesa toka kwa Mdogo wake mwanvita ambaye anawachuna akina Rostam yaani anasaka njia ya ikulu kwa pesa za na-buzi
 
Nimemsikiliza Januari Makamba wakati akitangaza nia, amezungumza mambo mengi lakini ameharibu utamu wa hotuba hiyo kwa kusema uongo.

Makamba katika hotuba yake amesema itachukua miaka mingi hata kumi kwa Tanzania kuanza kuvuna gesi na rais ajaye anaweza akaondoka madarakani bado gesi haijaanza kutumika.

Huu ni uongo wa wazi ana pengine inaweza kuwa ni kutojua kwamba tayari gesi imeanza kutumika kwenye maeneo mengi ikiwemo kweye viwanda mbalimbali hususani kwenye jiji la Dar es Salaam na kuna maeneo mengine kwenye majumba inatumika.

Namshangaa Januari anaposema gesi haitotumika kwa miaka ya karibu, anataka kutuambia hata mioundo mbinu ya gesi iliyojengwa itaanza kufanya kazi baada ya miaka kumi?

Namshauri aache kuzungumzia mambo ambayo hayajui na kama anatamani kuyazungumzia basi angeuliza kwa wataalamu wa masuala ya gesi kabla ya kufungua mdomo kuongea asiyoyajua.

Kwa mujibu wa wizara ya nishati na madini gesi itaanza kutumika miezi michache ijayo na tayari mabomba ya gesi yamekamilika kwa asilimia 90 na hata kiwanda cha DANGOTE kinachojengwa kitatumia gesi hiyo ambapo kiwanda hicho kitaanza uzalishaji mwezi wa nane kwa maana hiyo gesi itaanza kutumika kabla ya kiwanda hicho kuanza uzalishaji,
 
Nilimkubali sana Muhongo alipoliongelea hilo swala la gesi. Alichambua kila kitu kuhusiana na gesi na kiwango ambacho inaweza kuzalishwa mpaka kumfikia mtumiaji wa mwisho..
Muhongo yuko poa sana kichwani. Statistics za kiuchumi alizokuwa akitoa kati ya China, Brazil, Kenya na Tanzania kwa kweli ziliibeba sana hotuba yake....
Go Muhongo! Go....
 
Nilimkubali sana Muhongo alipoliongelea hilo swala la gesi. Alichambua kila kitu kuhusiana na gesi na kiwango ambacho inaweza kuzalishwa mpaka kumfikia mtumiaji wa mwisho..
Muhongo yuko poa sana kichwani. Statistics za kiuchumi alizokuwa akitoa kati ya China, Brazil, Kenya na Tanzania kwa kweli ziliibeba sana hotuba yake....
Go Muhongo! Go....

Comrade, watu hawamtaki Muhongo lakini wanaimba kumtaka kiongozi makini.Hakuna kiongozi makini zaidi ya Muhongo.Na kwa hilo nashawishika kuamini kuwa tatizo letu si Marais wala vyama vyao, bali sisi wenyewe tumekosa akili za utambuzi.
 
Back
Top Bottom