Kutokuwepo kwa Mabalozi wa US, UK, Sweden, Norway, Denmark, EU, Japan na South Korea leo Dodoma, kuna nini kinaendelea jikoni?

Kutokuwepo kwa Mabalozi wa US, UK, Sweden, Norway, Denmark, EU, Japan na South Korea leo Dodoma, kuna nini kinaendelea jikoni?

Kwani hapo ulipo haubebwi???
Hayo ndio mambo yamelichelewesha bara la Africa kijiamlia mambo yake na kujitegemea!!

Misaada misaada, hata kwangu binafsi siitaki, kubebwa bebwa kumelifanya hata soka letu liwe la hovyo hovyo, tunakuwa na timu nzuri ndani Tu kwa sababu ya kubebwa bebwa tu!

Tanzania bila hao, inawezekana bhana, Isipokuwa, Tanzania bila Mungu, haiwezekani
 
Ni swali muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu.

Amani iwe nanyi wadau!

Usiku wa Jana, Wakili Robert Amserdam ameitaliifu dunia kupitia Twitter yake kuwa amefikia hatua nzuri kupeleka mashtaka katika mahakama ya ICC Uholanzi dhidi ya Magufuli na Serikali yake.

Leo alfajiri, Magufuli akateua mawaziri wawili -- wa Mambo ya Nje, na wa Fedha.

Muda mchache uliopita kwa mara ya kwanza, wawakilishi wa nchi zinazoisadia zaidi Tanzania kifedha na kimisaada yaani Marekani, Uingereza, Sweden, Norway, Japan, Ujerumani, Finland, Korea ya Kusini na Umoja wa Ulaya hawajaudhuria hotuba ya Rais Magufuli Bungeni.

Naomba mnaojua mtuelezee humu, kuna nini kinaendelea jikoni? Au ndo mambo yashakuwa mambo?

Naomba michango yenu!
Sasa kama kila kitu kina/kimefanyika kwa fedha za ndani ,huoni uwepo wao ulikuwa haina maana?
Na hata wangelikuwepo huoni kama labda wangeliona soni?
 
Kweli,sisi ni nchi huru,yenye uchumi wa kati..

Yenye kuiba kura wakati wa Uchaguzi,yenye kuonea watu wake,kuwanyima Uhuru wa kuamua ...NK

Mkuu,bado hatuko huru,bado hatujitambui, bado hatujaweza kujitawala..
Hujitambui wewe na familia yako! Hatuko huru wakati upo Nyuma ya keyboard una type hapa kuiponda serikali! Unaujua Uhuru wewe ni uhuru upi unaozungumzia? Temechoka na hoja zenu hizi mfu kila kukicha! Uchaguzi umeshakwisha sasa tunajenga Nchi!.
 
Kwan mwaka Gan walienda na wanaenda mule kama kina Nan [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]makamanda hata ivyo ongeren Mnatumia nguvu nyingi wasinge enda kwenye kuapishwa apo sawa
 
Mie viongozi wetu wa dini (ila sio akina gwajima) nawalaumu sana kwa ukimya na kutokemea haya yanayoendelea.
Nawasimu sana viongozi majasiri kama Askofu Bagoza na Sheikh Ponda. walisimama ktk kweli siku zote,
 
Hujitambui wewe na familia yako! Hatuko huru wakati upo Nyuma ya keyboard una type hapa kuiponda serikali! Unaujua Uhuru wewe ni uhuru upi unaozungumzia? Temechoka na hoja zenu hizi mfu kila kukicha! Uchaguzi umeshakwisha sasa tunajenga Nchi!.
Kwani hapo nyuma ya keyboard yake ametumia actual id?
 
Maisha ya kinafiki ndiyo yamekutawala
Kama hawakupewa mwaliko je?
Na ni lazima wawepo ndiyo nchi uendelee?
Watanzania tujifunze kujitegemea
Mtegemea cha nduguye ufa masikini
 
Back
Top Bottom