Kutomuamini Mungu ni ujasiri?

Kwani ni watoyo wangapi wamezaliwa na wakafa siku hiyo hiyo?

Kwanini asiwasaidie hao kwanza?

Wengine wanafia tumboni hata fursa ya kuiona dunia hawaipati, huyo Mungu anakuwa wapi wakati hayo yanafanyika?
 
Weka mfano halisi mfano ulio utoa ni mfano mfu.
Mfano mfu?

Kwani haya mabaya ya huu ulimwengu yapo kwa bahati mbaya au kwa makusudi?

Je "mabaya" ni mabaya kiasi iwe kosa endapo itabainika kuwa kuna mabaya?

Au mabaya sio jambo baya hivyo ni jambo zuri na tunapaswa kufurahi tunapoyaona?

Kama mabaya ni mabaya in any sort basi msababishi wa kwanza wa mabaya ndio "Mbaya"

Sasa binadamu hawezi kuingizwa kwenye hii lawama kwasababu yeye sio chanzo cha ubaya.

Mungu aliyeumba huu ulimwengu wenye kuruhusu mabaya kwa lengo la kuwatahini watu wake, ndio mbaya.

Ukisema Mungu hawezi kuwa mbaya licha ya kwamba yeye kuumba ulimwengu wenye kuruhusu mabaya basi hapo hapo tutakubaliana kuwa binadamu anayefanya ubaya uliokuwa sehemu ya asili yake hawezi kulaumiwa kivyovyote.
 
Unalazimisha Mungu awepo tu, hyo ni hypothesis tu kwenye mambo ya asili usiyoyaelewa.

Wewe umeyatungia hadithi na unayaforce yawe kweli.

Tunaprove vipi hiyo hypothesis yako ili tuthibitishe pasina shaka!?

Unaweza thibitisha Mungu yupo!?
 
Mola alipo tuumba akatupa uhuru, tukipenda tumshukuru na tukiamua tukufuru, huo uhuru uko nao wewe pia.
Unaelewa mantiki ya uhuru haiambatani na adhabu?

Unampa mtoto uhuru wa kuchagua kula Biriani au Pizza, huo ndio uhuru.

Kumuambia mwanamke unaye mtongoza achague kati ya kukupenda wewe au kutokupenda halafu ukasema akichagua kutokupenda wewe utamuua. Huo sio uhuru wa kuchagua

Hiyo ni amri.

Sasa Mungu anasema amekupa uhuru wa kuchagua mema na mabaya, ukichagua mabaya unaenda motoni kuchomwa milele.

Huo sio uhuru hiyo ni amri yenye kitisho.

Ameweka kitisho kilichowalazimisha watu wawe wanafki wafanye anayotaka ilimradi tu wasichomwe moto.
 
How matatizo (mabaya) ni moja ya kipimo cha imani ya mwanadamu!?

Kwanini kuamini kumefanywa kuwa muhimu sana kuliko kujua!?
 
Mungu mjuzi wa yote anapimaje imani ya mtu!?

Au Mungu wao hajui yote?
 
Allah anajua hata kile ambacho hakipo kikiwepo kingekuwaje.

Ana njia nyingi za kuwazindua watu bali hata angetaka wote tumuamini angefanya hivyo, ila ameweka utaratibu huu ili tufikie lengo la kuwepo duniani.
Wakati anafanya hivyo, lengo lake si lilikuwa kuufanya ulimwengu uwe bora?

Sasa kama aliweza kuona yatayojiri kabla hayajatokea maana yake aliona imperfections zote.

Na alikuwa na uwezo wa kubadili au kuboresha kuondoa hizo imperfections lakini akaziacha.

Maana yake huu ulimwengu wenye njaa, masunami, vimbunga, matetemeko, magonjwa, yanayoua mamilioni ya watu ikiwemo watoto wadogo wasiojua baya na zuri.

Kwa Mungu huu ndio ulikuwa ulimwengu bora kwake wakati anachagua aina gani ya ulimwengu bora kwa ajili ya viumbe wake anaosema anawapenda kwa upendo wote.

Kwa maana hiyo sasa ndio tunarudi kwenye hoja yangu kuwa ni Mungu anayetengeneza ugonjwa kisha anataka umlilie ili akupe dawa.

Halafu ukipona uanze kumsifia kuwa anakujali wakati kiuhalisia yeye ndiye aliyekutengenezea tatizo.

So Mungu huyu ana inferiority haamini kwenye kupendwa bila kutengeneza drama, haamini kuwa anaweza kusifiwa bila kutengeneza tatizo ili umrejee kumlilia.

Ni Mungu wakijinga anayependa sifa za kishamba.
 
Kwamba Allah aliweka milima ili kuweka stability dunia isiyumbishwe!?

Yani mtu anakwambia kwamba nyota ni mapambo!?

Mungu huyo hajui hata kuwa jua ni nyota then unakuja kutaka kuhadaa watu hapa waamini na unawaita wajinga wasioamini?

Kabisa Homo sapiens wa karne ya 21 unakubali mambo hayo?

Imani za kidini ni shambulio la akili
 
Yes the epic of Gilgamesh,

Hapo unamkuta Atrahasis ndiye mhusika mkuu (Noah wa biblia)

Nakumbuka alikuwa ni Mungu wa maji anajulikana kama Enlil ndiye alimwambia Atrahasis atengeneze safina kwani anataka kukata bomba.

"Kwasababu suala la kiimani limekaa kisaikolojia zaidi, utawaskia tu waamini wakisema kuwa sisi tunafanya kazi ya shetani kupotosha ukweli"
 
Je makosa ya kisayansi yaliyoandikwa kwenye quran unayachukuliaje?

Mungu hajakupa access ya kuyaona!?
 

Maandiko ni hadithi za uongo tu. Zisizo na uhalisia.

"Right kama sio utandawazi, waisrael wangetunga Exodus part 2 juu ya Holocaust kumtoroka farao wa kijerumani."
 
Vipi kuhusu milima kutengeneza stability dunia isiyumbishwe?

Vipi kuhusu nyota kuwa ni mapambo?
 
Habari ya Mungu ni kweli na ushahidi upo..

Kwa sisi waislam, Qur an imeeleza vitu vingi ambavyo tunajionea wenyewe sasa hivi na wanasayansi wanazidi kugundua vitu ambavyo Qur'an ilishavielezea miaka 1400+ iliyopita.

Hata mimi nishawahi kuwa na mashaka juu ya uwepo wa Mungu na juu ya imani yangu. Ila baada ya kusoma Qur'an na kuifuatilia pamoja na kufuatilia vitu vilivyogunduliwa na wanasayansi basi shaka yangu yote iliondoka
 
Vitabu vya dini havithibitishi hata kwa 1% uwepo wa Mungu.
 
Umesoma Qur'an au unaleta ujuaji?
Sijasoma! Ila najua haiwezi kuthibitisha uwepo wa Mungu. Kama unalielewa neno "thibitisha" utajua namaanisha nini.

Hakuna ushahidi wa kuweza kuthibitisha uwepo wa Mungu. Hata mimi siwezi kuthibitisha kama kweli Mungu hayupo. Tofauti ni kwamba wewe unaishi kwa imani wakati mimi nimekosa imani kwa mambo ambayo hayana ushahidi.

Kabla ya kuuliza kama naleta ujuaji inabidi uwe open-minded kujadili mada kama hizi. Kila mtu ana mtazamo wake linapokuja suala la uwezekano wa kuwepo na Mungu.
 
Hofu ya matokeo fulani ukifanya vitendo vya hovyo lazima iwepo Ili kutunza amani. Ndio maana tuna sheria za nchi.

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
Kwahy unaamini bila ya sheria za nchi hakuna amani??

Na vip kabla ya mambo ya nchi hapo kale watu hawakuwa na amani ?? Je, ilisababishwa na hofu ya nani??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…