Kutotimia kwa ndoto yangu jana ya Mwigulu Nchemba kutangaza kujiuzulu hakunishangaza!

Kutotimia kwa ndoto yangu jana ya Mwigulu Nchemba kutangaza kujiuzulu hakunishangaza!

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592
Toka siku niliposikia kuwa WIZARA ya Fedha ingetoaa ufafanuzi kuhusu tozo ya miamala ya simu na benki, nimekuwa nikiota ndoto.

Kuna ndoto na kuna ndoto. Kuna ndoto za usiku na kuna ndoto za mchana.

Ndoto za usiku ama ni za kuleta tumaini au kutia hofu na ingawa kwa muda huweza kuleta tumaini, hazitekelezeki!

Kuna ndoto unaaamka kwa hofu na inakuchukua muda kuamini ni ndoto tu na kushukuru kwa kutokuwa kweli.

Kuna ndoto unaamka kwa furaha na inakuchukua muda kuamini ni ndoto tu na kulaani kwa nini haikuwa kweli.

Binadamu tumejaaliwa akili zinazotuwezesha kupanga namna ya kuendesha maisha yetu hapa duniani.

Mipango kama hii ni ndoto pia lakini ni ndoto za mchana na tofauti na za usiku uwezo wa kuzitekeleza tunao.

Tumaini langu hadi jana lilikuwa ni kujiuzulu kwa Waziri wa Fedha, Dr. Mwigulu Nchemba PhD kwa tuhuma zilizomkabili.

Tuhuma za kusimamia, kwa niaba ya dola, zoezi la kutuibia sisi walipa kodi wa taifa hili kupitia kinachoitwa tozo!

Pamoja na leo kuamka kwa furaha kubwa, imenichukua toka asubuhi kuamini kuwa tumaini langu hilo halikutimia.

Ngoja niendelee kulaani tu kwa nini halikutimia...
 
Toka siku niliposikia kuwa WIZARA ya Fedha ingetoaa ufafanuzi kuhusu tozo ya miamala ya simu na benki, nimekuwa nikiota ndoto.

Kuna ndoto na kuna ndoto. Kuna ndoto za usiku na kuna ndoto za mchana.

Ndoto za usiku ama ni za kuleta tumaini au kutia hofu na ingawa kwa muda huleta tumaini, hazitekelezeki!

Kuna ndoto unaaamka kwa hofu na inakuchukua muda kuamini ni ndoto tu na kushukuru kwa kutokuwa kweli.

Kuna ndoto unaamka kwa furaha na inakuchukua muda kuamini ni ndoto tu na kulaani kwa nini haikuwa kweli.

Binadamu tumejaaliwa akili zinazotuwezesha kupanga namna ya kuendesha maisha yetu hapa duniani.

Mipango kama hii ni ndoto pia lakini ni ndoto za mchana na tofauti na za usiku uwezo wa kuzitekeleza tunao.

Tumaini langu hadi jana lilikuwa ni kujiuzulu kwa Waziri wa Fedha, Dr. Mwigulu Nchemba PhD kwa tuhuma zilizomkabili.

Pamoja na leo kuamka kwa furaha kubwa, imenichukua toka asubuhi kuamini kuwa tumaini langu hilo halikutimia.

Ngoja niendelee kulaani tu kwa nini halikutimia...
Ndoto hutimia kwa nyakati zake... Na baadhi huja kinyume...!
 
Ndoto hutimia kwa nyakati zake... Na baadhi huja kinyume...!
Hizo ndio hasa ni ndoto za usiku, hatuna uwezo nazo. Za mchana ni habari nyingine!

Mwigulu mwenyewe kakiri kuwa pesa wananzotuibia kupitia tozo zinatumika kwenye miradi ya kimkakati!

Hii yawezekana ni kweli kwani hata tozo yenyewe nayo yaonekana ni mradi wa kimkakati!

Hii miradi ya kimikakati...nadhani bado niko ndotoni! Ndoto ya usiku!
 
Viongozi wa kiafrika bora wafie ofisini kwa risasi kuliko kujiuzulu .

Hawa viongozi wa kiafrika ni kama cotter pin huwa inaingia kwa nyundo na inatokewa kwa nyundo
 
Back
Top Bottom