Kutumia jina Tanzania kama jina la biashara inaruhusiwa kisheria au nayo ni kama bendera mpaka kibali maalum?

Kutumia jina Tanzania kama jina la biashara inaruhusiwa kisheria au nayo ni kama bendera mpaka kibali maalum?

Nanye Go

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
10,856
Reaction score
14,607
Nauliza kama inawezekana kutumia Jina Tanzania kwenye Biashara, Kwa mfano huwa naona Kenya Commercial Bank(KBC), Kenya Air Ways(KQ).

Kwa Tanzania hili linakubalika?
 
Japo sijajua kama inaruhusiwa lakini kwa uelewa wangu KCB na Kenya Airways kuna hisa za serikali ya Kenya ndio maana zinatumia majina hayo. wa mfano hata Makao Makuu ya KCB hapa nchini yapo jengo la Harambee House ulipo ubalozi wa Kenya pia
 
Japo sijajua kama inaruhusiwa lakini kwa uelewa wangu KCB na Kenya Airways kuna hisa za serikali ya Kenya ndio maana zinatumia majina hayo. wa mfano hata Makao Makuu ya KCB hapa nchini yapo jengo la Harambee House ulipo ubalozi wa Kenya pia
Nashukuru kwa majibu mazuri. Na ingekuwa Serikali haina hisa wasingeruhusiwa kama hapa kwetu au ikitokea serikali ikauza share zake zote itabidi mmiliki mpya abadili jina?
 
Nashukuru kwa majibu mazuri. Na ingekuwa Serikali haina hisa wasingeruhusiwa kama hapa kwetu au ikitokea serikali ikauza share zake zote itabidi mmiliki mpya abadili jina?
Kwa maoni yangu nadhani wasingeruhusiwa.Kama serikali ikondoa hisa zake zote yawezekana wakatakiwa kubadili jina au kama KCB basi zikabaki initials tu bila kusomeka kwa kirefu chake kama ilivokua kwa CRDB sasa hivi ambapo haisomwi tena kama Cooperative and Rural Development Bank kama wakati ule ilipokua inamilikiwa na serikali. Baada ya serikali kuondoa/kuuza shares zake ikawa inajulikana tu kama CRDB Bank
 
Haiwezekani kwa mtu binafsi kutumia jina Tanzania kwenye biashara zake labda iwe ni kikundi cha watu na lazima jina liwe na muendelezo fulani haitaruhusiwa mjiite mfano Tanzania Company.
 
Haiwezekani kwa mtu binafsi kutumia jina Tanzania kwenye biashara zake labda iwe ni kikundi cha watu na lazima jina liwe na muendelezo fulani haitaruhusiwa mjiite mfano Tanzania Company.
Na ikiwa nyie pekee ndio wawakilishi wa kampuni fulani iliyo nje ya nchi, mfano mkajiita Tanzania Bajaji Distributors Haikubaliki hiyo pia?!
 
Hairuhusiwi kutumia jina, bendera wala nembo yoyote ya taifa katika jina la biashara yako
 
Hairuhusiwi.
Nakumbuka kuna mwaka chama fulani cha siasa walikuwa wanajitahidi sana kuchanganya mambo zao na rangi za bendera walipigwa stop
 
Na vipi kama unafungua kampuni pale Nairibi ukaiita Tanzania Sisal dealer?!
 
Hairuhusiwi.
Nakumbuka kuna mwaka chama fulani cha siasa walikuwa wanajitahidi sana kuchanganya mambo zao na rangi za bendera walipigwa stop
Lakini sidhani mbona DP bendera yao ni kama ile ya Tanganyika mpaka leo?
 
Hairuhusiwi.
Nakumbuka kuna mwaka chama fulani cha siasa walikuwa wanajitahidi sana kuchanganya mambo zao na rangi za bendera walipigwa stop
Na sababu hasa ni nini?!
 
Lakini kuna kampuni naifahamu wanajiita Mkonge Tanzania LTD, hiyo inakuwaje sawa?!

Unaweza kuiita Mkonge (T) Ltd kuonyesha tuu ni kampuni iliyosajiliwa Tanzania, mfano Norman & Dawbarn (Tanzania) Ltd lakini ipo ya UK au COWI (T) Ltd lakini zipo Cowi za nchi nyingine huwezi kuanza na Tanzania Mkonge Ltd
 
Na ikiwa nyie pekee ndio wawakilishi wa kampuni fulani iliyo nje ya nchi, mfano mkajiita Tanzania Bajaji Distributors Haikubaliki hiyo pia?!
Haitakubalika!... mtakua mnaua ushindani wa ndani
 
Haitakubalika!... mtakua mnaua ushindani wa ndani
Yani neno Tanzania linaua ushindani wa ndani?! Yani Tanzania haitakiwi kutumika au kutumiwa na kampuni binafsi popote pale?!
 
Back
Top Bottom