Kuunga Mkono Nia ya Makongoro Nyerere (Urais 2015)

Kuunga Mkono Nia ya Makongoro Nyerere (Urais 2015)

Zakumi

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2008
Posts
5,063
Reaction score
2,478
Utangulizi: Kwa wanaonifahamu hapa JF, wanafahamu kuwa siasa zangu ni za mkondo wa kulia zenye kuhimiza maendeleo ya watu binafsi na wakati huohuo kulinda maslahi ya wanyonge (ubebari mwema A.K.A compassionate capitalism). Kwa mtaji huu sijawahi kuunga mkono chama chochote cha kisiasa. Na kinadharia nisingeweza kuunga mkono mgombea kutoka CCM.

Lakini kutokana na kufanana kwa ahadi wanazotoa wanasiasa kutoka vyama vyote vya siasa wenye nia ya kuwa rais, nimehamua kuunga mkono nia za Makongoro Nyerere (AKA Mako). Sababu za kufanya hivi nimeziweka kwenye makundi matatu. Kundi la kwanza, iwapo CCM itashinda. Kundi la pili, iwapo upinzani utashinda. Kundi la tatu, iwapo itaundwa serikali ya mseto.

Tuanze na kundi la kwanza: Hata kama wewe ni mpinzani ni lazima uamini kuwa CCM wanayo asilimia fulani ya kushinda uchaguzi. Je CCM ikishinda, ni nani ungependelea awe rais? Kumbuka rais mtarajiwa atakaa madarakani kwa miaka mitano au kumi ijayo. Je unapendelea maumivu yaendelee?

Mako hana uzoefu mkubwa lakini huo ni mtaji na sio upungufu. Kwani hata wasafi walio upinzani hawana uzoefu wa uwaziri, urais au madaraka yoyote makubwa ya kiserikali.

CCM ni mali ya watanzania. Kwa wale wenye upeo mdogo wa historia, wakati wa mfumo wa chama kimoja, watanzania walilazimishwa kukijenga hiki chama. Wakulima, wafanyakazi, na wafanyabiashara walikatwa mapato yao bila kupenda kujenga hiki chama. Dr. Slaa, Mkandara, Lipumba, Seif Ahmed, Warioba, Mzee Mwanakijiji, Mzee Mtei, Kichuguu walichangia hiki chama. Hivyo wakati umefika kukirudisha chama kwa wananchi. Japokuwa wengine tumejitoa kwa matakwa yetu, waliobaki wasikilizwe.

Katika tangazo lake la nia ya kugombea, Makongoro ameonyesha kuwa anafahamu asili ya chama. CCM ni chama cha wananchi na sio wagombea nafasi za uongozi. Ninaamini akipewa nafasi ya kugombea atawakilisha wananchi na sio matakwa yake binafsi.

Kundi la pili, iwapo upinzani utashinda:
Upinzani ukishinda, sio mwisho wa CCM. CCM itabidi ijisafishe na kuwa mpinzani wa kweli. Kiongozi wa kuijenga CCM upya ni lazima atoke nje ya kundi lolote la mafisadi na awe tayari kukijenga upya chama. Makongoro anao uwezo huo kwa sababu yupo tayari kusema ukweli. Sio mwoga. Kweli hotuba yake alisema maneno bila kuzunguka mbuyu.

Kundi la tatu, iwapo itaundwa serikali ya mseto: Kwa historia za serikali za kiAfrika uwezekano huu ni mkubwa sana. Uchaguzi unaweza kuja na matatizo ambayo yakalazimisha uundaji wa serikali ya mseto. Wewe kama mpinzani, je ungemtaka nani kutoka CCM awe mwakilishi katika meza ya kuunda serikali ya mseto? Kama viongozi wa sasa wa CCM wanaleta matatizo ndani ya chama chao kwa ubinafsi, hawatasahu ubinafsi wao ndani ya serikali ya mseto. Kwa mtaji huu ni Mako mwenye sifa za kuwakilisha CCM kwenye serikali ya mseto kwa sababu anazosifa sawa na viongozi wa upinzani. Yeye ni outsider katika shughuli za kiutawala.

Wenu Z10.

cc: Mkandara, Jasusi, Mchambuzi, Nguruvi3, Kichuguu, alinda, gfsonwin, Jokakuu, Barubaru, Mag3, etc
 
... .. nimekusoma, ila nitakujibu Jumatatu nikishamaliza sherehe za weekend.
 
Mimi sijavutiwa wala kushawishiwa kabisa na huyo Makongoro.

Kwangu anaonekana kama ni mtu mbabaishaji aliye mwingi wa maneno matupu.

Naona kinachowavuta watu kwake ni jina lake na familia anayotoka.

Napatwa na hisia huenda atakuwa bomu zaidi kuliko hata Kikwete.

Badala ya kuwa amiri jeshi mkuu ataishia kuwa amiri mchekeshaji mkuu.

Fanyeni hilo kosa la kumteua na kumchagua na mtaja nambia.

Msije sema sikuwaonya.
 
Mimi sijavutiwa wala kushawishiwa kabisa na huyo Makongoro.

Kwangu anaonekana kama ni mtu mbabaishaji aliye mwingi wa maneno matupu.

Naona kinachowavuta watu kwake ni jina lake na familia anayotoka.

Napatwa na hisia huenda atakuwa bomu zaidi kuliko hata Kikwete.

Badala ya kuwa amiri jeshi mkuu ataishia kuwa amiri mchekeshaji mkuu.

Fanyeni hilo kosa la kumteua na kumchagua na mtaja nambia.

Msije sema sikuwaonya.
Nyani Ngabu umenitoa kwenye starehe zangu za wikiendi kwa sababu ya post yako hiyo hapo juu nikaona nikujioibu kabla thread haijajaa.


.......... Mimi nilisoma naye sekondari na ninamfahamu vizuri sana. Kutumia lugha ya kuchekesha au kuwa na jina la Nyerere haku-define uwezo wake; ni mtendaji imara anayejua organizesheni, na mwenye kusimamia malengo akiwa tayari kumwadhibu mmtu yeyote hata rafiki yake bila kumwonea aibu. Ni tofauti kabisa na unavyodhani. Ninadhani upungufu wake ni kuwa anaweza hana hela inayotakiwa kuendesha kampeini imara ndani ya CCM leo hii.

Ni nadra sana mimi kumsema vizuri mtu aliyeko ndani ya CCM.
 
..I dont see why I should vote for Makongoro and overlook ppl like Dr.Slaa, Tundu Lissu, Prof.Lipumba, Freeman Mbowe, etc ambao wamekuwa wakipiga vita ufisadi kwa muda mrefu sasa.

..What Makongoro said is nothing new to some of us. Labda ni mambo mapya kutamkwa na mwana-CCM, lakini ni mambo yanayosemwa kila kukicha na wa-Tz wenzetu walioko vyama vya upinzani. Tofauti ni kwamba Makongoro doesnt have to pay the price ambayo wapinzani wanalazimika.

..Makongoro hapigwi virungu, au mabomu ya machozi, au kuzuliwa kesi za ajabu-ajabu, au kuchafuliwa binafsi, kama inavyotokea kwa wapinzani.

NB:

..Kuhusu serikali ya mseto, I would rather have Prof.Mark Mwandosya aki-negotiate kwa niaba ya CCM. Katika wagombea wote wa CCM nadhani huyu mzee ndiye muungwana na anayeweza kutanguliza maslahi ya wananchi kuliko wenzake.

cc Nyani Ngabu, Zakumi, Nguruvi3, Monstgala, Nguruvi3, Kigogo
 
Last edited by a moderator:
Asante sana Zakumi kwa andiko lako..

Ingawaje nafahamu kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu ni lazima Rais atoke Ukawa au CCM. Ila ninapata tatizo, kwa wale wote ambao wameisha tangaza nia,sijaona wa kunishawishi kuwa anagombe urais kwa kusukumwa na matatizo ya nchi yetu.

Kuhusu Makongoro sijaona kama anakitu cha kunifanya mimi nimpe kura yangu. kwanini ninasema hivi..

Kwa sababu mgombea urais ni lazima tumpima kwa mafanikio yake katika yadhifa mbali mbali alizowahi/alizonazo.

Tumpime kwa jinsi alivyopiga vita ufisadi na rushwa kwa nguvu zake zote,

Tumpime kwa kusaidia jamii iliyomzunguka katika swala zima la kujiletea maendeleo,
Tuangalie matarajio yake ndani ya miaka 5 au 10 anataka kuona Tanzania ya aina gani ndani ya hiyo miaka, na atafanya nini kuhakikisha Tanznia ya aina hiyo inapatikana.

Hivyo basi nikimangalia Makongoro naona anapwaya tena sana, labda inawezekana simfahamu vizuri au sifatilii siasa zake. Ndo maana sijaona kitu chochote ambacho anaweza kusimama kifua mbele na kusema nimefanya hiki au kile zaidi ya ile vita ya Kagera.

Na hapa ningependa wanaomfahamu vizuri watupe record zake hasa baada ya vita ya Kagera maana hatuwezi kuchagua rais kwa vile tu alipiga vita ya Kagera, tunahitaji zaidi ya hapo.

Record nilizona ni kuwa aliwahi kuwa Mbuge wa Arusha lakini alivuliwa Ubunge sijui kwa kosa lipi???
Na kwa sasa ni Mbunge wa East Afrika lakini sina kumbumbuku yeyote kama kule kuna kitu alichotetea.. Nitaomba watu wanaofahamu zaidi watujuze ni kwa jinsi gani anamekuwa mtetezi wa nchi yetu wawapo bungeni. Ni ni mafaniko yapi Tanzania imeyapata kupitia kwa Makongoro katika hilo bunge.

Mpaka sasa naona kama Makongoro anabebwa zaidi na jina la Baba yake, hana dhamira ya kweli ya kumkomboa mtanzania, Na hata katika kutangania nia alionyesha kuwa ni mtu ambaye hakuwa "seriuos" maana hata alishindwa kutaja ni sababu gani iliyomsukuma kutaka urais. Sana sana alisema yeye anasubiri ilani ya chama (ni vizuri kusubiri ilani ya chama) lakini hata hivyo wewe kama mgombea urais lazima huwe na kitu ambacho unatamani kukirekebisha au kukiboresha, ni lazima uwe ni malengo ya kutoa watu wako hapa na kuwapeleka pale kwa bahati mbaya Makongoro hakuonyesha dhamira ya kweli sana sana aliadithia jinsi alivyojiunga na NCCR miaka 20 iliyopita...


Na nafikri hata hakuwa na nia ya kugombea lakni baada ya CCM kuona kila mtu ana "skendo" ndo wakamtafuta Makongoro ili aokoe janga.
 
Last edited by a moderator:
Zakumi, mimi ninalo swali moja tu kwako; unamtenganisha vipi Makongoro na wanachama pamoja na viongozi wengine ndani ya CCM? Kabla hujanijibu ningependa nikukumbushe tukio ambalo limepelekea watu wengi kupoteza kabisa imani na CCM nao ni uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995. Wengi waliaminishwa kwamba safari hiyo, baada ya Mzee Rukhsa, CCM inatuletea ideal candidate, mtu msafi asiye na tone la kashfa, William Benjamin Mkapa, Mr. Clean! Kwa miaka kumi tuliushuhudia na kuuvumilia huo usafi wake ikiwa ni pamoja na kufanya biashara akiwa Ikulu.

Mwaka 2005, CCM ilituletea waliyedai ni kijana anayejua matatizo ya Watanzania na hivyo kupewa ridhaa ya uongozi wa taifa hili kwa asilimia 80%! Huyo kijana aliyeingia kimachachari kwa ari na nguvu mpya katumia zaidi ya robo ya muda wake kutalii kwa kisingizio cha kuomba hadi kuchokwa ndani na nje ya nchi yetu. Kwa ufanisi mkubwa ameweza kuligawa taifa hili kikanda, kikabila na kidini na hata pale alipooneshwa kushindwa, CCM ilihakikisha anapata awamu ya pili.

Sasa unapendekeza aingie Makongoro Nyerere kwa laghai zile zile kwamba ataleta kipya na kufanikisha mabadiliko; ndio maana nimeuliza hapo mwanzo, unamtenganisha vipi na wanachama wenziye anaoshindana nao, kula nao na kuafikiana nao?
 
Last edited by a moderator:
Zakumi msome Mag3 hapo juu.

Ninachotaka kuongezea ni hiki, Mako alikuwa mwenyekiti wa Mkoa wa CCM. Na sasa ni mbungewa
EA.


Mako anakuja na ukali kuhusu rushwa. Anasema Rais ni mtu anayechukia rushwa, kwa bahati mbaya amezungukwa na wala rushwa. Kauli hii tu inaonyeshaMakongoro ni mwoga na hawezi kukabiliana na kundi lililonunua CCM

Rais anaposhindwa kukabiliana na wala rushwa, au anapochagua kundi la wala rushwa kumzunguka, tatizo si wala rushwa.
Kazi ya wala
rushwa ni kula rushwa.

Tuliyempa kila zana na rasilimali za nch
kupambana na rushwa ni Rais.


Mako angesema Rais ameshindwa kukabiliana na rushwa kama ilivyokuwa kwa Mkapa

Kauli yake haionyeshi utayari wa kukabiliana na rushwa, bali woga wa jina kutemwa! Anatufaa kweli?

Lakini pia tuonyeshe, ni lini na wapi Makongoro akiwa Mwanachama au Mwenyekiti aliwahi kusimama na kukemea, kukabiliana au kuzomea rushwa inayofanywa na kundi alilomo?

Kuhusu, nani wa mwenye afadhali, ni ukweli ndani ya CCM hakuna.

Hata mseto ukitokea litakachotokea ni 'pick the best from the garbage'kama si hivyo, unatushawishi 'choose the lesser evil'
 
Mimi sijavutiwa wala kushawishiwa kabisa na huyo Makongoro.

Kwangu anaonekana kama ni mtu mbabaishaji aliye mwingi wa maneno matupu.

Naona kinachowavuta watu kwake ni jina lake na familia anayotoka.

Napatwa na hisia huenda atakuwa bomu zaidi kuliko hata Kikwete.

Badala ya kuwa amiri jeshi mkuu ataishia kuwa amiri mchekeshaji mkuu.

Fanyeni hilo kosa la kumteua na kumchagua na mtaja nambia.

Msije sema sikuwaonya.

Ngabu:
Ni kweli katika hotuba yake kulikuwa hakuna substance zaidi ya tangazo. Vilevile watoto wa Nyerere wamekuwa chini ya kivuli cha baba yao. Hivyo itamfanya achukue juhudi za ziada kuondoka katika kivuli hicho.
Kwa kumuangalia na kupima maendeleo ya matukio ya kisiasa yanavyoendelea, kwa maoni yangu naona kuna network iliyomsukuma kutanganiza nia hii. Na kama hakuna network, basi platform yake ni kupingana na wanaotumia pesa katika kampeni.
Kuhusiana na hotuba. Hana substance lakini ana uwezo mkubwa wa kujieleza. Hivyo akipata watu wa kumwandikia hotuba na yeye kuwa na juhudi za kufuata Script anaweza kuwa very effective kwenye milolongo ya kampeni.
 
Zakumi na Nyani Ngabu.

Nashangaa kuwa hamkuona substance katika hotube yake, lakini kwa uhakika hotuba hiyo ndiyo iliyokuwa na substance sana kuliko wengine wote waliotoa hotuba za nia: Lowassa, Makongoro, Januari, Nchemba, Wassira, Ngereja na Membe

Inawezekana substance ni relative, lakini nimefuatilia hotuba zote za niolwataja hapo juu, wote walikuwa wanatoa ahadi rahisi rahisi za kawaida za kuwa wataleta maisha ya neema - yaani aina ya ahadi za Kikwete za 2005 na 2010. Hakuna aliyeainisha kuwa anajua chanzo halisi cha matatizo ya watanzania jinsi atakavyopambana na chanzo hicho - huwezi kuleta neema bila kuondoa chanzo cha matatizo. Wengine wanachukulia kuwa watakuwa na hela nyingi sana za kujenga mabarabara ya ghorofa nchi nzima au watakuwa na hela za kujenga Academis za kisasa za michezo nchi nzima. Wengine wanachukulia kuwa kuwapo kwao madarakani tu ni tosha kuleta neema bila kufanya lolote.

Makongoro kaaninisha matatizo mawili tu ambayo ndiyo anataka kupambana nayo, na ninakubaliana naye kuwa akipambana na matatizo hayo akayaonyyosha, basi maisha mazuri yatakuja yenyewe. Alisema tatizo la kwanza ni watu kutokufuata taratibu, ambalo ukilipanua zaidi ni lile la viongozi wenyewe na raia kwa jumla kutokufuata sheria za nchi. Alitumia muda kusema kuwa utaratibu uliopo ni kuwa wagombea watakuwa wananadi ilani ya CCM, lakini wagombea wote hao badala ya kufuata utaratibu huo wa kuahdi ilani wao wanakuja na ahadi zao ambazo hazijapitishwa kuwa ilani ya CCM. Hilo limewahusu wagombea wengine wote ispokuwa yeye

Tatizo la pili aliloliongelea ni ubinafsi wa viongozi ambao hupelekea kuwa wezi wa mali ya umma na wala rushwa- yaani viongozi wanakuwa hawafanya kazi kwa ajili ya taifa bali kwa ajili yao na familia zao tu. Ingawa alitumia muda mfupi tu kulizungumzia hilo la pili, alibainisha kuwa kuna tatizo kubwa sana nchini ni pale viongozi wanapoendekeza maslahi yao binasfi na kusahau maslahi ya taifa. Alitumia maneno vibaka, na akatolea mfano wa wale waliotaka kumpindua mwenyekiti wa chama chao.
 
Last edited by a moderator:
..I dont see why I should vote for Makongoro and overlook ppl like Dr.Slaa, Tundu Lissu, Prof.Lipumba, Freeman Mbowe, etc ambao wamekuwa wakipiga vita ufisadi kwa muda mrefu sasa.

..What Makongoro said is nothing new to some of us. Labda ni mambo mapya kutamkwa na mwana-CCM, lakini ni mambo yanayosemwa kila kukicha na wa-Tz wenzetu walioko vyama vya upinzani. Tofauti ni kwamba Makongoro doesnt have to pay the price ambayo wapinzani wanalazimika.

..Makongoro hapigwi virungu, au mabomu ya machozi, au kuzuliwa kesi za ajabu-ajabu, au kuchafuliwa binafsi, kama inavyotokea kwa wapinzani.

NB:

..Kuhusu serikali ya mseto, I would rather have Prof.Mark Mwandosya aki-negotiate kwa niaba ya CCM. Katika wagombea wote wa CCM nadhani huyu mzee ndiye muungwana na anayeweza kutanguliza maslahi ya wananchi kuliko wenzake.

cc Nyani Ngabu, Zakumi, Nguruvi3, Monstgala, Nguruvi3, Kigogo

Jokakuu:
Certainly candidates from the opposition parties have paid a heavier price than those from the ruling party. But we shouldn't forget that, on the Election Day, voters aren't going to reward the opposition simply because they have done a marvelous job in the past 10 or 20 years. Politics doesn't work that way.
Voters have their priorities too. Some are looking for effective leaders while others looking for somebody they could relate too. The question is does Makongoro have these two attributes? I believe he has, even though he's still a member of CCM.
 
..I dont see why I should vote for Makongoro and overlook ppl like Dr.Slaa, Tundu Lissu, Prof.Lipumba, Freeman Mbowe, etc ambao wamekuwa wakipiga vita ufisadi kwa muda mrefu sasa.

..What Makongoro said is nothing new to some of us. Labda ni mambo mapya kutamkwa na mwana-CCM, lakini ni mambo yanayosemwa kila kukicha na wa-Tz wenzetu walioko vyama vya upinzani. Tofauti ni kwamba Makongoro doesnt have to pay the price ambayo wapinzani wanalazimika.

..Makongoro hapigwi virungu, au mabomu ya machozi, au kuzuliwa kesi za ajabu-ajabu, au kuchafuliwa binafsi, kama inavyotokea kwa wapinzani.

NB:

..Kuhusu serikali ya mseto, I would rather have Prof.Mark Mwandosya aki-negotiate kwa niaba ya CCM. Katika wagombea wote wa CCM nadhani huyu mzee ndiye muungwana na anayeweza kutanguliza maslahi ya wananchi kuliko wenzake.

cc Nyani Ngabu, Zakumi, Nguruvi3, Monstgala, Nguruvi3, Kigogo
JokaKuu Point yako kubwa hapa ni kwamba tusichague CCM; which I fully support. Lakini iwapo itatokea CCM ikichaguliwa ni nani kati ya waliotangaza nia ambaye ana nafuu? Tunapokuwa tunaangalia ndani ya CCM, sioni mwingine zaid ya Makongoro na Mwandosya; iwapo tutakubaliana tusichague CCM basi hatuna haja ya kuwaongelea wagombea wake.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana Zakumi kwa andiko lako..

Ingawaje nafahamu kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu ni lazima Rais atoke Ukawa au CCM. Ila ninapata tatizo, kwa wale wote ambao wameisha tangaza nia,sijaona wa kunishawishi kuwa anagombe urais kwa kusukumwa na matatizo ya nchi yetu.

Kuhusu Makongoro sijaona kama anakitu cha kunifanya mimi nimpe kura yangu. kwanini ninasema hivi..

Kwa sababu mgombea urais ni lazima tumpima kwa mafanikio yake katika yadhifa mbali mbali alizowahi/alizonazo.

Tumpime kwa jinsi alivyopiga vita ufisadi na rushwa kwa nguvu zake zote,

Tumpime kwa kusaidia jamii iliyomzunguka katika swala zima la kujiletea maendeleo,
Tuangalie matarajio yake ndani ya miaka 5 au 10 anataka kuona Tanzania ya aina gani ndani ya hiyo miaka, na atafanya nini kuhakikisha Tanznia ya aina hiyo inapatikana.

Hivyo basi nikimangalia Makongoro naona anapwaya tena sana, labda inawezekana simfahamu vizuri au sifatilii siasa zake. Ndo maana sijaona kitu chochote ambacho anaweza kusimama kifua mbele na kusema nimefanya hiki au kile zaidi ya ile vita ya Kagera.

Na hapa ningependa wanaomfahamu vizuri watupe record zake hasa baada ya vita ya Kagera maana hatuwezi kuchagua rais kwa vile tu alipiga vita ya Kagera, tunahitaji zaidi ya hapo.

Record nilizona ni kuwa aliwahi kuwa Mbuge wa Arusha lakini alivuliwa Ubunge sijui kwa kosa lipi???
Na kwa sasa ni Mbunge wa East Afrika lakini sina kumbumbuku yeyote kama kule kuna kitu alichotetea.. Nitaomba watu wanaofahamu zaidi watujuze ni kwa jinsi gani anamekuwa mtetezi wa nchi yetu wawapo bungeni. Ni ni mafaniko yapi Tanzania imeyapata kupitia kwa Makongoro katika hilo bunge.

Mpaka sasa naona kama Makongoro anabebwa zaidi na jina la Baba yake, hana dhamira ya kweli ya kumkomboa mtanzania, Na hata katika kutangania nia alionyesha kuwa ni mtu ambaye hakuwa "seriuos" maana hata alishindwa kutaja ni sababu gani iliyomsukuma kutaka urais. Sana sana alisema yeye anasubiri ilani ya chama (ni vizuri kusubiri ilani ya chama) lakini hata hivyo wewe kama mgombea urais lazima huwe na kitu ambacho unatamani kukirekebisha au kukiboresha, ni lazima uwe ni malengo ya kutoa watu wako hapa na kuwapeleka pale kwa bahati mbaya Makongoro hakuonyesha dhamira ya kweli sana sana aliadithia jinsi alivyojiunga na NCCR miaka 20 iliyopita...


Na nafikri hata hakuwa na nia ya kugombea lakni baada ya CCM kuona kila mtu ana "skendo" ndo wakamtafuta Makongoro ili aokoe janga.
Alinda

Unafanya makosa kudai kuwa utamachagua Rais kwa kuangalia nyadhifa alizowahi kuwa nazo. Kwa maana nyingine umejichimbia katika mawazo kuwa Rais lazima atokane na watu waliowahi kuwa na Nyadhifa. Unasahau kuwa viongozi hao waliowahi kuwa na nyadhifa wako most likely kuendeleza system waliyokuwamo na hivyo kuturidhsa kule kule tunakotaka kutoka. Viongozi wengi waliowahi kuwa na mafanikio makubwa kwenye uongozi wao ni wale waliotoka nje ya system. Ingawa watu wanamchukia Kagame, lakini tukubali kuwa pamoja na mapungufu yake binafsi, ameiendeleza sana Rwanda; hakuwa na sifa yoyote ya uongozi kabla ya hapo bali alikuwa ofisa wa jeshi tu. Kuna mifano mingi ya aina hiyo. Ukitaka kumchagua mtu aliyewahi kuwa na wadhifa basi huna haja hata ya kufikiria vyama vya upinzani, bali itakubidi uwe unazunguka CCM tu, kwani ndio wenye nyadhifa serikalini.

Jambo la pili ni kuwa kwa vile hujafuatilia siasa zake, ni afadhali ufanye hivyo kwanza kabla ya kumdiscredit kuhusu ufisadi. Ungekuwa unajua ni nani aliyepingana na mafisadi ndani ya CCM na kuingiza ule msamiati wa "KULE SITE" tena akiwataja mafisadi hao kwa majina waziwazi, nadhani labda usingesema hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Zakumi na Nyani Ngabu.

Nashangaa kuwa hamkuona substance katika hotube yake, lakini kwa uhakika hotuba hiyo ndiyo iliyokuwa na substance sana kuliko wengine wote waliotoa hotuba za nia: Lowassa, Makongoro, Januari, Nchemba, Wassira, Ngereja na Membe

Inawezekana substance ni relative, lakini nimefuatilia hotuba zote za niolwataja hapo juu, wote walikuwa wanatoa ahadi rahisi rahisi za kawaida za kuwa wataleta maisha ya neema - yaani aina ya ahadi za Kikwete za 2005 na 2010. Hakuna aliyeainisha kuwa anajua chanzo halisi cha matatizo ya watanzania jinsi atakavyopambana na chanzo hicho - huwezi kuleta neema bila kuondoa chanzo cha matatizo. Wengine wanachukulia kuwa watakuwa na hela nyingi sana za kujenga mabarabara ya ghorofa nchi nzima au watakuwa na hela za kujenga Academis za kisasa za michezo nchi nzima. Wengine wanachukulia kuwa kuwapo kwao madarakani tu ni tosha kuleta neema bila kufanya lolote.

Makongoro kaaninisha matatizo mawili tu ambayo ndiyo anataka kupambana nayo, na ninakubaliana naye kuwa akipambana na matatizo hayo akayaonyyosha, basi maisha mazuri yatakuja yenyewe. Alisema tatizo la kwanza ni watu kutokufuata taratibu, ambalo ukilipanua zaidi ni lile la viongozi wenyewe na raia kwa jumla kutokufuata sheria za nchi. Alitumia muda kusema kuwa utaratibu uliopo ni kuwa wagombea watakuwa wananadi ilani ya CCM, lakini wagombea wote hao badala ya kufuata utaratibu huo wa kuahdi ilani wao wanakuja na ahadi zao ambazo hazijapitishwa kuwa ilani ya CCM. Hilo limewahusu wagombea wengine wote ispokuwa yeye

Tatizo la pili aliloliongelea ni ubinafsi wa viongozi ambao hupelekea kuwa wezi wa mali ya umma na wala rushwa- yaani viongozi wanakuwa hawafanya kazi kwa ajili ya taifa bali kwa ajili yao na familia zao tu. Ingawa alitumia muda mfupi tu kulizungumzia hilo la pili, alibainisha kuwa kuna tatizo kubwa sana nchini ni pale viongozi wanapoendekeza maslahi yao binasfi na kusahau maslahi ya taifa. Alitumia maneno vibaka, na akatolea mfano wa wale waliotaka kumpindua mwenyekiti wa chama chao.

Kichuguu:

Mambo unayozungumza niliyasikia kwenye hotuba yake. Kilichonishawishi mimi kumuunga mkono ni kuchukua jukwaa la kuwa mpinzani ndani ya chama chake hili chama kirudi kwenye nafasi yake. Wengi ndani ya CCM ni wapinzani kwa nia zao za kibinafsi na sio kwa manufaa ya chama au taifa. Hiki ni kitu alichofanya hakijatokea ndani ya vyama vya siasa.

Kuhusiana na substance. Mimi kama mshabiki wake wa muda, ningependea aingie kwenye offensive mode. Hii ni kwa sababu toka ufe ujamaa, watanzania tumeonyesha uwezo wetu wa kujitegemea wenyewe bila kutegemea sana serikali. Kitu kinachokosekana ni maadili.

Ningependelea aanze offensive kwa kutumia jukwaa la maadili.
 
JokaKuu Point yako kubwa hapa ni kwamba tusichague CCM; which I fully support. Lakini iwapo itatokea CCM ikichaguliwa ni nani kati ya waliotangaza nia ambaye ana nafuu? Tunapokuwa tunaangalia ndani ya CCM, sioni mwingine zaid ya Makongoro na Mwandosya; iwapo tutakubaliana tusichague CCM basi hatuna haja ya kuwaongelea wagombea wake.

Hata kama kuna mtu ana nafuu ndani ya CCM bado atazungukwa na uchafu tu na mwishowe naye atachafuka.

Mimi hata ikitokea CCM ikachaguliwa (ingawa siamini kama uchaguzi ukiwa wa huru na haki wanaweza kuchaguliwa hususan kwenye urais) bado nitawapinga tu.

Hilo lichama ndo limetufikisha hapa tulipo leo. Kuendelea kuliunga mkono kisa tu waliyemchagua hana kashfa za ufisadi na/ au keshawahi kutoa kauli za kukemea ufisadi kwangu hiyo haitoshi kwa sababu ni sawa tu na mazingaombwe.

Inavyoelekea ma grand pooh-bah wa CCM washawasoma vizuri wananchi na kubaini kwamba wanazugika kirahisi mno na mazingaombwe na hivyo safari hii watawaletea mtu ambaye yuko 'palatable' kuliko wengine na watu mtaingia kingi kirahisi sana.

Na mwishowe mifisadi papa na nyangumi haitafanywa lolote, sana sana itabadili tu mbinu za kifisadi na ufisadi utaendelea kushamiri huku maendeleo yakizi kudumaa.

Mimi kamwe sitaipigia kura CCM hata kama kwenye upande wa upinzani hakueleweki. Ni heri hata nisipige kura kabisa kuliko kuipigia kura CCM.
 
Asante sana Zakumi kwa andiko lako..

Ingawaje nafahamu kuwa katika uchaguzi wa mwaka huu ni lazima Rais atoke Ukawa au CCM. Ila ninapata tatizo, kwa wale wote ambao wameisha tangaza nia,sijaona wa kunishawishi kuwa anagombe urais kwa kusukumwa na matatizo ya nchi yetu.

Kuhusu Makongoro sijaona kama anakitu cha kunifanya mimi nimpe kura yangu. kwanini ninasema hivi..

Kwa sababu mgombea urais ni lazima tumpima kwa mafanikio yake katika yadhifa mbali mbali alizowahi/alizonazo.

Tumpime kwa jinsi alivyopiga vita ufisadi na rushwa kwa nguvu zake zote,

Tumpime kwa kusaidia jamii iliyomzunguka katika swala zima la kujiletea maendeleo,
Tuangalie matarajio yake ndani ya miaka 5 au 10 anataka kuona Tanzania ya aina gani ndani ya hiyo miaka, na atafanya nini kuhakikisha Tanznia ya aina hiyo inapatikana.

Hivyo basi nikimangalia Makongoro naona anapwaya tena sana, labda inawezekana simfahamu vizuri au sifatilii siasa zake. Ndo maana sijaona kitu chochote ambacho anaweza kusimama kifua mbele na kusema nimefanya hiki au kile zaidi ya ile vita ya Kagera.

Na hapa ningependa wanaomfahamu vizuri watupe record zake hasa baada ya vita ya Kagera maana hatuwezi kuchagua rais kwa vile tu alipiga vita ya Kagera, tunahitaji zaidi ya hapo.

Record nilizona ni kuwa aliwahi kuwa Mbuge wa Arusha lakini alivuliwa Ubunge sijui kwa kosa lipi???
Na kwa sasa ni Mbunge wa East Afrika lakini sina kumbumbuku yeyote kama kule kuna kitu alichotetea.. Nitaomba watu wanaofahamu zaidi watujuze ni kwa jinsi gani anamekuwa mtetezi wa nchi yetu wawapo bungeni. Ni ni mafaniko yapi Tanzania imeyapata kupitia kwa Makongoro katika hilo bunge.

Mpaka sasa naona kama Makongoro anabebwa zaidi na jina la Baba yake, hana dhamira ya kweli ya kumkomboa mtanzania, Na hata katika kutangania nia alionyesha kuwa ni mtu ambaye hakuwa "seriuos" maana hata alishindwa kutaja ni sababu gani iliyomsukuma kutaka urais. Sana sana alisema yeye anasubiri ilani ya chama (ni vizuri kusubiri ilani ya chama) lakini hata hivyo wewe kama mgombea urais lazima huwe na kitu ambacho unatamani kukirekebisha au kukiboresha, ni lazima uwe ni malengo ya kutoa watu wako hapa na kuwapeleka pale kwa bahati mbaya Makongoro hakuonyesha dhamira ya kweli sana sana aliadithia jinsi alivyojiunga na NCCR miaka 20 iliyopita...


Na nafikri hata hakuwa na nia ya kugombea lakni baada ya CCM kuona kila mtu ana "skendo" ndo wakamtafuta Makongoro ili aokoe janga.


Alinda:

NCCR ilipata viti vingi vya ubunge mikoa ya kanda ya Kaskazini katika uchaguzi wa 1995. Mbinu kubwa CCM iliyochukua baada ya kushinda urais ni kutumia mahakama kuvua viti vya ubunge. Katika uchaguzi wowote kuna issue za technical irregularities. Sidhani technical irregularities hizo zilikuwa kubwa kiasi cha kuathiri matokeo ya kiti chake cha ubunge. Na sidhani kama yeye binafsi alihusika katika issues hizo

Kuhusiana na sifa na nafasi za kazi walizowahi kushika wanaowania urais, wengi wamekuwepo madarakani kwa muda mrefu lakini hawachafanya kitu chochote cha maana. Na kibaya zaidi hawaonyeshi kuwa wana nia ya kujirekebisha. Ni kitu gani kikubwa amekifanya Lowassa toka 2007? Ni kutu gani kikubwa amekifanya Mwigulu, Dr. Slaa au Mbowe?
 
Alinda

Unafanya makosa kudai kuwa utamachagua Rais kwa kuangalia nyadhifa alizowahi kuwa nazo. Kwa maana nyingine umejichimbia katika mawazo kuwa Rais lazima atokane na watu waliowahi kuwa na Nyadhifa. Unasahau kuwa viongozi hao waliowahi kuwa na nyadhifa wako most likely kuendeleza system waliyokuwamo na hivyo kuturidhsa kule kule tunakotaka kutoka. Viongozi wengi waliowahi kuwa na mafanikio makubwa kwenye uongozi wao ni wale waliotoka nje ya system. Ingawa watu wanamchukia Kagame, lakini tukubali kuwa pamoja na mapungufu yake binafsi, ameiendeleza sana Rwanda; hakuwa na sifa yoyote ya uongozi kabla ya hapo bali alikuwa ofisa wa jeshi tu. Kuna mifano mingi ya aina hiyo. Ukitaka kumchagua mtu aliyewahi kuwa na wadhifa basi huna haja hata ya kufikiria vyama vya upinzani, bali itakubidi uwe unazunguka CCM tu, kwani ndio wenye nyadhifa serikalini.

Jambo la pili ni kuwa kwa vile hujafuatilia siasa zake, ni afadhali ufanye hivyo kwanza kabla ya kumdiscredit kuhusu ufisadi. Ungekuwa unajua ni nani aliyepingana na mafisadi ndani ya CCM na kuingiza ule msamiati wa "KULE SITE" tena akiwataja mafisadi hao kwa majina waziwazi, nadhani labda usingesema hivyo.

Kichuguu:

Mfumo mzima wa kupata majina ya wagombea nafasi kupitia CCM umejaa rushwa. Hivyo kuna watu wengi sana hawajajenga majina yao au kuwa na nafasi kubwa ndani ya chama sio kwa sababu wanakosa uzoefu, bali hawapati nafasi kutokana na ukosefu wa pesa au kuwa na nidhamu.

Kama mfumo ungekuwa fair, nadhani Makongoro na wengine wengi wangekuwa mbali.
 
Zakumi, mimi ninalo swali moja tu kwako; unamtenganisha vipi Makongoro na wanachama pamoja na viongozi wengine ndani ya CCM? Kabla hujanijibu ningependa nikukumbushe tukio ambalo limepelekea watu wengi kupoteza kabisa imani na CCM nao ni uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995. Wengi waliaminishwa kwamba safari hiyo, baada ya Mzee Rukhsa, CCM inatuletea ideal candidate, mtu msafi asiye na tone la kashfa, William Benjamin Mkapa, Mr. Clean! Kwa miaka kumi tuliushuhudia na kuuvumilia huo usafi wake ikiwa ni pamoja na kufanya biashara akiwa Ikulu.

Mwaka 2005, CCM ilituletea waliyedai ni kijana anayejua matatizo ya Watanzania na hivyo kupewa ridhaa ya uongozi wa taifa hili kwa asilimia 80%! Huyo kijana aliyeingia kimachachari kwa ari na nguvu mpya katumia zaidi ya robo ya muda wake kutalii kwa kisingizio cha kuomba hadi kuchokwa ndani na nje ya nchi yetu. Kwa ufanisi mkubwa ameweza kuligawa taifa hili kikanda, kikabila na kidini na hata pale alipooneshwa kushindwa, CCM ilihakikisha anapata awamu ya pili.

Sasa unapendekeza aingie Makongoro Nyerere kwa laghai zile zile kwamba ataleta kipya na kufanikisha mabadiliko; ndio maana nimeuliza hapo mwanzo, unamtenganisha vipi na wanachama wenziye anaoshindana nao, kula nao na kuafikiana nao?


Mag3:

In 1995 I was a die hard Mrema follower. Nilikuwa najua mapungufu ya Mrema lakini nilitaka ashinde hili ndani ya CCM waweze kujipanga na kujisafisha. Hicho hakikutokea na watu wakarudi kuikumbatia CCM na kutuletea Kikwete.

Toka ashindwa Mrema niliachana na siasa moja kwa moja na hii ni mara ya kwanza kusupport mgombea wa nafasi ya kisiasa.

Kujibu swali lako, naunga mkono juhudi za Makongoro kwa sababu naona ni mmoja wa wanaCCM wanaoweza kuleta mabadiliko ya kweli iwapo watapewa nafasi. Kama CCM itashindwa, basi abakie ndani ya chama kuleta mabadiliko hayo.

Pamoja na kuwa hatuipendi CCM, ni lazima tukubali kuwa wanayo nafasi kubwa ya kushinda. Je wakishinda tuendelee na maumivu kwa miaka 5 au 10 ijayo?
 
Mag3:

In 1995 I was a die hard Mrema follower. Nilikuwa najua mapungufu ya Mrema lakini nilitaka ashinde hili ndani ya CCM waweze kujipanga na kujisafisha. Hicho hakikutokea na watu wakarudi kuikumbatia CCM na kutuletea Kikwete.

Toka ashindwa Mrema niliachana na siasa moja kwa moja na hii ni mara ya kwanza kusupport mgombea wa nafasi ya kisiasa.

Kujibu swali lako, naunga mkono juhudi za Makongoro kwa sababu naona ni mmoja wa wanaCCM wanaoweza kuleta mabadiliko ya kweli iwapo watapewa nafasi. Kama CCM itashindwa, basi abakie ndani ya chama kuleta mabadiliko hayo.

Pamoja na kuwa hatuipendi CCM, ni lazima tukubali kuwa wanayo nafasi kubwa ya kushinda. Je wakishinda tuendelee na maumivu kwa miaka 5 au 10 ijayo?

Hapa yaani wewe ni kama mimi. Nakumbuka nilivyokwenda kuhudhuria mkutano wa Mrema pale shule ya Uhuru muda mfupi kabla ya uchaguzi Dar nzima ikawa imesimama kwa ajili ya Mrema.

Mwaka 2010 nilifunga safari za dharura za kwenda kujiandikisha kama mpiga kura, safari zilizonigharimu zaidi ya $8000, lakini bado CCM ikabaki madarakani!!!.
 
Zakumi msome Mag3 hapo juu.

Ninachotaka kuongezea ni hiki, Mako alikuwa mwenyekiti wa Mkoa wa CCM. Na sasa ni mbungewa
EA.


Mako anakuja na ukali kuhusu rushwa. Anasema Rais ni mtu anayechukia rushwa, kwa bahati mbaya amezungukwa na wala rushwa. Kauli hii tu inaonyeshaMakongoro ni mwoga na hawezi kukabiliana na kundi lililonunua CCM

Rais anaposhindwa kukabiliana na wala rushwa, au anapochagua kundi la wala rushwa kumzunguka, tatizo si wala rushwa.
Kazi ya wala
rushwa ni kula rushwa.

Tuliyempa kila zana na rasilimali za nch
kupambana na rushwa ni Rais.


Mako angesema Rais ameshindwa kukabiliana na rushwa kama ilivyokuwa kwa Mkapa

Kauli yake haionyeshi utayari wa kukabiliana na rushwa, bali woga wa jina kutemwa! Anatufaa kweli?

Lakini pia tuonyeshe, ni lini na wapi Makongoro akiwa Mwanachama au Mwenyekiti aliwahi kusimama na kukemea, kukabiliana au kuzomea rushwa inayofanywa na kundi alilomo?

Kuhusu, nani wa mwenye afadhali, ni ukweli ndani ya CCM hakuna.

Hata mseto ukitokea litakachotokea ni ‘pick the best from the garbage’kama si hivyo, unatushawishi ‘choose the lesser evil’

Nguruvi3:

Mimi sio CCM. Lakini nakiombea chama hicho kipate kiongozi mzuri na mwenye maadili. Hivyo kwa mtaji huu siwezi kumshutumu Makongoro kwa kutosema maneno yake miaka mitano iliyopita.

CCM ni kama mgonjwa anayekataa kwenda hospital kupata matibabu kwa muda mrefu. Mtu yoyote atayejitolea kumtibu mgonjwa huyu, asilaumiwe kwanini hakujitokeza miaka 10 iliyopita.
 
Back
Top Bottom