Kuunga Mkono Nia ya Makongoro Nyerere (Urais 2015)

Kuunga Mkono Nia ya Makongoro Nyerere (Urais 2015)

Hata kama kuna mtu ana nafuu ndani ya CCM bado atazungukwa na uchafu tu na mwishowe naye atachafuka.

Mimi hata ikitokea CCM ikachaguliwa (ingawa siamini kama uchaguzi ukiwa wa huru na haki wanaweza kuchaguliwa hususan kwenye urais) bado nitawapinga tu.

Hilo lichama ndo limetufikisha hapa tulipo leo. Kuendelea kuliunga mkono kisa tu waliyemchagua hana kashfa za ufisadi na/ au keshawahi kutoa kauli za kukemea ufisadi kwangu hiyo haitoshi kwa sababu ni sawa tu na mazingaombwe.

Inavyoelekea ma grand pooh-bah wa CCM washawasoma vizuri wananchi na kubaini kwamba wanazugika kirahisi mno na mazingaombwe na hivyo safari hii watawaletea mtu ambaye yuko 'palatable' kuliko wengine na watu mtaingia kingi kirahisi sana.

Na mwishowe mifisadi papa na nyangumi haitafanywa lolote, sana sana itabadili tu mbinu za kifisadi na ufisadi utaendelea kushamiri huku maendeleo yakizi kudumaa.

Mimi kamwe sitaipigia kura CCM hata kama kwenye upande wa upinzani hakueleweki. Ni heri hata nisipige kura kabisa kuliko kuipigia kura CCM.


Ngabu:

Ingawa hawana nia ya kujenga nchi, CCM ina watu wenye uvumilivu wa kisiasa. Ndani ya CCM kuna watu wanakubali kukaa kimya au kubeba lawama kwa ajili ya chama. Hii sifa ndio inayotofautisha CCM na vyama vingine vya kisiasa nchini Tanzania. Watu wanaharibu mambo na wakipata kashfa wanakaa kimya kwa muda fulani na baadaye kurudi tena.

Changamoto kwa Makongoro kama hatapata nafasi ni kukikisha kuwa hawafufuki kisiasa.
 
Alinda

Unafanya makosa kudai kuwa utamachagua Rais kwa kuangalia nyadhifa alizowahi kuwa nazo. Kwa maana nyingine umejichimbia katika mawazo kuwa Rais lazima atokane na watu waliowahi kuwa na Nyadhifa. Unasahau kuwa viongozi hao waliowahi kuwa na nyadhifa wako most likely kuendeleza system waliyokuwamo na hivyo kuturidhsa kule kule tunakotaka kutoka. Viongozi wengi waliowahi kuwa na mafanikio makubwa kwenye uongozi wao ni wale waliotoka nje ya system. Ingawa watu wanamchukia Kagame, lakini tukubali kuwa pamoja na mapungufu yake binafsi, ameiendeleza sana Rwanda; hakuwa na sifa yoyote ya uongozi kabla ya hapo bali alikuwa ofisa wa jeshi tu. Kuna mifano mingi ya aina hiyo. Ukitaka kumchagua mtu aliyewahi kuwa na wadhifa basi huna haja hata ya kufikiria vyama vya upinzani, bali itakubidi uwe unazunguka CCM tu, kwani ndio wenye nyadhifa serikalini.

Mkuu Kichuguu nipozungumzia nyadhifa si maanishi utumishi wa serikali tu bali nimaanisha katika swala zima la utumishi wake katika sehemu yeyote ile. Yaani hapa mimi nitampima mgombea urais kwa kuagalia ni nini amefanya, wapi, lini, na nini mafanikio yake. Hata Kagame unayemsema hakuwa "jobless" bali alikuwa ni mwajiriwa na bila shaka kwa kuona mafanikio ndo maana walimshawishi/walimchugua kuwa rais wao. Hivyo basi simaanish mtu wa system maana nafahamu kuwa system yetu kwa asilimia 99 imeoza.

Na hapo ndipo ninapopata kigugumizi kumwamini mwanaccm yeyote yule kuwa anaweza kuisaidia Tanzania kupiga hatua kwenda mbele. Haiwezekeni uzungukwe na watu ambao ni wala rushwa na wewe husiwe mla rushwa, au kwa namna moja au nyingine husifaidike na hizi pesa za rushwa.

Swali je Makongoro anaweza kusafisha uchafu wa Meremeta hali wahusika ndo watu anaowategemea wapande majukwaani wamuombe kura? Je vp kuhusu Richmond? na je Radar? vp kuhusu nyumba za serikali? je swala la Escrow? kwa hiyo ukiangalia haya madudu yote hakuna mwanaccm yeyote ambaye anaweza kusafisha uozo huu maana wahusika ni viongozi ambao anawategemea wafaye kazi pamoja.

Hebu niambie ni kitu gani Makongoro atafanya kusafisha huo uozo?

Kuna mtu amesema kuwa nyuma ya Makongoro kuna Mkono, Kwa hili tu usafi wa Makongoro huko wapi kama anashirikiana na mafisadi? kuna tofauti gani kati ya Mkono na Lowassa katika swala zima la ufisadi? Kuna mtu kapiga pesa za Tanesco kama Mkono? kuna mtu katoa ushauri mbovu kwa Tanesco kama Mkono?

Hivyo basi nafikiri tukubaliane kuwa inawezekana kabisa kuwa Makongoro ni msafi lakini yeye pekee yake hawezi kuondoa rushwa maana rushwa ya Tanzania imefika mbali hiko ndani ya system. Ninaweza kusema karibia viongozi wote wa CCM ni wala rushwa.

Jambo la pili ni kuwa kwa vile hujafuatilia siasa zake, ni afadhali ufanye hivyo kwanza kabla ya kumdiscredit kuhusu ufisadi. Ungekuwa unajua ni nani aliyepingana na mafisadi ndani ya CCM na kuingiza ule msamiati wa "KULE SITE" tena akiwataja mafisadi hao kwa majina waziwazi, nadhani labda usingesema hivyo.[/QUOTE]

Ni kweli sijafatilia siasa zake maana sijui nizifatilie wapi.. Na ndo maana nikawaomba watu kama nyie mtupe ndoo ndoo walau hata mie niweza kumfahamu maana mpaka sasa ninchofahamu ni kuwa alipigana vita ya Kagera baada ya hapo akapotea kaja kuibuka mwaka 1995, kawa mbuge wa NCCR, baada ya kuvuliwa ubunge na mahakama, akapotea tena kaibuka kwenye 2008??2010? (sina uhakika) na ile kauli ya "kule Site" baada ya hapo kapotea kaibuka tena katika kuwaia ubunge wa EA. kwangu mimi kwa hii storia yake bado anapwaya sana katika swala zima la uongozi. Sijaona lini wapi na kafanya nini.Sijawahi sikia kaitisha mkutano wowote na wanakijiji kuongelea matatizo yanayowakabili na jinsi ya kuyatatua, au sijui ni wapi anafanya shughuli zake, na ni vipi anaguswa na umasikini wa watanzania na vitu vya namna hiyo.

Swala la kuongelea rushwa ya Lowassa si jambo la ajabu kwani hata Nape alizunguka Tanzania nzima na wimbo wake wa mafisadi. Lakni swali la kujiuliza ndani ya CCM mla rushwa ni Lowassa peke yake? Je swala la Katibu mkuu wake na "Meli" yake aliliongeleaje? Vipi kuhusu Radar, Richmond, Escrow, Meremeta?
 
Alinda:

NCCR ilipata viti vingi vya ubunge mikoa ya kanda ya Kaskazini katika uchaguzi wa 1995. Mbinu kubwa CCM iliyochukua baada ya kushinda urais ni kutumia mahakama kuvua viti vya ubunge. Katika uchaguzi wowote kuna issue za technical irregularities. Sidhani technical irregularities hizo zilikuwa kubwa kiasi cha kuathiri matokeo ya kiti chake cha ubunge. Na sidhani kama yeye binafsi alihusika katika issues hizo

Kuhusiana na sifa na nafasi za kazi walizowahi kushika wanaowania urais, wengi wamekuwepo madarakani kwa muda mrefu lakini hawachafanya kitu chochote cha maana. Na kibaya zaidi hawaonyeshi kuwa wana nia ya kujirekebisha. Ni kitu gani kikubwa amekifanya Lowassa toka 2007? Ni kutu gani kikubwa amekifanya Mwigulu, Dr. Slaa au Mbowe?


Na ndo maana nikasema tusichangue mtu kwa pesa zake, au kwa uzuri wake, bali tumwangalie kwa utendaji wake. Kwangu mimi si Lowassa, Mwigulu au mwanaccm yeyote ambaye anafaaa kuwa rais wangu maana sijaona walichokifnaya. Kama mtu amekaa madarakani zaidi ya 5 na tunaangalia alichokifanya kwa kutupia "loupe" basi huyu hatufai.

Ukija kwa Dr. Slaa nafikiri tutakuwa hatutendi haki kama tusipo"appreciate" kwa alichokifanya Dr. Slaa katika siasa za nchi hii. Si vitu vya kuadithiwa bali tumeshuhudia kwa macho yetu jinsi huyu mzee alivyokuwa anapigania walalahoi miaka yote 15 aliyokaa bungeni, ni Mwenyekiti wa bodi ya walemavu CCBRT sifa za hii hospital na jinsi inavyofanya kazi nafikiri kila mtanzania ni shaidi, ni Katibu wa Chadema, tumeshuhudia wenyewe walipoitoa Chadema na ilipo sasa ni jitihada za Dr. Slaa, tumeshuhudia wenyewe alivyokuwa anafanya kazi usiku na mchana, jua ni lake, mvua ni yake, kazunguka vijijini kuliko viongozi wote walioko madarakani kwa sasa, anafahamu matatizo ya watanzania si kwa kuwambiwa bali kwa kuona yeye mwenyewe,kapopolewa mawe akijenga chama, hakuna tusi ambalo hajawahi kutukanwa kwa ajili ya chama, na leo tunashuhudia Chadema imeimalika zaidi pamoja na mapambano makali ya vyombo vya dola. Tunashuhudia wananchi hasa wa vijijini wanavyoanza kudai haki zao. Elimu ya kudai haki zao hawakuipata kutoka kwa viongozi wa CCM bali kwa viongozi wa upanzani ambao Dr. Slaa ni miongoni mwao. Na viongozi wa jinsi hii ndio chaguo langu.
 
Inafurahisha kuona bado kuna watu wanaoamini kwamba CCM itakuja kubadilika kuwa chama kisafi, Kwamba siku moja atatokea masihi wa kukibadilisha chama hiki kurudi kwenye misingi yake ya awali kilipoasisiwa. Hili haliwezi kutokea kamwe as long as CCM ipo madarakani, NEVER! Hakuna kiongozi msafi yeyote anayeweza ku-survive kwenye mfumo wa kifisadi ukiokomaa ndani ya CCM...unless afanye kama alivyofanya Mutharika wa Malawi ambaye baada ya kuingia ikulu akaamua kuachana na chama kilichomweka pale akaanzisha cha kwake! Otherwise namna pekee CCM inaweza kubadilika ikiwa ni chama cha upinzani!
 
I refuse to be hoodwinked into supporting CCM just because some of their candidates seems to be clean....
 
Alinda i support you

Hawa wote wameshakuwa viongozi somewhere

Huyu Makongoro amekuwa mwenyekiti wa CCM Mara.....Rushwa ni tatizo kwa CCM nzima...hata hapo mkoani kwake mara...Amefanya nini?

Lakini pia Mkoani mara,haswa Musoma....Ndani ya miaka 5 imeshuhudiwa kukua kwa uungwaji mkono wa CHADEMA kuliko kipindi chochote kile...Kama Makongoro ni kiongozi mzuri hivyo tusingeshuhudia kukataliwa kwa CCM kiasi hichi...hasa makao makuu ya mkoa wake.

Rushwa ni tatizo la kimfumo ambalo kupambana nalo hauihitaji CCM tena.....Ili kuweza kupona ni sawa na kusema CCM ife ndio tupate mtu safi "aliyewahi kuwa CCM" kwa maana rahisi iwe kama kifo cha kinyonga anapokuwa anazaa.

Kwa kifupi...Makongoro sio na hajaonesha kama ni mtu sahihi wa kuubadili mfumo........Anatakiwa kwanza atuoneshe kwa muda wote huo hadi anafikia uzee wake sasa...amepambana vipi kuuondoa mfumo huu wa CCM
 
Last edited by a moderator:
Ngabu:

Ingawa hawana nia ya kujenga nchi, CCM ina watu wenye uvumilivu wa kisiasa. Ndani ya CCM kuna watu wanakubali kukaa kimya au kubeba lawama kwa ajili ya chama. Hii sifa ndio inayotofautisha CCM na vyama vingine vya kisiasa nchini Tanzania. Watu wanaharibu mambo na wakipata kashfa wanakaa kimya kwa muda fulani na baadaye kurudi tena.

Changamoto kwa Makongoro kama hatapata nafasi ni kukikisha kuwa hawafufuki kisiasa.

Lakini mkuu Zakumi hicho unachojaribu kukitafsiri kama Uvumilivu wa kisiasa sicho.

Katika ahadi ya Nne ya Mwanachama wa CCM wanasema hivi

4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa

5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.

http://ccmuk.org/files/Katibaccm.pdf

Maana yake ni kwamba chama makini ambacho kinafuata katiba yake kinatakiwa kuchukua hatua pale mwanachama anaposhindwa kutimiza ahadi hizi....

CCM imekuwa bubu kuwashughulikia wanachama wake kadri ya katiba ya chama chao.

Unadhani ni kwa nini?

Unachukulia huo kama uvumilivu wa kisiasa?
 
Last edited by a moderator:
Na ndo maana nikasema tusichangue mtu kwa pesa zake, au kwa uzuri wake, bali tumwangalie kwa utendaji wake. Kwangu mimi si Lowassa, Mwigulu au mwanaccm yeyote ambaye anafaaa kuwa rais wangu maana sijaona walichokifnaya. Kama mtu amekaa madarakani zaidi ya 5 na tunaangalia alichokifanya kwa kutupia "loupe" basi huyu hatufai.

Ukija kwa Dr. Slaa nafikiri tutakuwa hatutendi haki kama tusipo"appreciate" kwa alichokifanya Dr. Slaa katika siasa za nchi hii. Si vitu vya kuadithiwa bali tumeshuhudia kwa macho yetu jinsi huyu mzee alivyokuwa anapigania walalahoi miaka yote 15 aliyokaa bungeni, ni Mwenyekiti wa bodi ya walemavu CCBRT sifa za hii hospital na jinsi inavyofanya kazi nafikiri kila mtanzania ni shaidi, ni Katibu wa Chadema, tumeshuhudia wenyewe walipoitoa Chadema na ilipo sasa ni jitihada za Dr. Slaa, tumeshuhudia wenyewe alivyokuwa anafanya kazi usiku na mchana, jua ni lake, mvua ni yake, kazunguka vijijini kuliko viongozi wote walioko madarakani kwa sasa, anafahamu matatizo ya watanzania si kwa kuwambiwa bali kwa kuona yeye mwenyewe,kapopolewa mawe akijenga chama, hakuna tusi ambalo hajawahi kutukanwa kwa ajili ya chama, na leo tunashuhudia Chadema imeimalika zaidi pamoja na mapambano makali ya vyombo vya dola. Tunashuhudia wananchi hasa wa vijijini wanavyoanza kudai haki zao. Elimu ya kudai haki zao hawakuipata kutoka kwa viongozi wa CCM bali kwa viongozi wa upanzani ambao Dr. Slaa ni miongoni mwao. Na viongozi wa jinsi hii ndio chaguo langu.

Alinda:

Nadhani tutakuwa hatujitendei haki iwapo hatutataka CCM ibadilike. CCM ni taasisi iliyojengwa kwa jasho la watanzania wote. Hivyo iwapo kutatokea mtu ambaye atataka kuibadilisha CCM, ni lazima tumuunge mkono au kumtakia mafanikio mema katika safari yake.

Vilevile safu za wapinzani zinaweza kujisahau kama ilivyojisahau CCM pale zitakapochukua madaraka. Hivyo ni nani atakeyekuwa katika upinzani kukemea watawala wapya?
 
Inafurahisha kuona bado kuna watu wanaoamini kwamba CCM itakuja kubadilika kuwa chama kisafi, Kwamba siku moja atatokea masihi wa kukibadilisha chama hiki kurudi kwenye misingi yake ya awali kilipoasisiwa. Hili haliwezi kutokea kamwe as long as CCM ipo madarakani, NEVER! Hakuna kiongozi msafi yeyote anayeweza ku-survive kwenye mfumo wa kifisadi ukiokomaa ndani ya CCM...unless afanye kama alivyofanya Mutharika wa Malawi ambaye baada ya kuingia ikulu akaamua kuachana na chama kilichomweka pale akaanzisha cha kwake! Otherwise namna pekee CCM inaweza kubadilika ikiwa ni chama cha upinzani!

Kuna ukweli kuwa CCM haitabadilika ikiwa kwenye madaraka. Lakini chama hiki kibadilike kikiwa katika upinzani ni lazima watu ndani ya chama waanze kukikosoa. Hakuna mgogoro unaosaidia kuleta mafanikio unaozuka bila ya watu kupania.

Hata Dr. Slaa naye alianza kwa kupania ubunge. Hivyo mtu yoyote anayoonyesha nia ya kufanya mabadiliko ndani ya taasisi yoyote hile tusimkatishe tamaa.
 
Lakini mkuu Zakumi hicho unachojaribu kukitafsiri kama Uvumilivu wa kisiasa sicho.

Katika ahadi ya Nne ya Mwanachama wa CCM wanasema hivi

4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa

5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.

http://ccmuk.org/files/Katibaccm.pdf

Maana yake ni kwamba chama makini ambacho kinafuata katiba yake kinatakiwa kuchukua hatua pale mwanachama anaposhindwa kutimiza ahadi hizi....

CCM imekuwa bubu kuwashughulikia wanachama wake kadri ya katiba ya chama chao.

Unadhani ni kwa nini?

Unachukulia huo kama uvumilivu wa kisiasa?


Freeland:

Tusichukue mafundisho ya siasa kama imani za dini au scientific postulation. Ni lazima tuwe na ujasiri wa kuuliza na kusema kitu ambacho Makongoro ameonyesha.
 
Kuna ukweli kuwa CCM haitabadilika ikiwa kwenye madaraka. Lakini chama hiki kibadilike kikiwa katika upinzani ni lazima watu ndani ya chama waanze kukikosoa. Hakuna mgogoro unaosaidia kuleta mafanikio unaozuka bila ya watu kupania.

Hata Dr. Slaa naye alianza kwa kupania ubunge. Hivyo mtu yoyote anayoonyesha nia ya kufanya mabadiliko ndani ya taasisi yoyote hile tusimkatishe tamaa.

Ni mpaka pale CCM itakapotupwa nje ndipo walio ndani wataweza kuwa na guts za kuambiana ukweli na ikibidi kutimuana kabisa! Kwa hivi sasa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuwapindua "wenye chama/wenye pesa" ambao nio chimbuko la ufisadi na ulevi unaoendelea sasa. Hata ikitokea kuna mwana CCM msafi akapitishwa kugombea lakini mwisho wa siku bado amezungukwa na wezi na mafisadi wale wale na ndio watampigia kampeni kwa pesa za wizi na unga...sasa hapo unategemea nini kitafuata? Unafikiri atakuja kuwageuka wafadhili wake waliomweka pale? Ndio maana Alber Einstein alitamka haya "Insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results."
 
Tunaingiza sana hisia kwenye mambo muhimu ya nchi ambayo hayahitaji hisia bali maamuzi mujarabu ili tufike kule tuendapo.

Nashangaa inapotolewa dai kuwa Makongoro anaweza kukemea rushwa. Seriously? Ndani ya chama kinachonuka rushwa kwa kila jambo? Sidhani.

Huyo Makongoro ni sehemu ya system iliyoharibika hawezi leta chochote au kubadili chochote kwa masilahi mapana ya watanzania. Na ninasema tunaongozwa na hisia za "kijinga" kudhani dhani tu.

Maendeleo katika nchi hii yataletwa na weledi wa mawazo mapya. Na mawazo hayo mapya yatakoka kwa watu wapya. Hebu sasa watanzania tuseme imetosha kwa hili dudu liitwalo CCM hata kama wakimsimamisha nani.
 
Alinda:

Nadhani tutakuwa hatujitendei haki iwapo hatutataka CCM ibadilike. CCM ni taasisi iliyojengwa kwa jasho la watanzania wote. Hivyo iwapo kutatokea mtu ambaye atataka kuibadilisha CCM, ni lazima tumuunge mkono au kumtakia mafanikio mema katika safari yake.

Vilevile safu za wapinzani zinaweza kujisahau kama ilivyojisahau CCM pale zitakapochukua madaraka. Hivyo ni nani atakeyekuwa katika upinzani kukemea watawala wapya?

Swala la CCM kubadilika au kutobadilika liko mikononi mwa viongozi wa CCM na wanaccm wenyewe. Kazi yangu mimi na wewe ni kuhakikisha ili dudu linatoka madarakani. Kama kujirekebisha likajirekebishe likiwa nje ya madaraka.. Wakavuane magamba huku huku..

Nakuhakikishia ndani ya CCM si Makongoro au sijui nani anaweza kusafisha rushwa maana rushwa imeanzia juu kwa Mwenyekiti wao.. (rejea Richmond na Lowassa) ikatelemka kwa Katibu wao (rejea Meli na nyara za serikali) na ikasambaa kwa viongozi mbali mbali. Sasa huyu Makongoro atakuwa na "guts" gani kushughulikia wala rushwa?? Hili ndilo swali langu na ningependa wewe pamoja na Kichuguu mnipe ufafanuzi jinsi Makongoro atavyosafisha nyumba!

Ila tunachokiona ni nguvu nyingi kutumika kutuaminisha kuwa ndani ya CCM mla rushwa ni Lowassa tu!! hivi kweli ni Lowassa peke yake?
 
Swala la CCM kubadilika au kutobadilika liko mikononi mwa viongozi wa CCM na wanaccm wenyewe. Kazi yangu mimi na wewe ni kuhakikisha ili dudu linatoka madarakani. Kama kujirekebisha likajirekebishe likiwa nje ya madaraka.. Wakavuane magamba huku huku..

Nakuhakikishia ndani ya CCM si Makongoro au sijui nani anaweza kusafisha rushwa maana rushwa imeanzia juu kwa Mwenyekiti wao.. (rejea Richmond na Lowassa) ikatelemka kwa Katibu wao (rejea Meli na nyara za serikali) na ikasambaa kwa viongozi mbali mbali. Sasa huyu Makongoro atakuwa na "guts" gani kushughulikia wala rushwa?? Hili ndilo swali langu na ningependa wewe pamoja na Kichuguu mnipe ufafanuzi jinsi Makongoro atavyosafisha nyumba!

Ila tunachokiona ni nguvu nyingi kutumika kutuaminisha kuwa ndani ya CCM mla rushwa ni Lowassa tu!! hivi kweli ni Lowassa peke yake?
Alinda, mimi ninakubaliana nawe kabisa kuwa CCM ni janga linalotakiwa kutokomezwa lisiwe madarakani tena. Tatzi ni kuwa kwa miaka ishirini sasa tumeshindwa kulitokomeza hata pale ambapo hali ilikuwa ni wazi kabisa kuwa CCM imechoka bado walio wengi (japo kama ni kwa sababu ya Khanga Kofia na Ubwabwa) bado waliichagua.

Sasa basi iwapo bado watu hao wakiichagua CCM, itaendelea kututawala. Ninadhani kuwa mjadala uliopo hapa siyo kuwa tumchague Makongoro, la hasa kwa vile bado hatujaona mgombea wa Ukawa. Tunachosema ni kuwa hao walioko CCM ni nani anafaa. Kumbuka kuwa CCM ina kaukiritimba fulani kuwa mwenyekiti ana nguvu sana, na kwa vile mfumo wao ni kuwa mgombea wao ndiye vile vile atakuwa mwenyekiti, basi Makongoro akishakuwa mgombea ndiye vile vile atakayekuwa mwenyekiti, hivyo atakuwa na power zaidi ya vigogo aliowakuta. Ni kama ambavyo Kikwete alivyoishia kuwa na power kuliko Malecela.
 
Alinda, mimi ninakubaliana nawe kabisa kuwa CCM ni janga linalotakiwa kutokomezwa lisiwe madarakani tena. Tatzi ni kuwa kwa miaka ishirini sasa tumeshindwa kulitokomeza hata pale ambapo hali ilikuwa ni wazi kabisa kuwa CCM imechoka bado walio wengi (japo kama ni kwa sababu ya Khanga Kofia na Ubwabwa) bado waliichagua.

Sasa basi iwapo bado watu hao wakiichagua CCM, itaendelea kututawala. Ninadhani kuwa mjadala uliopo hapa siyo kuwa tumchague Makongoro, la hasa kwa vile bado hatujaona mgombea wa Ukawa. Tunachosema ni kuwa hao walioko CCM ni nani anafaa. Kumbuka kuwa CCM ina kaukiritimba fulani kuwa mwenyekiti ana nguvu sana, na kwa vile mfumo wao ni kuwa mgombea wao ndiye vile vile atakuwa mwenyekiti, basi Makongoro akishakuwa mgombea ndiye vile vile atakayekuwa mwenyekiti, hivyo atakuwa na power zaidi ya vigogo aliowakuta. Ni kama ambavyo Kikwete alivyoishia kuwa na power kuliko Malecela.
Shida ya CCM sio nani anafaa au hafai, chama chote kimeoza kimfumo kwa rushwa, ufisadi etc. Hakuna msafi anayeweza kuingia pale akabaki msafi! Mwinyi, Mkapa na Kikwete wote waliingia pale wakiwa hawana image mbaya wala kashfa za ufisadi lakini angalia wameondoka kama walivyoingia? Wote wameondoka wakiwa na uvundo wa rushwa, wizi na ufisadi tena kiwango kikiongezeka kwa kila mmoja wao... Mwinyi alianza kidogo kidogo na "RUKSA", Mkapa akapanda viwango kwa kupiga dili akiwa ndani ya ikulu, na sasa Kikwete anafunga kazi kwa msururu wa kashfa! Ndio maana hata sasa hao CCM wanajitahidi kuchakura kwenye jalala kutafuta mwenye "afadhali" manake waadilifu wote walishatupwa nje ya system siku nyingi!
 
Alinda, mimi ninakubaliana nawe kabisa kuwa CCM ni janga linalotakiwa kutokomezwa lisiwe madarakani tena. Tatzi ni kuwa kwa miaka ishirini sasa tumeshindwa kulitokomeza hata pale ambapo hali ilikuwa ni wazi kabisa kuwa CCM imechoka bado walio wengi (japo kama ni kwa sababu ya Khanga Kofia na Ubwabwa) bado waliichagua.

Sasa basi iwapo bado watu hao wakiichagua CCM, itaendelea kututawala. Ninadhani kuwa mjadala uliopo hapa siyo kuwa tumchague Makongoro, la hasa kwa vile bado hatujaona mgombea wa Ukawa. Tunachosema ni kuwa hao walioko CCM ni nani anafaa. Kumbuka kuwa CCM ina kaukiritimba fulani kuwa mwenyekiti ana nguvu sana, na kwa vile mfumo wao ni kuwa mgombea wao ndiye vile vile atakuwa mwenyekiti, basi Makongoro akishakuwa mgombea ndiye vile vile atakayekuwa mwenyekiti, hivyo atakuwa na power zaidi ya vigogo aliowakuta. Ni kama ambavyo Kikwete alivyoishia kuwa na power kuliko Malecela.


Mkuu kama ni kuangalia ndani ya CCM na kuchagua mwenye unafuu mpaka sasa sioni inawezekana ni kwa vile sina imani na hawa watu. Maana haiwezekani mtu msafi apite kwenye mkono ya watu wachafu na aiendelee kuwa msafi hii kitu haiwezekani. Mfno halisi tunayo Mzee Mkapa aliitwa Mr. Clean lakini kilichotokea tunakifahamu, Rais Kikwete hakuwa mla rushwa au fisadi lakini yanatokea hvi sasa ni kama ndoto.

Hivyo basi kwa kutumia hiyo mfano miwili sina imani na CCM pamoja na wagombea wao. Mfn Mdogo tu Makongoro yuko na Mkono sote tunafahamu ufisadi wa Mkono sasa hapo unategemea Makongoro anakapoukwaa Urasi atamgeuka Mkono? Na kama hasipomgeuka mkono atawezaje kushughulikia rushwa?

Na ninavyofahamu si Mkono tu huko mbeleni tutashuhudia mengi si ajabu hata Lowassa akaumbwa kuokoa jahazi maana uchaguzi wa mwaka huu si lelema kama miaka ya nyuma kwamba ukishapitishwa na CCM basi umeisha kuwa rais.

Uchanguzi wa mwaka huu kila kura ya kila mwananchi inahitajika. Na kampeni za kila mbunge kwa mgombea kiti cha urais zinahitajika, hapo ndipo utakapokuta Makongoro anakwenda kuwapigia mafisadi magoti maana wana nguvu za kipesa hawa watu.

Na pia mpaka sasa bado Makongoro hajanishawishi maana Charles Makongoro anabebwa na jina la Nyerere hakuna kitu kingine. Kama kipo na unakifahamu naomba unipe shule.
 
Swala la CCM kubadilika au kutobadilika liko mikononi mwa viongozi wa CCM na wanaccm wenyewe. Kazi yangu mimi na wewe ni kuhakikisha ili dudu linatoka madarakani. Kama kujirekebisha likajirekebishe likiwa nje ya madaraka.. Wakavuane magamba huku huku..

Nakuhakikishia ndani ya CCM si Makongoro au sijui nani anaweza kusafisha rushwa maana rushwa imeanzia juu kwa Mwenyekiti wao.. (rejea Richmond na Lowassa) ikatelemka kwa Katibu wao (rejea Meli na nyara za serikali) na ikasambaa kwa viongozi mbali mbali. Sasa huyu Makongoro atakuwa na "guts" gani kushughulikia wala rushwa?? Hili ndilo swali langu na ningependa wewe pamoja na Kichuguu mnipe ufafanuzi jinsi Makongoro atavyosafisha nyumba!

Ila tunachokiona ni nguvu nyingi kutumika kutuaminisha kuwa ndani ya CCM mla rushwa ni Lowassa tu!! hivi kweli ni Lowassa peke yake?

Alinda:

CCM inatumia resources za nchi kuwa hai. Hivyo ni lazima tuwe na interests ya chama hicho kufanya vizuri. Wangekuwa wanajiendesha kama Simba na Yanga kwa kutegemea michango ya wanachama, nisingetia mguu. Ningewaacha wamalize mambo yao wenyewe. Hawa wanatumia ruzuku.

Anyway, inahitaji nguvu kumnadi mtu wa CCM hapa JF.
 
Alinda:

CCM inatumia resources za nchi kuwa hai. Hivyo ni lazima tuwe na interests ya chama hicho kufanya vizuri. Wangekuwa wanajiendesha kama Simba na Yanga kwa kutegemea michango ya wanachama, nisingetia mguu. Ningewaacha wamalize mambo yao wenyewe. Hawa wanatumia ruzuku.

Anyway, inahitaji nguvu kumnadi mtu wa CCM hapa JF.


Kama kutumia resource za nchi hata Chadema, Cuf,Nccr wanatumia hivyo si CCM pekee yao.

Ni kweli kama uchaguzi ungekuwa unafanyika JF tu basi tusingekuwa na wasiwasi mwaka huu ilikuwa ni bye bye CCM lakini kwa vile uchanguzi unafanyika nchi nzima, na kule kuna watu ambao wanafikiri ni lazima watawaliwe na CCM hivyo
mkuu wangu Zakumi husikate tamaa inawezekana kabisa mwaka huu MaCCM yakarudi tena madarakani..:angry::angry:
 
Last edited by a moderator:
Utangulizi: Kwa wanaonifahamu hapa JF, wanafahamu kuwa siasa zangu ni za mkondo wa kulia zenye kuhimiza maendeleo ya watu binafsi na wakati huohuo kulinda maslahi ya wanyonge (ubebari mwema A.K.A compassionate capitalism). Kwa mtaji huu sijawahi kuunga mkono chama chochote cha kisiasa. Na kinadharia nisingeweza kuunga mkono mgombea kutoka CCM.

Lakini kutokana na kufanana kwa ahadi wanazotoa wanasiasa kutoka vyama vyote vya siasa wenye nia ya kuwa rais, nimehamua kuunga mkono nia za Makongoro Nyerere (AKA Mako). Sababu za kufanya hivi nimeziweka kwenye makundi matatu. Kundi la kwanza, iwapo CCM itashinda. Kundi la pili, iwapo upinzani utashinda. Kundi la tatu, iwapo itaundwa serikali ya mseto.

Tuanze na kundi la kwanza: Hata kama wewe ni mpinzani ni lazima uamini kuwa CCM wanayo asilimia fulani ya kushinda uchaguzi. Je CCM ikishinda, ni nani ungependelea awe rais? Kumbuka rais mtarajiwa atakaa madarakani kwa miaka mitano au kumi ijayo. Je unapendelea maumivu yaendelee?

Mako hana uzoefu mkubwa lakini huo ni mtaji na sio upungufu. Kwani hata wasafi walio upinzani hawana uzoefu wa uwaziri, urais au madaraka yoyote makubwa ya kiserikali.

CCM ni mali ya watanzania. Kwa wale wenye upeo mdogo wa historia, wakati wa mfumo wa chama kimoja, watanzania walilazimishwa kukijenga hiki chama. Wakulima, wafanyakazi, na wafanyabiashara walikatwa mapato yao bila kupenda kujenga hiki chama. Dr. Slaa, Mkandara, Lipumba, Seif Ahmed, Warioba, Mzee Mwanakijiji, Mzee Mtei, Kichuguu walichangia hiki chama. Hivyo wakati umefika kukirudisha chama kwa wananchi. Japokuwa wengine tumejitoa kwa matakwa yetu, waliobaki wasikilizwe.

Katika tangazo lake la nia ya kugombea, Makongoro ameonyesha kuwa anafahamu asili ya chama. CCM ni chama cha wananchi na sio wagombea nafasi za uongozi. Ninaamini akipewa nafasi ya kugombea atawakilisha wananchi na sio matakwa yake binafsi.

Kundi la pili, iwapo upinzani utashinda:
Upinzani ukishinda, sio mwisho wa CCM. CCM itabidi ijisafishe na kuwa mpinzani wa kweli. Kiongozi wa kuijenga CCM upya ni lazima atoke nje ya kundi lolote la mafisadi na awe tayari kukijenga upya chama. Makongoro anao uwezo huo kwa sababu yupo tayari kusema ukweli. Sio mwoga. Kweli hotuba yake alisema maneno bila kuzunguka mbuyu.

Kundi la tatu, iwapo itaundwa serikali ya mseto: Kwa historia za serikali za kiAfrika uwezekano huu ni mkubwa sana. Uchaguzi unaweza kuja na matatizo ambayo yakalazimisha uundaji wa serikali ya mseto. Wewe kama mpinzani, je ungemtaka nani kutoka CCM awe mwakilishi katika meza ya kuunda serikali ya mseto? Kama viongozi wa sasa wa CCM wanaleta matatizo ndani ya chama chao kwa ubinafsi, hawatasahu ubinafsi wao ndani ya serikali ya mseto. Kwa mtaji huu ni Mako mwenye sifa za kuwakilisha CCM kwenye serikali ya mseto kwa sababu anazosifa sawa na viongozi wa upinzani. Yeye ni outsider katika shughuli za kiutawala.

Wenu Z10.

cc: Mkandara, Jasusi, Mchambuzi, Nguruvi3, Kichuguu, alinda, gfsonwin, Jokakuu, Barubaru, Mag3, etc

Mkuu unaona kuna uwezekano wowote wa CCM kurudi kwa wenye nayo? yaani wakulima na wafanyakazi? Kwa sasa ni wazi kuwa CCM imeshikwa na mafisadi, na sio CCM ya JKN, sio CCM ya Karume. Unadhani Makongoro Nyerere can do that?

Kusema kweli i do not see him having a hint of ability to perform that miracle. Let us be honest to each other, two realistic candidates are Prof Mwandosya and Eddo, wapo wengine kama Jaji na former intel Chief.
 
Kama kutumia resource za nchi hata Chadema, Cuf,Nccr wanatumia hivyo si CCM pekee yao.

Ni kweli kama uchaguzi ungekuwa unafanyika JF tu basi tusingekuwa na wasiwasi mwaka huu ilikuwa ni bye bye CCM lakini kwa vile uchanguzi unafanyika nchi nzima, na kule kuna watu ambao wanafikiri ni lazima watawaliwe na CCM hivyo
mkuu wangu Zakumi husikate tamaa inawezekana kabisa mwaka huu MaCCM yakarudi tena madarakani..:angry::angry:

Alinda:

Nisingependa warudi madarakani. Lakini hata die hard wa upinzani wanajua kuwa uchaguzi huu ni 50-50. Na vilevile CCM wanaweza kucheza rafu. Kwa mtaji huu ni afadhari apatikane kiongozi wa CCM atakayejali nchi na watu wake.

Kuhusiana na resources, je ukimpa mlinzi wako bunduki, utajisikia vipi akiitumia kufanya ujambazi wa kukuibia? Watanzania wanaibiwa kwa resources zao wenyewe. Mtanzania yoyote anatakiwa kuwa na haki ya kufuatilia jinsi resource za nchi zinavyotumika.
 
Back
Top Bottom