Kuungua mara kwa mara shule za Waislam. BAKWATA na makundi mengine wakae chini wajitafakari

Mi nadhani katika hili suala siku tukisikia shehe Fulani,mwalimu fulani, ustazi Fulani katiwa ndani au kapotea tusipige kelele kama wale wa Uamsho,shida yako na kiongozi Fulani wa kidini au taasisi uende ukachome watoto wakiwa mabwenini kama ni Mimi nikikukamata basi lazima nikugeuze ndafu kimyakimya na nadhani hili linachimbwa kimyakimya kama ilivyokuwa kibiti washenzi walivyoanza kupotea ndipo tulipoanza kupiga kelele.
 
Alafu TISS ipo tu...!! Busy inashughulikia wapinzani akati kazii zipo nyingi
 
Zingekua zinaungua za upande ule ingesemwa ni upande huu
Basi tuwe wapole tuone hatma yake mimi na wewe ni watazamaji tu.
Kitu pekee tunachoweza kufanya ni kusubiri tu vyombo vinavyohusika na uchunguzi vitakapotoa ripoti.
 
Inaumiza sana ndugu. Nawazano mpaka nachoka
Hakika kiongozi ujue hii hali jinsi inavyoendelea inaendelea kuleta taharuki.
Ripoti za uchunguzi sijui zimefikia wapi.
Ngoja tuendelee kusubiri vyombo husika watapokuwa tayari, tuone nani yuko nyuma ya haya matukio ya moto mashuleni.
 
Pamoja na hayo nadhani serikali haichukulii umuhimu hili swala la shule za kiislamu kuungua, tangu shule mbili za Mwanzo zilipoungua walitakiwa waanze uchunguzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…