Kuvunja ahadi ya kuoa au kuolewa: Sheria inasemaje?

Kuvunja ahadi ya kuoa au kuolewa: Sheria inasemaje?

Kwani Wazee wa "nani umuuzie mbuzi kwenye gunia" wanasemaje kwanza?
Uchumba wenu vijana wa sasa mnakulana kila kitu, mpaka mwanaume haoni sababu ya kutoa posa na kufunga ndoa wakati unamfulia, unampikia, unamaana tendo la ndoa. Anajua unavyokoroma. Sasa excitement iko wapi tena ya kufunga ndoa.
 
Ila kwanini huu uchumba wa kujuana kabla ya kuoana unagharimu sana kupoteza ladha ya mapenzi ya kudumu muda mrefu kwa wanandoa?
Uchumba wenu vijana wa sasa mnakulana kila kitu, mpaka mwanaume haoni sababu ya kutoa posa na kufunga ndoa wakati unamfulia, unampikia, unamaana tendo la ndoa. Anajua unavyokoroma. Sasa excitement iko wapi tena ya kufunga ndoa.
 
Kwani haujui kuwa bongo wanawake wengi wanataka kuolewa ila wanaume wengi hawataki kuoa? Sasa mwanamke akiwa na wanaume tu bila malengo ya kuolewa mwisho wa siku atatembea na wangapi na wabongo tulivyo na mitazamo ya ajabu eti mwanamke akitembea na wanaume wengi ni malaya ila mwanaume akitembea na wanawake wengi ni kidume?
Acha uwongo wewe, una uhakika gani kuwa mimi sitaki kukuoa zaidi ya imani zako potofu tu juu yangu kwako?
 
Ndiyo nasema sasa huyo mwanamke asingepate mwingine huyo mwanaume angemuoa? Waoaji wenyewe wako wapi siku hizi?
Suala la kisheria haliendi kwa assumptions, iwe angemuoa au la inamaana kosa ni ku'move on kwa kuona mwanaume husika si muoaji.
Hapo ina maana akishitakiwa lazima alipe fidia kwa uvunjifu wa makubaliano ya kuoana.
 
Hapana, umekaa na msichana kwa kipindi flani ni wachumba mmeahidiana, sio iyo ya ghafla mnatakiwa pawepo na mashuhuda walio waona mkawatamkia wewe au mdada mkawaambia kuwa Mungu akipenda tutaoana wakajua hivyo. huo ndio ushahidi huwa unaenda mahakamani
Mzee Baba, uchumba hautamkwi na maneno, huo unaozungumzia wewe ni urafiki na sidhani kama ukiwa na akili timamu unaweza kumdai mtu eti kwa kuwa alikwambia atakuoa au utamuoa. Uchumba hurasimishwa kwa POSA.
 
Sasa ndiyo nini? Basi kumbe dawa ya wanaume ni kukataliwa tu hadi watakapojiongeza na wasiposema kuwa watawaoa hao wanawake wanaowatongoza basi waendelee kutafuta!
Usinichekeshe. Hivi unafikiri ni nani ana presha ya kuingia kwenye ndoa kati ya MUOAJI na MUOLEWAJI? Siku hizi hatutafuti, tunachagua tu kati ya wanaojitegesha 😀😀😀
 
Mzee Baba, uchumba hautamkwi na maneno, huo unaozungumzia wewe ni urafiki na sidhani kama ukiwa na akili timamu unaweza kumdai mtu eti kwa kuwa alikwambia atakuoa au utamuoa. Uchumba hurasimishwa kwa POSA.
Kwani tukizungumzia ushahidi wa uchumba ni nini fafanua kwanza kama ulielewa text zote, Evidence ya Uchumba ni upi
 
Kwani tukizungumzia ushahidi wa uchumba ni nini fafanua kwanza kama ulielewa text zote, Evidence ya Uchumba ni upi
Msichana hawi mchumba wako mpaka pale utakapopeleka POSA kwa wazazi au walezi wake. Posa yako ikikubaliwa na wazazi, msichana akakuridhia, utamvisha pete... na tangu hapo nyie wawili ni wachumba. Huyu ndio anaweza kukushitaki kuwa umevunja ahadi ya ndoa, sio viruka njia ambao hata jamaa na familia hawawafahamu
 
We we kama wewe una define vipi ahadi ya uchumba/ kumuahidi kumuoa mdada. kila case lazima iwe na ushahidi bila ushahidi hamna kesi. sasa ahadi ya uchuma ikoje na ushahidi wake ni upi, ujue ni trick ndogo sana mwanamke akiwa tu na evidence ambayo utaulizwa na mahakama kama kweli umekubali mahakama ipokee evidence hiyo maana inaweza ikawa ya maandishi au ya mtu aliyekuwepo mkisema na kuahidiana au kukubaliana. etu toa definition ya ahadi
Ninacho define mimi si muhimu kwa sababu.

1. Mimi si sheria.
2. Mimi si mtunga sheria.
3. Mimi naweza kuwa na uelewa mbovu wa sheria.

Sheria inasemaje kuhusu ahadi ya uchumba?

Ahadi ya uchumba ni lazima iwe katika au baada ya posa?

Mtu ambaye ameahidiwa kwa maneno tu bila posa, mbele ya macho ya sheria amepewa ahadi ya uchumba?

Kama mtu ambaye hajapeea posa amepewa ahadi ya uchumba, unatenganisha vipi maneno ya huyo mlevi aliyoyatoa kwa mshawasha wa mapenzi ya kikevi siku ya kwanza kumuona mwanamke, kabla ya salamu, akisema "nakupenda kweli, nataka kukuoa" na mtu ambaye amemuahidi mwanamke kwa miaka kadhaa bila posa?

Ahadi ya uchumba kisheria ni nini? Imeandikwa katika sheria gani? Kifungu gani?

Kama sheria haijaandika hili wazi, haya ni mapungufu makubwa sana.
 
Kiranga sagaciR Suala la ndoa ni muunganiko unaohitaji ridhaa ya mwanaume na mwanamke (au wanawake kama ndoa ni ya mke zaidi ya mmoja). Lord Kenyon katika kesi ya Atchinson v. Baker alisema, nanukuu; “….it would be most mischievous to compel parties marry who could never live happily together.” Maneno haya yanadhihirisha kua hakuna sheria au mamlaka yoyote inayoweza kulazimisha watu kuoana, isipokua kwa ridhaa yao na pia kuzingatia misingi na vigezo vingine vilivyowekwa na kutambuliwa kisheria. Kimsingi, andiko hili linalenga kukupa mwanga juu ya namna gani suala la kuvunja ahadi ya ndoa (breach of promise to marry) linatambulika na kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania, hasa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 na kueleza kwa kifupi haki za wahusika katika uchumba huo pindi ahadi kuoana inapovunjika.
Hujajibu swali nililouliza, na kama kuna swali umejibu, sijauliza hilo.

Ama umeshindwa kujieleza vizuri nikakuelewa.

Nimeuliza swali fupi na linaloeleweka kirahisi tu.

Kwa sheria za Tanzania, ahadi ya kuoa au kuolewa ni nini?

Tukisema huyu kamuahidi yule kumuoa au kuolewa naye, halafu akaivunja hiyo ahadi, tunachoangalia ni kipi?

Nini kimevunjwa? Ili itambulike hapa kulikuwa na ahadi, kisheria inabidi vigezo gani vitimizwe?

Hujajibu swali hili.
 
Tukisema huyu kamuahidi yule kumuoa au kuolewa naye, halafu akaivunja hiyo ahadi, tunachoangalia ni kipi?
Hujasoma comments zilizoandikwa huko juu na hata wengine kuhusu Evidence ya ahadi, au unataka nikuandikie yakwako peke yako
 
Mbona wanaume huwa mnaamua hapo hapo na hamtaki ushahidi?
Hivi unafikiri kila unachokiona au unacho kutana nacho kwenye ndoa unaweza ukakiamulia papo hapo au inahitaji muda kidogo ili kupata ukweli na ushahidi
 
Kwahiyo na huyo mwanaume naye anaenda kufungua mashitaka wakati moyoni mwake anajua kabisa hakuwa na mpango wa kumuoa huyo mwanamke haoni hata haya sasa alitaka mwanamke afanyaje?
Suala la kisheria haliendi kwa assumptions, iwe angemuoa au la inamaana kosa ni ku'move on kwa kuona mwanaume husika si muoaji.
Hapo ina maana akishitakiwa lazima alipe fidia kwa uvunjifu wa makubaliano ya kuoana.
 
Sasa ndiyo nini? Basi kumbe dawa ya wanaume ni kukataliwa tu hadi watakapojiongeza na wasiposema kuwa watawaoa hao wanawake wanaowatongoza basi waendelee kutafuta!
Kwa Mimi baby lazima nikuwowe. Tafadhali usinipeleke kwenye mukono wa sheria.
 
Back
Top Bottom