Kuwa Mbunge kwenye eneo moja isizidi miaka 10 na Mawaziri wasitokane na Wabunge isipokuwa Waziri Mkuu

Kuwa Mbunge kwenye eneo moja isizidi miaka 10 na Mawaziri wasitokane na Wabunge isipokuwa Waziri Mkuu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Nafikiri kuna umuhimu wa kubadili sheria na kuweka sheria mpya kuwa Mbunge wa eneo Fulani asiongoze eneo hilo Kwa zaidi ya Miaka Kumi. Awamu Mbili zinatosha Kabisa kuwakilisha wananchi wa Jimbo Husika.
Sioni tija ya Mbunge kukaa Miaka nenda rudi. Kama nia ni kuwakilisha Wananchi Vizuri Miaka Kumi inatosha Kabisa.

Kwa upande wa Mawaziri, ni Vizuri Mawaziri wasitokane na Wabunge labda Waziri Mkuu pekee ndiye anaweza akatokana na wabunge kama mwakilishi wa mhimili Serikali ndani ya Mhimili wa Bunge.

Mbunge kuwa papohapo Waziri ni kuwakosea Wananchi wa Jimbo husika na kumweka Mbunge huyo katikati asijue awawakilishe wananchi au serikali. Na kikawaida binadamu hupendelea kumwakilisha mwenye nguvu.

Lakini pia itaondoa uchawa Kwa wabunge wanaotaka kujipendekeza Kwa Serikali ili wapate teuzi za Hapa na pale kama vile Uwaziri.

Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.
 
Baraza la mawaziri likiongozwa na Rais ni uwakilishi wa wananchi katika kufanya maamuzi mazito ya kinchi,kutaka Waziri asitokane na mbunge maana yake hutaki uwakilishi wa wananchi juu ya mustakabali wa nchi yao, rejea maana ya demokrasia
 
Haya mambo yanaletwa na wananchi wenye akili na siyo wanaojazana uwanja wa taifa eti sijui Simba day. BTW uchawa wa wabunge utaondoka kuwa na uchaguzi huru na wa haki, na kuruhusu wagombea binafsi.
 
Haya mambo yanaletwa na wananchi wenye akili na siyo wanaojazana uwanja wa taifa eti sijui Simba day. BTW uchawa wa wabunge utaondoka kuwa na uchaguzi huru na wa haki, na kuruhusu wagombea binafsi.
Kama kutakuwa na uchaguzi huru , haki na uwazi basi wabunge watatolewa na watu pale wakiwa hawa leti manufaa.
Kwai sasa huwa wanafanya watakavyo wakijuwa kuwa ukimchaguwa usimchaguwe yeye atapita kwanguvu ya dola na CCM.

Pia wananchi wafahamu kuwa hakiyao nikupiga kura na kuchaguwa mtu anaye faa na sio kuchaguwa chama.

Rushwa haileti maendeleo
 
Kwema Wakuu!

Nafikiri kûna umuhimu wa kubadili sheria na kuweka sheria mpya kuwa Mbunge wa eneo Fulani asiongoze eneo hilo Kwa zaidi ya Miaka Kumi. Awamu Mbili zinatosha Kabisa kuwakilisha wananchi wa Jimbo Husika
Sioni tija ya Mbunge kukaa Miaka nenda rudi. Kama Nia NI kuwakilisha wananchi Vizuri Miaka Kumi inatosha Kabisa.

Kwa upande wa Mawaziri, NI Vizuri Mawaziri wasitokane na wabunge labda Waziri Mkuu pekee ndiye anaweza akatokana na wabunge kama mwakilishi wa mhimili serikali ndàni ya mhimili WA Bunge.

Mbunge kuwa papohapo Waziri ni kuwakosea wananchi wa Jimbo Husika na kumweka Mbunge huyo katikati asijue awawakilishe wananchi au serikali. Na kikawaida binadamu hupendelea kumwakilisha mwenye Ñguvu.

Lakini pia itaondoa uchawa Kwa wabunge wanaotaka kujipendekeza Kwa serikali ili wapate teuzi za Hapa na pale kama vile Uwaziri.

Ñawatakia maandalizi mema ya Sabato.
Kabisa maana vinginevyo ni ujangili tupu
 
Baraza la mawaziri likiongozwa na rais ni uwakilishi wa wananchi katika kufanya maamuzi mazito ya kinchi,kutaka Waziri asitokane na mbunge maana yake hutaki uwakilishi wa wananchi juu ya mustakabali wa nchi yao, rejea maana ya demokrasia

Ukishakuwa Waziri unakuwa wa kitaifa na zaidi unakuwa mserikali huku majukumu ya kibunge ukiwa umeyaweka Pembeni Kwa Kile kiitwacho Uwakilishi
 
Baraza la mawaziri likiongozwa na rais ni uwakilishi wa wananchi katika kufanya maamuzi mazito ya kinchi,kutaka Waziri asitokane na mbunge maana yake hutaki uwakilishi wa wananchi juu ya mustakabali wa nchi yao, rejea maana ya demokrasia
Unadhani ni sahihi mtu huyo huyo kuwa kwenye mihimili 2 tofauti? Kwa nini mbunge hawezi kuwa jaji au hakimu?
 
Ukishakuwa Waziri unakuwa WA kitaifa na zaidi unakuwa mserikali huku majukumu ya kibunge ukiwa umeyaweka Pembeni Kwa Kile kiitwacho Uwakilishi
Lazima separation of powers ionekane!
Kama Rais ana vipindi 2 kikatiba, ni ajabu na jambo la kusikitisha mbunge hana ukomo..hakuna demokrasia ya namna hii! Lazima ubunge uwe na ukomo pia!
 
Lazima separation of powers ionekane!
Kama Rais ana vipindi 2 kikatiba, ni ajabu na jambo la kusikitisha mbunge hana ukomo..hakuna demokrasia ya namna hii! Lazima ubunge uwe na ukomo pia!

Alafu hii hufanya Baadhi ya Watu kujimilikisha Baadhi ya majimbo na kuona ni Haki Yao Miaka yote kuongoza
 
Na issue ya professionalism imekaaje kwa mawaziri?
Hii badilibadili waziri anaweza hudumia wizara mbalimbali kwa kipindi kifupi tu, wana akili hizo za kusolve changamoto za wizara hata zaidi ya 3 ndani ya miaka 2 tuu??

Je waziri ni mwamuzi wa mwisho wa maamuzi ya wizara husika?
Na raisi huwa anatumia nini/ vigezo gani hasa kuchagua mawaziri.. ni elimu zao au uanasiasa bora..?

Anaejuwa kidogo anifunulie haya..
 
Na issue ya professionalism imekaaje kwa mawaziri?
Hii badilibadili waziri anaweza hudumia wizara mbalimbali kwa kipindi kifupi tu, wana akili hizo za kusolve changamoto za wizara hata zaidi ya 3 ndani ya miaka 2 tuu??

Je waziri ni mwamuzi wa mwisho wa maamuzi ya wizara husika?
Na raisi huwa anatumia nini/ vigezo gani hasa kuchagua mawaziri.. ni elimu zao au uanasiasa bora..?

Anaejuwa kidogo anifunulie haya..

Ngoja wataalamu waje.
 
Waje kwakweli, hizi mambo za mawaziri kwakeli huwa zinanichanganya.

Kidogo wanaokuaga kwenye wizara ya sheria wengi huwa ni wamesomea sheria. Ila hizi wizara nyingine ni basi tu na wewe kaa hapo, wewe kaa kule.

Ungekuwa vizuri wakaweka Mawaziri weñye Taaluma Husika.
 
Na issue ya professionalism imekaaje kwa mawaziri?
Hii badilibadili waziri anaweza hudumia wizara mbalimbali kwa kipindi kifupi tu, wana akili hizo za kusolve changamoto za wizara hata zaidi ya 3 ndani ya miaka 2 tuu??

Je waziri ni mwamuzi wa mwisho wa maamuzi ya wizara husika?
Na raisi huwa anatumia nini/ vigezo gani hasa kuchagua mawaziri.. ni elimu zao au uanasiasa bora..?

Anaejuwa kidogo anifunulie haya..
Tatizo tuna miongozo dhaifu ya kusimamia mambo yetu km taifa ukianzia na katiba..si lazima waziri wa eneo fulani awe na fani ya eneo husika, muhimu ni UWEZO usiotiliwa shaka kwamba anaweza kusimamia wizara fulani..nikisema usiotiliwa shaka ninamaanisha waziri akipendekezwa kuwepo na mahojiano/interview kupima uwezo wake kwenye eneo husika kabla ya kuthibitishwa kuteuliwa..
Ilivyo sasa uteuzi ni fursa ya mtu kujikimu au kulipa fadhila kadiri mteuzi na wanaomfanyia vetting wanataka..tumefeli pakubwa sana kushikilia mfumo huu..a total failure!
 
Unadhani ni sahihi mtu huyo huyo kuwa kwenye mihimili 2 tofauti? Kwa nini mbunge hawezi kuwa jaji au hakimu?
Siyo suala la kudhani but facts on the ground, serikali kuu ni msimamizi wa utendaji wa kila siku wa serikali,hapo unahitaji Wananchi wenyewe serikalini,haiwezekani,basi unatumia wawakilishi wao
 
Ukishakuwa Waziri unakuwa wa kitaifa na zaidi unakuwa mserikali huku majukumu ya kibunge ukiwa umeyaweka Pembeni Kwa Kile kiitwacho Uwakilishi
Jukumu la bunge ni kutunga sheria,la serikali kuu ni kutunga sera na kuzisimamia,kilimo,afya,elimu etc, serikali kuu inahitaji wawakilishi wa wananchi
 
Rasimu ya katiba ya jaji Sinde Warioba ilipendekeza mawaziri wasitokane na Wabunge.
Lakini wale wasiolitakia mema taifa hili(ccm) hawataki kwa sababu matumbo yao kama mahandaki wanataka kula ubunge na uwaziri. Wanataka kukusanya mahela kwa speed kubwa kwa kushikilia vyeo viwili.
 
Siyo suala la kudhani but facts on the ground, serikali kuu ni msimamizi wa utendaji wa kila siku wa serikali,hapo unahitaji Wananchi wenyewe serikalini,haiwezekani,basi unatumia wawakilishi wao
Wananchi wenyewe lazima wawe wabunge?
Kwa hiyo mahakama si msimamizi wa utendaji wa kila siku wa mambo yake na hivyo haihitaji wananchi wenyewe km unavyosema..?
Zipi kazi za dola (serikali, mahakama na bunge) na yupi anahitaji wananchi wenyewe(kwa tafsiri yako) na yupi hahitaji na kwa nini..Pse!
 
Jukumu la bunge ni kutunga sheria,la serikali kuu ni kutunga sera na kuzisimamia,kilimo,afya,elimu etc, serikali kuu inahitaji wawakilishi wa wananchi
Kwa nini inahitaji wawakilishi wa wananchi kuzisimamia, kwani wananchi wasiokuwa wawakilishi wakisimamia iko shida mahali?
 
Baraza la mawaziri likiongozwa na Rais ni uwakilishi wa wananchi katika kufanya maamuzi mazito ya kinchi,kutaka Waziri asitokane na mbunge maana yake hutaki uwakilishi wa wananchi juu ya mustakabali wa nchi yao, rejea maana ya demokrasia
Rudia kusoma ulichokiandika ujione ulivyoboronga
 
Back
Top Bottom