Kuwa sehemu ya historia ya katiba mpya kwa kuweka maoni yako hapa

Kuwa sehemu ya historia ya katiba mpya kwa kuweka maoni yako hapa

Yangu haya hapa
1.Bunge lisiwe la kudumu, wabunge wafike tu bungeni nyakati za vikao vya bunge na kulipwa posho za kujikimu za kawaida kwa viwango vya watumishi wa serikali.. Wabunge wawe ni watumishi wa sekta nyingine za serikali

2. Wabunge wawe ni wanataaluma waliobobea kwenye taaluma mbali mbali..na vikao vya bunge vizingatie mahitaji ya lazima ya taifa kama kipaumbele no 1

3.Thamani kubwa iliyowekwa kwenye siasa ibadilishwe na kuwekwa kwenye taaluma na wanataaluma ili kuchochea maendeleo

4. Mishahara na marupurupu ya wabunge visiwe tofauti na mapato ya wanataaluma kama walimu, mabwana afya shamba nk
Hapa umeweka mawazo yako ambayo yanainesha wazi chuki ulizonazo kwa wabunge ungejikita kwenye Mambo ambayo yanamgusa mojakwamoja mtanzania siyo kwanini mbunge apate hiki huyu apate kile hayo ni mawazo ya wivu jikiye kwenye maslahi ya mtanzania hapo sijaona point kabisa
 
Bunge bora lazima haya yawepo:
1. Rais akitoka chama A spika lazima atoke chama B.
2. Mawaziri wasiwe Wabunge.
Hii itakuwa ngumu maana chama B kwamfano kwa sasa hakuna wamesusa waliobaki hawawezi kugombea uspika wakashinda maana wako wachache katiba ielekeze chama Cha siasa kikisusa kifutwe
 
Hapa umeweka mawazo yako ambayo yanainesha wazi chuki ulizonazo kwa wabunge ungejikita kwenye Mambo ambayo yanamgusa mojakwamoja mtanzania siyo kwanini mbunge apate hiki huyu apate kile hayo ni mawazo ya wivu jikiye kwenye maslahi ya mtanzania hapo sijaona point kabisa
Haimaanishi kama wewe hujaona point basi iwe ni pointless.. Haya ni yangu mimi nawe jitahidi uweke ya kwako.. Ukosoaji wako hautabadili hata nukta wa kile nilichoandika
 
Kenya wameandika katiba mpya nzuri baada ya vita wakati wa uchaguzi, Marekani waliandika katiba mpa baada ya vita ya kiraia " Civil War".
Ktk mazingira ya Tanzania ambapo walioko madarakani hawataki katiba mpya kwa kuhofia kupoteza madaraka, katiba mpya haitopatikana.
Inatakiwa kutengenezwe mazingira ambayo kila upande utapata kiu kubwa ya katiba mpya ili hali fulani isije kutokea tena.
Umeweka fumbo hakuna mtu atajuwa ulikuwa na maana Gani hayo mazingira ni yapi?
 
Tuwe na katiba ambayo Kila mtu yupo chini ya sheria kuepusha haya tunayoyaona Sasa[emoji1545]
Mtu anakuambia anafuata katiba kwa maneno lakini kiuhalisia hafanyi kwakuwa Yuko madarakani utafanyaje? Cha msingi kiangaliwe kitu kinachochochea uchumi na kuahusha garama za maisha basi katiba ni siasa na siasa ni mchezo mchafu Kenya unasifia wanakatiba mpya inawasaidia nini?
 
Haimaanishi kama wewe hujaona point basi iwe ni pointless.. Haya ni yangu mimi nawe jitahidi uweke ya kwako.. Ukosoaji wako hautabadili hata nukta wa kile nilichoandika
Utakuwa bado hujawaelemisha watu juu ya nini unakitaka zaidi utaonekana mchochezi
 
Katiba mpya yaja na hili sio jambo geni wala la kubahatisha tena. Tumetoka mbali na tumepitia mengi mabaya na mazuri ya kushangaza na ya kuleta matumaini pia. MOJA LILILO WAZI ni kwamba KATIBA MPYA haizuiliki tena!

Jamii Forums ni mtandao tegemewa kwa mengi hapa Tanzania hasa linapokuja suala la mawazo mbadala yenye tija na chanzo kikubwa cha habari za kuaminika na kujenga.

Mawazo na makala nyingi za katiba mpya aina vinapitia hapa ama vinaanzia hapa
Viongozi wengi serikalini ni watumiaji wakubwa wa huu mtandao wa JF
Vyama vya kijamii, wananchi, waandishi mbalimbali, na watu wengine wote wa kaliba zote ni watumiaji mahiri wa JF

Kwa maana hiyo basi tunapoingia kwenye mchakato muhimu wa katiba mpya, Jamii Forums kupitia wewe inaweza kutoa mchango muhimu na mkubwa kwenye kupata katiba mpya Tanzania

Kuwa sehemu ya historia tukuka! Weka wazo/mawazo yako sasa kuhusu katiba mpya. Kumbuka kati ya mengi tutakayoyaandika hapa machache yataingia kwenye katiba mpya. Historia itakukumbuka, historia itatukumbuka. Jamii Forums itakumbukwa!

Unawaza nini kuhusu katiba mpya? Karibu sasa kama mzalendo na mhitaji wa katiba mpya kwa manufaa yetu sote na vizazi vyetu vijavyo!

Karibuni kwa furaha na moyo wa kujitoa kushiriki hili[emoji1545]

View attachment 2086468
hakuna haja ya kuanza kupoteza pesa kwenye kutengeneza katiba nyingie, ile ya warioba ilikuwa hela za kutosha, wachukue tu ile webandike tuanze kuitumia. ni nzuri na inatibu maswali mengi.
 
Katiba mpya yaja na hili sio jambo geni wala la kubahatisha tena. Tumetoka mbali na tumepitia mengi mabaya na mazuri ya kushangaza na ya kuleta matumaini pia. MOJA LILILO WAZI ni kwamba KATIBA MPYA haizuiliki tena!

Jamii Forums ni mtandao tegemewa kwa mengi hapa Tanzania hasa linapokuja suala la mawazo mbadala yenye tija na chanzo kikubwa cha habari za kuaminika na kujenga.

Mawazo na makala nyingi za katiba mpya aina vinapitia hapa ama vinaanzia hapa
Viongozi wengi serikalini ni watumiaji wakubwa wa huu mtandao wa JF
Vyama vya kijamii, wananchi, waandishi mbalimbali, na watu wengine wote wa kaliba zote ni watumiaji mahiri wa JF

Kwa maana hiyo basi tunapoingia kwenye mchakato muhimu wa katiba mpya, Jamii Forums kupitia wewe inaweza kutoa mchango muhimu na mkubwa kwenye kupata katiba mpya Tanzania

Kuwa sehemu ya historia tukuka! Weka wazo/mawazo yako sasa kuhusu katiba mpya. Kumbuka kati ya mengi tutakayoyaandika hapa machache yataingia kwenye katiba mpya. Historia itakukumbuka, historia itatukumbuka. Jamii Forums itakumbukwa!

Unawaza nini kuhusu katiba mpya? Karibu sasa kama mzalendo na mhitaji wa katiba mpya kwa manufaa yetu sote na vizazi vyetu vijavyo!

Karibuni kwa furaha na moyo wa kujitoa kushiriki hili[emoji1545]

View attachment 2086468
Wazo murua kabisa na hapa ni mahali pake sahihi kwa kila raia
 
Mtu anakuambia anafuata katiba kwa maneno lakini kiuhalisia hafanyi kwakuwa Yuko madarakani utafanyaje? Cha msingi kiangaliwe kitu kinachochochea uchumi na kuahusha garama za maisha basi katiba ni siasa na siasa ni mchezo mchafu Kenya unasifia wanakatiba mpya inawasaidia nini?
Nadhani hujaelewa ama hujui nini maana ya KATIBA..! Ndugu SINGLE WINDOW katiba sio siasa .. Hivi ni vitu viwili tofauti kabisa
 
Utakuwa bado hujawaelemisha watu juu ya nini unakitaka zaidi utaonekana mchochezi
Siko hapa kumuelewesha yoyote bali kila mmoja awe sehemu ya katiba mpya kwa ajili ya kuweka mawazo yake hapa..hebu rudi mada kuu usome muktadha wake tafadhali
 
Point safi lakini sasa likishavunjwa lipangweje? Wamo humu wanasima ilikujuwa raia wanamaoni Gani liweje unavyofikiri ukisema livunjwe tu bado hujaeleweka
Katiba mpya haitengenezwi na polisi bali na wananchi wote kupitia wawakilishi wao kwenye makundi mbali mbali ndani ya jamii
 
Lakini jamani hizi zingine zitakuwa ni ndoto hakuna katiba itakayokuja kuweka usawa kati ya mpiga kura wa kwa mtogole na mwanasiasa wa masaki never hebu tuangalie vya maana
Tabaka ziko kwenye jamii lakini zisisababishwe na ukwasi wa kisiasa.. Wala siasa isiwe uchochoro wa kujipatia utajiri
 
Neno moja kwa bibi
FB_IMG_1657372513148.jpg
 

Katiba mpya yaja na hili sio jambo geni wala la kubahatisha tena. Tumetoka mbali na tumepitia mengi mabaya na mazuri ya kushangaza na ya kuleta matumaini pia. MOJA LILILO WAZI ni kwamba KATIBA MPYA haizuiliki tena!

Jamii Forums ni mtandao tegemewa kwa mengi hapa Tanzania hasa linapokuja suala la mawazo mbadala yenye tija na chanzo kikubwa cha habari za kuaminika na kujenga.

Mawazo na makala nyingi za katiba mpya aina vinapitia hapa ama vinaanzia hapa
Viongozi wengi serikalini ni watumiaji wakubwa wa huu mtandao wa JF
Vyama vya kijamii, wananchi, waandishi mbalimbali, na watu wengine wote wa kaliba zote ni watumiaji mahiri wa JF

Kwa maana hiyo basi tunapoingia kwenye mchakato muhimu wa katiba mpya, Jamii Forums kupitia wewe inaweza kutoa mchango muhimu na mkubwa kwenye kupata katiba mpya Tanzania

Kuwa sehemu ya historia tukuka! Weka wazo/mawazo yako sasa kuhusu katiba mpya. Kumbuka kati ya mengi tutakayoyaandika hapa machache yataingia kwenye katiba mpya. Historia itakukumbuka, historia itatukumbuka. Jamii Forums itakumbukwa!

Unawaza nini kuhusu katiba mpya? Karibu sasa kama mzalendo na mhitaji wa katiba mpya kwa manufaa yetu sote na vizazi vyetu vijavyo!

Karibuni kwa furaha na moyo wa kujitoa kushiriki hili[emoji1545]

View attachment 2086468
Hivi majuzi nilitakiwa na DW nitoe maoni kuhusu miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania tangu 1992. Ni suala ambalo naulizwa mara nyingi ila majibu yangu hayazingatiwi au hupuuzwa, pamoja na ukweli au uhalisia wa hoja zangu.

Ukweli na/au uhalisia ni kwamba Tanzania haina mfumo wa vyama vingi vya siasa na haujawahi kuwepo tangu hiyo 1992. Ila tuna "mfumo wa chama kimoja cha siasa" wenye vyama vingi vya siasa. Vyama vyote vimo ndani ya mfumo wa chama kimoja! Hata katiba inayotumika sasa ni ile iliyoundwa na chama kimoja 1977

Kipengele kinachoruhusu vyama vingi vya siasa kilichomekwa tu ndani ya katiba ya chama kimoja kinachotamalaki kila pembe. Hata serikali huitwa ya CCM, si taasisi ya umma!

CCM ni chama dola na kinadumu kwa kutegemea zaidi dola. Tunahitaji tuwe na katiba mpya inayoweka mfumo, mazingira au uwanja sawa wa vyama vingi vya siasa.

Nahitimisha kwa kusema tena katiba mpya ije sasa itakayokidhi na kutoa haki kwa wote, pamoja na vyama vingi vya siasa.
 
Hivi majuzi nilitakiwa na DW nitoe maoni kuhusu miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania tangu 1992. Ni suala ambalo naulizwa mara nyingi ila majibu yangu hayazingatiwi au hupuuzwa, pamoja na ukweli au uhalisia wa hoja zangu.

Ukweli na/au uhalisia ni kwamba Tanzania haina mfumo wa vyama vingi vya siasa na haujawahi kuwepo tangu hiyo 1992. Ila tuna "mfumo wa chama kimoja cha siasa" wenye vyama vingi vya siasa. Vyama vyote vimo ndani ya mfumo wa chama kimoja! Hata katiba inayotumika sasa ni ile iliyoundwa na chama kimoja 1977

Kipengele kinachoruhusu vyama vingi vya siasa kilichomekwa tu ndani ya katiba ya chama kimoja kinachotamalaki kila pembe. Hata serikali huitwa ya CCM, si taasisi ya umma!

CCM ni chama dola na kinadumu kwa kutegemea zaidi dola. Tunahitaji tuwe na katiba mpya inayoweka mfumo, mazingira au uwanja sawa wa vyama vingi vya siasa.

Nahitimisha kwa kusema tena katiba mpya ije sasa itakayokidhi na kutoa haki kwa wote, pamoja na vyama vingi vya siasa.
CCM ni chama dola na kinadumu kwa kutegemea zaidi dola. Tunahitaji tuwe na katiba mpya inayoweka mfumo, mazingira au uwanja sawa wa vyama vingi vya siasa.

Nahitimisha kwa kusema tena katiba mpya ije sasa itakayokidhi na kutoa haki kwa wote, pamoja na vyama vingi vya siasa.[emoji1545][emoji1545]
 
Back
Top Bottom