Kuwabagua waliosoma private mikopo elimu ya juu kunaenda kuigharimu Serikali

Kuwabagua waliosoma private mikopo elimu ya juu kunaenda kuigharimu Serikali

Chief nina rafiki yangu anafanya kazi jeshini na mshahara mnono tu. Watoto wake wawili wamesoma shule za serikali o-level na A-Level. Wote wamepata mkopo. Hawa wana baba na mama. Kwahiyo kumbe wote tupeleke watoto shule za serikali maana inaonesha ukipeleka private umefungiwa milango mkopo
Kazi za wazazi sio kiwazo kwenye kupata mkopo.
Na kuna udanganyifu ujue.
Anaweza akajaza peasants ilhali mzazi wake ni CEO.
Na wengine huwa wanafanya siri anaomba mkopo.
Afu wazazi anawaambia sina mkopo.
 
Kazi za wazazi sio kiwazo kwenye kupata mkopo.
Na kuna udanganyifu ujue.
Anaweza akajaza peasants ilhali mzazi wake ni CEO.
Na wengine huwa wanafanya siri anaomba mkopo.
Afu wazazi anawaambia sina mkopo.
kwaiyo unashauri watu wadanganye ili wapate mkopo ?
 
Bro/ Sister huo mtazamo wako sio sahihi kabisa katika maisha halisi ya mwanafunzi elimu ya juu.
Njoo na hoja. Pesa ipo ya kuwatosha wanafunzi 100, walio-apply 300, ebu shusha vigezo mzee. Wewe ndio Mkurugenzi pale HESLB.
 
Mjue nyinyi watoto kuwa mzazi kumsomesha mtoto private, sio kuwa anä uwezo kivile. Walio wengi wamejinyima kwa kukopa kwenye SAcos na vikoba. Mkumbuke pia sio wakati wote mzazi útakūwa na pesa, ajira n.k . Pia kuna watoto wengine nao wanasoma kwa kipato hicho hicho. Kumsomesha mtoto přivate ni kuhairisha mambo mengine ya maEndeleo binafsi angalau mtoto apate elimu bora. Ikumbukwe kuwa kuwa na kiwango duni cha ubora wa elimu kwa shule za serikali ndio sababu ya wazaži ku opt private, sio uwezo. NILITEGEMEA serikali ingewapunguzia mzigo wazazi waliopeleka watoto private kwani ilikuwa ni jukumu la Serikali kuhakiķisha watoto wanapata elimu bora.
Sasa Si waendelee kukopa huko saccos
 
Watu masikini tuna choyo sana, yaani kusomesha mtoto private unaonekana tajiri mwenye uwezo na ni anasa, inashangaza sana
Wakati huo huo mtu anasomesha mtoto kayumba lakini anakula bata za 40 kwa siku fedha ambayo mtu anaesomesha private anaidunduliza ili amlipie mwanae ada
 
Watu masikini tuna choyo sana, yaani kusomesha mtoto private unaonekana tajiri mwenye uwezo na ni anasa, inashangaza sana
Wakati huo huo mtu anasomesha mtoto kayumba lakini anakula bata za 40 kwa siku fedha ambayo mtu anaesomesha private anaidunduliza ili amlipie mwanae ada
Kwani umelazimishwa kumpeleka mtoto private.
Kama wewe elimu ni bora kuliko bata. Better for you. And viceversa
 
Kwani umelazimishwa kumpeleka mtoto private.
Kama wewe elimu ni bora kuliko bata. Better for you. And viceversa
Mtu mzima halazimishwi, huwa ana amua
Maamuzi ya mwenzio kumpeleka mtoto private yasiwe kigezo cha kumuona ana uwezo hivyo hastahili kupewa keki ya mkopo kijana wake anapokwenda chuo kikuu
 
Pesa za mikopo zinatokana na Kodi za watz kama hawataki kuwapa watoto wao na Kodi zao wasichukue
Kwahiyo, Kodi inatumika kwenye mikopo tu?, Vipi kuhusu ulinzi na usalama?, Barabara, huduma za jamii, mitihani, nk.
Mikopo ya elimu ya juu haiwezekani kupewa wote na katika nchi yoyote mwenye nacho anatozwa Kodi kubwa ili kumsaidia masikini. Mikopo ya elimu ya juu imewekwa kwa ajili ya masikini (Si kila anayesoma Shule za umma ni masikini). Rejea wanafunzi wanaosoma TABORA GIRLS na Boys, Mzumbe, Kibaha, MSALATO, Kilakala, Ilboru, nk( hawa baadhi Yao wana uwezo, lakini wanatafuta STATUS). Ila SECONDARY za kata na zile zisizokuwa na majina wengi wao ni masikini.
Na pia wako masikini waliofadhiliwa tu kwenye Shule za private lakini wazazi wao ni masikini. Kwahiyo, kigezo cha kusoma Shule fulani siyo sahihi sana ila ni Kigezo kizuri zaidi (tusije tukawakosesha mikopo wanaostahili).
 
Spoiler Alert.... Kitakachoigharimu nchi wala sio kupewa mkopo ambao mwisho wa siku wala hautaweza kurudisha.....

Kitakachogharimu nchi / taifa la kesho / dunia ya kesho ni kuwa na majority wasio na ajira ya kujipatia ujira...

Ni kwamba hata hao wenye nacho watakuwa hatarini kunyanganywa na wasionacho....
 
Mtu mzima halazimishwi, huwa ana amua
Maamuzi ya mwenzio kumpeleka mtoto private yasiwe kigezo cha kumuona ana uwezo hivyo hastahili kupewa keki ya mkopo kijana wake anapokwenda chuo kikuu
Kinachoangaliwa vigezo vilivyopo.
 
Kwahiyo, Kodi inatumika kwenye mikopo tu?, Vipi kuhusu ulinzi na usalama?, Barabara, huduma za jamii, mitihani, nk.
Mikopo ya elimu ya juu haiwezekani kupewa wote na katika nchi yoyote mwenye nacho anatozwa Kodi kubwa ili kumsaidia masikini. Mikopo ya elimu ya juu imewekwa kwa ajili ya masikini (Si kila anayesoma Shule za umma ni masikini). Rejea wanafunzi wanaosoma TABORA GIRLS na Boys, Mzumbe, Kibaha, MSALATO, Kilakala, Ilboru, nk( hawa baadhi Yao wana uwezo, lakini wanatafuta STATUS). Ila SECONDARY za kata na zile zisizokuwa na majina wengi wao ni masikini.
Na pia wako masikini waliofadhiliwa tu kwenye Shule za private lakini wazazi wao ni masikini. Kwahiyo, kigezo cha kusoma Shule fulani siyo sahihi sana ila ni Kigezo kizuri zaidi (tusije tukawakosesha mikopo wanaostahili).
Tangia mikopo ianze kutolewa wafaidika wakubwa ni watoto wa viongozi mtu kupeleka mtoto wake private si kigezo kwamba ana uwezo mkubwa Bali anataka mtoto wake apate elimu Bora huwezi kupeleka mtoto kwenye shule ambayo vitabu shida walimu haeajitoshelezi
 
Tangia mikopo ianze kutolewa wafaidika wakubwa ni watoto wa viongozi mtu kupeleka mtoto wake private si kigezo kwamba ana uwezo mkubwa Bali anataka mtoto wake apate elimu Bora huwezi kupeleka mtoto kwenye shule ambayo vitabu shida walimu haeajitoshelezi
Sahihi kabisa mfano halisi ni mke wa mtoto wa namba moja wa nne
 
Utanzania ni kigezo pekee sio hayo mengine yaliyojaa ujinga, na sababu Tanzania wajinga ni wengi ndio maana tunaona sawa tu, mikopo sio hisani au msaada mikopo ni kodi zetu na inarudishwa
Bajeti ndogo.
Ungekuwa wewe ndio mkurugenzi wa HESLB ungefanayaje?
 
Back
Top Bottom