Kuwaita wafadhili wetu “mabeberu”, kabla hatujaweza kujitegemea, ni ushamba unaoweza kuliangamiza Taifa tusipokuwa makini!

Kuwaita wafadhili wetu “mabeberu”, kabla hatujaweza kujitegemea, ni ushamba unaoweza kuliangamiza Taifa tusipokuwa makini!

Mkuu yapo Mambo umeandika yamenigusa,mfano swala la mabeberu,asilimia KUBWA za hospital,mashule na majengo mengine yalikuwa yao, japo Kama serikali kwa Sasa asilimia KUBWA wanayatumia.

Hili jina beberu sio zuri linatuabisha watz ,kwa maana beberu kwa ni mbuzi dume, na hufika mahala Kama ni mbegu nzuri wenye mbuzi jike hupeleka kwa beberu ili apandwe Sasa ndugu Wana JF

Wale watusaidiao tunawaita mabeberu, na wamekupa msahada mkubwa tangu Uhuru na mh BASHIRU ni shaidi.
Swali
Je, watanzania wote bila kujali vyma,dini ,wadhifa wako katika jamii,baba au mama wa familia ,kijana tunapandwa na beberu? KWA maana nyingine sie ni mbuzi jike,maana mh jk aliwai sema ukutaka kula lazima uliwe!

Sasa miaka yote tumekula vingi vya hao muaitao mabeberu, Sasa maana yake ni Nini ,?

Ushauri
Turudishe kila kitu anzia tangu Uhuru then ndo tuwaite majina ya mahajabu vinginevyo kwa majina yenu hayo mnatuzalilisha watanzania, kwamba sie ni mbuzi jike na beberu yuko tiyari kwa kuja au kwenda wenyewe kupanda,STOP Mara moja huo msemo watanzania sio wa hivyo
Aibu sn
 
Sawa toa msaada ila USITUNYANYASE ... Maana hata sisi tuna mioyo.. BLM ...
 
Uzalendo wa CCM ya sasa ni kuwabambikia kesi kesi kuwapiga risasi wapinzani kutafuna pesa za corona na kuubaka kuunajisi kuulawiti uchaguzi mkuu huo ndiyo Uzalendo wa CCM ya sasa
Hilo la uzalendo, ni kuwadanganya wananchi ili waendelee kutafuna nchi na kufanya wanavyotaka! Ni hawa hawa ccm ambao ni mafisadi wa kutupwa, leo hii eti ni wazalendo! Hivi watu wameshasahau kuhusu akaunti zao nje ya nchi na kwenye vile visiwa? Si ni hawa walisema pesa waliozoweka kwenye akaunti nje ile usd milioni moja kuwa ni “vijisenti” endapo za wengine nazo zingechunguzwa? Na nyingine kuitwa “pesa ya mboga” na mmojawapo wa hao mboga mboga!

Leo hii, hata mara baada ya uhuru, wao ndo wameamuwa kuwa wakoloni weusi huku wakilaumu hawa weupe kuwa ndo wanatuletea shida tusiweze kuondokana na umasikini na kuweza kujitegemea!

Mataifa mengine yametupiga bao, ambayo yalikuwa masikini kuliko sisi wakati tu napata uhuru mfano Malaysia na mengine mengi tu.
 
Sawa toa msaada ila USITUNYANYASE ... Maana hata sisi tuna mioyo.. BLM ...
Kwanini na wewe unanyasa watanzania wenzako? Kwanini unakiuka misingi ya ki demokrasia na utawala bora?

Tumia akili, ungana na watanzania wengine kudai katiba mpya ili na wewe uwe na sauti ya kweli kwenye mustakabali wa Taifa lako! Badala ya kusubiri na kumeza matango pori ya “mabeberu” ndiyo wameendelea kutufanya sisi ni masikini!

Hizo ni kelele tu na sababu za kijinga pale mtu anaposhindwa kazi.
 
Back
Top Bottom