Kuweka akiba ni tabia au uwezo wa kipato?

Kuweka akiba ni tabia au uwezo wa kipato?

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Kuweka akiba ya fedha kumeongezeka umaarufu katika miaka ya hivi karibuni, kutokana na sababu kama ongezeko la gharama za maisha, maendeleo ya huduma za kifedha, elimu ya fedha, upatikanaji wa habari na mengine.

Hata hivyo, kwa mtazamo wa mazingira yetu, wengi wanaona kuweka akiba kuwa changamoto kutokana na hali duni ya kiuchumi. Wakati mwingine, inaonekana kuwa ni tabia inayowezekana kwa wenye vipato vikubwa pekee.

Swali ni: Je, kuweka akiba ya fedha ni uwezo wa kila mtu, au ni tabia inayoweza kupatikana hata kwa wenye kipato kidogo?

Ni hivi, uwekaji akiba una mizizi katika tamaduni za Kitanzania kupitia mazoea kama upatu na vikoba, ambapo wanachama huchangia fedha kwenye mfuko wa pamoja kwa manufaa ya baadaye.
 
Hao wa vikoba sidhani kama ni akiba, maana wengi wanahitaji kufanyia kitu ila sio akiba
Kuweka akiba sio lazima uwe na kipato kikubwa bali ni malengo unayojiwekea mtu na mtu
Unaamua kuficha akiba hata kiasi kidogo kama 15% ya mshahara kila mwezi kwa miaka kadhaa ukiwa na lengo la kufanya kitu
 
Back
Top Bottom