Kwa android phone security: Je kuna tracking app/software yoyote inayoweza kukwepa 'factory/hard reset'?

Ahsante kwa kunitaja.

IMEI International Mobile Equipment Identity) number ni namba pekee (unique) ya simu yako na kuibadili ni kosa la jinai.

Ndio maana katika nchi zilizo katika dunia ya kwanza, simu ikipotea na IMEI pia huandikwa kwa "blacklisted".

Hata hivyo IMEI namba ni rahisi kuipata ili kuweza kuwapatia polisi pale inapoibiwa kwa kupiga namba *#06# na IMEI kujionyesha bila shida.

Kwa sasa tracking app iliyopo ni ile ya "google trace my location" au ingine ya "find my device" ila hizi ni lazima simu yako iwe iko "on" wakati wote lakini yaweza kurekodiwa last location yake na mnara ulio karibu.

Njia ingine ya uhakika kabisa ni kuhakikisha wajiandikisha na Google account na kusajili simu yako/zako na taarifa zote muhimu zitawekwa pale zikiwemo IMEI number, model, manufacturer, kampuni unotumia na last activity ya simu yako.

Nafikiri ntakuwa nimekupa mwanga wapi pa kuanzia.
 
pegasus spyware, hii hata ukireset au kubadili imei bado ita track tu, ina install kwenye firmware na wala haihitaji tracker kushika simu yako ili ku install
Problem haiuzwi kwa matumizi binafsi, inauzwa kwa mamlaka za nchi na labda mashirika ya kimataifa
 
Ndio, hiyo ni software ya kijasusi itumikayo kufuatilia nyendo za simu na mtumiaji wake nini azungumza au kuandika.

Kitaalam yaitwa "zero -click surveillance" yaani mambo kimyakimya nyuma ya pazia.

Wateja wa kampuni hiyo (Pegasus0 ni serikali nyingi tu duniani zenye dhamira ya kuwadhibiti raia wake kwa sababu mbalimbali.

Tumsaidie mleta mada kupata uwezo wa kulinda simu yake isipotee na hata ikipotea aweze kuipata akiwa na bahati.
 

Thanks mkuu Rich. Yes nimepata mwanga, na ninaendelea kujifunza haya mambo ya tech kwenye phone security.
 

Ni kwanini haiuzwi kwa individuals? Hiyo ndiyo ingekuwa mwarobaini kamili kwa hawa wezi wanaoreset simu na kuchange IMEI number.
 
Ni kwanini haiuzwi kwa individuals? Hiyo ndiyo ingekuwa mwarobaini kamili kwa hawa wezi wanaoreset simu na kuchange IMEI number.
Kwa sababu inaingilia uhuru wa faragha za watu, hivyo ni kinyume na haki za binadamu. Hata mamlaka za nchi wayotumia bado si kwa mujibu wa sheria, wanatumia kwa kificho ili kufuatilia wanaowalenga kuchunguzwa. Lakini hata ingeruhusiwa kuuzwa kwa kila mtu bado bei yake ni mamilioni ya dola.

Fikiria spyapp ina install kwenye kifaa unahokilenga kwa kumpigia huyo mtu simu tu, halafu apokee au asipokee software inakua imesha install na tayari unaanza kuona na kusikia kila kinachofanyika kwenye simu yake
 
Njia nzuri na salama kwa simu yako ni kuitunza vizuri na kuwa makini isipoteee. Na ikisha potea sio simu yako tena ni ya mwingine hiyo.

Hata iPhone yenyewe inaibiwa inauzwa spare part koo hamna utakacho kwepa kwenye kuibiwa.
 
Mkuu nahitaji hiyo elimu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…