Kwa Askofu Kakobe - Baada ya kufunga ndoa, maharusi wapanda daladala na pikipiki kwenda makwao

Kwa Askofu Kakobe - Baada ya kufunga ndoa, maharusi wapanda daladala na pikipiki kwenda makwao

Kwanini utumie mamillion kwa shughuri ya siku moja
emoji1787.png
Kama mtu binafsi pamoja na ndugu plus marafiki wana hali nzuri ya uchumi sioni ubaya wowote wa kutumia millions. Jikune pale mkono unapofika.
 
Pete sio amri, Ni Kama zilivyo nguo ndefu za mkia kwenye harusi
Kama hamna pete sawa, ikiwa nayo inaongeza mashamsham
 
Ni Jambo jema lakini kwa Karne hii mtihani mkubwa ni kumpata mwanamke atakayekubali kufunga ndoa bila sherehe kubwa. Wengi wanataka sherehe ya kifahari, msafara wa magari na miosho mingi ili mji mzima wajue kuwa ameolewa. Ukigusia swala la ndoa bila sherehe wanakukimbia
Anayekimbia hajakupenda
 
Mi nadhani ndoa inahitaji kushuhudiwa na watu kama ishara ya baraka pia. Kama bible imeweza kuhusianisha tukio la kuokolewa na bwana kama ni mfano wa harusi na kila jicho litashuhudia nadhani its a blessing zaidi watu wakishuhudia.
 
Tunachokereka nii kutusumbua michango
...kubaliana na mwenzako, itisheni wazazi na mchungaji, tawanyikeni
Kama hauna pesa mwambie mtu ukweli kwamba, "ndugu yangu hongera kwa kuamua kufunga ndoa lakini mimi nipo katika hali mbaya sana ki-uchumi"
 
Sema waumini wa Kakobe wanaona(ga) kama vile tumewavamia kwenye sayari yao. Tuondoke.
 
Safi sana, Mungu akawaongoze katika maisha yao.
 
Yaani nalo niswala lakujinadi nalo?
Huko nje Kakobe amepaki V8 lake,waumini wengi ni wasaga lami
 
Mi nadhani ndoa inahitaji kushuhudiwa na watu kama ishara ya baraka pia. Kama bible imeweza kuhusianisha tukio la kuokolewa na bwana kama ni mfano wa harusi na kila jicho litashuhudia nadhani its a blessing zaidi watu wakishuhudia.
Ndoa hizi zimeshuhudiwa na maelfu ya watu; na kati yao ni ndugu na marafiki zao
 
Masihi mwenyewe alikuwepo kwenye harusi moja huko kana, divai ikaisha akafanya mambo yake watu wakaendelea kunywa kwa furaha.
Si kila neno katika divai katika Biblia maana yake ni pombe kama wengi wanavyofikiri lazima pombe iwepo katika sherehe zao kama hizi std7
 
Ilikuwa siku ya Ijumaa 19.2.2021, ni siku nyingine ya kukumbukwa, katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam, lililoko Barabara ya Sam Nujoma; pale ambapo jumla ya wahusika 84 waliposhiriki katika kufungwa kwa Ndoa 21, zilizofungwa kwa pamoja katika Ibada ya Ndoa iliyoanza saa 5 asubuhi. Wahusika hao 84, walikuwa ni Mabwana Arusi 21, na Mabibi Arusi 21, ambao hawajawahi kuishi pamoja; na jumla ya Mashahidi 42 (waume 21 na wake zao 21).

Kama ilivyo ada, katika Arusi hizo, viwango vya mavazi ya Mabwana na Mabibi Arusi, vilikuwa ni vilevile ambavyo vimekuwa vikizingatiwa, katika Ndoa mamia kwa mamia, zilizofungwa katika Kanisa la FGBF, kwa miaka zaidi ya 30; hususan tangu Askofu Mkuu Zachary Kakobe alipoliasisi Kanisa hili, tarehe 30.4.1989.

Katika Ibada hiyo ya Ndoa, Askofu Kakobe alihubiri kwanza ujumbe wa Neno la Mungu lisiloghoshiwa, wenye kichwa, "WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII" (WARUMI 12:2); kisha ndipo alipofungisha Ndoa hizo 21 kwa pamoja.

Suala lililowavutia sana wageni, waliohudhuria kwa mara ya kwanza, katika Ibada za Ndoa za Kanisa la FGBF, ni jinsi walivyowashuhudia Maarusi hao, wakitumia usafiri uleule wa kawaida ambao wamekuwa wakiutumia, wanapokwenda Kanisani, katika Ibada nyingine za kawaida. Baada ya kufunga Ndoa zao, Bwana Arusi mmoja mwenye gari lake, alikwenda na mkewe, nyumbani kwake, na gari lake hilohilo, huku akiliendesha mwenyewe.

Baadhi ya Maarusi, walikwenda kwao, kwa kutembea tu kwa miguu, huku wameshikana mikono kwa upendo na furaha isiyoelezeka; na kuwasisimua watu wengi. Siyo hilo tu, Maarusi wengine wengi walitembea kwa miguu, huku wamejaa bashasha, mpaka kwenye kituo cha daladala kilichoko jirani na Kanisa hilo, na kupanda daladala hizo zilizowapeleka majumbani kwao. Taarifa zilizopatikana baadaye, zinaeleza jinsi baadhi yao walivyokuwa wakihubiri Injili ndani ya daladala hizo walizozipanda.


Bwana Arusi mmoja, ambaye hutumia pikipiki (bodaboda) yake kuja Kanisani, alimvisha helmet (kofia ngumu) mkewe, kisha akampakia mkewe (Bibi Arusi), kwenye bodaboda hiyo, na kuondoka naye kwenda nyumbani, huku watu wengi walioshuhudia tukio hilo, wakishangilia kwa nderemo, vifijo na vigelegele !

"Basi atukuzwe Yeye (Mungu) awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina" (WAEFESO 3:20-21). MARANATHA !!!

Tazama picha zao

View attachment 1708770

View attachment 1708771View attachment 1708772View attachment 1708773View attachment 1708774View attachment 1708775View attachment 1708776View attachment 1708777View attachment 1708778View attachment 1708779View attachment 1708780View attachment 1708781View attachment 1708782View attachment 1708783View attachment 1708785View attachment 1708786View attachment 1708787View attachment 1708788View attachment 1708789View attachment 1708791View attachment 1708792View attachment 1708793View attachment 1708794View attachment 1708795View attachment 1708796View attachment 1708797View attachment 1708798View attachment 1708800View attachment 1708801View attachment 1708802

Ilikuwa siku ya Ijumaa 19.2.2021, ni siku nyingine ya kukumbukwa, katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam, lililoko Barabara ya Sam Nujoma; pale ambapo jumla ya wahusika 84 waliposhiriki katika kufungwa kwa Ndoa 21, zilizofungwa kwa pamoja katika Ibada ya Ndoa iliyoanza saa 5 asubuhi. Wahusika hao 84, walikuwa ni Mabwana Arusi 21, na Mabibi Arusi 21, ambao hawajawahi kuishi pamoja; na jumla ya Mashahidi 42 (waume 21 na wake zao 21).

Kama ilivyo ada, katika Arusi hizo, viwango vya mavazi ya Mabwana na Mabibi Arusi, vilikuwa ni vilevile ambavyo vimekuwa vikizingatiwa, katika Ndoa mamia kwa mamia, zilizofungwa katika Kanisa la FGBF, kwa miaka zaidi ya 30; hususan tangu Askofu Mkuu Zachary Kakobe alipoliasisi Kanisa hili, tarehe 30.4.1989.

Katika Ibada hiyo ya Ndoa, Askofu Kakobe alihubiri kwanza ujumbe wa Neno la Mungu lisiloghoshiwa, wenye kichwa, "WALA MSIIFUATISHE NAMNA YA DUNIA HII" (WARUMI 12:2); kisha ndipo alipofungisha Ndoa hizo 21 kwa pamoja.

Suala lililowavutia sana wageni, waliohudhuria kwa mara ya kwanza, katika Ibada za Ndoa za Kanisa la FGBF, ni jinsi walivyowashuhudia Maarusi hao, wakitumia usafiri uleule wa kawaida ambao wamekuwa wakiutumia, wanapokwenda Kanisani, katika Ibada nyingine za kawaida. Baada ya kufunga Ndoa zao, Bwana Arusi mmoja mwenye gari lake, alikwenda na mkewe, nyumbani kwake, na gari lake hilohilo, huku akiliendesha mwenyewe.

Baadhi ya Maarusi, walikwenda kwao, kwa kutembea tu kwa miguu, huku wameshikana mikono kwa upendo na furaha isiyoelezeka; na kuwasisimua watu wengi. Siyo hilo tu, Maarusi wengine wengi walitembea kwa miguu, huku wamejaa bashasha, mpaka kwenye kituo cha daladala kilichoko jirani na Kanisa hilo, na kupanda daladala hizo zilizowapeleka majumbani kwao. Taarifa zilizopatikana baadaye, zinaeleza jinsi baadhi yao walivyokuwa wakihubiri Injili ndani ya daladala hizo walizozipanda.


Bwana Arusi mmoja, ambaye hutumia pikipiki (bodaboda) yake kuja Kanisani, alimvisha helmet (kofia ngumu) mkewe, kisha akampakia mkewe (Bibi Arusi), kwenye bodaboda hiyo, na kuondoka naye kwenda nyumbani, huku watu wengi walioshuhudia tukio hilo, wakishangilia kwa nderemo, vifijo na vigelegele !

"Basi atukuzwe Yeye (Mungu) awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; naam atukuzwe katika Kanisa na katika Kristo Yesu hata vizazi vyote vya milele na milele. Amina" (WAEFESO 3:20-21). MARANATHA !!!

Tazama picha zao

View attachment 1708770

View attachment 1708771View attachment 1708772View attachment 1708773View attachment 1708774View attachment 1708775View attachment 1708776View attachment 1708777View attachment 1708778View attachment 1708779View attachment 1708780View attachment 1708781View attachment 1708782View attachment 1708783View attachment 1708785View attachment 1708786View attachment 1708787View attachment 1708788View attachment 1708789View attachment 1708791View attachment 1708792View attachment 1708793View attachment 1708794View attachment 1708795View attachment 1708796View attachment 1708797View attachment 1708798View attachment 1708800View attachment 1708801View attachment 1708802


Tujikumbushe habari ya kijana Ezekiel Zachary Kakobe, mtoto wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe; naye alifunga ndoa na GRACE MATHIAS MWANGU, katika Ibada ya Ndoa iliyofanyika katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Dar-Es-Salaam; lililoko Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge; siku ya JUMATANO, tarehe 10.Feb.2021.
1614368728677.png

Katika kanisa la Full Gospel Bible Fellowship ndoa zote ziko sawa kama yanenavyo maandiko matakatifu katika Biblia. Sasa unaweza kufungua link >>> Album ya tukio la ndoa ya Kijana Ezekiel wa askofu Zachary Kakobe

Baba Askofu mkuu Kakobe, alihubiri ujumbe wa Neno la Mungu lisiloghoshiwa, wenye kichwa, "LAKINI TANGU MWANZO HAIKUWA HIVI (MATHAYO 19:8). Tazama sehemu ya matukio ya ibada ya ndoa hii kupitia video kwa hisani ya wapendwa wa Chomoza Tv
1614369330522.png
1614370034444.png

1614370253873.png
Imeandikwa katika Biblia Takatifu "mwanamume atamwacha baba yake na mama yake; naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja".
 

Attachments

  • 1614367873262.png
    1614367873262.png
    1.1 MB · Views: 1
Si kila neno katika divai katika Biblia maana yake ni pombe kama wengi wanavyofikiri lazima pombe iwepo katika sherehe zao kama hizi std7
Mimi siko huko kwenye pombe, mimi nasema Yesu alkuwepo kwenye harusi yaani ukumbini kwenye sherehe, na alitoa mchango wake kwenye hiyo harusi kwaiyo harusi ni kitu cha baraka.
Sasa mlokole kama anajitenga na watu, na ndugu, jamaa na marafiki,
Kwanini siku akioa hasiwe kama mwana mkiwa.
 
Back
Top Bottom