Kwa hali ilivyo CCM Bernard Membe ametudanganya hana ushawishi mkubwa ndani ya chama, hasira ya CCM ni juu ya wahamiaji.

Kwani ujuha ni nini?
Hivi we chukulia mfano Jimbo la kawe wagombea zaidi 170 hebu wape dk 20 za kujieleza kila mmoja itachukua muda gani?
Ungekuwa wewe ndio mratibu wa huo uchaguzi ungeruhusu kitu kama hicho?
We unadhani hao watu hawafahamiki kwenye hayo majimbo? Huko kwenye kata waliokuwa wanazunguka walikuwa wanaenda kufanya nini?
 
Nani aliwaruhusu kuzunguka kwenye Kata?
 

Hao watu 170 walipata wapi nafasi ya kuuza sera hapa kawe? Au unadhani kawe ni US kiasi kwamba watu wauze sera wasionekana? Kufahamika na watu ndio sera zako kueleweka? Muite Paskali Mayalla aseme ni lini alikuwa anazunguka hiyo kawe kuuza sera zake, mpaka apewe dakika 2 kueleza sera zake? Au unadhani hatujui kuwa sio ruhusa kuanza kujinadi kwa wapiga kura kabla ya muda rasmi? Hivi unajua kuanza kampeni kabla ya muda ni kosa? Unafahamu unachotetea?
 
Membe hana mvuto,walau angekua hata nusu ya Lowasa kidogo angetikisa,we umesahau kupita kwa Magu 2015 ilikua kwa sababu wanaCCM walimkataa membe baada ya Lowasa kukatwa..hivyo hata huko ndani ya CCM membe hana washabiki,..labda Lissu ndo ataleta amshaamsha kidogo ila mwaka huu upinzani ungekausha tu
 
Mkuu huko upinzani manapewa dakika ngapi za kujinadi?
 
Wapotee mara ngapi?! Yaani sasahivi wameachwa washambuliane wao kwa wao (ACT na Chadema). Yaani by the time campaign zinaanza watakuwa wameshagawana fito. Teh teh teh....
 
Mkuu huko upinzani manapewa dakika ngapi za kujinadi?

Sio chini ya dakika 15, na nafasi ya kutosha kujibu maswali. Kimsingi upinzani hawapati ushindi wa mbeleko, hivyo hawajitokezi wengi. Ccm wamejitokeza wengi safari hii baada ya kuvutika na Hadaa kuwa ccm ni mpya, na mtu yoyote anaweza kushinda bila rushwa. Matokea yake kila mmoja kajua ccm ni ileile ya ushindi wa rushwa. Pia hiki kitendo cha box la kura kunajisiwa na mgombea yoyote wa ccm kutangazwa bila kujali matokeo, kimechangia watu wanaopenda madaraka ya mteremko kujitokeza kwa wingi.
 
Wapotee mara ngapi?! Yaani sasahivi wameachwa washambuliane wao kwa wao (ACT na Chadema). Yaani by the time campaign zinaanza watakuwa wameshagawana fito. Teh teh teh....

Hao watoa rushwa ndio wafanye wapinzani wapoteane?
 
Sasa subilia uchaguzi ufanyike ndio utatueleza kujieleza dakika 30 na dakika 2 nani atakuwa mshindi
 
Sisi tulishalitambua Hilo kitambo saana!
 
Sasa subilia uchaguzi ufanyike ndio utatueleza kujieleza dakika 30 na dakika 2 nani atakuwa mshindi

Kwa tume hii ya uchaguzi isiyo huru, unaweza kusimama mbele ya wanaume na kutambia atakayetangazwa mshindi?
 
Watu wanakamatwa na kutupwa ndani hata wanapofanya vikao vya ndani kwanini vyama visidhoofike. La ajabu ni kwamba baadhi ya wapuuzi wanafurahia udikteta huu.
 
Kuna uwezekano mkubwa akahairisha kugombea mwaka huu akasubiri 2025 , kipindi hiki akakitumia kukiimarisha chama na kujipanga kwa ajili ya 2025
 
CHADEMA Ubinafsi wenu utakiangamiza chama chenu. Juzi tu mlikuwa mnamshabikia huyo Membe baada ya kujiunga ACT Wazalendo badala ya Cdm kama mlivyokuwa mnafikiri eti Membe hana maajabu .
 
Miaka yote alipokuwa CCM Membe alikuwa akisafiria nyota ya JK.
otherwise ana zero network ndani ya CCM.
plus, hana cha maana cha kuonyesha alichokifanya kikaonekana machoni pa Watanzania akiwa kiongozi katika serekali ya CCM.

wapinzani wakimsimamisha kama mgombea kupitia coalition yao basi watambue kuwa sisi sympathizers wao kura ya urais hatutapiga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…