Kwa hali niliyoiona sitashawishika tena kupima UKIMWI


Mh una moyo
 
Ukienda hospital yeyote ambayo kuna CTC basi ukijieleza na pia iwe masaa 72 hayajapita tangu upate exposure watakupima wakikukuta negative watakupa pep za kumeza kwa siku 28

Ok unaweza kuzitaja hizo hospital?
 

Hivi kwa kawaida virusi huwa detected baada ya siku ngapi toka kuingia mwilini?
 
Mh eti mwanaume akichezea papuchi kwa kidole mpaka ikachubuka anaweza kukuambukiza VVU? but hamjakiss wala kunyonyana sehemu yeyote na mlitumia condom ku sex?
 
Ndoto yake kubwa ilikuwa Kwenda Marekani, na Kwa Kuwa ukiwa positive huwezi kupewa Visa ya kwenda Marekani, ndoto imepotea na msongo wa mawazo juu ...
Sent using Jamii Forums mobile app


Mkuu Kanyunyu, kuweka records sahihi... pitia site hii ili ufahamu ni nchi zipi zina ENTRY/VISA restrictions basing on HIV+ Status. Na ni nchi zipi ambazo hazina any kind of ENTRY/VISA restrictions basing on HIV Status. Ni global database kuhusu countries with or without Entry or Residence restrictions based on HIV Status: HIVTravel - Home .

For the case of USA, people with HIV wanaingia USA bila zengwe lolote. Tangu mwaka 2010, hakuna tena entry/residence restrictions based on HIV+ Status...

HIVTravel - Regulations on Entry, Stay and Residence for PLHIV




-Kaveli-
 
Ok unaweza kuzitaja hizo hospital?
Hospital yeyote kubwa ya mkoa au ya wilaya ina CTC..



Hivi kwa kawaida virusi huwa detected baada ya siku ngapi toka kuingia mwilini?


Inategemea kulingana na aina ya kipimo, rapid test Mfano SD Bioline HIV 1&2 ambacho ndio hutumika zaidi hapa tz kinagundua maambukizi kuanzia siku ya 21, lakn ni vizuri kupima baada ya siku 28 Kwani kimeonyesha uwezo wa kugundua 95% ya maambukizi.
Vipo vipimo vya 4th generation Elisa au rapid test combo ambayo ina uwezo wa kudetect both antibody and antigen huchukua wiki 2 kuweza kudetect maambukizi, PCR hudetect kuanzia siku ya 10..


Mh eti mwanaume akichezea papuchi kwa kidole mpaka ikachubuka anaweza kukuambukiza VVU? but hamjakiss wala kunyonyana sehemu yeyote na mlitumia condom ku sex?
VVU huambukiza iwapo kuna mwingiliano wa damu. Kama una kidonda kikagusa damu yenye maambukizi basi utapata.
Iwapo amekuchubua na yeye kwenye kidole ana kidonda halafu vidonda vikagusana basi utapata. La kama hana kidonda hauwezi kupata. Mate hayaambukizi VVU kwani mate yana enzyme wanao inhibit virus. Hivyo kunyonyana denda kakuambukizi.
 


Ok thanx prince 22
 

Captain, pole Kwa kuwa na msimamo hasi dhidi ya HIV test kwa ku refer case ya jamaa yako (Tumuite Mr X).
Kuna mambo kadhaa ambayo huenda yamechangia Mr X kupatwa na hayo uliyoeleza( Kukonda ghafla na kupoteza siha na haiba baada ya kupima)

1. Inawezekana hakupata fursa ya kufanyiwa ushauri nasaha kabla na baada ya vipimo

2. Kama alifanyiwa ushauri nasaha Inawezekana hakuandaliwa vyema/ hakuelimishwa vyema kabla na baada ya kupima (Pre & Post test counselling)
Good counselling inatakiwa (it is a must, not optional hasa kwa HIV +ve results) ili ku minimise crisis kama hizi.

3. Failure ya counsellor kutimiza vigezo na procedure za ushauri nasaha. (Ethically, counsellor anatakiwa kumuandaa client kupokea majibu na kujirthisha kwamba somo limeeleweka kwa kumuuliza maswali na kuruhusu maswali bila kujali muda wa hiyo session. When there is any doubt kwamba huyu client hayo majibu yatasababisha crisis/kutokuyakubali/kujidhuru/ etc basi session inaweza kuahirishwa, client akaja kufuata results siku nyingine muafaka baada ya maridhiano)
4. Hata hivyo, sio mara zote procedure za counseling huhitajika (necessity doesn't apply to all),
Inategemea na ni nani aliye leta wazo la haja ya kupima kati ya client na mtoa huduma.
 
Kama muathirika ana status hiyo niliyosema na anatumia dawa asiyemwathirika hawezi kupata madhara lakini pia ni muhimu khudhuria kitengo pamoja na kupata ushauri nasaha
Ajee kwa kutumia kipimo cha Unigold ukimwi waweza gundulika kwa kipindi gani na kinafanya kazi kwa uhakika wa asilimia ngapi?
 
Kupima ukimwi kuna faida japo unahitaji moyo mgumu kuamua kupima
 
Mkuu Mungu ni mwema, tuwe makini tuache dhambi tuoe
 
Katika Maisha yangu sikuwahi kupima ukimwi ila kwa ajili safari nililazimika kupima ingawa nilikuwa najiamini kutokana na kutokuwa kweny mahusiano muda lkn niliingiwa na hofu, tulipelekwa watu wengi wa mataifa mbalimbali hapo nilipata hofu Kubwa na sijui ilitoka wapi
Ila Majibu yalikuwa mazuri
Nimetulia tuli nasubir kupima tena nikitaka kuingia kweny ndoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…