Kwa hapa alipotufikisha Rais Samia anastahili kupongezwa, kuungwa mkono na kutiwa moyo, alipokea nchi katika kipindi kigumu sana

Hongera Rais wetu Kwa kitufikisha uchumi wa chini
Hali ya uchumi wetu Ni nzuri na miradi ya maendeleo inaendelea kila Kona ya nchi yetu Hali Inayosaidia kutoa ajira za moja kwa moja kwa vijana na kusaidia mzunguko wa fedha mitaani
 

Leo tumeshinda siku nzima bila umeme ndio umerudi nusu saa iliyopita. Kwa kweli hata leo aondoke.
 
Ukifuatilia Hali ya maisha Katika nchi za ukanda huu na Afrika yote kwa ujumla utagundua kuwa Tanzania pekee ndio sehemu ambayo Rais wetu amefanya kazi kubwa ya kutunusuru wananchi wake na mfumuko wa Bei na mtikisiko wa uchumi wa Dunia,

Nakushauri kamfuatilie mwana CCM mmoja alikuwa anaitwa kalihose, utajifunza mengi Sana.
 

Wewe wakuangalie kwa jicho la huruma hata wakupe utendaji wa Kijiji.
 
DC Mtarajiwa au siyo

Ni ajqbu kwamba ukweli ukielezwa mnaingia mitini.

Samia anatoka chama gani kwanza tujue au ni mgombea binafsi? So long as ni chama ambacho ndo jinamizi la nchi yetu anastahili kukaa pembeni na chama chake ili nchi ipate maendeleo.

Ulichoandika hapo ni ufundi wenye uongp mwingi. Kama mlivyo mafundi wa kufisadi pesa za umma
 
Nakubaliana na wewe, ameliponya Taifa na tunasonga mbele. Aongezwe mitano
Nakuunga mkono mkuu ,Mh Rais Anastahili kupewa nafasi ya Kuendelea kututumikia watanzania maana ndani ya muda mfupi Tumeona juhudi zake katika ujenzi wa Taifa letu, hakika kaiheshimisha Tanzania
 
Hali ya uchumi wetu Ni nzuri na miradi ya maendeleo inaendelea kila Kona ya nchi yetu Hali Inayosaidia kutoa ajira za moja kwa moja kwa vijana na kusaidia mzunguko wa fedha mitaani

Mfumuko wa Bei unapokuwa mkubwa, thamani ya pesa hushuka.
 
Nakuunga mkono mkuu ,Mh Rais Anastahili kupewa nafasi ya Kuendelea kututumikia watanzania maana ndani ya muda mfupi Tumeona juhudi zake katika ujenzi wa Taifa letu, hakika kaiheshimisha Tanzania
Kiitikio kisicho na verse
 
Mh Rais wetu mpendwa mama Samia kajitahidi Sana kuijenga uchumi wa nchi yetu hasa kwa kuzingatia aina ya mazingira aliyoyakuta kiuchumi ambayo yalikuwa yamechangiwa na ugonjwa wa CORONA uliokuwa umeikumba ulimwengu na kutikisa uchumi wa kila Taifa, Juhudi za mh Rais kututoa katika mdororo huo wa uchumi umekuwa Ni mkubwa Sana na bado kazi hiyo anaendelea nayo kwa Kasi ya kuridhisha na kutia moyo na matumaini
 
Mfumuko wa Bei unapokuwa mkubwa, thamani ya pesa hushuka.
Mfumuko wa Bei amekuwa akikabiliana nao vizuri,wewe Ni shahidi uliona namna serikali ya Rais Samia ikitoa Ruzuku ya billion Mia moja kila mwezi katika mafuta na billion Mia moja hamsini katika mbolea Hali iliyosaidia kushuka kwa Bei ya mafuta pamoja na mbolea na kuongeza Kasi ya uzalishaji katika secta ya kilimo
 
Wewe wakuangalie kwa jicho la huruma hata wakupe utendaji wa Kijiji.
Jadili hoja mkuu, Tanzania yetu itajengwa nasisi wenyewe watanzania, Tumuunge mkono Rais wetu maana ameonyesha dhamira ya dhati na uchungu na Taifa hili,ameonyesha kutujali watanzania na kuwa na kiu ya kuona tukisonga mbele kimaendeleo
 
Hali ya uchumi wetu Ni nzuri na miradi ya maendeleo inaendelea kila Kona ya nchi yetu Hali Inayosaidia kutoa ajira za moja kwa moja kwa vijana na kusaidia mzunguko wa fedha mitaani
Ni kweli ndo maana mfumuko wa bei upo juu Kwa Sababu watanzania wanahela Kwa mfano bando bei juu, vyakula bei juu Kwa sababu Watanzania wanahela pia umeme wa mashakamashaka kwanini umeme uwepo wa uhakika serikali imeona uchumi wetu ni mzuri Kwa hiyo wameona umeme wa uhakika ni wanini.Miradi mikubwa Mingi anaendeleza Tu lakini wanatumia kwenye upigaji wa hela kama ile 1.5 T ya umeme.Alafu pia uchumi wetu upo juu mpaka mshahara umeongezeka Kwa asilimia 2.3.hongereni.
 
Umerogwa wewe
 
Leo tumeshinda siku nzima bila umeme ndio umerudi nusu saa iliyopita. Kwa kweli hata leo aondoke.
Hata mm huku Kaskazini nilikuwa nimelala sina kazi maana dah[emoji848] Sasa kama leo sijaingiza hata mia sjui huo mzunguko wa hela uko wapi[emoji2955][emoji2955][emoji2955] Au mim sipo Tanzania maana wenzangu wanaisifia[emoji58][emoji58][emoji58]

Ila mama anaupiga mwingi[emoji16][emoji16][emoji16] ndiyo maana tushazoea umeme ni wa mgao siku zote
 
Hali ya umeme itarejea katika hali yake, matatizo ya umeme kwa kiasi kikubwa yamechangiwa na ukame mkubwa ambao ulipelekea kina Cha maji kushuka na kupungua katika mabwawa yetu ya kuzalisha umeme, hata hivyo mvua muda siyo mrefu zinakwenda kuanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini mwetu Hali itakayosaidia upatikanaji wa umeme wa uhakika na wa muda wote,,huku serikali ya mama yetu mama Samia ikiendelea kutengeneza vyanzo vingine vya Nishati Kama vile gasi,upepo,jua n.k ili hata ukame ukitokea Basi tusipate athari ya kukatika katika kwa umeme na kukwamisha shughuli za uzalishaji ambazo nyingi zinategemea umeme

Lakini pia Tuendelee kupeana Elimu juu ya utunzaji wa mazingira, tusikate Miti hovyo hasa katika vyanzo vya maji , tusichome misitu hovyo , tupande Miti kwa kadri ya uwezo wetu ili kurudisha ukijani wa nchi yetu na kutunza mazingira yetu ili yatutunze na kutusaidia
 
Hali y umeme inakwenda kutengemaa muda siyo mrefu na kuanza kupatikana muda wote maana mvua zinakwenda kuanza kunyesha maeneo yote nchini hivyo kujaza mabwawa yetu ya kuzalisha umeme yaliyo athiriwa na ukame, lakini pia tumesikia mikakati ya serikali yetu kubuni vyanzo vingine vya umeme ili hata ukame ukitokea Basi tusiweze kuathirika na kupata umeme wa mgao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…