Nilibahatika kumuona Thiery Henry niliwahi kujiita Ronaldinho namkumbuka Peter Schmeichel, nimemshuhudia Xavi nilimpenda David Beckham. Japo sikumfaidi Zizou vizuri, lskini Nawakumbuka kina Shevshenko, Kaka wote walikua wakali. Nachojivunia ni kitu kimoja tu, Kuwashuhudia Liones Mess na Cristiano Ronaldo wakifanya vitu ambavyo kabla ya uwepo wao vilikua ni vitu vya kufikirika tu. Hakuna aliyeamini kwamba vinaweza kutokea.
Nachosikitika ni kwamba FIFA wamebadili maana halisi ya mpira wa miguu, wameibadili tuzo ya mchezaji bora wa dunia [ Ballon D'Or] kua tuzo ya mfungaji bora wa Madrid na Barcelona. Mbaya zaidi vichwa vya Wendawazimu pale FIFA vimepewa jukumu la kumchagua wanaetaka atwae tuzo na sio anayestahili kutwaa tuzo. Leo hii anaetwaa tuzo ni aliyefunga magoli mengi kuliko mwenzie na wala sio mchezaji bora.
Nazikumbuka zama za kina Fabio Cannavaro Matthias Sammer, Michel Platini na wengine wengi najiuliza wangekuwepo uwanjani leo hii je wangepata hii tuzo? jibu ni hapana, Ukiniuliza ni nini kilichomuweka David Luis kwenye kikosi bora cha dunia sina jibu na hata yeye mwenyewe akiulizwa hajui. Iniesta anafanya nini kwenye kikosi bora cha dunia ndio kabisa sielewi. Ukimuuliza Tony Kross ni nini kilichomuweka kwenye kikosi bora cha dunia hawezi kukujibu.
Davidi Luis & Kroos hawakua na namba za kudumu kwenye timu zao ( Chelsea & B Munich ) kabla ya kuhamia timu nyingine. Kombe la dunia Iniesta alirudi nyumban bado asubuhi, David Luis licha ya kukosa namba Chelsea lakini pia aliliangusha taifa lake kombe la dunia , alikuwepo kwenye kikosi kilichofungwa 7, Je, waliyoyafanya ndani ya miezi hii minne baada ya World cup (august to December) ni bora kuliko waliyofanya wenzao ndani ya mwaka mzima?
Fifa inazidi wanazidi kunidanganya, Najiuliza tena, Kwanini Yaya Toure hayupo kwenye hiki kikosi? Nakuja kugundua bado ni kazi ya jopo la wendawazimu, Mchezaji bora wa bara la Africa, Club ya Manchester city na ligi ya Uingereza anakosa namba kikosi bora cha dunia? Najiuliza , ni kigezo kipi kilichotumika kumpa tuzo ya goli bora James Rodriquez ? nagundua ni Kazi ya wendawazimu tena. Waliamua kumpa tuzo waliyetaka ashinde badala ya kumpa aliyestahili kushinda.
Adidas na Nike wanaupeleka mpira wapi? Sioni sababu ya kuziita tuzo za mchezaji bora wakati wachezaji bora hawatunukwi. Wanatunukwa wenye faida na Adidas au Nike, wanatunukiwa wenye sura za Hollywood kwa sababu za kibiashara. John Cruyff anasema tuzo za mwanasoka bora wa dunia kupigiwa kura ni utaratibu wa kishenzi maana watu huwapigia marafiki zao. " Ballon D'Or? A bunch of journalists and people voting for their friends"
Mfumo ndio tatizo , ifike mahali mfumo ubadilike, mfumo uliopo wa kupiga kura unawakandamiza wanaostahili kupata tuzo, viwekwe vigezo na masharti atakayekidhi ndiye mshindi. Mtindo wa kura ni wa kipuuzi. We unadhani leo Toure akishindana na mchezaji wa ligi daraja la kwanza Uingereza kwa mtindo wa kura nani atashinda? Licha ya Toure kuwa bora lakini atashindwa kwa sababu hana watu wa kutosha kumpigia kura.
Hata waafrika tujikusanye wote wenye smart phones tupige kura, waingereza wakicomand system mara moja tu wanatuzidi kura mara milioni. So mtindo wa kupima ubora wa mtu kwa kura ni mtindo wa hovyo sana kuwahi kutokea. Ni kura hizi hizi zilitumika kumnyima tuzo Sneidjer 2010, kura hizi hizi zimemnyima Frank Ribery uchezaji bora wa dunia mwaka Jana , kura hizihizi zimetumika kumnyima Manuel Neur haki yake mwaka huu.
Cha kushangaza Kikosi bora cha dunia hakina mshambuliaji wa kati, kazi ya wendawazimu. Kikosi bora cha dunia kina washambuliaji wanne wa pembeni , wawil kulia wawili kushoto, tokea lini timu ikawa na four wingers? Nafasi ya Yaya Toure ndio iliibiwa hapa . Lakini utamlaumu nani? Kazi wamepewa wendawazimu!
Kilaza