Kwa haya ya Baltazar, kuna nyaya kwenye maisha hupaswi kuzikanyaga na pia privacy kwenye mambo ya familia ni muhimu

Swali la kujiuliza hapa ni kwanini mamlaka za Guinea hazijasema kwamba hizo picha ni AI ?
Sasa mfano wewe umpige mwanao unaweza kujiuliza wewe mwenyewe..?? Kwa case ya huyo jamaa mie Sina utaalamu wa kujua hiyo ni AI or not...lakini kama kuonana na shetani inawezekana...basi hakuna linaloshindikana
 
Deals
Mwanamke akikuamini unafanya nae chochote
Vijana hamsikii soma hii:


Na Jayne Augoye
"Nimedhalilishwa. Ni sifa yangu, heshima yangu. Nataka kujua video hizi zilitoka wapi na kwa nini alizihifadhi".
Cristel Nchama, mmoja wa wanawake katika kanda za ngono za Baltasar Engonga, ana malalamiko rasmi na Gendarmerie ya Kitaifa ya Malabo (The Armed Forces of Equatorial Guinea).

Real Equatorial Guinea inasema Bi Nchama ndiye mtu wa kwanza kuwasilisha malalamiko rasmi dhidi ya Bw Engonga; ya wanawake wote katika kanda za ngono ambamo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi nao,

Bw Engonga, kwa jina la utani Bello, aliondolewa hivi majuzi kama Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Kifedha (ANIF) baada ya kusambazwa kwa video za ngono zinazomhusisha na wanawake wengi kusambaa mtandaoni wikendi.

Bw Engonga ni mtoto wa Baltasar Engonga Edjo, rais wa sasa wa Jumuiya ya Kiuchumi na Fedha ya Afrika ya Kati (CEMAC).

'Nilidanganywa'

Gazeti hilo liliripoti Bi Nchama akisema alidanganywa na mpenzi wake wa zamani, akijiona kuwa "mhasiriwa" baada ya video za ngono za Bello kuwekwa hadharani.

Kulingana na mwanadada huyo, alikataa kurekodiwa na mpenzi wake wa zamani, Bello, mara kadhaa lakini alikiri kwamba walirekodi matukio yaliyofutwa mara moja.


"Nimefedheheshwa. Ni sifa yangu, heshima yangu. Nataka kujua video hizi zilitoka wapi na kwa nini alizihifadhi," Bi Cristel alilalamika.

Amedai katika Gendarmerie kwamba Bw Engonga arekebishe uharibifu na hasara iliyosababishwa na video hizi.

Kulingana na Guinea24 , alisema ni kawaida kwa watu wazima wawili kupata wakati wa shauku na kufanya mambo ya kichaa wakati wa tendo, lakini haoni kuwa ni busara kuweka aina hiyo ya maudhui kwenye kifaa.

Baada ya malalamiko haya ya kwanza, Gendarmerie ya Kitaifa iliwaalika wanawake wengine walioonekana kwenye video zilizorekodiwa kwa siri kuripoti kesi na kuwasilisha malalamiko yao.

Eneo la mahakama

Katika habari zinazohusiana na hizi, Waziri wa Sheria, Dini na Haki za Kibinadamu, Reginaldo Biyogo Mba Ndong, alifika kwenye bafu la Mahakama Nambari 1, eneo la video moja ya Bw Ebang.

Kulingana na Impresario Ge , Bw Ndong aliulizwa kuhusu ukweli kwamba maudhui ya wazi yalirekodiwa katika vyoo vya mahakama na kusisitiza kwamba hatua mpya za udhibiti na usalama zitapitishwa.
 
Sasa wale wanaosema Al waje waseme kama haya malalamiko ya huyu mwanamke nayo ni Al

Binafsi naamini kabisa kama yangekuwa ni Al lazima serikali ya Guinea ingepata uchochoro wa kutokea kutokana na kashfa hiyo

Lakini hata Baltasar mwenyewe asingekubali kashfa ambayo si ya kweli,kwahiyo huenda kuna baadhi Al lkn si sawa kusema eti zote ni Al video
 
Upo sahihi. Na hata hizo za AI wahusika ni kuwa alikuwa anawagonga kweli
 
Acha kudanganya watu hapa
 
Fact , watu wanauwezo mdogo wa kuchanganua mambo
 
Ni kweli hujaona wanawake wakiuana?
 
Kuna kitu hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…