Kwa haya ya Masanja nitakuwa wa mwisho kuamini Watanzania tuna akili timamu!

Ile dini ina mazwa mazwa wengi wengine wapo kwa mwamposa wanagombea mafuta huko sisi watu kama hao tunachapa fimbo
 
Ile dini ina mazwa mazwa wengi wengine wapo kwa mwamposa wanagombea mafuta huko sisi watu kama hao tunachapa fimbo
Ndomana kagame aliwachana mapema....
Alishangaa eh kuna vijumba vya ibada kama 600,kutwa watu kupukutishwa hela tu wakihaidiwa miujiza

Ova
 
Mi nadhani suala la imani ni suala gumu kidogo.Unaweza kuta wewe unashangaa waumini wa masanja kwakuwa unamfahamu masanja.Hii dunia kuna watu wanafanya mambo ya ajabu sana ila kwakuwa huna ukaribu nao /huwajui vizuri..unaweza ukawa unawaheshimu.

Hujawahi sikia hii kauli “nilikuwa namuheshimu sana,ila toka jana/siku ile .. etc” What i mean wachunguze vizur hata viongozi wako wa dini unaweza ukashangaa kwanini umewaamini wakuongoze kiroho[emoji38][emoji38].
 
Ni sahihi hivyo inabidi tujitathimini kama Taifa!
 
Tuyachukue haya kama mawazo ya kampuni au ya admin?
 
Tatizo tumepewa uhuru uliopitiliza kwenye dini, ifike mahali serikali iweke standards zinazokubalika kwa mtu anaetaka kufungua kanisa maana kwa hapa tulipofika watu wanachukulia kanisa kama kijiwe cha kufanyia uhuni na kula pesa za waumini

Sijui watanzania kwa nini wanadanganyika kirahisi, anaweza akatokea muhuni yu akafungua kanisa na watu wakajaa
 
Hakika nakuunga mkono. Hakuna mchungaji pale ila ni mpigaji tu kupitia jina la Mungu na Mungu wetu hadhihakiwi. Atajibu kwa wakati ufaao.

Wanaomuamini na kumfuata kwa hakika haziwatoshi!!
 
Nitajie imani yako nikuoneshe mizaha yake
 
Huyu jamaa yeye ndo hana akili timamu

Yani kanisa lenye watu hamsini ndo utumie kuhukumu watanzania zaidi ya milioni 60?
Kwani hao 50 ni Wanyarwanda? Mbona manabii na mitume feki wako kibao Tanzania na wana wafuasi pia???
 
Na bado serikali ikalisajiri kanisa lake! Serikali inayoongoza Watanzania zaidi ya milioni 60!
Ndio uamini tuna tatizo kama taifa. Hatuna hata vigezo vya kueleweka. Bora hata Kagame, huna digrii ya theolojia, biashara ya kanisa haikuhusu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…