Kwa hii sheria ya Tanzania ya kuzuia ugaidi - Mbowe na wenzake wapambane sana mahakamani

Kwa hii sheria ya Tanzania ya kuzuia ugaidi - Mbowe na wenzake wapambane sana mahakamani

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825

kwa kifupi
UGAIDI NA TAFSIRI KATIKA SHERIA YA KUZUIA UGAIDI SURA YA 19 YA MWAKA 2002.

Tafsiri na kuzuiwa kwa vitendo vya ugaidi.kifungu cha

4.-(1) Hapana mtu yeyote katika Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania nahapana raia wa Tanzania aishiye nje ya Jamhuri ya Muungano akayeruhusiwa kufanyakitendo cha kigaidi na mtu yeyote atakaye fanya hivyo atakuwa ametenda kosa la jinai.
(2) Mtu atatenda kosa la kigaidi ikiwa kwa nia ya ugaidi atatenda au hatatenda kitendo ambacho-
(a) kinaweza kufanya uharibifu mkubwa kwa nchi au shirika
la kimataifa; au
(b) kimekusudiwa au kinaweza kusemekana kuwa kimekusudiwa-
(i) kutishia uma kwa kiwango kikubwa;
(ii) kuilazimisha Serikali kufanya au kutokufanya kitendo
chochote;
(iii) kudhoofisha au kuharibu kwa kiwango kikubwa misingi ya kisiasa, kikatiba, kiuchumi au miundo ya kijamii ya nchi au shirika la kimataifa; au
(iv) kuishawishi Serikali hiyo au shirika hilo la kimataifa; au
(c) kinahusisha au kusababisha, kulingana na mazingira-
(i)shambulio kwa maisha ya mtu ambalolinaweza kusababisha kifo;
(ii) shambulokwa uadilifu wa mtu;
(iii) utekaji wa mtu.

(3) Kitendo kitatafsiriwa kuwa ni ugaidi kwa mujibu wa Sheria hii ikiwa kitendo au tishio la kitendo ambacho-
(a) kinahusisha majeraha makubwa kwa mtu;
(b) kinahusisha uharibifu mkubwa wa mali;
(c) kinahatarisha maisha ya mtu;
(d) kinaasababisha hatari kubwa kwa afya au usalama wa uma au sehemu ya uma;
(e) kinahusisha utumiaji wa silaha za moto au milipuko;
(f) kinahusisha utolewaji kwenye mazingira au sehemu yake au kusambaza au kuiweka jamii au sehemu ya jamii katika
(i) hatari yoyote, miali au viini hatarishi;
(ii) kemikali za sumu;
(iii) viumbe maradhia au ajenti wa kibaologia au sumu;
(g) kimeundwa au kimedhamiriwa kivuruge mifumo ya kompyuta au utoaji wa huduma inayohusiana moja kwa moja na mitambo ya mawasiliano, huduma za kibenki au za kifedha, usafiri au mitambo mingine muhimu;
(h) kimeundwa au kimedhamiriwa kuvuruga utoaji wa huduma muhimu za dharura kama vile polisi, ulinzi wa raia au huduma za kitabibu;
(i) kinahusisha kuleta hatari kwa usalama wa taifa au usalama wa uma, na kudhamiriwa , au kwa jinsi kilivyo,
kinaweza kuonekana kuwa kimedhamiria -
(i) kuutisha uma au sehemu ya uma;
(ii) kuilazimisha Serikali au shirika la kimataifa kufanya au kuacha kufanya kitendo chochote, na kinatendwa kwa madhumuni ya kuonesha au kuunga mkono kitendo ambacho ni ugaidi kwa mujibu wa Sheria hii.

(4) Kitendo ambacho-
(a) kitavuruga huduma zozote;
(b) kimefanyika kuonyesha kupinga, kudhihirisha au kugoma kufanya kazi,hakitachukuliwa kuwa ni kitendo cha ugaidi kwa mujibu wa kifungu hiki,
ikiwa hakijadhamiriwa kuleta madhara yaliyotajwa katika aya, (a), (b), (c), au (d) ya kifungu kidogo cha (3).
 
Back
Top Bottom